< Ezekieli 27 >
1 Tena neno la Yahwe likanijia, kusema,
And the word of the Lord came to me saying,
2 “Sasa wewe, mwanadamu, anza kuomboleza kuhusiana na Tiro,
And thou, son of man, take up a lamentation against Sor;
3 na mwambie Tiro, aishiye kwenye malango ya bahari, manahodha wa watu hata visiwa vingi, Bwana Yahwe asema hivi kwako: Tiro, umesema, mimi ni ukamilifu katika uzuri.'
and thou shalt say to Sor that dwells at the entrance of the sea, to the mart of the nations coming from many islands, Thus saith the Lord to Sor; Thou hast said, I have clothed myself with my beauty.
4 Mipaka yako iko kwenye moyo wa bahari; majengo yako yamekamilisha uzuri wako.
In the heart of the sea thy sons have put beauty upon thee for Beelim.
5 Wametengeneza mbao nene na pana kwa mvinje kutoka Mlima Hermoni; wamechukua mkangazi kutoka Lebanoni kuufanya mlingoti.
Cedar in Senir was employed for thee in building: boards of cypress timber were taken out of Libanus, and wood to make thee masts of fir.
6 Wametengeneza makasia yako kutoka kwenye mialo ya Bashani; wametengeza sitaha zako kwa mbao za mvinje kutoka Kitimu, na wametengeneza kwa pembe.
They made thine oars [of wood] out of the land of Basan; thy sacred utensils they made of ivory, thy shady houses of wood from the isles of Chetiim.
7 Tanga zako zilikuwa za rangi za kitani kutoka Misri ambazo zilikuwa kama beramu!
Fine linen with embroidery from Egypt supplied the couch, to put honour upon thee, and to clothe thee with blue and purple from the isles of Elisai; and they became thy coverings.
8 Wale waliokuwa wakiishi Sidoni na Arvadi walikuwa wavuta makasia wako; wenye busara wa Tire walikuwa ndani yenu; walikuwa marubani wako.
And thy princes were the dwellers in Sidon, and the Aradians were thy rowers: thy wise men, O Sor, who were in thee, these were thy pilots.
9 Mafundistadi wenye uzoefu wa hali ya juu kutoka Gabeli walijaza mishono; meli zote za bahari na mabaharia wao miongoni mwenu walikuwa wakiwabeba manahodha kwaajili ya biashara.
The elders of the Biblians, and their wise men, who were in thee, these helped thy counsel: and all the ships of the sea and their rowers traded for thee to the utmost west.
10 Uajemi, Ludi, na Putu walikuwa katika jeshi lako, watu wako wa vita. Walining'iniza ngao na chapeo ndani yako; walionyesha uzuri wako.
Persians and Lydians and Libyans were in thine army: thy warriors hung in thee shields and helmets; these gave [thee] thy glory.
11 Watu wa Arvadi na Heleki katika jeshi lako walikuwa juu ya kuta zako wamekuzunguka, na watu wa Gamadi walikuwa kwenye minara yako. Walinin'giniza juu ngao zao juu ya kuta zako zote zilizokuzunguka! Wakaukamilisha uzuri wako.
The sons of the Aradians and thine army were upon the walls; there were guards in thy towers: they hung their quivers on thy battlements round about; these completed thy beauty.
12 Tarshishi alikuwa mdau wa biashara pamoja nawe kwa sababu ya wingi wa utajiri wako wa kuuza mizigo: fedha, chuma, bati, na risasi. Walinunua na kuuza bidhaa za biashara!
The Carthaginians were thy merchants because of the abundance of all thy strength; they furnished thy market with silver, and gold, and iron, and tin, and lead.
13 Yavani, Tubali, na Mesheki-waliwauza watumwa na katika vitu kutengeneza shaba. Walibeba bidhaa zako.
Greece, both the whole [world], and the adjacent coasts, these traded with thee in the persons of men, and they gave [as] thy merchandise vessels of brass.
14 Beth Togarma waliandaa farasi, farasi dume, na nyumbu kama kama bidhaa zako.
Out of the house of Thogarma horses and horsemen furnished the market.
15 Watu wa Dedani walikuwa wafanya biashara wako kwenye pwani nyingi. Bidhaa zilikuwa mkononi mwako; walikutumia pembe, pembe za ndovu, na mpingo kama ushuru!
The sons of the Rhodians were thy merchants; from the islands they multiplied thy merchandise, [even] elephants' teeth: and to them that came in thou didst return thy prices,
16 Shamu alikuwa mchuuzi katika bidhaa zako nyingi; waliandaa zumaridi, zambarau, nguo zenye rangi mbali mbali, kitambaa kizuri, lulu, na kito chekundu cha thamani kama bidhaa zako.
[even] men [as] thy merchandise, from the multitude of thy trading [population], myrrh and embroidered works from Tharsis: Ramoth also and Chorchor furnished thy market.
17 Yuda na nchi ya Israeli walikuwa wafanyabiashara pamoja nawe. Waliandaa ngano kutoka Minithi, keki, asali, mafuta, na lihamu kama bidhaa zako.
Juda and the children of Israel, these were thy merchants; in the sale of corn and ointments and cassia: and they gave the best honey, and oil, and resin, to thy trading [population].
