< Ezekieli 3 >

1 Akanambia, “Mwanadamu, kile ulichokikuta, kula. Kula hili gombo, kisha nenda kaongee na nyumba ya Israeli.”
Moreover he saide vnto me, Sonne of man, eate that thou findest: eate this roule, and goe, and speake vnto the house of Israel.
2 Basi nikafungua kinywa changu, na akanilisha hilo gombo.
So I opened my mouth, and he gaue mee this roule to eate.
3 Akanambia, “Mwana wa adamu, lisha tumbo lako na jaza tumbo lako kwa hili gombo ambalo nimekupa!” Basi nikalila, na lilikuwa tamu kama asali kwenye mdomo wangu.
And he said vnto me, Sonne of man, cause thy belly to eate, and fill thy bowels with this roule that I giue thee. Then did I eate it, and it was in my mouth as sweete as honie.
4 Kisha akanambia, “Mwana wa adamu, nenda kwenye nyumba ya Israeli na ongea maneno yangu kwao.
And he said vnto me, Sonne of man, goe, and enter into the house of Israel, and declare them my wordes.
5 Kwa kuwa hujatumwa kwa watu wenye maneno ya kushangaza au lugha ngumu, lakini kwa nyumba ya Israeli-
For thou art not sent to a people of an vnknowen tongue, or of an hard language, but to the house of Israel,
6 sio kwa taifa lenye nguvu ya maneno ya ajabu au lugha ngumu ambao maneno yao hutaweza kuyaelewa! Kama nikikutuma kwao, watakusikiliza.
Not to many people of an vnknowen tongue, or of an harde language, whose wordes thou canst not vnderstand: yet if I should sende thee to them, they would obey thee.
7 Lakini nyumba ya Israeli haitakuwa tayari kukusikiliza, kwa kuwa hawako tayari kunisikiliza mimi. Hivyo nyumba yote ya Israeli ni paji gumu na moyo mgumu.
But the house of Israel will not obey thee: for they will not obey me: yea, all the house of Israel are impudent and stiffe hearted.
8 Kumbe nimeufanya uso wako kama kaidi kama nyuso zao na paji lako kuwa gumu kama mapaji yao.
Beholde, I haue made thy face strong against their faces, and thy forehead harde against their foreheads.
9 Nimekufanya paji lako kama almasi, gumu kuliko jiwe la kiberiti! Usiwaogope wala kufadhaika kwa nyuso zao, kwa kuwa ni nyumba ya uasi.”
I haue made thy forehead as the adamant, and harder then the flint: feare them not therefore, neither be afraid at their lookes: for they are a rebellious house.
10 Kisha akanambia, “Mwana wa adamu, maneno yote niliyokutangazia-yachukue kwenye moyo wako na wasikize kwa sikio lako!
He said moreouer vnto me, Sonne of man, receiue in thine heart al my words that I speake vnto thee, and heare them with thine eares,
11 Kisha nenda kwa watumwa, kwa watu wako, na uzungumze nao. Waambie, 'Hivi ndivyo Bwana Yahwe asemavyo; iwapo watasikia au hapana.”
And goe and enter to them that are led away captiues vnto the children of thy people, and speake vnto them, and tell them, Thus saith the Lord God: but surely they will not heare, neither will they in deede cease.
12 Kisha Roho akaniinua juu, na nikasikia nyuma yangu sauti yenye tetemeko la aridhi: “Ubarikiwe utukufu wa Yahwe kutoka mahali pake!”
Then the spirite tooke me vp, and I heard behinde me a noise of a great russhing, saying, Blessed be ye glorie of the Lord out of his place.
13 Ilikuwa sauti ya mabawa ya viumbe hai vilipokuwa vikigusana kila kimoja, na sauti ya magurudumu ambayo yalikuwa pamoja na hivyo viumbe, na sauti ya tetemeko kubwa arithi.
I heard also the noyse of the wings of the beasts, that touched one another, and the ratling of the wheeles that were by them, euen a noyse of a great russhing.
14 Roho akaniinua juu na kunichukua, Nikaenda kwa uchungu katika hasira kali rohoni mwangu, kwa kuwa mkono wa Yahwe ulikuwa na nguvu ukigandamiza juu yangu!
So the spirit lift me vp, and tooke me away and I went in bitternesse, and indignation of my spirite, but the hand of the Lord was strong vpon me.
15 Hivyo nikaenda kwa watumwa huko Tel Abibu waliokuwa wakiishi karibu na Kebari Kanali, na niliishi miongoni mwao huko kwa mda wa miaka saba, kushinda kabisa katika mshangao.
Then I came to them that were led away captiues to Tel-abib, that dwelt by the riuer Chebar, and I sate where they sate, and remained there astonished among them seuen dayes.
