< Ezekieli 27 >
1 Tena neno la Yahwe likanijia, kusema,
And it came [the] word of Yahweh to me saying.
2 “Sasa wewe, mwanadamu, anza kuomboleza kuhusiana na Tiro,
And you O son of humankind take up on Tyre a lamentation.
3 na mwambie Tiro, aishiye kwenye malango ya bahari, manahodha wa watu hata visiwa vingi, Bwana Yahwe asema hivi kwako: Tiro, umesema, mimi ni ukamilifu katika uzuri.'
And you will say to Tyre (that sits *Q(K)*) at [the] entrances of [the] sea [the] trader of the peoples to islands many thus he says [the] Lord Yahweh O Tyre you you have said I [am] perfect of beauty.
4 Mipaka yako iko kwenye moyo wa bahari; majengo yako yamekamilisha uzuri wako.
[were] in [the] heart of [the] seas Territories your builders your they perfected beauty your.
5 Wametengeneza mbao nene na pana kwa mvinje kutoka Mlima Hermoni; wamechukua mkangazi kutoka Lebanoni kuufanya mlingoti.
Fir trees from Senir they built of you all planks a cedar from Lebanon they took to make a mast on you.
6 Wametengeneza makasia yako kutoka kwenye mialo ya Bashani; wametengeza sitaha zako kwa mbao za mvinje kutoka Kitimu, na wametengeneza kwa pembe.
Oaks from Bashan they made oars your boards your they made ivory inlaid in pine from [the] islands of (Kittim. *Q(k)*)
7 Tanga zako zilikuwa za rangi za kitani kutoka Misri ambazo zilikuwa kama beramu!
Fine linen with colorful weaving from Egypt it was sail your to become of you a sail blue and purple from [the] islands of Elishah it was covering your.
8 Wale waliokuwa wakiishi Sidoni na Arvadi walikuwa wavuta makasia wako; wenye busara wa Tire walikuwa ndani yenu; walikuwa marubani wako.
[the] inhabitants of Sidon and Arvad they were rowers of you skillful [people] your O Tyre they were in you they [were] sailors your.
9 Mafundistadi wenye uzoefu wa hali ya juu kutoka Gabeli walijaza mishono; meli zote za bahari na mabaharia wao miongoni mwenu walikuwa wakiwabeba manahodha kwaajili ya biashara.
[the] elders of Gebal and wise [people] its they were in you [the] repairers of leaks your all [the] ships of the sea and mariners their they were in you to trade merchandise your.
10 Uajemi, Ludi, na Putu walikuwa katika jeshi lako, watu wako wa vita. Walining'iniza ngao na chapeo ndani yako; walionyesha uzuri wako.
Persia and Lud and Put they were in army your men of war your shield and helmet they hung up in you they they gave splendor your.
11 Watu wa Arvadi na Heleki katika jeshi lako walikuwa juu ya kuta zako wamekuzunguka, na watu wa Gamadi walikuwa kwenye minara yako. Walinin'giniza juu ngao zao juu ya kuta zako zote zilizokuzunguka! Wakaukamilisha uzuri wako.
[the] people of Arvad and Helech [were] on walls your all around and [the] Gammadites in towers your they were shields their they hung up on walls your all around they they perfected beauty your.
12 Tarshishi alikuwa mdau wa biashara pamoja nawe kwa sababu ya wingi wa utajiri wako wa kuuza mizigo: fedha, chuma, bati, na risasi. Walinunua na kuuza bidhaa za biashara!
Tarshish [was] trader your from [the] abundance of all wealth for silver iron tin and lead they exchanged wares your.
13 Yavani, Tubali, na Mesheki-waliwauza watumwa na katika vitu kutengeneza shaba. Walibeba bidhaa zako.
Javan Tubal and Meshech they [were] traders your for [the] life of human[s] and vessels of bronze they exchanged merchandise your.
14 Beth Togarma waliandaa farasi, farasi dume, na nyumbu kama kama bidhaa zako.
From Beth Togarmah horses and horsemen and mules they exchanged wares your.
15 Watu wa Dedani walikuwa wafanya biashara wako kwenye pwani nyingi. Bidhaa zilikuwa mkononi mwako; walikutumia pembe, pembe za ndovu, na mpingo kama ushuru!
[the] people of Dedan [were] traders your islands many [were] [the] merchandise of hand your horns of ivory (and ebony *Q(k)*) they brought tribute your.
16 Shamu alikuwa mchuuzi katika bidhaa zako nyingi; waliandaa zumaridi, zambarau, nguo zenye rangi mbali mbali, kitambaa kizuri, lulu, na kito chekundu cha thamani kama bidhaa zako.
Aram [was] trader your from [the] abundance of products your for turquoise purple and multicolored cloth and fine linen and corals and ruby they exchanged for wares your.
17 Yuda na nchi ya Israeli walikuwa wafanyabiashara pamoja nawe. Waliandaa ngano kutoka Minithi, keki, asali, mafuta, na lihamu kama bidhaa zako.
Judah and [the] land of Israel they [were] traders your for [the] wheat of Minnith and cake and honey and oil and balm they exchanged merchandise your.
18 Dameski alikuwa mfanya biashara wa bidhaa zako zote, za utajiri mkubwa mno, na ya divai ya Helboni na sufu ya Zahari.
Damascus [was] trader your in [the] abundance of products your from [the] abundance of all wealth for [the] wine of Helbon and wool of Zahar.
