< Ezekieli 37 >

1 Mkono wa Yahwe ulikuwa juu yangu, na akanitoa kwa Roho wa Bwana Yahwe na kuniweka chini katikati ya bonde; lilikuwa limejaa mifupa.
The hand of the Lord was set upon me, and he led me away in the Spirit of the Lord, and he released me in the midst of a plain which was full of bones.
2 Kisha akanifanya kupita kati yao kuizunguka pande zote. Tazama! Mingi yao mikubwa ilikuwa katika bonde! Ilikuwa mikavu sana.
And he led me around, through them, on every side. Now they were very many upon the face of the plain, and they were exceedingly dry.
3 Akanambia, “Mwanadamu, Je! Hii mifupa inaweza kuishi kinyume?” Hivyo nikasema, “Bwana Yahwe, wajua wewe pekee.”
And he said to me, “Son of man, do you think that these bones will live?” And I said, “O Lord God, you know.”
4 Kisha akanambia, “Tabiri juu ya hii mifupa na iambie, 'Mifupa mikavu. Lisikilizeni neno la Yahwe.
And he said to me, “Prophesy about these bones. And you shall say to them: Dry bones, listen to the word of the Lord!
5 Bwana Yahwe asema hivi kwenye hii mifupa: Tazama! nakaribia kuweka pumzi juu yenu, nanyi mtaishi.
Thus says the Lord God to these bones: Behold, I will send spirit into you, and you shall live.
6 Nitaweka mishipa juu yenu na kuleta nyama juu yenu. Nitawafunika kwa ngozi na kuweka pumzi ndani yenu hivyo mtaishi. Kisha mtajua kwamba mimi ni Yahwe.”'
And I will set sinews upon you, and I will cause flesh to grow over you, and I will extend skin over you. And I will give you spirit, and you shall live. And you shall know that I am the Lord.”
7 Hivyo nimetoa unabii kama nilivyokuwa nimeamriwa: nimetabiri, tazama, sauti ikaja, iliyokuwa ya mtetememo. Kisha mifupa ikasogeleana pamoja-mfupa juu ya mfupa.
And I prophesied, just as he had instructed me. But a noise occurred, as I was prophesying, and behold: a commotion. And the bones joined together, each one at its joint.
8 Nikatazama na, kumbe, mishipa ilikuwa juu sasa, na nyama ikatoka juu na ngozi ikazifunika. Lakini hapakuwa na pumzi juu yao.
And I saw, and behold: sinews and flesh rose up over them; and skin was extended over them. But they had no spirit within them.
9 Kisha Yahwe akanambia, “Itabirie pumzi, tabiri, mwanadamu, na iambie pumzi, 'Bwana Yahwe asema hivi: Pumzi, hutoka pepo nne, na pumzi juu ya hawa walioawa, hivyo wanaweza kuishi.”'
And he said to me: “Prophesy to the spirit! Prophesy, O son of man, and you shall say to the spirit: Thus says the Lord God: Approach, O spirit, from the four winds, and blow across these ones who were slain, and revive them.”
10 Hivyo nimetabiri kama nilivyokuwa nimeamriwa; pumzi ikawajilia na wakaishi. Kisha wakasimama kwa miguu yao, jeshi moja kubwa sana.
And I prophesied, just as he had instructed me. And spirit entered into them, and they lived. And they stood upon their feet, an exceedingly great army.
11 Kisha Yahwe akanambia, “Mwanadamu, mifupa hii yote ni ya nyumba ya Israeli. Tazama! Wanasema, 'Mifupa yetu imekauka, na tumaini letu limepotea. Tumekatwa.'
And he said to me: “Son of man: All these bones are the house of Israel. They say: ‘Our bones are dried out, and our hope has perished, and we have been cut off.’
12 Kwa hiyo tabiri na waambie, 'Bwana Yahwe asema hivi: Tazama! Nitayafunua makabiri yenu na kuwapandisha kutoka kwayo, watu wangu. Nitakurudisha hata katika nchi ya Israeli.
Because of this, prophesy, and you shall say to them: Thus says the Lord God: Behold, I will open your tombs, and I will lead you away from your sepulchers, O my people. And I will lead you into the land of Israel.
13 Kisha mtajua kwamba mimi ni Yahwe, nitakapo yafunua makaburi yenu na kuwatoa kutoka kwao, watu wangu.
And you shall know that I am the Lord, when I will have opened your sepulchers, and when I will have led you away from your tombs, O my people.
14 Nitaweka Roho wangu ndani yenu hivyo mtaishi, na nitawafanya kupumzika katika nchi yenu mtakapojua yakwamba mimi ni Yahwe. Nasema na nitayafanya hayo-hivi ndivyo Bwana Yahwe asemavyo.”'
And I will place my Spirit within you, and you shall live. And I will cause you to rest upon your own soil. And you shall know that I, the Lord, have spoken and acted, says the Lord God.”