16 Kisha ikatokea baada ya siku saba kwamba neno la Yahwe likanijia, likisema,
And at the ende of seuen dayes, the worde of the Lord came againe vnto me, saying,
17 “Mwana wa adamu, nimekufanya uwe mwangalizi kwa ajili ya nyumba ya Israeli, hivyo sikiliza neno kutoka kinywani mwangu, na uwapatie onyo langu.
Sonne of man, I haue made thee a watchman vnto the house of Israel: therefore heare the worde at my mouth, and giue them warning from me.
18 Nitakaposema kwa waovu, 'Utakufa hakika' na usimuonye au kuzungumza onyo kwa waovu kuhusu matendo yao maovu hivyo anaweza kuishi-yule muovu atakufa kwa ajili ya dhambi yake, lakini nitaitaka damu yake kutoka kwenye mkono wako.
When I shall say vnto the wicked, Thou shalt surely die, and thou giuest not him warning, nor speakest to admonish the wicked of his wicked way, that he may liue, the same wicked man shall die in his iniquitie: but his blood will I require at thine hande.
19 Lakini kama ukimuonya muovo, na asiuache uovu wake au kutoka matendo yake maovu, kisha atakufa kwa dhambi yake, lakini utaokoa maisha yako mwenyewe.
Yet if thou warne the wicked, and he turne not from his wickednesse, nor from his wicked way, he shall die in his iniquitie, but thou hast deliuered thy soule.
20 Kama mwenye haki ataicha haki yake na kutenda yasiyohaki, na nikaweka kizuizi mbele yake, atakufa. Kwasababu hukumuonya, atakufa katika dhambi yake, na sintokumbuka matendo ya haki aliyoyafanya, lakini nitaitaka damu yake kutoka kwenye mkono wako.
Likewise if a righteous man turne from his righteousnesse, and commit iniquitie, I will lay a stumbling blocke before him, and he shall die, because thou hast not giuen him warning: he shall die in his sinne, and his righteous deedes, which he hath done, shall not be remembred: but his blood will I require at thine hand.
21 Lakini kama ukimuonya mwenye mtu mwenye haki kuacha kufanya dhambi halafu akaacha kutenda dhambi, ataishi hakika tangu alipo unywa; na utakuwa umeokoa maisha yako mwenyewe.”
Neuerthelesse, if thou admonish that righteous man, that the righteous sinne not, and that he doeth not sinne, he shall liue because he is admonished: also thou hast deliuered thy soule.
22 Hivyo mkono wa Yahwe ulikuwa juu yangu huko, akanambia, “Inuka! nenda uwandani, na nitaongea na wewe huko!”
And the hande of the Lord was there vpon me, and he said vnto me, Arise, and goe into the fielde, and I will there talke with thee.
23 Nikainuka na kwenda uwandani, na huko utukufu wa Yahwe ulisimama, kama utukufu ambao niliokuwa nimeuona karibu na Kebari Kanali; hivyo nikaanguka kifudifudi.
So when I had risen vp, and gone foorth into the fielde, beholde, the glorie of the Lord stoode there, as the glorie which I sawe by the riuer Chebar, and I fell downe vpon my face.
24 Roho akaja kwangu na kusimama juu ya miguu yangu; akaongea na mimi, na kunambia, “Nenda na jifungie mwenyewe kwenye nyumba yako,
Then the Spirit entred into me, which set me vp vpon my feete, and spake vnto me, and said to me, Come, and shut thy selfe within thine house.
25 kwa sasa, mwana wa adamu, wataweka kamba juu yako na kukufunga ili usiweze kutoka nje miongoni mwao.
But thou, O sonne of man, beholde, they shall put bandes vpon thee, and shall binde thee with them, and thou shalt not goe out among them.
26 Nitaufanya ulimi wako ugandamane na paa ya mdomo wako, ili kwamba uwe kimya, na hutaweza kuwakemea, kwa kuwa ni nyumba ya waasi.
And I will make thy tongue cleaue to the roofe of thy mouth, that thou shalt be dume, and shalt not be to them as a man that rebuketh: for they are a rebellious house.
27 Lakini nitakapozungumza na wewe, nitafungua mdomo wako hivyo utawaambia, 'Hivi ndivyo Bwana Yahwe asemavyo.' Yeye asikiaye na asikie; yeye asiyesikia na asisikie, kwa kuwa wao ni nyumba ya kuasi!”
But when I shall haue spoken vnto thee, I will open thy mouth, and thou shalt say vnto them, Thus saith the Lord God, He that heareth, let him heare, and he that leaueth off, let him leaue: for they are a rebellious house.

< Ezekieli 3 >