< Ezekieli 30 >

1 Neno la Yahwe likanijia, kusema,
Another message from the Lord came to me, saying,
2 “Mwanadamu, toa unabii na sema, 'Bwana Yahwe asema hivi: Maombolezo. “Ole unakuja siku hiyo.”
“Son of man, prophesy and announce that this is what the Lord God says: Weep! This is a terrible day!
3 siku ikaribu. Siku ikaribu kwa ajili ya Yahwe. Itakuwa siku ya mawingu, mda wa hukumu kwa ajili ya mataifa.
The day is soon coming—the Day of the Lord is near. It will be a gloomy, cloudy day, a time of judgment for the nations.
4 Kisha upanga utakuja dhidi ya Misri, na huko kutakuwa na maumivu makali katika Kushi wakati wauaji wa watu watakapoanguka katika Misri-wakati watakapochukua utajiri, na wakati misingi yake itakapoharibiwa.
A sword will come to attack Egypt, and there will be anguish in Cush when people are killed in Egypt, when it's robbed of its wealth and the country ruined.
5 Kushi, Putu, na Ludi, na wageni wote, pamoja na watu wa nyumba ya agano-wote wataanguka chini kwa upanga.
Cush, Put, and Lud, and many other peoples, as well as Arabia, Kub, and the people of the promised land, they all, like Egypt, will be killed by the sword.
6 Yahwe asema hivi: Basi wale wanaoisaidia Misri wataanguka, na kiburi cha uweza wake kitashuka chini. Kutoka Migdoli hata Sewene maaskari wao wataanguka kwa upanga-hivi ndivyo Bwana Yahwe asemavyo.
This is what the Lord says: Egypt's allies will fall, and the country will lose its prestigious position. From Migdol in the north to Syene in the south, they will be killed by the sword, declares the Lord God.
7 Wataogofya kati ya nchi zilizotupwa, na miji yao itakuwa miongoni mwa miji yote iliharibika.
Egypt will become more of a wasteland than any other country, and its towns will be left in ruins.
8 Kisha watajua kwamba mimi ni Yahwe, nitakapouweka moto katika Misri, na wakati wasaidizi wake wote watakapoharibiwa.
Then they will acknowledge that I am the Lord when I set fire to Egypt and all its allies are crushed.
9 Katika siku hiyo wajumbe watatoka mbele yangu katika meli ili kuitia hofu Kushi iliyo salama, na kutakuwa na maumivu makali miongoni mwao katika siku ya kuangamizwa Misri. Kwa kuwa tazama! inakuja.
At that time I will send messengers in ships to shock Cush out of its sense of security. They will tremble in fear when disasters hit Egypt. Watch out! It's definitely coming!
10 Bwana Yahwe asema hivi: Nitaufanya mwisho wa watu wa Misri kwa mkono wa Nebukadreza, mfalme wa Babeli.
This is what the Lord God says: I will use Nebuchadnezzar king of Babylon to take away Egypt's wealth.
11 Yeye na jeshi lake pamoja naye, hofu ya mataifa, italetwa kuiharibu nchi; watafuta panga zao juu ya Misri na kuijaza nchi pamoja na watu waliokufa.
He and his army from the cruelest nation in the world will be brought to destroy the country. They will use their swords to attack Egypt, and they will fill the land with dead bodies.
12 Nitaifanya mito kuwa nchi kavu, na nitaiuza nchi kwenye mkono wa watu waovu. Nitaifanya nchi na viijazavyo ukiwa kwa mkono wa wageni-mimi, Yahwe, nimesema.
I will dry up the rivers and sell the land to wicked people. Using these foreigners I will ruin the land and everything in it. I the Lord have spoken.
13 Bwana Yahwe asema hivi: Nitaziharibu sanamu, na nitaleta mwisho wa sanamu za ubatili za Nofu. Hakutakuwa na mkuu katika Misri, na nitaweka hofu katika nchi ya Misri.
This is what the Lord God says: I'm going to destroy the idols and get rid of the images in Memphis. There won't be a prince in Egypt any longer, and I will make everyone in the country terrified.
