< Ezekieli 30 >

1 Neno la Yahwe likanijia, kusema,
Yahweh gave me another message. [He said, ]
2 “Mwanadamu, toa unabii na sema, 'Bwana Yahwe asema hivi: Maombolezo. “Ole unakuja siku hiyo.”
“You human, prophesy [about what will happen to Egypt]. Say, ‘This is what Yahweh the Lord says: “Weep and wail [DOU], because terrible things will happen some day.
3 siku ikaribu. Siku ikaribu kwa ajili ya Yahwe. Itakuwa siku ya mawingu, mda wa hukumu kwa ajili ya mataifa.
That day is near, the day when I, Yahweh, [will punish people]; it will be a day of [dark] clouds and disaster for [many] nations.
4 Kisha upanga utakuja dhidi ya Misri, na huko kutakuwa na maumivu makali katika Kushi wakati wauaji wa watu watakapoanguka katika Misri-wakati watakapochukua utajiri, na wakati misingi yake itakapoharibiwa.
[An enemy army] [PRS] will come to attack Egypt with their swords, and there will be great distress [among the people] in Ethiopia. [Many] people will be killed in Egypt; everything valuable will be taken away, and [even] the foundations [of the buildings] will be torn down.
5 Kushi, Putu, na Ludi, na wageni wote, pamoja na watu wa nyumba ya agano-wote wataanguka chini kwa upanga.
[Soldiers of] Ethiopia, Libya, Lydia, and from all of Arabia, and [all the other] groups who are their allies, will be killed in the battles.”
6 Yahwe asema hivi: Basi wale wanaoisaidia Misri wataanguka, na kiburi cha uweza wake kitashuka chini. Kutoka Migdoli hata Sewene maaskari wao wataanguka kwa upanga-hivi ndivyo Bwana Yahwe asemavyo.
This is what [I], Yahweh say: “The allies of Egypt will be defeated, and the power that [the people of Egypt] are proud of will end. From Migdol [city in the north] to Aswan [city in the south], the soldiers of Egypt will be killed by their enemies’ swords”; [that is what I], Yahweh the Lord, declare.
7 Wataogofya kati ya nchi zilizotupwa, na miji yao itakuwa miongoni mwa miji yote iliharibika.
Egypt will become the most deserted country in the world, and its cities will be ruined, surrounded by ruined cities [in nearby nations].
8 Kisha watajua kwamba mimi ni Yahwe, nitakapouweka moto katika Misri, na wakati wasaidizi wake wote watakapoharibiwa.
Then, when I cause [everything in] Egypt to be burned in fires, and all their allies are defeated, people will know that I, Yahweh, [have the power to do what I say that I will do].
9 Katika siku hiyo wajumbe watatoka mbele yangu katika meli ili kuitia hofu Kushi iliyo salama, na kutakuwa na maumivu makali miongoni mwao katika siku ya kuangamizwa Misri. Kwa kuwa tazama! inakuja.
At that time, I will send messengers to go [swiftly up the Nile River] in boats to cause the people of Ethiopia who (are complacent/confident/think that nothing terrible will happen to them) to become afraid. They will be terrified [PRS] when Egypt is destroyed; and it will soon be that time!”
10 Bwana Yahwe asema hivi: Nitaufanya mwisho wa watu wa Misri kwa mkono wa Nebukadreza, mfalme wa Babeli.
This is what [I], Yahweh the Lord, say: “By the power of [MTY] of King Nebuchadnezzar of Babylon I will get rid of very many people in Egypt.
11 Yeye na jeshi lake pamoja naye, hofu ya mataifa, italetwa kuiharibu nchi; watafuta panga zao juu ya Misri na kuijaza nchi pamoja na watu waliokufa.
Nebuchadnezzar and his army, whose soldiers are extremely ruthless, will come to destroy Egypt. They will pull out their swords and fill Egypt with [the corpses of] those whom they have killed.
12 Nitaifanya mito kuwa nchi kavu, na nitaiuza nchi kwenye mkono wa watu waovu. Nitaifanya nchi na viijazavyo ukiwa kwa mkono wa wageni-mimi, Yahwe, nimesema.
I will cause the Nile [River] to become dry, and I will sell the nation to evil men. By the power [MTY] of foreigners I will ruin the land and everything that is in it. [That will surely happen because] I, Yahweh, have predicted it.”
13 Bwana Yahwe asema hivi: Nitaziharibu sanamu, na nitaleta mwisho wa sanamu za ubatili za Nofu. Hakutakuwa na mkuu katika Misri, na nitaweka hofu katika nchi ya Misri.
This is [also] what [I], Yahweh the Lord, say: “I will cause the idols and statues [of idols] [DOU] in Memphis [city] to be destroyed. No longer will there be a king in Egypt, and all over the land, people will be terrified. I will cause [the people of] Egypt to be very afraid.
