< Ezekieli 37 >

1 Mkono wa Yahwe ulikuwa juu yangu, na akanitoa kwa Roho wa Bwana Yahwe na kuniweka chini katikati ya bonde; lilikuwa limejaa mifupa.
One day Yahweh gave me another vision. In the vision I felt the power [MTY] of God on me, and by his Spirit he took me to the middle of a valley. It was full of bones [of people who had been killed].
2 Kisha akanifanya kupita kati yao kuizunguka pande zote. Tazama! Mingi yao mikubwa ilikuwa katika bonde! Ilikuwa mikavu sana.
He led me to walk back and forth among those bones. I saw that there were very many bones there, bones that were very dry.
3 Akanambia, “Mwanadamu, Je! Hii mifupa inaweza kuishi kinyume?” Hivyo nikasema, “Bwana Yahwe, wajua wewe pekee.”
He asked me, “You human, [do you think that] these bones can become living [people again]?” I replied, “Yahweh my Lord, only you know [if that can happen].”
4 Kisha akanambia, “Tabiri juu ya hii mifupa na iambie, 'Mifupa mikavu. Lisikilizeni neno la Yahwe.
Then he said to me, “Prophesy to these bones. Say to them, ‘You dry bones, listen to what Yahweh says.
5 Bwana Yahwe asema hivi kwenye hii mifupa: Tazama! nakaribia kuweka pumzi juu yenu, nanyi mtaishi.
This is what Yahweh the Lord says to you bones: I will put my breath into each of you, and you will become alive again.
6 Nitaweka mishipa juu yenu na kuleta nyama juu yenu. Nitawafunika kwa ngozi na kuweka pumzi ndani yenu hivyo mtaishi. Kisha mtajua kwamba mimi ni Yahwe.”'
I will fasten tendons to your bones, and cause your bones to be covered with flesh. I will cover the flesh with skin. Then I will breathe into you, and you will become alive. When that happens, you will know that I, Yahweh, [have the power to do what I say that I will do].’”
7 Hivyo nimetoa unabii kama nilivyokuwa nimeamriwa: nimetabiri, tazama, sauti ikaja, iliyokuwa ya mtetememo. Kisha mifupa ikasogeleana pamoja-mfupa juu ya mfupa.
So I spoke to the bones what Yahweh commanded me to speak. As I was speaking, there was a noise, a rattling sound, and the bones came together, bones joining to each other.
8 Nikatazama na, kumbe, mishipa ilikuwa juu sasa, na nyama ikatoka juu na ngozi ikazifunika. Lakini hapakuwa na pumzi juu yao.
While I was looking, I saw tendons fastening to them and flesh covering them, and then skin covered the flesh, but they did not breathe.
9 Kisha Yahwe akanambia, “Itabirie pumzi, tabiri, mwanadamu, na iambie pumzi, 'Bwana Yahwe asema hivi: Pumzi, hutoka pepo nne, na pumzi juu ya hawa walioawa, hivyo wanaweza kuishi.”'
Then he said to me, “You human, prophesy to the wind. Say to the wind, ‘Wind [APO], Yahweh says to you, blow from all four directions. Breathe into these people who have been killed, in order that they can become alive again!’”
10 Hivyo nimetabiri kama nilivyokuwa nimeamriwa; pumzi ikawajilia na wakaishi. Kisha wakasimama kwa miguu yao, jeshi moja kubwa sana.
So I said what he commanded me to say, and then breath entered them. They became alive and stood up, like a huge army.
11 Kisha Yahwe akanambia, “Mwanadamu, mifupa hii yote ni ya nyumba ya Israeli. Tazama! Wanasema, 'Mifupa yetu imekauka, na tumaini letu limepotea. Tumekatwa.'
Then he said to me, “You human, these bones represent all the Israeli people [MTY]. The people say, ‘[It is as though] our bones are dried up; there are no more good things that we can (hope for/confidently expect to happen to us); our nation is destroyed/finished.’
12 Kwa hiyo tabiri na waambie, 'Bwana Yahwe asema hivi: Tazama! Nitayafunua makabiri yenu na kuwapandisha kutoka kwayo, watu wangu. Nitakurudisha hata katika nchi ya Israeli.
So prophesy and say to them, ‘This is what Yahweh the Lord says: My people, [it will be as though] I will open your graves and cause your corpses to become alive again. I will bring you back to Israel.
13 Kisha mtajua kwamba mimi ni Yahwe, nitakapo yafunua makaburi yenu na kuwatoa kutoka kwao, watu wangu.
Then, what that happens, you my people will know that I, Yahweh the Lord, [have the power to do what I say that I will do].
14 Nitaweka Roho wangu ndani yenu hivyo mtaishi, na nitawafanya kupumzika katika nchi yenu mtakapojua yakwamba mimi ni Yahwe. Nasema na nitayafanya hayo-hivi ndivyo Bwana Yahwe asemavyo.”'
I will put my Spirit in you, and [it will be as though] you will become alive again, and I will enable you to live in your own land again. Then you will know that it is I, Yahweh, who said [that it would happen] and who has caused it to happen. That is what I, Yahweh, declare.’”