14 Kisha nitaifanya Pathrosi ukiwa na kuweka moto katika Soani, nitatekeleza matendo ya hukumu katika No.
I will destroy Pathros, set Zoan on fire, and punish Thebes.
15 Kwa kuwa nitamwaga ghadhabu yangu juu Sini, ngome ya Misri, na kuwakatilia mbali watu wa mataifa.
I will pour out my wrath on Pelusium, Egypt's fortress town, and wipe out the army at Thebes.
16 Kisha nitaweka moto katika Misri; Sini itakuwa katika dhiki kuu, No itavunjika, na Nofu itakabiliana na maadui kila siku.
I will set fire to Egypt, Pelusium will suffer, Thebes will be ripped apart, and Memphis will face trouble every day.
17 Vijana katika Oni na Pi-besethi wataanguka kwa upanga, na miji yao itaenda utumwani.
The young soldiers of Heliopolis and Bubastis will fall by the sword, and the people from those towns will be taken captive.
18 Huko Tapanesi, siku itabadilika kuwa usiku nitakapo ivunja nira ya Misri huko, na kiburi cha uwezo wake kitaisha. Kutakuwa na wingu likimfunika, na binti zake wataenda utumwani.
It will be a dark day in Tahpanhes when I break Egypt's power and bring to an end their proud strength. It will be under a cloud as the people go into captivity.
19 Nitatekeleza matendo ya hukumu katika Misri, hivyo watajua kwamba mimi ni Yahwe.”'
This is how I'm going to punish Egypt, and they will acknowledge that I am the Lord.”
20 Kisha ikawa katika mwaka wa kumi na moja, katika mwezi wa kwanza, katika siku ya saba ya mwezi, lile neno la Yahwe likanijia, kusema,
On the seventh day of the first month of the eleventh year, a message from the Lord came to me, saying,
21 “Mwanadamu, nimeuvunja mkono wa Farao, mfalme wa Misri. Tazama! Haukufungwa, au kufungwa kwa kitambaa cha bendeji ili upone, hivyo basi uweze kuwa imara kushika upanga.
“Son of man, I have broken the arm of Pharaoh king of Egypt. You can see that it hasn't been bandaged up to heal it, or put it in a splint to provide enough strength to hold a sword.
22 Kwa hiyo Bwana Yahwe asema hivi, 'Tazama, mimi niko juu ya Farao, mfalme wa Misri. Kwa kuwa nitauvunja mkono wake, wote yule aliye hodari na yule aliyevunjika, nitaufanya upanga wangu kuanguka kutoka kwenye mkono wake.
So this is what the Lord God says: Watch out, because I'm condemning Pharaoh king of Egypt! I will break his arms, both the one that's still good and the one already broken, and I will make him drop his sword.
23 Kisha nitaitawanya Misri miongoni mwa mataifa na kuwatawanya katika nchi mbali mbali.
I will scatter the Egyptians among the different nations and countries.
24 Nitaunyoosha mikono kwa mfalme wa Babeli na kuweka upanga wangu katika mkono wake ili kwamba niweze kuiharibu mikono ya Farao. Atagugumia mbele ya mfalme wa Babeli kwa mgumio wa mtu anayekufa.
I will make the arms of the king of Babylon strong, and put my sword in his hand, but I will break Pharaoh's arms, and he will moan in pain like someone who's about to die.
25 Kwa kuwa nitainyoosha mikono ya mfalme wa Babeli, wakati mkono wa Farao utakapoanguka. Kisha watajua yakwamba mimi ni Yahwe, nitakapoweka upanga wangu kwenye mkono wa mfalme wa Babeli; kwa kuwa ataishambulia nchi ya Misri kwa huo.
I will make the arms of Babylon's king strong, but Pharaoh's arms will drop to his sides, weak and useless. Then they will acknowledge that I am the Lord, when I put my sword in the hand of the king of Babylon and he uses it to attack Egypt.
26 Hivyo nitaitawanya miongoni mwa mataifa na kuyatawanya kwenye nchi tofauti tofauti. Kisha watajua yakwamba mimi ni Yahwe.”'
When I scatter the Egyptians among the different nations and countries, they will acknowledge that I am the Lord.”

< Ezekieli 30 >