14 Kisha nitaifanya Pathrosi ukiwa na kuweka moto katika Soani, nitatekeleza matendo ya hukumu katika No.
I will cause the Pathros [area in southern Egypt] to be abandoned. I will start fires in Zoan [city in northeast Egypt] and punish [the people in] Thebes, [the capital of southern Egypt].
15 Kwa kuwa nitamwaga ghadhabu yangu juu Sini, ngome ya Misri, na kuwakatilia mbali watu wa mataifa.
I will pour out my punishment [MTY] on [the fortress in] Pelusium [at the eastern end of Egypt], and I will get rid of very many people in Thebes.
16 Kisha nitaweka moto katika Misri; Sini itakuwa katika dhiki kuu, No itavunjika, na Nofu itakabiliana na maadui kila siku.
I will burn Egypt by fires; [the people in] Pelusium will suffer severe pain. [Enemies] will conquer Thebes, and [the people in] Memphis will constantly be terrified.
17 Vijana katika Oni na Pi-besethi wataanguka kwa upanga, na miji yao itaenda utumwani.
[Many] young men in Heliopolis and Bubastis [cities in northern Egypt] will be killed by [their enemies] swords, and the others [from those cities] will be captured and taken [to Babylon].
18 Huko Tapanesi, siku itabadilika kuwa usiku nitakapo ivunja nira ya Misri huko, na kiburi cha uwezo wake kitaisha. Kutakuwa na wingu likimfunika, na binti zake wataenda utumwani.
It will be a dark day [of destruction] at Tahpenes [city in northeast Egypt] when I cause the power [MET] of Egypt to end; that country will no longer be proud of being strong. [It will be as though] a dark cloud will cover Egypt, because the people of its villages will be captured and forced to go [to Babylon].”
19 Nitatekeleza matendo ya hukumu katika Misri, hivyo watajua kwamba mimi ni Yahwe.”'
That is how I will punish Egypt, and people will know that I, Yahweh, [have the power to do what I say that I will do].’”
20 Kisha ikawa katika mwaka wa kumi na moja, katika mwezi wa kwanza, katika siku ya saba ya mwezi, lile neno la Yahwe likanijia, kusema,
Almost eleven years [after we had been taken to Babylon], on the seventh day of the first month [of that year], Yahweh gave me another message. [He said, ]
21 “Mwanadamu, nimeuvunja mkono wa Farao, mfalme wa Misri. Tazama! Haukufungwa, au kufungwa kwa kitambaa cha bendeji ili upone, hivyo basi uweze kuwa imara kushika upanga.
“You human, I [have enabled the army of Nebuchadnezzar to defeat the army of] the King of Egypt. [It is as though] I have broken one of the arms of the King of Egypt, and it has not been bandaged in order that it could be healed, and it has not been put in splints in order that [after it heals] the arm will be strong [enough] to hold a sword.
22 Kwa hiyo Bwana Yahwe asema hivi, 'Tazama, mimi niko juu ya Farao, mfalme wa Misri. Kwa kuwa nitauvunja mkono wake, wote yule aliye hodari na yule aliyevunjika, nitaufanya upanga wangu kuanguka kutoka kwenye mkono wake.
Therefore, this is what [I], Yahweh the Lord, say: ‘I am the enemy of the King of Egypt. [I will completely destroy the power of Egypt; it is as though] now I will break both of the king’s arms, the good/strong one and the broken one, and cause the sword to fall from his hand.
23 Kisha nitaitawanya Misri miongoni mwa mataifa na kuwatawanya katika nchi mbali mbali.
I will cause the people of Egypt to be scattered among the nations [DOU].
24 Nitaunyoosha mikono kwa mfalme wa Babeli na kuweka upanga wangu katika mkono wake ili kwamba niweze kuiharibu mikono ya Farao. Atagugumia mbele ya mfalme wa Babeli kwa mgumio wa mtu anayekufa.
[It is as though] I will strengthen the arms of the King of Babylon and put a sword in his hand, and [as though] I will break the arms of the king of Egypt, and he will groan in front of the King of Babylon like [SIM] a soldier who is wounded and about to die.
25 Kwa kuwa nitainyoosha mikono ya mfalme wa Babeli, wakati mkono wa Farao utakapoanguka. Kisha watajua yakwamba mimi ni Yahwe, nitakapoweka upanga wangu kwenye mkono wa mfalme wa Babeli; kwa kuwa ataishambulia nchi ya Misri kwa huo.
I will cause the power [MTY] of the King of Babylon to become greater, and the power of the king of Egypt will be useless [MET]. When that happens, when I give power to the army of the King of Babylon, they will use that power to attack Egypt.
26 Hivyo nitaitawanya miongoni mwa mataifa na kuyatawanya kwenye nchi tofauti tofauti. Kisha watajua yakwamba mimi ni Yahwe.”'
I will cause the people of Egypt to be scattered among the nations [DOU]. And when that happens, the people [of Egypt] will know that I, Yahweh, [have the power to do what I say that I will do] [DOU].’”

< Ezekieli 30 >