< Ezekieli 35 >
1 Kisha neno la Yahwe likanijia, kusema,
Then the word of the Lord came to me, saying,
2 “Mwanadamu, weka uso wako juu ya Mlima Seiri na tabiri dhidi yake.
Son of man, let your face be turned to Mount Seir, and be a prophet against it,
3 Uiambie, 'Bwana Yahwe asema hivi: Tazama! ni juu yako, Mlima Seiri, nitakupiga kwa mkono wangu na kukufanya ukiwa na tishio.
And say to it, This is what the Lord has said: See, I am against you, O Mount Seir, and my hand will be stretched out against you, and I will make you a waste and a cause for wonder.
4 Nitaiharibu miji yenu, na wewe mwenyewe utakuwa ukiwa; kisha utajua kuwa mimi ni Yahwe.
I will make your towns unpeopled and you will be a waste; and you will be certain that I am the Lord.
5 Kwa sababu umekuwa adui kwa watu wangu Israeli siku zote, na kwa sababu umewatoa kwenye mikono ya upanga wakati wa mateso yao, wakati adhabu yao itakapokuwa katika ukubwa wake.
Because yours has been a hate without end, and you have given up the children of Israel to the power of the sword in the time of their trouble, in the time of the punishment of the end:
6 Kwa hiyo, kama niishivyo-hivi ndivyo Bwana Yahwe asemavyo-nitaandaa kwa ajili ya damu, na damu na kukufutilia! Kwa kuwa hukuchukia damu, damu itakufuatilia.
For this cause, by my life, says the Lord, because you have been sinning through blood, blood will come after you.
7 Nitaufanya Mlima Seiri mkamilifu na ukiwa wakati nitakapoukatilia mbali kutoka huo yeyote apitaye na arudiye tena.
And I will make Mount Seir a cause for wonder and a waste, cutting off from it all comings and goings.
8 Kisha nitaijaza milima kwa watu wao waliokufa. Milima yako na mabonde na mifereji-wale walioawa kwa upanga wataanguka kati yao.
I will make his mountains full of those who have been put to death; in your valleys and in all your water-streams men will be falling by the sword.
9 Nitakufanya mkiwa daima. Miji yako haitakaliwa na watu, lakini mtajua kwamba mimi ni Yahwe.
I will make you waste for ever, and your towns will be unpeopled: and you will be certain that I am the Lord.
10 Umesema, “Haya mataifa mawili na hizi nchi mbili zitakuwa zangu, na tutazimiliki,” hata wakati Yahwe alipokuwa pamoja nao.
Because you have said, The two nations and the two countries are to be mine, and we will take them for our heritage; though the Lord was there:
11 Kwa hiyo, kama niishivyo-hivi ndivyo Bwana Yahwe asemavyo-hivyo nitafanya kulingana na hasira yako na kulingana na wivu wako ambao uliousikia katika chuki yako ya Israeli, na nitajidhihirisha kwao nitakapokuhukumu.
For this cause, by my life, says the Lord, I will do to you as you have done in your wrath and in your envy, which you have made clear in your hate for them; and I will make clear to you who I am when you are judged by me.
12 Hivyo utajua kwamba mimi ni Yahwe. Nimeyasikia matukano yako yote uliyasema dhidi ya milima ya Israeli, uliposema, “Wameharibiwa; wametolewa kwetu tuwale.
And you will see that I the Lord have had knowledge of all the bitter things which you have said against the mountains of Israel, saying, They have been made waste, they are given to us to take for our heritage.
13 “Nanyi mmejitukuza juu yangu kwa kile mlichokisema, na mmeongeza maneno juu yangu; na kuyasikia yote.
And you have made yourselves great against me with your mouths, increasing your words against me; and it has come to my ears.
14 Bwana Yahwe asema hivi: Nitakufanya ukiwa, wakati dunia nzima itakapofurahi.
This is what the Lord has said: Because you were glad over my land when it was a waste, so will I do to you:
15 Kama vile unavyofurahi juu ya urithi wa watu wa Israeli kwa sababu ukiwa ya wake, ndivyo nitakavyokutenda wewe. Utakuwa ukiwa, Mlima Seiri, na Edomu yote! Kisha watajua kwamba mimi ni Yahwe.”'
You will become a waste, O Mount Seir, and all Edom, even all of it: and you will be certain that I am the Lord.