< Ezekieli 32 >

1 Kisha ikawa katika mwezi wa kumi na mbili wa mwaka wa kumi na mbili, siku ya kwanza ya mwezi, lile neno la Yahwe likanijia, kusema,
And it came to pass in the twelfth year, in the twelfth month, on the first day of the month, that the word of the Lord came unto me, saying,
2 “Mwanadamu, inua maombolezo kuhusu Farao mfalme wa Misri; mwambie, 'Wewe ni kama simba mdogo juu ya mataifa, lakini kama jitu la kutisha, unatoka kwenye maji, unayachafua maji kwa miguu yako na kuyachafua maji yao.
Son of man, take up a lamentation for Pharaoh the king of Egypt, and say unto him, Thou didst deem thyself like a young lion among the nations: while thou art as a crocodile in the seas; and thou issuedst forth with thy rivers, and madest turbid the waters with thy feet, and didst stir up their rivers.
3 Bwana Yahwe asema hivi: Basi nitautandaza wavu wangu juu yako katika kusanyiko la watu wengi, na watawainua juu katika wavu wangu.
Thus hath said the Lord Eternal, I will therefore spread out my net over thee through the assemblage of many people, and they shall draw thee up in my net.
4 Nitakuacha katika nchi. Nitakutupa kwenye shamba na kufanya ndege wote wa angani watue juu yako; njaa ya wanyama wote waishio juu ya nchi watashibishwa na wewe.
Then will I cast thee upon the land, upon the open field will I hurl thee, and will cause all the fowls of the heaven to dwell upon thee, and I will satisfy off thee the beasts of all the earth.
5 Kwa kuwa nitaiweka nyama yako juu ya milima, na nitayajaza mabonde kwa funza wako waliokufa.
And I will lay thy flesh upon the mountains, and fill the valleys with thy carcass.
6 Kisha nitamwaga damu yako juu ya milima, na vitanda vya kijito vitajazwa kwa damu yako.
I will also saturate the land wherein thou swimmest with thy blood, even to the mountains; and the ravines shall be full of thee.
7 Kisha wakati nitakapokuzimisha, nitazifunika mbingu na kuzitia giza nyota zake; nitalifunika jua kwa mawingu, na mwezi hautatoa nuru yake usiku.
And I will cover up the heavens, when thou art quenched, and make their stars obscure: the sun will I cover up with a cloud, and the moon shall not let shine her light.
8 Mianga ya mbinguni nitaiweka giza juu yako, na nitaweka giza juu ya nchi-hivi ndivyo asemavyo Bwana Yahwe.
All the light-dispensing lights of the heavens—these will I make obscure because of thee, and I will lay darkness upon thy land, saith the Lord Eternal.
9 Hivyo nitaitisha mioyo ya watu wengi katika nchi ambao huwajui, wakati nitakapoleta kuhusu uvunjifu miongoni mwa mataifa, miongoni mwa nchi ambazo hukuzijua.
And I will aggrieve the heart of many people, when I bring those who are broken off from thee among the nations, into countries which thou hast not known.
10 Nitawashangaza watu wengi kuhusiana na wewe; wafalme wao watatetemeka kwa hofu kuhusiana na wewe nitakapoutikisa upanga wangu mbele yao. Kila wakati kila mmoja atatetemeka kwa sababu yako, katika siku ya kuanguka kwako.
Yea, I will make many people amazed at thee, and on their kings the hair shall stand on end because of thee, when I brandish my sword before their faces: and they shall tremble at every moment, every man for his own life, on the day of thy downfall.
11 Kwa kuwa Bwana Yahwe asema hivi: Upanga wa mfalme wa Babeli utakuja juu yako.
For thus hath said the Lord Eternal, The sword of the king of Babylon shall come over thee.
12 Nitawafanya watu wako kuanguka kwa panga za mashujaa-kila shujaa ni tishio la mataifa. Hawa mashujaa watateketeza kiburi cha Misri na kuangamiza watu wake wote.
By the swords of the mighty will I cause thy multitude to fall, the fiercest of nations are all of them: and they shall destroy the pride of Egypt, and all her multitude shall be annihilated.