15 Kisha neno la Yahwe likanijia, likisema,
And the word of the Lord came to me, saying:
16 “Sasa wewe, mwanadamu, chukua fimbo moja kwa ajili yako na andika juu yake, 'Kwa ajili Yuda na kwa ajili ya watu wa Israeli, wenzake,' Kisha fimbo nyingine andika juu yake, 'Kwa kuwa Yusufu, tawi la Efraimu, na kwa ajili ya watu wa Israeli, wenzake.
“And as for you, son of man, take up a piece of wood for yourself, and write upon it: ‘For Judah, and for the sons of Israel, his companions.’ And take up another piece of wood, and write upon it: ‘For Joseph, the wood of Ephraim, and for the entire house of Israel, and for his companions.’
17 Walete wote pamoja kwenye fimbo moja, ili wawe kitu kimoja katika mkono wako.
And join these, one to the other, for yourself, as one piece of wood. And they will be united in your hand.
18 Wakati watu wako watakapokwambia na kusema, 'Je! hutatuambia haya mambo yako yana maana gani?'
Then, when the sons of your people will speak to you, saying: ‘Will you not tell us what you intend by this?’
19 kisha waambie, 'Bwana Yahwe asema hivi: Tazama! Nalichukua tawi la Yusufu ambalo lipo kwenye mkono wa Efraimu na kabila za Israeli wenzake na kuungana nalo hata kwenye tawi la Yuda, ili kwamba wawe tawi moja, na watakuwa kitu kimoja katika mikono yangu.'
you shall say to them: Thus says the Lord God: Behold, I will take up the wood of Joseph, which is in the hand of Ephraim, and the tribes of Israel, which are joined to him, and I will put them together with the wood of Judah, and I will make them one piece of wood. And they will be one in his hand.
20 Shika kwenye mkono wako na matawi uliyoandika mbele ya macho yao.
Then the pieces of wood, on which you have written, will be in your hand, before their eyes.
21 Waambie, 'Bwana Yahwe asema hivi: Tazama! nakaribia kuwachukua watu wa Israeli kutoka miongoni mwa mataifa walipoenda. Nitawakusanya kutoka nchi zilizozunguka na nitawaleta kwenye nchi yao.
And you shall say to them: Thus says the Lord God: Behold, I will take up the sons of Israel, from the midst of the nations to which they have gone, and I will gather them together on every side, and I will lead them onto their own soil.
22 Nitawafanya kuwa taifa moja katika nchi, juu ya milima ya Israeli, na kutakuwa na mfalme mmoja kama mfalme juu yao wote, na hawatakuwa mataifa mawili tena. Hawatagawanyika kwenye falme mbili tena.
And I will make them one nation in the land, on the mountains of Israel, and one king will be ruler over all. And they will no longer be two nations, nor will they be divided any more into two kingdoms.
23 Kisha hawatajitia unajisi tena kwa sanamu zao, mambo yao yachukizao, au dhambi zao nyingine. Kwa kuwa nitawaokoa kutoka matendo yao ya uongo ambayo wamefanya dhambi, na nitawatakasa, hivyo watakuwa watu wangu nami nitakuwa Mungu wao.
And they will no longer be defiled by their idols, and by their abominations, and by all their iniquities. And I will save them, out of all the settlements in which they have sinned, and I will cleanse them. And they will be my people, and I will be their God.
24 Daudi mtumishi wangu atakuwa mfalme juu yao. Hivyo kutakuwa na mchungaji mmoja juu yao wote, na wataishi kulingana na sheria zangu na watazitunza amri zangu na kuzitii.
And my servant David shall be the king over them, and they shall have one shepherd. They shall walk in my judgments, and they shall keep my commandments, and they shall do them.
25 Wataishi katika nchi niliwapatia watumishi wangu Yakobo, ambapo baba zenu walipoishi. Wataishi humo milele-wao, watoto wao, na wajukuu zao, kwa Daudi mtumishi wangu atakuwa mkuu wao milele.
And they shall live upon the land that I gave to my servant Jacob, in which your fathers lived. And they shall live upon it, they and their sons, and the sons of their sons, even for all time. And David, my servant, shall be their leader, in perpetuity.
26 Nitaweka agano la amani pamoja nao. Litakuwa agano la milele pamoja nao. Nitawaweka na kuwazidisha na kupaweka mahali patakatifu pangu katikati yao milele.
And I will strike a covenant of peace with them. This will be an everlasting covenant for them. And I will establish them, and multiply them. And I will set my sanctuary in their midst, unceasingly.
27 Maskani yangu yatakuwa pamoja nao; Nitakuwa Mungu wao, na watakuwa watu wangu.
And my tabernacle shall be among them. And I will be their God, and they will be my people.
28 Kisha mataifa watajua yakwamba mimi ni Yahwe niliyewatenga Israeli, wakati mahali pangu patakatifu patakapokuwa katikati yao milele.”
And the Gentiles shall know that I am the Lord, the Sanctifier of Israel, when my sanctuary will be in their midst, forever.”

< Ezekieli 37 >