< Ezekieli 32 >

1 Kisha ikawa katika mwezi wa kumi na mbili wa mwaka wa kumi na mbili, siku ya kwanza ya mwezi, lile neno la Yahwe likanijia, kusema,
And it came to pass in the twelfth year, in the twelfth month, on the first day of the month, that the word of Jehovah came to me, saying:
2 “Mwanadamu, inua maombolezo kuhusu Farao mfalme wa Misri; mwambie, 'Wewe ni kama simba mdogo juu ya mataifa, lakini kama jitu la kutisha, unatoka kwenye maji, unayachafua maji kwa miguu yako na kuyachafua maji yao.
Son of man, take up a lamentation over Pharaoh, the king of Egypt, and say to him: —Thou art like a young lion among the nations; Thou art like a dragon in the seas; And thou camest forth into thy rivers, And troubledst the waters with thy feet, And didst disturb their rivers.
3 Bwana Yahwe asema hivi: Basi nitautandaza wavu wangu juu yako katika kusanyiko la watu wengi, na watawainua juu katika wavu wangu.
Thus saith the Lord Jehovah: I will therefore spread my net over thee, Amidst an assembly of many nations; And they shall draw thee up in my net.
4 Nitakuacha katika nchi. Nitakutupa kwenye shamba na kufanya ndege wote wa angani watue juu yako; njaa ya wanyama wote waishio juu ya nchi watashibishwa na wewe.
And I will throw thee upon the land, I will cast thee forth upon the open field, And I will cause all the birds of heaven to remain upon thee. And I will fill the beasts of the whole earth with thee;
5 Kwa kuwa nitaiweka nyama yako juu ya milima, na nitayajaza mabonde kwa funza wako waliokufa.
And I will lay thy flesh upon the mountains, And fill the valleys with thy heaps.
6 Kisha nitamwaga damu yako juu ya milima, na vitanda vya kijito vitajazwa kwa damu yako.
And I will water the land in which thou swimmest with thy blood, even to the mountains, And the streams shall be full of thee.
7 Kisha wakati nitakapokuzimisha, nitazifunika mbingu na kuzitia giza nyota zake; nitalifunika jua kwa mawingu, na mwezi hautatoa nuru yake usiku.
And I will cover the heavens, when I quench thee, And make the stars thereof dark; I will cover the sun with a cloud, And the moon shall not give her light.
8 Mianga ya mbinguni nitaiweka giza juu yako, na nitaweka giza juu ya nchi-hivi ndivyo asemavyo Bwana Yahwe.
All the bright lights of heaven will I make dark over thee, And bring darkness upon thy land, Saith the Lord Jehovah.
9 Hivyo nitaitisha mioyo ya watu wengi katika nchi ambao huwajui, wakati nitakapoleta kuhusu uvunjifu miongoni mwa mataifa, miongoni mwa nchi ambazo hukuzijua.
And I will grieve the hearts of many nations, When I bring thy destruction among the nations, In lands which thou knowest not.
10 Nitawashangaza watu wengi kuhusiana na wewe; wafalme wao watatetemeka kwa hofu kuhusiana na wewe nitakapoutikisa upanga wangu mbele yao. Kila wakati kila mmoja atatetemeka kwa sababu yako, katika siku ya kuanguka kwako.
Yea, I will make many people amazed at thee, And their kings shall shudder on account of thee, When I brandish my sword before them; And they shall tremble every moment, every one for his life, in the day of thy fall.
11 Kwa kuwa Bwana Yahwe asema hivi: Upanga wa mfalme wa Babeli utakuja juu yako.
For thus saith the Lord Jehovah: The sword of the king of Babylon shall come upon thee;
12 Nitawafanya watu wako kuanguka kwa panga za mashujaa-kila shujaa ni tishio la mataifa. Hawa mashujaa watateketeza kiburi cha Misri na kuangamiza watu wake wote.
By the swords of the mighty will I cause thy multitude to fall, All of them the terrible of the nations. And they shall bring to nothing the pride of Egypt, And all her multitude shall be destroyed.