13 Kwa kuwa nitaiharibu mifugo yote kutoka karibu na maji mengi; na mguu wa mtu hautayatibua tena, wala kwato za wanyama hazitayatibua.
And I will cause to vanish all her beasts from beside the great waters; and the foot of man shall not make them turbid any more, nor shall the hoofs of beasts make them turbid.
14 Kisha nitayafanya maji yao kuwa matulivu na kufanya mito yao kukimbia kama mafuta-hivi ndivyo asemavyo Bwana Yahwe.
Then will I make clear their waters, and cause their rivers to flow like oil, saith the Lord Eternal;
15 Wakati nitakapoifanya nchi ya Misri sehemu iliyojitenga, wakati nchi iliyopungukiwa na vitu viijazavyo, wakati nitakapo washambulia wakaao ndani yake, watajua yakwamba mimi ni Yahwe.
When I render the land of Egypt desolate and wasted, the country bereft of what now filleth it, when I smite all those that dwell therein: and they shall know that I am the Lord.
16 Kutakuwa na maombolezo; binti za mataifa wataomboleza juu yake; wataomboleza juu ya Misri, juu ya watu wake wote wataomboleza-hivi ndivyo Bwana Yahwe asemavyo.”'
This is the lamentation wherewith they shall lament for her; the daughters of the nations shall lament for her: for Egypt, and for all her multitude, shall they lament with it, saith the Lord Eternal.
17 Kisha ikawa katika mwaka wa kumi na mbili, siku ya kumi na tano ya mwezi, lile neno la Yahwe likanijia, kusema,
And it came to pass in the twelfth year, on the fifteenth day of the month, that the word of the Lord came unto me, saying,
18 “Mwanadamu, omboleza kwa ajili watu wa misri na walete chini-yeye na binti za mataifa mashuhuri-hata chini ya dunia pamoja na wale walioshuka chini kwenye shimo.
Son of man, moan for the multitude of Egypt, and say that it shall go down, yea, she, and the daughters of powerful nations, unto the land of the nether world, with those that go down to the pit.
19 'Je! wewe ni mzuri zaidi kuliko mtu mwingine yeyote? Nenda chini na lala chini pamoja na wasiotahiriwa.'
Whom dost thou surpass in loveliness? go down [then], and be thou laid with the [other] uncircumcised.
20 Wataanguka miongoni mwao waliokuwa wameuawa kwa upanga. Upanga ulikuwa umewekwa! Alikuwa amepatiwa upanga; watamkamata na watu wake.
In the midst of those that are slain by the sword shall they fall: to the sword is she given up; drag her away and all her multitudes.
21 Hodari wa wapiganaji katika Sheoli atasema kuhusu Misri na rafiki zake, 'Wameshuka chini hapa! Watalala pamoja na wasiotahiriwa, pamoja na wale waliokuwa wameuawa kwa upanga.' (Sheol h7585)
Then will speak of him the strongest among the mighty out of the midst of the nether world with those that once helped him, They are gone down, there lie the uncircumcised, —slain by the sword. (Sheol h7585)
22 Ashuru yupo huko pamoja na kusanyiko lake. Makaburi yake yamemzunguka; wote waliuawa kwa upanga.
There is Asshur and all his assemblage; round about him are his graves; all of them the slain that are fallen by the sword;
23 Wale ambao makaburi yao yamewekwa katika maficho ya mashimo yaliyo huko, pamoja na kusanyiko lake. Makaburi yake yakiwazunguka wote waliokuwa wameuawa, walioanguka kwa upanga, wale walioleta hofu juu ya nchi ya walio hai.
Whose graves are placed in the lowest depth of the pit, and his assemblage is round about his grave; all of them are slain, fallen by the sword, who once spread terror in the land of the living.
24 Elamu yupo huko pamoja na watu wake wote. Makaburi yake yamemzunguka; wote walikuwa wameuawa. Wale walioawa kwa upanga, walioshuka chini wasiotahiriwa hata sehemu ya chini kabisa ya dunia, waliowatia hofu juu ya nchi ya walio hai na wale waliobeba aibu yao wenyewe, pamoja na wale washukao chini kwenye shimo.
