< Ezekieli 30 >

1 Neno la Yahwe likanijia, kusema,
Et la parole de l'Éternel me fut adressée en ces mots:
2 “Mwanadamu, toa unabii na sema, 'Bwana Yahwe asema hivi: Maombolezo. “Ole unakuja siku hiyo.”
Fils de l'homme, prophétise et dis: Ainsi parle le Seigneur, l'Éternel: Gémissez! malheur pour le jour!…
3 siku ikaribu. Siku ikaribu kwa ajili ya Yahwe. Itakuwa siku ya mawingu, mda wa hukumu kwa ajili ya mataifa.
car le jour approche, il approche le jour de l'Éternel! le moment des nations sera une sombre journée.
4 Kisha upanga utakuja dhidi ya Misri, na huko kutakuwa na maumivu makali katika Kushi wakati wauaji wa watu watakapoanguka katika Misri-wakati watakapochukua utajiri, na wakati misingi yake itakapoharibiwa.
L'épée fond sur l'Egypte, et l'angoisse est en Ethiopie, quand les blessés tombent en Egypte, et qu'on emmène son peuple, et que ses fondements sont démolis.
5 Kushi, Putu, na Ludi, na wageni wote, pamoja na watu wa nyumba ya agano-wote wataanguka chini kwa upanga.
Éthiopiens et Libyens, et Lydiens, et tous les confédérés, et Chub et les fils des pays alliés, avec eux succomberont sous l'épée.
6 Yahwe asema hivi: Basi wale wanaoisaidia Misri wataanguka, na kiburi cha uweza wake kitashuka chini. Kutoka Migdoli hata Sewene maaskari wao wataanguka kwa upanga-hivi ndivyo Bwana Yahwe asemavyo.
Ainsi parle l'Éternel: Ils succombent les appuis de l'Egypte, et elle est abattue son orgueilleuse puissance; de Migdol à Siène ils y périront par l'épée, dit le Seigneur, l'Éternel.
7 Wataogofya kati ya nchi zilizotupwa, na miji yao itakuwa miongoni mwa miji yote iliharibika.
Ils seront dévastés entre les terres dévastées, et ses villes seront au nombre des villes en ruines;
8 Kisha watajua kwamba mimi ni Yahwe, nitakapouweka moto katika Misri, na wakati wasaidizi wake wote watakapoharibiwa.
et ils comprendront que je suis l'Éternel, quand je mettrai le feu à l'Egypte et que tous ses auxiliaires seront taillés en pièces.
9 Katika siku hiyo wajumbe watatoka mbele yangu katika meli ili kuitia hofu Kushi iliyo salama, na kutakuwa na maumivu makali miongoni mwao katika siku ya kuangamizwa Misri. Kwa kuwa tazama! inakuja.
Dans ce jour-là des messagers s'en iront de par moi sur des navires porter l'épouvante dans l'Ethiopie en sécurité, et il y aura parmi eux de l'angoisse, comme à la journée de l'Egypte, car voici, elle arrive.
10 Bwana Yahwe asema hivi: Nitaufanya mwisho wa watu wa Misri kwa mkono wa Nebukadreza, mfalme wa Babeli.
Ainsi parle le Seigneur, l'Éternel: Je mettrai fin au peuple de l'Egypte par le bras de Nébucadnézar, roi de Babel.
11 Yeye na jeshi lake pamoja naye, hofu ya mataifa, italetwa kuiharibu nchi; watafuta panga zao juu ya Misri na kuijaza nchi pamoja na watu waliokufa.
Lui et son peuple avec lui, les plus violents des hommes, s'avancent pour ravager le pays, et ils tireront leurs épées contre l'Egypte, et rempliront le pays de morts;
12 Nitaifanya mito kuwa nchi kavu, na nitaiuza nchi kwenye mkono wa watu waovu. Nitaifanya nchi na viijazavyo ukiwa kwa mkono wa wageni-mimi, Yahwe, nimesema.
et je mettrai les canaux à sec, et livrerai le pays aux mains d'hommes méchants, et je dévasterai le pays et ce qu'il contient par les bras d'étrangers. Moi, l'Éternel, je l'ai dit.
13 Bwana Yahwe asema hivi: Nitaziharibu sanamu, na nitaleta mwisho wa sanamu za ubatili za Nofu. Hakutakuwa na mkuu katika Misri, na nitaweka hofu katika nchi ya Misri.
