< Ezekieli 3 >

1 Akanambia, “Mwanadamu, kile ulichokikuta, kula. Kula hili gombo, kisha nenda kaongee na nyumba ya Israeli.”
He said to me, “You human, eat this scroll that is in front of you. Then go and speak to the Israeli people [MTY].”
2 Basi nikafungua kinywa changu, na akanilisha hilo gombo.
So I opened my mouth, and he gave me the scroll to eat it.
3 Akanambia, “Mwana wa adamu, lisha tumbo lako na jaza tumbo lako kwa hili gombo ambalo nimekupa!” Basi nikalila, na lilikuwa tamu kama asali kwenye mdomo wangu.
Then he said to me, “You human, eat the scroll that I have given to you. Fill your stomach with it.” So I ate it, and in my mouth it tasted as sweet as honey.
4 Kisha akanambia, “Mwana wa adamu, nenda kwenye nyumba ya Israeli na ongea maneno yangu kwao.
Then he said to me, “You human, go to the Israeli people [MTY] and tell them my message.
5 Kwa kuwa hujatumwa kwa watu wenye maneno ya kushangaza au lugha ngumu, lakini kwa nyumba ya Israeli-
The people to whom I am sending you are not people whose language is very [to learn], a language which you do not understand. I am sending you to your Israeli people [MTY].
6 sio kwa taifa lenye nguvu ya maneno ya ajabu au lugha ngumu ambao maneno yao hutaweza kuyaelewa! Kama nikikutuma kwao, watakusikiliza.
I am sending you to people whose language you understand very well. If I were sending you to people whose language was difficult for you to understand, they [be surprised and] pay attention to what [say to them].
7 Lakini nyumba ya Israeli haitakuwa tayari kukusikiliza, kwa kuwa hawako tayari kunisikiliza mimi. Hivyo nyumba yote ya Israeli ni paji gumu na moyo mgumu.
But the Israeli people do not want to listen to you because they do not want to listen to me. [They do not want to listen because] they are all very stubborn [DOU].
8 Kumbe nimeufanya uso wako kama kaidi kama nyuso zao na paji lako kuwa gumu kama mapaji yao.
But I will enable you [SYN] to be as stubborn and tough as they are.
9 Nimekufanya paji lako kama almasi, gumu kuliko jiwe la kiberiti! Usiwaogope wala kufadhaika kwa nyuso zao, kwa kuwa ni nyumba ya uasi.”
I will cause you to be as firm/unbreakable as [SIM] the hardest stone, like flint. So, [even though] they are very rebellious people, do not be afraid of them; do not allow them to cause you to be afraid.”
10 Kisha akanambia, “Mwana wa adamu, maneno yote niliyokutangazia-yachukue kwenye moyo wako na wasikize kwa sikio lako!
He also said to me, “You human, listen very carefully to what I say, and keep thinking about it [IDM].
11 Kisha nenda kwa watumwa, kwa watu wako, na uzungumze nao. Waambie, 'Hivi ndivyo Bwana Yahwe asemavyo; iwapo watasikia au hapana.”
Go to your fellow Israelis who [here after being] (exiled/forced to leave their country), and speak to them. Say to them, ‘This is what Yahweh the Lord says,’ [and then tell them my message], whether they want to hear it or whether they do not want to hear it.”
12 Kisha Roho akaniinua juu, na nikasikia nyuma yangu sauti yenye tetemeko la aridhi: “Ubarikiwe utukufu wa Yahwe kutoka mahali pake!”
[in the vision] the [of God] lifted me up, and I heard behind [someone speaking very loudly], like a loud rumbling sound. [I heard someone say, ] “Praise our glorious Yahweh in the place where he [in heaven]!”
13 Ilikuwa sauti ya mabawa ya viumbe hai vilipokuwa vikigusana kila kimoja, na sauti ya magurudumu ambayo yalikuwa pamoja na hivyo viumbe, na sauti ya tetemeko kubwa arithi.
[I heard] the sound of the wings of the four living creatures brushing against each other, [I also heard] the sound of the wheels that were beside them. It was a loud rumbling sound.
14 Roho akaniinua juu na kunichukua, Nikaenda kwa uchungu katika hasira kali rohoni mwangu, kwa kuwa mkono wa Yahwe ulikuwa na nguvu ukigandamiza juu yangu!
The Spirit took me away. Within me I was very bitter and angry [DOU], but I felt Yahweh holding me very powerfully.
15 Hivyo nikaenda kwa watumwa huko Tel Abibu waliokuwa wakiishi karibu na Kebari Kanali, na niliishi miongoni mwao huko kwa mda wa miaka saba, kushinda kabisa katika mshangao.