13 Kwa kuwa nitaiharibu mifugo yote kutoka karibu na maji mengi; na mguu wa mtu hautayatibua tena, wala kwato za wanyama hazitayatibua.
I will also destroy all her beasts From beside the great waters; Neither shall the foot of man trouble them any more, Nor shall the hoofs of beasts trouble them.
14 Kisha nitayafanya maji yao kuwa matulivu na kufanya mito yao kukimbia kama mafuta-hivi ndivyo asemavyo Bwana Yahwe.
Then will I make their waters clear, And cause their rivers to run like oil, Saith the Lord Jehovah,
15 Wakati nitakapoifanya nchi ya Misri sehemu iliyojitenga, wakati nchi iliyopungukiwa na vitu viijazavyo, wakati nitakapo washambulia wakaao ndani yake, watajua yakwamba mimi ni Yahwe.
When I shall make the land of Egypt desolate, And the country shall be destitute of all that was therein, When I shall smite all that dwell therein, That they may know that I am Jehovah.
16 Kutakuwa na maombolezo; binti za mataifa wataomboleza juu yake; wataomboleza juu ya Misri, juu ya watu wake wote wataomboleza-hivi ndivyo Bwana Yahwe asemavyo.”'
This is the lamentation which they shall utter; the daughters of the nations shall utter it. For Egypt and for all her multitude shall they utter it, saith the Lord Jehovah.
17 Kisha ikawa katika mwaka wa kumi na mbili, siku ya kumi na tano ya mwezi, lile neno la Yahwe likanijia, kusema,
It came to pass also in the twelfth year, [[in the twelfth month, ]] on the fifteenth day of the month, that the word of Jehovah came to me, saying:
18 “Mwanadamu, omboleza kwa ajili watu wa misri na walete chini-yeye na binti za mataifa mashuhuri-hata chini ya dunia pamoja na wale walioshuka chini kwenye shimo.
Son of man, wail for the multitude of Egypt, and cast her down, even her and the daughters of the famous nations, to the lower parts of the earth, to them that have gone down to the pit.
19 'Je! wewe ni mzuri zaidi kuliko mtu mwingine yeyote? Nenda chini na lala chini pamoja na wasiotahiriwa.'
Art thou more beautiful than another? Come down and be laid with the uncircumcised!
20 Wataanguka miongoni mwao waliokuwa wameuawa kwa upanga. Upanga ulikuwa umewekwa! Alikuwa amepatiwa upanga; watamkamata na watu wake.
They shall fall in the midst of them that are slain by the sword. The sword is given; drag her away and all her multitudes!
21 Hodari wa wapiganaji katika Sheoli atasema kuhusu Misri na rafiki zake, 'Wameshuka chini hapa! Watalala pamoja na wasiotahiriwa, pamoja na wale waliokuwa wameuawa kwa upanga.' (Sheol h7585)
The mightiest heroes from the midst of the pit shall speak to him and his helpers; For they are gone down, they lie uncircumcised, slain by the sword. (Sheol h7585)
22 Ashuru yupo huko pamoja na kusanyiko lake. Makaburi yake yamemzunguka; wote waliuawa kwa upanga.
There is Assyria and all her company; Her graves are round about her; All of them are slain, fallen by the sword;
23 Wale ambao makaburi yao yamewekwa katika maficho ya mashimo yaliyo huko, pamoja na kusanyiko lake. Makaburi yake yakiwazunguka wote waliokuwa wameuawa, walioanguka kwa upanga, wale walioleta hofu juu ya nchi ya walio hai.
Her grave is made in the depths of the pit, And her company is round about her grave, All of them slain, fallen by the sword, They who caused terror in the land of the living.
24 Elamu yupo huko pamoja na watu wake wote. Makaburi yake yamemzunguka; wote walikuwa wameuawa. Wale walioawa kwa upanga, walioshuka chini wasiotahiriwa hata sehemu ya chini kabisa ya dunia, waliowatia hofu juu ya nchi ya walio hai na wale waliobeba aibu yao wenyewe, pamoja na wale washukao chini kwenye shimo.
There is Elam and all her company round about her grave, All of them slain, fallen by the sword; They are gone down uncircumcised to the lower parts of the earth, Who caused terror in the land of the living; They bear their shame with them that have gone down to the pit.
