< Ezekieli 27 >

1 Tena neno la Yahwe likanijia, kusema,
A message from the Lord came to me, saying,
2 “Sasa wewe, mwanadamu, anza kuomboleza kuhusiana na Tiro,
“Son of man, sing a funeral song for Tyre.
3 na mwambie Tiro, aishiye kwenye malango ya bahari, manahodha wa watu hata visiwa vingi, Bwana Yahwe asema hivi kwako: Tiro, umesema, mimi ni ukamilifu katika uzuri.'
Tell Tyre, the city that stands at the gateway to the sea, supplying goods to many overseas nations, that this is what the Lord God says: Tyre, you say to yourself, ‘I'm so beautiful!’
4 Mipaka yako iko kwenye moyo wa bahari; majengo yako yamekamilisha uzuri wako.
Your borders extend far across the sea. Your builders put you together perfectly like a beautiful ship.
5 Wametengeneza mbao nene na pana kwa mvinje kutoka Mlima Hermoni; wamechukua mkangazi kutoka Lebanoni kuufanya mlingoti.
They built you with pine timber from Mount Hermon. They used a cedar from Lebanon to make your mast.
6 Wametengeneza makasia yako kutoka kwenye mialo ya Bashani; wametengeza sitaha zako kwa mbao za mvinje kutoka Kitimu, na wametengeneza kwa pembe.
They made your oars with oaks from Bashan. They had wood from the island of Cyprus brought to make your deck and inlaid it with ivory.
7 Tanga zako zilikuwa za rangi za kitani kutoka Misri ambazo zilikuwa kama beramu!
They made your sail with the best linen from Egypt—this was your flag that everyone recognized. They used cloth dyed blue and purple from the coastlands of Elishah to make your awnings.
8 Wale waliokuwa wakiishi Sidoni na Arvadi walikuwa wavuta makasia wako; wenye busara wa Tire walikuwa ndani yenu; walikuwa marubani wako.
Men from Sidon and Arvad did the rowing in your ship. You had your own skilled sailors from Tyre.
9 Mafundistadi wenye uzoefu wa hali ya juu kutoka Gabeli walijaza mishono; meli zote za bahari na mabaharia wao miongoni mwenu walikuwa wakiwabeba manahodha kwaajili ya biashara.
Expert craftsmen from Gebal were onboard to repair any leaks. All the other ships at sea came to trade with you and their sailors bartered for your goods.
10 Uajemi, Ludi, na Putu walikuwa katika jeshi lako, watu wako wa vita. Walining'iniza ngao na chapeo ndani yako; walionyesha uzuri wako.
Men from Persia, Lydia, and Put were soldiers in your army. They lived among you, hanging up their shields and helmets with you, making you famous.
11 Watu wa Arvadi na Heleki katika jeshi lako walikuwa juu ya kuta zako wamekuzunguka, na watu wa Gamadi walikuwa kwenye minara yako. Walinin'giniza juu ngao zao juu ya kuta zako zote zilizokuzunguka! Wakaukamilisha uzuri wako.
Men of Arvad and Helech defended all your city walls, while those from Gammad protected your towers. They hung their shields all around your walls. They made you so successful.
12 Tarshishi alikuwa mdau wa biashara pamoja nawe kwa sababu ya wingi wa utajiri wako wa kuuza mizigo: fedha, chuma, bati, na risasi. Walinunua na kuuza bidhaa za biashara!
Tarshish traded with you because you had so much of everything. They paid for your goods with silver, iron, tin, and lead.
13 Yavani, Tubali, na Mesheki-waliwauza watumwa na katika vitu kutengeneza shaba. Walibeba bidhaa zako.
Greece, Tubal, and Meshech traded with you. They bought your goods, paying with slaves and objects made of bronze.
14 Beth Togarma waliandaa farasi, farasi dume, na nyumbu kama kama bidhaa zako.
People from Beth-togarmah traded horses, war horses, and mules for your goods.
15 Watu wa Dedani walikuwa wafanya biashara wako kwenye pwani nyingi. Bidhaa zilikuwa mkononi mwako; walikutumia pembe, pembe za ndovu, na mpingo kama ushuru!
People from Dedan traded with you. You had marketplaces in many coastal areas where the people bartered with you using ivory tusks and ebony wood.
16 Shamu alikuwa mchuuzi katika bidhaa zako nyingi; waliandaa zumaridi, zambarau, nguo zenye rangi mbali mbali, kitambaa kizuri, lulu, na kito chekundu cha thamani kama bidhaa zako.
The Arameans traded with you because you had so much merchandise. They provided turquoise, purple cloth, embroidery, fine linen, coral, and red jasper in exchange for your goods.
17 Yuda na nchi ya Israeli walikuwa wafanyabiashara pamoja nawe. Waliandaa ngano kutoka Minithi, keki, asali, mafuta, na lihamu kama bidhaa zako.
Judah and the country of Israel traded with you, paying you with wheat from Minnith, pastries and honey, olive oil and balm in return for your goods.
