< Ezekieli 27 >
1 Tena neno la Yahwe likanijia, kusema,
And there is a word of YHWH to me, saying,
2 “Sasa wewe, mwanadamu, anza kuomboleza kuhusiana na Tiro,
“And you, son of man, lift up a lamentation concerning Tyre, and you have said to Tyre:
3 na mwambie Tiro, aishiye kwenye malango ya bahari, manahodha wa watu hata visiwa vingi, Bwana Yahwe asema hivi kwako: Tiro, umesema, mimi ni ukamilifu katika uzuri.'
O dweller on the entrances of the sea, Merchant of the peoples to many islands, Thus said Lord YHWH: O Tyre, you have said, I [am] the perfection of beauty.
4 Mipaka yako iko kwenye moyo wa bahari; majengo yako yamekamilisha uzuri wako.
Your borders [are] in the heart of the seas, Your builders have perfected your beauty.
5 Wametengeneza mbao nene na pana kwa mvinje kutoka Mlima Hermoni; wamechukua mkangazi kutoka Lebanoni kuufanya mlingoti.
They have built of firs from Senir all your double-boarded ships for you, They have taken of cedars from Lebanon to make a mast for you,
6 Wametengeneza makasia yako kutoka kwenye mialo ya Bashani; wametengeza sitaha zako kwa mbao za mvinje kutoka Kitimu, na wametengeneza kwa pembe.
They made your oars of oaks from Bashan, They have made your bench of ivory, A branch of Ashurim from islands of Chittim.
7 Tanga zako zilikuwa za rangi za kitani kutoka Misri ambazo zilikuwa kama beramu!
Your sail has been of fine linen with embroidery from Egypt, To be for your ensign, Your covering has been of blue and purple from islands of Elishah.
8 Wale waliokuwa wakiishi Sidoni na Arvadi walikuwa wavuta makasia wako; wenye busara wa Tire walikuwa ndani yenu; walikuwa marubani wako.
Inhabitants of Sidon and Arvad have been rowers for you, Your wise men, O Tyre, have been in you, They [are] your pilots.
9 Mafundistadi wenye uzoefu wa hali ya juu kutoka Gabeli walijaza mishono; meli zote za bahari na mabaharia wao miongoni mwenu walikuwa wakiwabeba manahodha kwaajili ya biashara.
The elderly of Gebal and its wise men have been in you, Strengthening your breach; All ships of the sea and their mariners, Have been in you, to trade your merchandise.
10 Uajemi, Ludi, na Putu walikuwa katika jeshi lako, watu wako wa vita. Walining'iniza ngao na chapeo ndani yako; walionyesha uzuri wako.
Persia and Lud and Phut Have been in your forces—your men of war. They hung up shield and helmet in you, They have given out your honor.
11 Watu wa Arvadi na Heleki katika jeshi lako walikuwa juu ya kuta zako wamekuzunguka, na watu wa Gamadi walikuwa kwenye minara yako. Walinin'giniza juu ngao zao juu ya kuta zako zote zilizokuzunguka! Wakaukamilisha uzuri wako.
The sons of Arvad, and your force, [Are] on your walls all around, And short swordsmen have been in your towers, They have hung up their shields on your walls all around, They have perfected your beauty.
12 Tarshishi alikuwa mdau wa biashara pamoja nawe kwa sababu ya wingi wa utajiri wako wa kuuza mizigo: fedha, chuma, bati, na risasi. Walinunua na kuuza bidhaa za biashara!
Tarshish [is] your merchant, Because of the abundance of all wealth, They have given silver, iron, tin, and lead [for] your wares.
13 Yavani, Tubali, na Mesheki-waliwauza watumwa na katika vitu kutengeneza shaba. Walibeba bidhaa zako.
Javan, Tubal, and Meshech—they [are] your merchants, They have given [the] soul of man, and vessels of bronze, [for] your merchandise.
14 Beth Togarma waliandaa farasi, farasi dume, na nyumbu kama kama bidhaa zako.
Those of the house of Togarmah, They have given horses, and riding steeds, and mules [for] your wares.
15 Watu wa Dedani walikuwa wafanya biashara wako kwenye pwani nyingi. Bidhaa zilikuwa mkononi mwako; walikutumia pembe, pembe za ndovu, na mpingo kama ushuru!
Sons of Dedan [are] your merchants, Many islands [are] the market of your hand, They sent back horns of ivory and ebony [for] your reward.
16 Shamu alikuwa mchuuzi katika bidhaa zako nyingi; waliandaa zumaridi, zambarau, nguo zenye rangi mbali mbali, kitambaa kizuri, lulu, na kito chekundu cha thamani kama bidhaa zako.
Aram [is] your merchant, Because of the abundance of your works, They have given emerald, purple, and embroidery, And fine linen, and coral, and agate for your wares.
17 Yuda na nchi ya Israeli walikuwa wafanyabiashara pamoja nawe. Waliandaa ngano kutoka Minithi, keki, asali, mafuta, na lihamu kama bidhaa zako.
Judah and the land of Israel—they [are] your merchants, They have given wheat of Minnith, and Pannag, And honey, and oil, and balm [for] your merchandise.