15 Kisha neno la Yahwe likanijia, likisema,
Yahweh gave me [another] message. He said,
16 “Sasa wewe, mwanadamu, chukua fimbo moja kwa ajili yako na andika juu yake, 'Kwa ajili Yuda na kwa ajili ya watu wa Israeli, wenzake,' Kisha fimbo nyingine andika juu yake, 'Kwa kuwa Yusufu, tawi la Efraimu, na kwa ajili ya watu wa Israeli, wenzake.
“You human, take a piece of wood and write on it, ‘This represents Judah and all the tribes of Judah.’ Then take another piece of wood and write on it, ‘This represents Israel and all the tribes of Israel.’
17 Walete wote pamoja kwenye fimbo moja, ili wawe kitu kimoja katika mkono wako.
Then join them together to become [as though they were] one piece of wood in your hand.
18 Wakati watu wako watakapokwambia na kusema, 'Je! hutatuambia haya mambo yako yana maana gani?'
When your fellow Israelis ask you, ‘What does (this action/what you just did) mean?’,
19 kisha waambie, 'Bwana Yahwe asema hivi: Tazama! Nalichukua tawi la Yusufu ambalo lipo kwenye mkono wa Efraimu na kabila za Israeli wenzake na kuungana nalo hata kwenye tawi la Yuda, ili kwamba wawe tawi moja, na watakuwa kitu kimoja katika mikono yangu.'
tell them, ‘This is what Yahweh the Lord says: One of the pieces of wood in my hand represents Israel and all the tribes of Israel. I am joining it to the piece of wood that represents Judah, to form one piece of wood in his hand.’
20 Shika kwenye mkono wako na matawi uliyoandika mbele ya macho yao.
Then, [you human], hold up the pieces of wood that you have written on, in order that the people can see them.
21 Waambie, 'Bwana Yahwe asema hivi: Tazama! nakaribia kuwachukua watu wa Israeli kutoka miongoni mwa mataifa walipoenda. Nitawakusanya kutoka nchi zilizozunguka na nitawaleta kwenye nchi yao.
Say to the people, ‘This is what Yahweh the Lord says: I will take you Israeli people out of the countries to which you have been forced to go. I will gather you from all those nations and bring you back to your own land.
22 Nitawafanya kuwa taifa moja katika nchi, juu ya milima ya Israeli, na kutakuwa na mfalme mmoja kama mfalme juu yao wote, na hawatakuwa mataifa mawili tena. Hawatagawanyika kwenye falme mbili tena.
And I will cause you to again be one nation in that land, on the mountains in Israel. And there will be one king to rule over all of you. Never again will you be two nations or divided into two kingdoms.
23 Kisha hawatajitia unajisi tena kwa sanamu zao, mambo yao yachukizao, au dhambi zao nyingine. Kwa kuwa nitawaokoa kutoka matendo yao ya uongo ambayo wamefanya dhambi, na nitawatakasa, hivyo watakuwa watu wangu nami nitakuwa Mungu wao.
No longer will you (defile yourselves/make yourselves unacceptable to me) by [worshiping] idols and disgusting statues [of your gods], because I will enable you to quit your sinful behavior and to stop rejecting me. You will be my people, and I will be your God.
24 Daudi mtumishi wangu atakuwa mfalme juu yao. Hivyo kutakuwa na mchungaji mmoja juu yao wote, na wataishi kulingana na sheria zangu na watazitunza amri zangu na kuzitii.
[Someone who will be like] [MET] [King] David who served [me well] will be the king [of your descendants], and [it will be as though] [MET] he will be their shepherd. They will carefully obey all my laws [DOU].
25 Wataishi katika nchi niliwapatia watumishi wangu Yakobo, ambapo baba zenu walipoishi. Wataishi humo milele-wao, watoto wao, na wajukuu zao, kwa Daudi mtumishi wangu atakuwa mkuu wao milele.
They will live in the land that I gave to Jacob, who also served [me well]; they will live in the land where your ancestors lived. They and their children and their grandchildren will live there forever, and [the one who will be like] [MET] [King] David will be their king forever.
26 Nitaweka agano la amani pamoja nao. Litakuwa agano la milele pamoja nao. Nitawaweka na kuwazidisha na kupaweka mahali patakatifu pangu katikati yao milele.
I will make a peace agreement with them; it will be an agreement that will endure forever. I will again give them that land and cause their population to increase. And I will put my temple among them forever.
27 Maskani yangu yatakuwa pamoja nao; Nitakuwa Mungu wao, na watakuwa watu wangu.
The place where I will live will be among them; I will be their God and they will be my people.
28 Kisha mataifa watajua yakwamba mimi ni Yahwe niliyewatenga Israeli, wakati mahali pangu patakatifu patakapokuwa katikati yao milele.”
Then, when my temple is forever there among them, the people of other nations will know that I, Yahweh, have caused the Israeli people to be set apart [to belong to me].’”

< Ezekieli 37 >