18 Dameski alikuwa mfanya biashara wa bidhaa zako zote, za utajiri mkubwa mno, na ya divai ya Helboni na sufu ya Zahari.
Because you had many different products, in fact so much of everything, Damascus traded with you using wine from Helbon, wool from Zahar.
19 Dani na Yavani kutoka Uzali walikwandalia bidhaa ya chuma kilichofuliwa, na mdalasini, na mchai. Hivi vikawa bidhaa yako.
Vedan and Javan from Izal bought your goods using wrought iron, cassia, and sweet calamus.
20 Dedani alikuwa mchuuzi katika nguo nzuri za kutandika.
Dedan traded with you, providing riding blankets.
21 Arabuni na wakuu wote wa Kedari walikuwa wafanyabiashara pamoja nawe; walikuandalia wanakondoo, kondoo dume na mbuzi.
Arabia and all the leaders of Kedar traded with you, supplying lambs, rams, and goats.
22 Wafanya biashara wa Sheba na Raama walikuja kukuuzia kila aina ya viungo vizuri katika vito vyote vya thamani; waliuza dhahabu kwa ajili ya bidhaa.
The merchants of Sheba and Raamah traded with you, exchanging gold, the very best spices, and precious stones for your goods.
23 Harani, Kane, na Adina walikuwa wafanya biashara pamoja nawe, karibu na Sheba, Ashuru, na Kilmadi.
Haran, Canneh, and Eden traded with you, as did Sheba, Asshur, and Chilmad.
24 Hawa walikuwa wachuuzi wako mapambo ya joho ya nguo za urujuani pamoja na rangi zilibuniwa, na nguo zilizo sanifiwa vizuri katika sehemu zako za soko.
In your marketplaces they traded with you, providing the finest blue clothing, embroidery, carpets made with different colored threads, and strong ropes of twisted strands.
25 Merikebu za Tarshishi zilikuwa misafara ya bidhaa yako! Hivyo ulijaa, shehena nzito katika moyo wa bahari!
Trade ships from Tarshish transported your goods. You were like a ship sailing the sea, filled with heavy cargo.
26 Wapiga makasia wako walikuleta kwenye bahari kuu mno; upepo wa mashariki umekuvunja kati yao.
Your rowers took you a long way out on the water, but the east wind broke you apart in there in the open ocean.
27 Utajiri wako, bidhaa, na mizigo ya biashara; wapiga makasia wako na marubani, na waunzi wa meli; wafanya biashara wako wa bidhaa na watu wote wa vita walio ndani yako, na jeshi lako-watazama kwenye kina cha bahari siku ya kuangamia kwako.
You've lost everything! You wealth, your goods, your cargo, your crew of sailors, officers, and repairmen, your traders and all the soldiers you had, along with everyone else on board, fall into the depths of the sea on the day of your shipwreck.
28 Miji iliyopo kwenye bahari sauti itatetemeka kulia kwa rubani zako;
The land around shakes when your sailors scream.
29 Wote wavutao kasia watashuka chini kutoka meli katika zao; wanamaji na marubani wote juu ya bahari watasimama juu ya nchi.
All the rowers abandon their ships. The sailors and all the ships' officers stand on the shore.
30 Kisha watakufanya kusikiliza sauti yao na kulia kwa uchungu; watarusha vumbi juu ya vichwa vyao. Watabingirika katika majivu.
They shout out for you and burst out crying. They mourn for you by throwing dust on their heads and rolling in ashes.
31 Watanyo vichwa vyao upara kwa ajili yako na kujifunga wenyewe kwa nguo za magunia, na watalia kwa sauti.
They shave their heads for you and clothe themselves in sackcloth. They weep for you, crying out in agony and heartfelt mourning
32 Watakuinulia maombolezo ya kuomboleza kwa ajili yako na kuimba nyimbo za maombolezo juu yako, ni nani aliye kama Tiro, ambaye sasa ameletwa kunyamazishwa kati ya bahari?
As they weep and wail over you, they sing a funeral song for you: ‘Who could compare to Tyre, now destroyed out in the sea?
33 Wakati bidhaa yako ilipoenda ufukweni kutoka kwenye bahari, imewarithisha watu wengi; uliwatajirisha wafalme wa dunia kwa wingi wa utajiri wako mkubwa na bidhaa!
You made many people happy when they received your goods from far across the sea. You made the kings of the earth rich with all your valuable goods and products.
34 Lakini wakati ulipo vunjwavunjwa kwa bahari, kwa vilindi vya maji, bidhaa yako na wafanya kazi wako wote kuzama!
Now you have been shipwrecked by the sea, sunk in deep water, and your cargo and your people have gone down with you.
35 Wote wakaao pwani walikuogopa, na wafalme wao kuvunjwa vunjwa katika kitisho! Nyuso zao zimetetemeka!
Everyone living on the coastlands is shocked at what happened to you. Their kings are horrified; their faces twisted with fear.
36 Wafanya biashara wa meli wa watu wakuzomea; umekuwa tishio, na hutakuwepo tena milele.”
The traders of the nations hiss at you in derision; disaster has brought you down and you're finished forever.”

< Ezekieli 27 >