18 Dameski alikuwa mfanya biashara wa bidhaa zako zote, za utajiri mkubwa mno, na ya divai ya Helboni na sufu ya Zahari.
Damascus [is] your merchant, For the abundance of your works, Because of the abundance of all wealth, For wine of Helbon, and white wool.
19 Dani na Yavani kutoka Uzali walikwandalia bidhaa ya chuma kilichofuliwa, na mdalasini, na mchai. Hivi vikawa bidhaa yako.
Dan and Javan go about with your wares, They have given shining iron, cassia, and cane, It has been in your merchandise.
20 Dedani alikuwa mchuuzi katika nguo nzuri za kutandika.
Dedan [is] your merchant, For clothes of freedom for riding.
21 Arabuni na wakuu wote wa Kedari walikuwa wafanyabiashara pamoja nawe; walikuandalia wanakondoo, kondoo dume na mbuzi.
Arabia, and all princes of Kedar, They [are] the traders of your hand, For lambs, and rams, and male goats, In these your merchants.
22 Wafanya biashara wa Sheba na Raama walikuja kukuuzia kila aina ya viungo vizuri katika vito vyote vya thamani; waliuza dhahabu kwa ajili ya bidhaa.
Merchants of Sheba and Raamah—they [are] your merchants, They have given the chief of all spices, And every precious stone, and gold [for] your wares.
23 Harani, Kane, na Adina walikuwa wafanya biashara pamoja nawe, karibu na Sheba, Ashuru, na Kilmadi.
Haran, and Canneh, and Eden, merchants of Sheba, Asshur—Chilmad—[are] your merchants,
24 Hawa walikuwa wachuuzi wako mapambo ya joho ya nguo za urujuani pamoja na rangi zilibuniwa, na nguo zilizo sanifiwa vizuri katika sehemu zako za soko.
They [are] your merchants for perfect things, For wrappings of blue, and embroidery, And for treasuries of rich apparel, With cords bound and girded, for your merchandise,
25 Merikebu za Tarshishi zilikuwa misafara ya bidhaa yako! Hivyo ulijaa, shehena nzito katika moyo wa bahari!
Ships of Tarshish are journeying [with] your merchandise for you, And you are filled and honored greatly, In the heart of the seas.
26 Wapiga makasia wako walikuleta kwenye bahari kuu mno; upepo wa mashariki umekuvunja kati yao.
Those rowing you have brought you into great waters, The east wind has broken you in the heart of the seas.
27 Utajiri wako, bidhaa, na mizigo ya biashara; wapiga makasia wako na marubani, na waunzi wa meli; wafanya biashara wako wa bidhaa na watu wote wa vita walio ndani yako, na jeshi lako-watazama kwenye kina cha bahari siku ya kuangamia kwako.
Your wealth and your wares, Your merchandise, your mariners, And your pilots, strengtheners of your breach, And the traders of your merchandise, And all your men of war, who [are] in you, And in all your assembly that [is] in your midst, Fall into the heart of the seas in the day of your fall,
28 Miji iliyopo kwenye bahari sauti itatetemeka kulia kwa rubani zako;
At the voice of the cry of your pilots the outskirts shake.
29 Wote wavutao kasia watashuka chini kutoka meli katika zao; wanamaji na marubani wote juu ya bahari watasimama juu ya nchi.
And all handling an oar come down from their ships, Mariners [and] all the pilots of the sea stand on the land,
30 Kisha watakufanya kusikiliza sauti yao na kulia kwa uchungu; watarusha vumbi juu ya vichwa vyao. Watabingirika katika majivu.
And have sounded with their voice for you, And cry bitterly, and cause dust to go up on their heads, They roll themselves in ashes;
31 Watanyo vichwa vyao upara kwa ajili yako na kujifunga wenyewe kwa nguo za magunia, na watalia kwa sauti.
And they have made themselves bald for you, And they have girded on sackcloth, And they have wept for you, In bitterness of soul—a bitter mourning.
32 Watakuinulia maombolezo ya kuomboleza kwa ajili yako na kuimba nyimbo za maombolezo juu yako, ni nani aliye kama Tiro, ambaye sasa ameletwa kunyamazishwa kati ya bahari?
And their sons have lifted up a lamentation for you, And they have lamented over you, Who [is] as Tyre? As the cut-off one in the midst of the sea?
33 Wakati bidhaa yako ilipoenda ufukweni kutoka kwenye bahari, imewarithisha watu wengi; uliwatajirisha wafalme wa dunia kwa wingi wa utajiri wako mkubwa na bidhaa!
With the outgoing of your wares from the seas, You have filled many peoples, With the abundance of your riches, and your merchandise, You have enriched [the] kings of earth.
34 Lakini wakati ulipo vunjwavunjwa kwa bahari, kwa vilindi vya maji, bidhaa yako na wafanya kazi wako wote kuzama!
At the time of [your] being broken by the seas in the depths of the waters, Your merchandise and all your assembly have fallen in your midst.
35 Wote wakaao pwani walikuogopa, na wafalme wao kuvunjwa vunjwa katika kitisho! Nyuso zao zimetetemeka!
All inhabitants of the islands have been astonished at you, And their kings have been severely afraid, They have been troubled in countenance.
36 Wafanya biashara wa meli wa watu wakuzomea; umekuwa tishio, na hutakuwepo tena milele.”
Merchants among the peoples have shrieked for you, You have been terrors, and you are not—for all time!”