There is 'Elam and all her multitude round about her grave, all of them the slain, that are fallen by the sword, who are gone down uncircumcised into the land of the nether world, who once spread their terror in the land of the living; and they have borne their confusion with those that go down to the pit.
25 Wamemuwekea kitanda kwa ajili ya Elamu na watu wake wote kati ya wachinjaji; kaburi lake limemzunguka. Wote hawajatahiriwa, kukatwa vipande kwa upanga, kwa sababu waliwaleta mashujaa wao juu ya nchi ya walio hai. Hivyo wamechukua aibu yao wenyewe, pamoja na wale washukao kwenye shimo miongoni mwa wote waliouawa, wale washukao kwenda shimoni. Elamu yu miongoni mwa wale waliokuwa wameuawa.
In the midst of the slain have they set a couch for her with all her multitude; all round about are her graves; all of them are uncircumcised, slain by the sword; because their terror was once spread in the land of the living; and they have borne their confusion with those that go down to the pit: in the midst of the slain was she placed.
26 Mesheki, Tubali, na watu wake wote wako huko! Makaburi yao yamewazunguka. Wote hawajatahiriwa, wameuawa kwa upanga, kwa sababu walileta utiisho wao juu ya nchi ya walio hai.
There is Meshech, Thubal, and all her multitude; all round about her are her graves: all of them are the uncircumcised, slain by the sword; because they once spread their terror in the land of the living.
27 Wasilale pamoja mashujaa walioanguka wa wasiotahiriwa walioshuka chini kwa Sheoli pamoja na silaha zao zote za vita, na pamoja na panga zao zote walizoziweka chini ya vichwa vyao na maovu yao juu ya mifupa yao. Kwa kuwa walikuwa tishio kwa mashujaa katika nchi ya walio hai. (Sheol h7585)
And those who are fallen of the uncircumcised shall not lie with the mighty, who are gone down to the nether world with their weapons of war, while men laid their swords under their heads, and the [instruments of] their iniquities were upon their bones; for the terror of the mighty was in the land of the living. (Sheol h7585)
28 Basi wewe, Misri, utavunjika kati yao wasiotahiriwa! Utalala karibu nao waliokuwa wamekatwa vipande vipande kwa upanga.
But thou shalt be broken in the midst of the uncircumcised, and shalt lie with those that are slain by the sword.
29 Edomu yuko huko na wafalme na viongozi wake wote. Walikuwa wamehifadhiwa katika uwezo wao pamoja na wale walioawa kwa upanga. Pamoja na wasiotahiriwa wamelala, pamoja na wale walioshuka kwenye shimo.
There are Edom, her kings, and all her princes, who are laid despite their prowess by those that are slain by the sword: they shall lie with the uncircumcised, and with those that go down to the pit.
30 Wakuu wa kaskazini wako huko-wote na Wasidoni wote walioshuka chini pamoja na hao waliokuwa wamekatwa vipande vipande. Walikuwa na nguvu na kuwafanya wengine kuogopa, lakini sasa wako huko kwa aibu, wasiotahiriwa pamoja na wale waliokatwa vipande vipande kwa upanga. Wamebeba aibu yao wenyewe, pamoja nao waendao kwenye shimo.
There are the chieftains of the north, all of them, and all the Zidonians, who are gone down with the slain: despite the terror they excited through their prowess are they made ashamed; and they lie uncircumcised with those that are slain by the sword, and bear their confusion with those that go down to the pit.
31 Farao ataona na kupata faraja kuhusu kundi lake waliokatwa vipande vipande kwa upanga -Farao na jeshi lake lote-hivi ndivyo Bwana Yahwe asemavyo.
These shall Pharaoh see, and he shall be comforted over all his multitude: slain by the sword are Pharaoh and all his army, saith the Lord Eternal.
32 Natamuweka kama utiisho wangu katika nchi ya walio hai, lakini atakuwa amelazwa chini katikati yao wasiotahiriwa, miongoni mwa wale walio katwa vipande kwa upanga, Farao na makundi yake yote-hivi ndivyo Bwana Yahwe asemavyo.
For I spread my terror in the land of the living; and he shall be laid in the midst of the uncircumcised with those that are slain by the sword, —yea, Pharaoh and all his multitude, saith the Lord Eternal.

< Ezekieli 32 >