< Ezekieli 35 >
1 Kisha neno la Yahwe likanijia, kusema,
Moveover the worde of the Lord came vnto me, saying,
2 “Mwanadamu, weka uso wako juu ya Mlima Seiri na tabiri dhidi yake.
Sonne of man, Set thy face against mount Seir, and prophesie against it,
3 Uiambie, 'Bwana Yahwe asema hivi: Tazama! ni juu yako, Mlima Seiri, nitakupiga kwa mkono wangu na kukufanya ukiwa na tishio.
And say vnto it, Thus sayth the Lord God, Behold, O mount Seir, I come against thee, and I wil stretch out mine hand against thee, and I will make thee desolate and waste.
4 Nitaiharibu miji yenu, na wewe mwenyewe utakuwa ukiwa; kisha utajua kuwa mimi ni Yahwe.
I wil lay thy cities waste, and thou shalt be desolate, and thou shalt knowe that I am the Lord.
5 Kwa sababu umekuwa adui kwa watu wangu Israeli siku zote, na kwa sababu umewatoa kwenye mikono ya upanga wakati wa mateso yao, wakati adhabu yao itakapokuwa katika ukubwa wake.
Because thou hast had a perpetuall hatred and hast put the children of Israel to flight by the force of the sword in the time of their calamitie, when their iniquitie had an ende,
6 Kwa hiyo, kama niishivyo-hivi ndivyo Bwana Yahwe asemavyo-nitaandaa kwa ajili ya damu, na damu na kukufutilia! Kwa kuwa hukuchukia damu, damu itakufuatilia.
Therefore as I liue, sayth the Lord God, I wil prepare thee vnto blood, and blood shall pursue thee: except thou hate blood, euen blood shall pursue thee.
7 Nitaufanya Mlima Seiri mkamilifu na ukiwa wakati nitakapoukatilia mbali kutoka huo yeyote apitaye na arudiye tena.
Thus will I make mount Seir desolate and waste, and cut off from it him that passeth out and him that returneth.
8 Kisha nitaijaza milima kwa watu wao waliokufa. Milima yako na mabonde na mifereji-wale walioawa kwa upanga wataanguka kati yao.
And I will fill his mountaines with his slayne men: in thine hilles, and in thy valleys and in all thy riuers shall they fall, that are slayne with the sworde.
9 Nitakufanya mkiwa daima. Miji yako haitakaliwa na watu, lakini mtajua kwamba mimi ni Yahwe.
I wil make thee perpetual desolations, and thy cities shall not returne, and ye shall knowe that I am the Lord.
10 Umesema, “Haya mataifa mawili na hizi nchi mbili zitakuwa zangu, na tutazimiliki,” hata wakati Yahwe alipokuwa pamoja nao.
Because thou hast said, These two nations, and these two countreys shalbe mine, and we wil possesse them (seeing the Lord was there)
11 Kwa hiyo, kama niishivyo-hivi ndivyo Bwana Yahwe asemavyo-hivyo nitafanya kulingana na hasira yako na kulingana na wivu wako ambao uliousikia katika chuki yako ya Israeli, na nitajidhihirisha kwao nitakapokuhukumu.
Therefore as I liue, sayth the Lord God, I wil euen do according to thy wrath, and according to thine indignation which thou hast vsed in thine hatred against them: and I wil make my selfe knowen among them whe I haue iudged thee.
12 Hivyo utajua kwamba mimi ni Yahwe. Nimeyasikia matukano yako yote uliyasema dhidi ya milima ya Israeli, uliposema, “Wameharibiwa; wametolewa kwetu tuwale.
And thou shalt know, that I the Lord haue heard all thy blasphemies which thou hast spoken against the mountaines of Israel, saying, They lye waste, they are giuen vs to be deuoured.
13 “Nanyi mmejitukuza juu yangu kwa kile mlichokisema, na mmeongeza maneno juu yangu; na kuyasikia yote.
Thus with your mouthes ye haue boasted against me, and haue multiplied your words against me: I haue heard them.
14 Bwana Yahwe asema hivi: Nitakufanya ukiwa, wakati dunia nzima itakapofurahi.
Thus sayth the Lord God, So shall all the world reioyce when I shall make thee desolate.
15 Kama vile unavyofurahi juu ya urithi wa watu wa Israeli kwa sababu ukiwa ya wake, ndivyo nitakavyokutenda wewe. Utakuwa ukiwa, Mlima Seiri, na Edomu yote! Kisha watajua kwamba mimi ni Yahwe.”'
As thou diddest reioyce at the inheritance of the house of Israel, because it was desolate, so will I doe vnto thee: thou shalt be desolate, O mount Seir, and all Idumea wholly, and they shall know, that I am the Lord.