I came to the exiles who lived at Tel [town] near the Kebar River/ [south of Babylon]. Then, where they were living, I sat for seven days. I was [about everything that I had seen].
16 Kisha ikatokea baada ya siku saba kwamba neno la Yahwe likanijia, likisema,
After those seven days had ended, Yahweh gave me this message:
17 “Mwana wa adamu, nimekufanya uwe mwangalizi kwa ajili ya nyumba ya Israeli, hivyo sikiliza neno kutoka kinywani mwangu, na uwapatie onyo langu.
“You human, I am appointing [to be like] a watchman [MET] for the Israeli people [MTY]. [So] listen to these messages that I will give you, and tell them those messages to warn them.
18 Nitakaposema kwa waovu, 'Utakufa hakika' na usimuonye au kuzungumza onyo kwa waovu kuhusu matendo yao maovu hivyo anaweza kuishi-yule muovu atakufa kwa ajili ya dhambi yake, lakini nitaitaka damu yake kutoka kwenye mkono wako.
When I say about some wicked people, ‘They will surely [because of their sins],’ if you do not warn them or tell them that they must turn from their wicked behavior if they want to (save their lives/remain alive), those wicked people will die because of the sins that they have committed, but I will consider that you are responsible for their deaths [MTY].
19 Lakini kama ukimuonya muovo, na asiuache uovu wake au kutoka matendo yake maovu, kisha atakufa kwa dhambi yake, lakini utaokoa maisha yako mwenyewe.
But if you warn the wicked people and they do not turn from all their wicked behavior [DOU], they will die because of their sins, but you will have saved [from my punishing you].
20 Kama mwenye haki ataicha haki yake na kutenda yasiyohaki, na nikaweka kizuizi mbele yake, atakufa. Kwasababu hukumuonya, atakufa katika dhambi yake, na sintokumbuka matendo ya haki aliyoyafanya, lakini nitaitaka damu yake kutoka kwenye mkono wako.
Similarly, when righteous people turn from their righteous behavior and do evil deeds, I will cause bad things to happen [IDM] to them. [But you must warn them. If you do not warn them], and if they do not stop their sinful behavior, they will die because of their sins; I will not think about the righteous things that they [previously], but I will consider that you are responsible for their deaths [MTY].
21 Lakini kama ukimuonya mwenye mtu mwenye haki kuacha kufanya dhambi halafu akaacha kutenda dhambi, ataishi hakika tangu alipo unywa; na utakuwa umeokoa maisha yako mwenyewe.”
But if you warn righteous people not to sin, and they do not sin, they will surely remain alive because they [your] warning, and you will have saved [from my punishing you].”
22 Hivyo mkono wa Yahwe ulikuwa juu yangu huko, akanambia, “Inuka! nenda uwandani, na nitaongea na wewe huko!”
[I felt] Yahweh take control [MTY] of me, and he said to me, “Get up and go [from the city down] to the plain/valley, and there I will speak to you.”
23 Nikainuka na kwenda uwandani, na huko utukufu wa Yahwe ulisimama, kama utukufu ambao niliokuwa nimeuona karibu na Kebari Kanali; hivyo nikaanguka kifudifudi.
So I got up and went down to the valley. And I saw the glory of Yahweh there, like the glory that I had seen along the Kebar River/Canal. And I prostrated myself on the ground.
24 Roho akaja kwangu na kusimama juu ya miguu yangu; akaongea na mimi, na kunambia, “Nenda na jifungie mwenyewe kwenye nyumba yako,
Then the [of God] entered me and enabled me to stand up. He said to me, “Go into your house and stay inside it.
25 kwa sasa, mwana wa adamu, wataweka kamba juu yako na kukufunga ili usiweze kutoka nje miongoni mwao.
People will tie you with ropes, with the result that you will be unable to go out among the people.
26 Nitaufanya ulimi wako ugandamane na paa ya mdomo wako, ili kwamba uwe kimya, na hutaweza kuwakemea, kwa kuwa ni nyumba ya waasi.
[Even though] they are very rebellious people, I will cause your tongue to stick to the roof of your mouth, with the result that you will be unable to talk and to rebuke them.
27 Lakini nitakapozungumza na wewe, nitafungua mdomo wako hivyo utawaambia, 'Hivi ndivyo Bwana Yahwe asemavyo.' Yeye asikiaye na asikie; yeye asiyesikia na asisikie, kwa kuwa wao ni nyumba ya kuasi!”
[then] when I speak to [again], I will enable you to talk [MTY], and you will say to them, ‘This is what Yahweh the Lord says,’ [and you will tell them my message]. Those who are willing to [to what you say] will listen, [many] will refuse to listen, because they are rebellious people [MTY].”

< Ezekieli 3 >