Ainsi parle le Seigneur, l'Éternel: Je détruirai les idoles, et anéantirai les faux dieux de Noph, et il n'y aura plus de princes du pays d'Egypte, et je répandrai la terreur sur le pays d'Egypte;
14 Kisha nitaifanya Pathrosi ukiwa na kuweka moto katika Soani, nitatekeleza matendo ya hukumu katika No.
et je dévasterai Pathros, et porterai le feu en Tsoan, et exercerai mes jugements sur No;
15 Kwa kuwa nitamwaga ghadhabu yangu juu Sini, ngome ya Misri, na kuwakatilia mbali watu wa mataifa.
et je verserai ma colère sur Sin, le boulevard de l'Egypte, et j'exterminerai le peuple de No;
16 Kisha nitaweka moto katika Misri; Sini itakuwa katika dhiki kuu, No itavunjika, na Nofu itakabiliana na maadui kila siku.
et je porterai le feu en Egypte: Sin sera tremblante, et No forcée, et Noph en plein jour prise par l'ennemi;
17 Vijana katika Oni na Pi-besethi wataanguka kwa upanga, na miji yao itaenda utumwani.
les jeunes hommes de On et de Bubaste périront par l'épée, et les femmes seront emmenées captives.
18 Huko Tapanesi, siku itabadilika kuwa usiku nitakapo ivunja nira ya Misri huko, na kiburi cha uwezo wake kitaisha. Kutakuwa na wingu likimfunika, na binti zake wataenda utumwani.
A Tachphanès le jour s'obscurcira, quand j'y briserai le joug de l'Egypte, et qu'il y sera mis fin à son orgueilleuse puissance: un noir nuage la couvrira, et ses filles seront emmenées captives.
19 Nitatekeleza matendo ya hukumu katika Misri, hivyo watajua kwamba mimi ni Yahwe.”'
Ainsi j'exécuterai mes jugements sur l'Egypte et ils sauront que je suis l'Éternel.
20 Kisha ikawa katika mwaka wa kumi na moja, katika mwezi wa kwanza, katika siku ya saba ya mwezi, lile neno la Yahwe likanijia, kusema,
Et la onzième année, le premier mois, le septième jour du mois, la parole de l'Éternel me fut adressée en ces mots:
21 “Mwanadamu, nimeuvunja mkono wa Farao, mfalme wa Misri. Tazama! Haukufungwa, au kufungwa kwa kitambaa cha bendeji ili upone, hivyo basi uweze kuwa imara kushika upanga.
Fils de l'homme, j'ai rompu le bras de Pharaon, roi d'Egypte, et voici, il n'est point bandé, pour qu'on y applique des remèdes, y mette un bandage pour le serrer, afin qu'il ait la force de saisir une épée.
22 Kwa hiyo Bwana Yahwe asema hivi, 'Tazama, mimi niko juu ya Farao, mfalme wa Misri. Kwa kuwa nitauvunja mkono wake, wote yule aliye hodari na yule aliyevunjika, nitaufanya upanga wangu kuanguka kutoka kwenye mkono wake.
C'est pourquoi ainsi parle le Seigneur, l'Éternel: Voici, j'en veux à Pharaon, roi d'Egypte, et je lui romprai les deux bras, celui qui est fort et celui qui est cassé, et je ferai tomber l'épée de sa main;
23 Kisha nitaitawanya Misri miongoni mwa mataifa na kuwatawanya katika nchi mbali mbali.
et je disperserai les Égyptiens parmi les nations et les disséminerai dans les pays divers.
24 Nitaunyoosha mikono kwa mfalme wa Babeli na kuweka upanga wangu katika mkono wake ili kwamba niweze kuiharibu mikono ya Farao. Atagugumia mbele ya mfalme wa Babeli kwa mgumio wa mtu anayekufa.
Mais je donnerai force aux bras du roi de Babel et mettrai mon épée en sa main, et je briserai les bras de Pharaon, afin qu'il pousse devant lui les soupirs des blessés.
25 Kwa kuwa nitainyoosha mikono ya mfalme wa Babeli, wakati mkono wa Farao utakapoanguka. Kisha watajua yakwamba mimi ni Yahwe, nitakapoweka upanga wangu kwenye mkono wa mfalme wa Babeli; kwa kuwa ataishambulia nchi ya Misri kwa huo.
Oui, je donnerai force aux bras du roi de Babel, mais les bras de Pharaon tomberont, afin qu'ils reconnaissent que je suis l'Éternel, quand je mettrai mon épée en la main du roi de Babel, afin qu'il l'étende sur le pays d'Egypte;
26 Hivyo nitaitawanya miongoni mwa mataifa na kuyatawanya kwenye nchi tofauti tofauti. Kisha watajua yakwamba mimi ni Yahwe.”'
et je disperserai les Égyptiens parmi les nations, et les disséminerai dans les pays divers, afin qu'ils reconnaissent que je suis l'Éternel.

< Ezekieli 30 >