< Ezekieli 30 >

1 Neno la Yahwe likanijia, kusema,
The word of Jehovah came again to me, saying,
2 “Mwanadamu, toa unabii na sema, 'Bwana Yahwe asema hivi: Maombolezo. “Ole unakuja siku hiyo.”
Son of man, prophesy, and say, Thus says the lord Jehovah: Wail ye, Alas for the day!
3 siku ikaribu. Siku ikaribu kwa ajili ya Yahwe. Itakuwa siku ya mawingu, mda wa hukumu kwa ajili ya mataifa.
For the day is near, even the day of Jehovah is near. It shall be a day of clouds, a time of the nations.
4 Kisha upanga utakuja dhidi ya Misri, na huko kutakuwa na maumivu makali katika Kushi wakati wauaji wa watu watakapoanguka katika Misri-wakati watakapochukua utajiri, na wakati misingi yake itakapoharibiwa.
And a sword shall come upon Egypt, and anguish shall be in Ethiopia, when the slain shall fall in Egypt, and they shall take away her multitude, and her foundations shall be broken down.
5 Kushi, Putu, na Ludi, na wageni wote, pamoja na watu wa nyumba ya agano-wote wataanguka chini kwa upanga.
Ethiopia, and Put, and Lud, and all the mixed people, and Cub, and the sons of the land that is in league, shall fall with them by the sword.
6 Yahwe asema hivi: Basi wale wanaoisaidia Misri wataanguka, na kiburi cha uweza wake kitashuka chini. Kutoka Migdoli hata Sewene maaskari wao wataanguka kwa upanga-hivi ndivyo Bwana Yahwe asemavyo.
Thus says Jehovah: They also who uphold Egypt shall fall, and the pride of her power shall come down. From the tower of Seveneh they shall fall in it by the sword, says the lord Jehovah.
7 Wataogofya kati ya nchi zilizotupwa, na miji yao itakuwa miongoni mwa miji yote iliharibika.
And they shall be desolate in the midst of the countries that are desolate, and her cities shall be in the midst of the cities that are wasted.
8 Kisha watajua kwamba mimi ni Yahwe, nitakapouweka moto katika Misri, na wakati wasaidizi wake wote watakapoharibiwa.
And they shall know at I am Jehovah when I have set a fire in Egypt, and all her helpers are destroyed.
9 Katika siku hiyo wajumbe watatoka mbele yangu katika meli ili kuitia hofu Kushi iliyo salama, na kutakuwa na maumivu makali miongoni mwao katika siku ya kuangamizwa Misri. Kwa kuwa tazama! inakuja.
In that day messengers shall go forth from before me in ships to make the careless Ethiopians afraid, and there shall be anguish upon them, as in the day of Egypt, for, lo, it comes.
10 Bwana Yahwe asema hivi: Nitaufanya mwisho wa watu wa Misri kwa mkono wa Nebukadreza, mfalme wa Babeli.
Thus says the lord Jehovah: I will also make the multitude of Egypt to cease by the hand of Nebuchadrezzar king of Babylon.
11 Yeye na jeshi lake pamoja naye, hofu ya mataifa, italetwa kuiharibu nchi; watafuta panga zao juu ya Misri na kuijaza nchi pamoja na watu waliokufa.
He and his people with him, the terrible of the nations, shall be brought in to destroy the land. And they shall draw their swords against Egypt, and fill the land with the slain.
12 Nitaifanya mito kuwa nchi kavu, na nitaiuza nchi kwenye mkono wa watu waovu. Nitaifanya nchi na viijazavyo ukiwa kwa mkono wa wageni-mimi, Yahwe, nimesema.
And I will make the rivers dry, and will sell the land into the hand of evil men. And I will make the land desolate, and all that is therein, by the hand of strangers. I, Jehovah, have spoken it.
13 Bwana Yahwe asema hivi: Nitaziharibu sanamu, na nitaleta mwisho wa sanamu za ubatili za Nofu. Hakutakuwa na mkuu katika Misri, na nitaweka hofu katika nchi ya Misri.
Thus says the lord Jehovah: I will also destroy the idols, and I will cause the images to cease from Memphis. And there shall no more be a ruler from the land of Egypt. And I will put a fear in the land of Egypt.