25 Wamemuwekea kitanda kwa ajili ya Elamu na watu wake wote kati ya wachinjaji; kaburi lake limemzunguka. Wote hawajatahiriwa, kukatwa vipande kwa upanga, kwa sababu waliwaleta mashujaa wao juu ya nchi ya walio hai. Hivyo wamechukua aibu yao wenyewe, pamoja na wale washukao kwenye shimo miongoni mwa wote waliouawa, wale washukao kwenda shimoni. Elamu yu miongoni mwa wale waliokuwa wameuawa.
Among the slain have they set her a bed with all her multitude; Her graves are round about her, All of them slain, uncircumcised, by the sword. Though they caused terror in the land of the living, Yet they bear their shame with them that have gone down to the pit; They are laid in the midst of the slain.
26 Mesheki, Tubali, na watu wake wote wako huko! Makaburi yao yamewazunguka. Wote hawajatahiriwa, wameuawa kwa upanga, kwa sababu walileta utiisho wao juu ya nchi ya walio hai.
There is Meshech, Tubal, and all their multitude; Their graves are around them; All of them slain, uncircumcised, by the sword, Though they caused terror in the land of the living.
27 Wasilale pamoja mashujaa walioanguka wa wasiotahiriwa walioshuka chini kwa Sheoli pamoja na silaha zao zote za vita, na pamoja na panga zao zote walizoziweka chini ya vichwa vyao na maovu yao juu ya mifupa yao. Kwa kuwa walikuwa tishio kwa mashujaa katika nchi ya walio hai. (Sheol h7585)
Shall they not lie with the mighty of the uncircumcised that are fallen, Who have gone down to the pit with their weapons of war, Having their swords laid under their heads, And their iniquity resting upon their bones, Though they were the terror of the mighty in the land of the living? (Sheol h7585)
28 Basi wewe, Misri, utavunjika kati yao wasiotahiriwa! Utalala karibu nao waliokuwa wamekatwa vipande vipande kwa upanga.
And thou also shalt be broken in the midst of the uncircumcised, And shalt lie down with them that are slain by the sword.
29 Edomu yuko huko na wafalme na viongozi wake wote. Walikuwa wamehifadhiwa katika uwezo wao pamoja na wale walioawa kwa upanga. Pamoja na wasiotahiriwa wamelala, pamoja na wale walioshuka kwenye shimo.
There is Edom, her kings and all her princes, Who in their might are laid with them that are slain by the sword; They lie down with the uncircumcised, With them that have gone down to the pit.
30 Wakuu wa kaskazini wako huko-wote na Wasidoni wote walioshuka chini pamoja na hao waliokuwa wamekatwa vipande vipande. Walikuwa na nguvu na kuwafanya wengine kuogopa, lakini sasa wako huko kwa aibu, wasiotahiriwa pamoja na wale waliokatwa vipande vipande kwa upanga. Wamebeba aibu yao wenyewe, pamoja nao waendao kwenye shimo.
There are the princes of the North, All of them, and all the Sidonians, Who have gone down to the slain; In the midst of the terror of their might they are put to shame; They lie down uncircumcised with them that are slain by the sword, And bear their shame with them that have gone down to the pit.
31 Farao ataona na kupata faraja kuhusu kundi lake waliokatwa vipande vipande kwa upanga -Farao na jeshi lake lote-hivi ndivyo Bwana Yahwe asemavyo.
Pharaoh shall see them, And shall comfort himself over all his multitude; Even Pharaoh and all his army are slain by the sword, Saith the Lord Jehovah.
32 Natamuweka kama utiisho wangu katika nchi ya walio hai, lakini atakuwa amelazwa chini katikati yao wasiotahiriwa, miongoni mwa wale walio katwa vipande kwa upanga, Farao na makundi yake yote-hivi ndivyo Bwana Yahwe asemavyo.
Though I suffered him to spread terror in the land of the living, Yet is he laid in the midst of the uncircumcised, With them that are slain by the sword, Even Pharaoh and all his multitude, Saith the Lord Jehovah.

< Ezekieli 32 >