19 Dani na Yavani kutoka Uzali walikwandalia bidhaa ya chuma kilichofuliwa, na mdalasini, na mchai. Hivi vikawa bidhaa yako.
Vedan and Javan from Uzal for wares your they exchanged iron wrought cassia and calamus for merchandise your it was.
20 Dedani alikuwa mchuuzi katika nguo nzuri za kutandika.
Dedan [was] trader your for clothes of material for riding.
21 Arabuni na wakuu wote wa Kedari walikuwa wafanyabiashara pamoja nawe; walikuandalia wanakondoo, kondoo dume na mbuzi.
Arabia and all [the] princes of Kedar they [were] [the] traders of hand your for lambs and rams and goats for them traders your.
22 Wafanya biashara wa Sheba na Raama walikuja kukuuzia kila aina ya viungo vizuri katika vito vyote vya thamani; waliuza dhahabu kwa ajili ya bidhaa.
[the] traders of Sheba and Raamah they [were] traders your for [the] best of every spice and for every stone precious and gold they exchanged wares your.
23 Harani, Kane, na Adina walikuwa wafanya biashara pamoja nawe, karibu na Sheba, Ashuru, na Kilmadi.
Haran and Canneh and Eden [the] traders of Sheba Asshur Chilmad [was] trader your.
24 Hawa walikuwa wachuuzi wako mapambo ya joho ya nguo za urujuani pamoja na rangi zilibuniwa, na nguo zilizo sanifiwa vizuri katika sehemu zako za soko.
They [were] traders your (for beautiful garments *LA(bh)*) for garments of blue and multicolored cloth and for blankets of variegated cloth for ropes bound and made firm in market place your.
25 Merikebu za Tarshishi zilikuwa misafara ya bidhaa yako! Hivyo ulijaa, shehena nzito katika moyo wa bahari!
[the] ships of Tarshish [were] travelers your merchandise your and you were filled and you were honored exceedingly (in [the] heart of *LB(ah)*) [the] seas.
26 Wapiga makasia wako walikuleta kwenye bahari kuu mno; upepo wa mashariki umekuvunja kati yao.
On waters many they brought you the rowers you [the] wind of the east it broke you in [the] heart of [the] seas.
27 Utajiri wako, bidhaa, na mizigo ya biashara; wapiga makasia wako na marubani, na waunzi wa meli; wafanya biashara wako wa bidhaa na watu wote wa vita walio ndani yako, na jeshi lako-watazama kwenye kina cha bahari siku ya kuangamia kwako.
Wealth your and wares your merchandise your mariners your and sailors your [the] repairers of leaks your and [the] traders of merchandise your and all [the] men of war your who [were] in you and with all company your which [was] in [the] midst of you they will fall in [the] heart of [the] seas on [the] day of downfall your.
28 Miji iliyopo kwenye bahari sauti itatetemeka kulia kwa rubani zako;
To [the] sound of [the] outcry of sailors your they will quake pasturelands.
29 Wote wavutao kasia watashuka chini kutoka meli katika zao; wanamaji na marubani wote juu ya bahari watasimama juu ya nchi.
And they will come down from ships their all [those who] wield an oar mariners all [the] sailors of the sea to the land they will stand.
30 Kisha watakufanya kusikiliza sauti yao na kulia kwa uchungu; watarusha vumbi juu ya vichwa vyao. Watabingirika katika majivu.
And they will make heard on you voice their so they may cry out bitter so they may bring up dust on heads their in ash[es] they will roll.
31 Watanyo vichwa vyao upara kwa ajili yako na kujifunga wenyewe kwa nguo za magunia, na watalia kwa sauti.
And they will make bald because of you baldness and they will gird themselves sackcloth and they will weep because of you with bitterness of emotion wailing bitter.
32 Watakuinulia maombolezo ya kuomboleza kwa ajili yako na kuimba nyimbo za maombolezo juu yako, ni nani aliye kama Tiro, ambaye sasa ameletwa kunyamazishwa kati ya bahari?
And they will take up concerning you in wailing their a lamentation and they will lament on you who? [is] like Tyre like one silenced in [the] middle of the sea.
33 Wakati bidhaa yako ilipoenda ufukweni kutoka kwenye bahari, imewarithisha watu wengi; uliwatajirisha wafalme wa dunia kwa wingi wa utajiri wako mkubwa na bidhaa!
When went out wares your from [the] seas you satisfied peoples many by [the] abundance of wealth your and merchandise your you made rich [the] kings of [the] earth.
34 Lakini wakati ulipo vunjwavunjwa kwa bahari, kwa vilindi vya maji, bidhaa yako na wafanya kazi wako wote kuzama!
[the] time Being broken from [the] seas in [the] depths of [the] water merchandise your and all company your in [the] midst of you they have fallen.
35 Wote wakaao pwani walikuogopa, na wafalme wao kuvunjwa vunjwa katika kitisho! Nyuso zao zimetetemeka!
All [the] inhabitants of the islands they have been appalled on you and kings their they have shuddered shuddering they have been disconcerted faces.
36 Wafanya biashara wa meli wa watu wakuzomea; umekuwa tishio, na hutakuwepo tena milele.”
Traders among the peoples they have hissed on you terrors you have become and there not [will be] you until perpetuity.