< Ezekieli 37 >
1 Mkono wa Yahwe ulikuwa juu yangu, na akanitoa kwa Roho wa Bwana Yahwe na kuniweka chini katikati ya bonde; lilikuwa limejaa mifupa.
And the hand of the Lord came upon me, and the Lord brought me forth by the Spirit, and set me in the midst of the plain, and it was full of human bones.
2 Kisha akanifanya kupita kati yao kuizunguka pande zote. Tazama! Mingi yao mikubwa ilikuwa katika bonde! Ilikuwa mikavu sana.
And he led me round about them every way: and, behold, [there were] very many on the face of the plain, very dry.
3 Akanambia, “Mwanadamu, Je! Hii mifupa inaweza kuishi kinyume?” Hivyo nikasema, “Bwana Yahwe, wajua wewe pekee.”
And he said to me, Son of man, will these bones live? and I said, O Lord God, you know this.
4 Kisha akanambia, “Tabiri juu ya hii mifupa na iambie, 'Mifupa mikavu. Lisikilizeni neno la Yahwe.
And he said to me, Prophesy upon these bones, and you shall say to them, You dry bones, hear the word of the Lord.
5 Bwana Yahwe asema hivi kwenye hii mifupa: Tazama! nakaribia kuweka pumzi juu yenu, nanyi mtaishi.
Thus says the Lord to these bones; Behold, I [will] bring upon you the breath of life:
6 Nitaweka mishipa juu yenu na kuleta nyama juu yenu. Nitawafunika kwa ngozi na kuweka pumzi ndani yenu hivyo mtaishi. Kisha mtajua kwamba mimi ni Yahwe.”'
and I will lay sinews upon you, and will bring up flesh upon you, and will spread skin upon you, and will put my Spirit into you, and you shall live; and you shall know that I am the Lord.
7 Hivyo nimetoa unabii kama nilivyokuwa nimeamriwa: nimetabiri, tazama, sauti ikaja, iliyokuwa ya mtetememo. Kisha mifupa ikasogeleana pamoja-mfupa juu ya mfupa.
So I prophesied as [the Lord] commanded me: and it came to pass while I was prophesying, that, behold, [there was] a shaking, and the bones approached each one to his joint.
8 Nikatazama na, kumbe, mishipa ilikuwa juu sasa, na nyama ikatoka juu na ngozi ikazifunika. Lakini hapakuwa na pumzi juu yao.
And I looked, and behold, sinews and flesh grew upon them, and skin came upon them above: but there was not breath in them.
9 Kisha Yahwe akanambia, “Itabirie pumzi, tabiri, mwanadamu, na iambie pumzi, 'Bwana Yahwe asema hivi: Pumzi, hutoka pepo nne, na pumzi juu ya hawa walioawa, hivyo wanaweza kuishi.”'
And he said to me, Prophesy to the wind, prophesy, son of man, and say to the wind, Thus says the Lord; Come from the four winds, and breathe upon these dead [men], and let them live.
10 Hivyo nimetabiri kama nilivyokuwa nimeamriwa; pumzi ikawajilia na wakaishi. Kisha wakasimama kwa miguu yao, jeshi moja kubwa sana.
So I prophesied as he commanded me, and the breath entered into them, and they lived, and stood upon their feet, a very great congregation.
11 Kisha Yahwe akanambia, “Mwanadamu, mifupa hii yote ni ya nyumba ya Israeli. Tazama! Wanasema, 'Mifupa yetu imekauka, na tumaini letu limepotea. Tumekatwa.'
And the Lord spoke to me, saying, Son of man, these bones are the whole house of Israel: and they say, Our bones are become dry, our hope has perished, we are quite spent.
12 Kwa hiyo tabiri na waambie, 'Bwana Yahwe asema hivi: Tazama! Nitayafunua makabiri yenu na kuwapandisha kutoka kwayo, watu wangu. Nitakurudisha hata katika nchi ya Israeli.
Therefore prophesy and say, Thus says the Lord; Behold, I [will] open your tombs, and will bring you up out of your tombs, and will bring you into the land of Israel.
13 Kisha mtajua kwamba mimi ni Yahwe, nitakapo yafunua makaburi yenu na kuwatoa kutoka kwao, watu wangu.
And you shall know that I am the Lord, when I have opened your graves, that I may bring up my people from [their] graves.
14 Nitaweka Roho wangu ndani yenu hivyo mtaishi, na nitawafanya kupumzika katika nchi yenu mtakapojua yakwamba mimi ni Yahwe. Nasema na nitayafanya hayo-hivi ndivyo Bwana Yahwe asemavyo.”'
And I will put my Spirit within you, and you shall live, and I will place you upon your own land: and you shall know that I [am] the Lord; I have spoken, and will do [it], says the Lord.