14 Kisha nitaifanya Pathrosi ukiwa na kuweka moto katika Soani, nitatekeleza matendo ya hukumu katika No.
And I will make Pathros desolate, and will set a fire in Zoan, and will execute judgments upon No.
15 Kwa kuwa nitamwaga ghadhabu yangu juu Sini, ngome ya Misri, na kuwakatilia mbali watu wa mataifa.
And I will pour my wrath upon Sin, the stronghold of Egypt, and I will cut off the multitude of No.
16 Kisha nitaweka moto katika Misri; Sini itakuwa katika dhiki kuu, No itavunjika, na Nofu itakabiliana na maadui kila siku.
And I will set a fire in Egypt. Sin shall be in great anguish, and No shall be broken up, and Memphis shall have adversaries in the daytime.
17 Vijana katika Oni na Pi-besethi wataanguka kwa upanga, na miji yao itaenda utumwani.
The young men of Aven and of Pi-beseth shall fall by the sword, and these cities shall go into captivity.
18 Huko Tapanesi, siku itabadilika kuwa usiku nitakapo ivunja nira ya Misri huko, na kiburi cha uwezo wake kitaisha. Kutakuwa na wingu likimfunika, na binti zake wataenda utumwani.
At Tehaphnehes also the day shall withdraw itself when I shall break the yokes of Egypt there, and the pride of her power shall cease in her. As for her, a cloud shall cover her, and her daughters shall go into captivity.
19 Nitatekeleza matendo ya hukumu katika Misri, hivyo watajua kwamba mimi ni Yahwe.”'
Thus I will execute judgments upon Egypt, and they shall know that I am Jehovah.
20 Kisha ikawa katika mwaka wa kumi na moja, katika mwezi wa kwanza, katika siku ya saba ya mwezi, lile neno la Yahwe likanijia, kusema,
And it came to pass in the eleventh year, in the first month, in the seventh day of the month, that the word of Jehovah came to me, saying,
21 “Mwanadamu, nimeuvunja mkono wa Farao, mfalme wa Misri. Tazama! Haukufungwa, au kufungwa kwa kitambaa cha bendeji ili upone, hivyo basi uweze kuwa imara kushika upanga.
Son of man, I have broken the arm of Pharaoh king of Egypt. And, lo, it has not been bound up, to apply medicines, to put a bandage to bind it, that it be strong to hold the sword.
22 Kwa hiyo Bwana Yahwe asema hivi, 'Tazama, mimi niko juu ya Farao, mfalme wa Misri. Kwa kuwa nitauvunja mkono wake, wote yule aliye hodari na yule aliyevunjika, nitaufanya upanga wangu kuanguka kutoka kwenye mkono wake.
Therefore thus says the lord Jehovah: Behold, I am against Pharaoh king of Egypt. And I will break his arms, the strong arm, and that which was broken, and I will cause the sword to fall out of his hand.
23 Kisha nitaitawanya Misri miongoni mwa mataifa na kuwatawanya katika nchi mbali mbali.
And I will scatter the Egyptians among the nations, and will disperse them through the countries.
24 Nitaunyoosha mikono kwa mfalme wa Babeli na kuweka upanga wangu katika mkono wake ili kwamba niweze kuiharibu mikono ya Farao. Atagugumia mbele ya mfalme wa Babeli kwa mgumio wa mtu anayekufa.
And I will strengthen the arms of the king of Babylon, and put my sword in his hand. But I will break the arms of Pharaoh, and he shall groan before him with the groanings of a mortally wounded man.
25 Kwa kuwa nitainyoosha mikono ya mfalme wa Babeli, wakati mkono wa Farao utakapoanguka. Kisha watajua yakwamba mimi ni Yahwe, nitakapoweka upanga wangu kwenye mkono wa mfalme wa Babeli; kwa kuwa ataishambulia nchi ya Misri kwa huo.
And I will hold up the arms of the king of Babylon, and the arms of Pharaoh shall fall down. And they shall know that I am Jehovah when I shall put my sword into the hand of the king of Babylon, and he shall stretch it out upon the land of Egypt.
26 Hivyo nitaitawanya miongoni mwa mataifa na kuyatawanya kwenye nchi tofauti tofauti. Kisha watajua yakwamba mimi ni Yahwe.”'
And I will scatter the Egyptians among the nations, and disperse them through the countries. And they shall know that I am Jehovah.

< Ezekieli 30 >