18 Dameski alikuwa mfanya biashara wa bidhaa zako zote, za utajiri mkubwa mno, na ya divai ya Helboni na sufu ya Zahari.
[The people of] Damascus were thy merchants by reason of the abundance of all thy power; wine out of Chelbon, and wool from Miletus; and they brought wine into thy market.
19 Dani na Yavani kutoka Uzali walikwandalia bidhaa ya chuma kilichofuliwa, na mdalasini, na mchai. Hivi vikawa bidhaa yako.
Out of Asel [came] wrought iron, and there is the sound of wheels among thy trading [population].
20 Dedani alikuwa mchuuzi katika nguo nzuri za kutandika.
[The people of] Daedan were thy merchants, with choice cattle for chariots.
21 Arabuni na wakuu wote wa Kedari walikuwa wafanyabiashara pamoja nawe; walikuandalia wanakondoo, kondoo dume na mbuzi.
Arabia and all the princes of Kedar, these were thy traders with thee, [bringing] camels, and lambs, and rams, in which they trade with thee.
22 Wafanya biashara wa Sheba na Raama walikuja kukuuzia kila aina ya viungo vizuri katika vito vyote vya thamani; waliuza dhahabu kwa ajili ya bidhaa.
The merchants of Sabba and Ramma, these were thy merchants, with choice spices, and precious stones: and they brought gold to thy market.
23 Harani, Kane, na Adina walikuwa wafanya biashara pamoja nawe, karibu na Sheba, Ashuru, na Kilmadi.
Charra, and Chanaa, these were thy merchants: Assur, and Charman, were thy merchants:
24 Hawa walikuwa wachuuzi wako mapambo ya joho ya nguo za urujuani pamoja na rangi zilibuniwa, na nguo zilizo sanifiwa vizuri katika sehemu zako za soko.
bringing [for] merchandise blue, and choice stores bound with cords, and cypress wood.
25 Merikebu za Tarshishi zilikuwa misafara ya bidhaa yako! Hivyo ulijaa, shehena nzito katika moyo wa bahari!
Ships were thy merchants, in abundance, with thy trading [population]: and thou wast filled and very heavily loaded in the heart of the sea.
26 Wapiga makasia wako walikuleta kwenye bahari kuu mno; upepo wa mashariki umekuvunja kati yao.
Thy rowers have brought thee into great waters: the south wind has broken thee in the heart of the sea.
27 Utajiri wako, bidhaa, na mizigo ya biashara; wapiga makasia wako na marubani, na waunzi wa meli; wafanya biashara wako wa bidhaa na watu wote wa vita walio ndani yako, na jeshi lako-watazama kwenye kina cha bahari siku ya kuangamia kwako.
Thy forces, and thy gain, and that of thy traders, and thy rowers, and thy pilots, and thy counselors, and they that traffic with thee, and all thy warriors that are in thee: and all thy company in the midst of thee shall perish in the heart of the sea, in the day of thy fall.
28 Miji iliyopo kwenye bahari sauti itatetemeka kulia kwa rubani zako;
At the cry of thy voice thy pilots shall be greatly terrified.
29 Wote wavutao kasia watashuka chini kutoka meli katika zao; wanamaji na marubani wote juu ya bahari watasimama juu ya nchi.
And all the rowers and the mariners shall come down from the ships, and the pilots of the sea shall stand on the land.
30 Kisha watakufanya kusikiliza sauti yao na kulia kwa uchungu; watarusha vumbi juu ya vichwa vyao. Watabingirika katika majivu.
And they shall wail over thee with their voice, and cry bitterly, and put earth on their heads, and spread ashes under them.
31 Watanyo vichwa vyao upara kwa ajili yako na kujifunga wenyewe kwa nguo za magunia, na watalia kwa sauti.
32 Watakuinulia maombolezo ya kuomboleza kwa ajili yako na kuimba nyimbo za maombolezo juu yako, ni nani aliye kama Tiro, ambaye sasa ameletwa kunyamazishwa kati ya bahari?
And their sons shall take up a [lament] for thee, even a lamentation for Sor, [saying],
33 Wakati bidhaa yako ilipoenda ufukweni kutoka kwenye bahari, imewarithisha watu wengi; uliwatajirisha wafalme wa dunia kwa wingi wa utajiri wako mkubwa na bidhaa!
How large a reward hast thou gained from the sea? thou hast filled nations out of thine abundance; and out of thy mixed merchandise thou hast enriched all the kings of the earth.
34 Lakini wakati ulipo vunjwavunjwa kwa bahari, kwa vilindi vya maji, bidhaa yako na wafanya kazi wako wote kuzama!
Now art thou broken in the sea, thy traders are in the deep water, and all thy company in the midst of thee: all thy rowers have fallen.
35 Wote wakaao pwani walikuogopa, na wafalme wao kuvunjwa vunjwa katika kitisho! Nyuso zao zimetetemeka!
All the dwellers in the islands have mourned over thee, and their kings have been utterly amazed, and their countenance has wept.
36 Wafanya biashara wa meli wa watu wakuzomea; umekuwa tishio, na hutakuwepo tena milele.”
Merchants from the nations have hissed at thee; thou art utterly destroyed, and shalt not be any more for ever.