15 Kisha neno la Yahwe likanijia, likisema,
And the word of the Lord came to me, saying,
16 “Sasa wewe, mwanadamu, chukua fimbo moja kwa ajili yako na andika juu yake, 'Kwa ajili Yuda na kwa ajili ya watu wa Israeli, wenzake,' Kisha fimbo nyingine andika juu yake, 'Kwa kuwa Yusufu, tawi la Efraimu, na kwa ajili ya watu wa Israeli, wenzake.
Son of man, take for yourself a rod, and write upon it, Juda, and the children of Israel his adherents; and you shall take for yourself another rod, and you shall inscribe it for Joseph, the rod of Ephraim, and all the children of Israel that belong to him.
17 Walete wote pamoja kwenye fimbo moja, ili wawe kitu kimoja katika mkono wako.
And you shall joint them together for yourself, so as that they should bind themselves into one stick; and they shall be in your hand.
18 Wakati watu wako watakapokwambia na kusema, 'Je! hutatuambia haya mambo yako yana maana gani?'
And it shall come to pass, when the children of your people shall say to you, Will you not tell us what you meanest by these things?
19 kisha waambie, 'Bwana Yahwe asema hivi: Tazama! Nalichukua tawi la Yusufu ambalo lipo kwenye mkono wa Efraimu na kabila za Israeli wenzake na kuungana nalo hata kwenye tawi la Yuda, ili kwamba wawe tawi moja, na watakuwa kitu kimoja katika mikono yangu.'
Then shall you say to them, Thus says the Lord; behold, I will take the tribe of Joseph, which is in the hand of Ephraim, and the tribes of Israel that belong to him, and I will add them to the tribe of Juda, and they shall become one rod in the hand of Juda.
20 Shika kwenye mkono wako na matawi uliyoandika mbele ya macho yao.
And the rods on which you did write shall be in your hand in their presence.
21 Waambie, 'Bwana Yahwe asema hivi: Tazama! nakaribia kuwachukua watu wa Israeli kutoka miongoni mwa mataifa walipoenda. Nitawakusanya kutoka nchi zilizozunguka na nitawaleta kwenye nchi yao.
And you shall say to them, Thus says the Lord God; Behold, I [will] take the whole house of Israel out of the midst of the nations, among whom they have gone, and I will gather them from all that are round about them, and I will bring them into the land of Israel.
22 Nitawafanya kuwa taifa moja katika nchi, juu ya milima ya Israeli, na kutakuwa na mfalme mmoja kama mfalme juu yao wote, na hawatakuwa mataifa mawili tena. Hawatagawanyika kwenye falme mbili tena.
And I will make them a nation in my land, even on the mountains of Israel; and they shall have one prince: and they shall be no more two nations, neither shall they be divided any more at all into two kingdoms:
23 Kisha hawatajitia unajisi tena kwa sanamu zao, mambo yao yachukizao, au dhambi zao nyingine. Kwa kuwa nitawaokoa kutoka matendo yao ya uongo ambayo wamefanya dhambi, na nitawatakasa, hivyo watakuwa watu wangu nami nitakuwa Mungu wao.
that they may no more defile themselves with their idols; and I will deliver them from all their transgressions whereby they have sinned, and will cleanse them; and they shall be to me a people, and I the Lord will be to them a God.
24 Daudi mtumishi wangu atakuwa mfalme juu yao. Hivyo kutakuwa na mchungaji mmoja juu yao wote, na wataishi kulingana na sheria zangu na watazitunza amri zangu na kuzitii.
And my servant David [shall be] a prince in the midst of them: there shall be one shepherd of [them] all; for they shall walk in mine ordinances, and keep my judgments, and do them.
25 Wataishi katika nchi niliwapatia watumishi wangu Yakobo, ambapo baba zenu walipoishi. Wataishi humo milele-wao, watoto wao, na wajukuu zao, kwa Daudi mtumishi wangu atakuwa mkuu wao milele.
And they shall dwell in their land, which I have given to my servant Jacob, where their fathers lived; and they shall dwell upon it: and David my servant [shall be their] prince forever.
26 Nitaweka agano la amani pamoja nao. Litakuwa agano la milele pamoja nao. Nitawaweka na kuwazidisha na kupaweka mahali patakatifu pangu katikati yao milele.
And I will make with them a covenant of peace; it shall be an everlasting covenant with them; and I will establish my sanctuary in the midst of them for ever.
27 Maskani yangu yatakuwa pamoja nao; Nitakuwa Mungu wao, na watakuwa watu wangu.
And my tabernacle shall be among them; and I will be to them a God, and they shall be my people.
28 Kisha mataifa watajua yakwamba mimi ni Yahwe niliyewatenga Israeli, wakati mahali pangu patakatifu patakapokuwa katikati yao milele.”
And the nations shall know that I am the Lord that sanctifies them, when my sanctuary is in the midst of them for ever.