< Ezekieli 26 >

1 Hivyo ilikuwa katika mwaka wa kumi na moja, siku ya kwanza ya mwezi, lile neno la Yahwe likanijia, kusema,
La onzième année, le premier du mois, la parole de l'Éternel me fut adressée, en ces termes:
2 “Mwanadamu, kwa sababu Tiro amesema juu ya Yerusalemuu, 'Aha! Malango ya watu waliovunjika! Amenigeukia; Nitajazwa kwa sababu ameharibika.'
« Fils d'homme, parce que Tyr a dit de Jérusalem: « Ah! elle est brisée! Celle qui était la porte des peuples m'a été rendue.
3 Kwa hiyo Bwana Yahwe asema hivi, 'Tazama! Niko juu yako, Tiro, na nitayainua mataifa mengi juu yako kama bahari iiunuavyo mawimbi yake.
C'est pourquoi le Seigneur Yahvé dit: Voici, j'en veux à toi, Tyr, et je ferai monter contre toi de nombreuses nations, comme la mer fait monter ses flots.
4 Wataziharibu kuta za Tiro na kuiangusha chini minara yao. Nitafagia mavumbi yake mbali na kumfanya kama jiwe tupu.
Elles détruiront les murs de Tyr, elles abattront ses tours. Je raclerai sa poussière, et je ferai d'elle un rocher nu.
5 Atakuwa sehemu ya kuwekea nyavu kati ya bahari, kwa kuwa nimesema hilo-hivi ndivyo Bwana Yahwe asemavyo-na atakuwa mateka kwa ajili ya mataifa.
Elle sera un lieu où l'on étendra les filets au milieu de la mer, car j'ai parlé, dit le Seigneur Yahvé. Elle sera le butin des nations.
6 Binti zake walioko mashambani watachinjwa kwa panga, na watajua kwamba mimi ni Yahwe.'
Ses filles, qui sont aux champs, seront tuées par l'épée. Alors ils sauront que je suis Yahvé.
7 Kwa kuwa hivi ndivyo Bwana Yahwe asemavyo: Tazama, kutoka kaskazini namleta Nebukadreza mfalme wa Babeli, mfalme wa wafalme, dhidi ya Tiro, pamoja na farasi na magari ya farasi, na pamoja na waendesha farasi na watu wengi.
Car le Seigneur Yahvé dit: « Voici que je vais faire venir du nord sur Tyr Nabuchodonosor, roi de Babylone, roi des rois, avec des chevaux, des chars, des cavaliers, et une armée nombreuse.
8 Atawaua binti zako katika shamba. Ataweka kazi ya boma na kujenga ulaghai dhidi ya kuta zako na kuziinua ngao dhidi yao.
Il tuera par l'épée tes filles dans les champs. Il fera contre toi des retranchements, il élèvera contre toi un monticule, il dressera contre toi le bouclier.
9 Ataweka vyombo vya kubomolea dhidi ya kuta zako, na vyombo vyake vitaanguka chini ya minara yako.
Il dressera ses voitures contre tes murs, et il démolira tes tours avec ses haches.
10 Farasi zake zitakuwa nyingi kwamba mavumbi yao yatawafunika. Kuta zako zitatikisika kwa mlio wa waendesha farasi, magurudumu, na magari ya farasi. Wakati atakapoingia malango yako, ataingia kama watu waingiavyo kwenye mji ambao kuta zimebomolewa.
A cause de l'abondance de ses chevaux, leur poussière te couvrira. Tes murs trembleront au bruit des cavaliers, des chariots et des chars, quand il entrera par tes portes, comme on entre dans une ville ouverte.
11 Kwato za farasi zake zitaikanyaga mitaa yako yote. Atawaua watu wako kwa upanga na nguzo za uweza wako zitaanguka chini.
Il foulera toutes tes rues avec les sabots de ses chevaux. Il tuera ton peuple par l'épée. Les piliers de ta force tomberont à terre.
12 Watauteka nyara utajiri wako na bidhaa iliyoporwa. Watabomoa kuta zako na kuziharibu nyumba zako za kifahari. Mawe yako, mbao zako, na kokoto watazitupa kwenye maji.
Ils pilleront tes richesses et feront une proie de tes marchandises. Ils abattront tes murs et détruiront tes maisons de plaisance. Ils déposeront tes pierres, ton bois et ta poussière au milieu des eaux.
13 Nitaikomesha sauti ya nyimbo zako. Sauti ya vinubi haitasikika tena.
Je ferai cesser le bruit de vos chants. On n'entendra plus le son de tes harpes.
14 Nitakufanya jiwe tupu, utakuwa mahali ambapo nyavu zitasambazwa kuzikausha. Hutajengwa tena, kwa kuwa mimi, Bwana Yahwe nimesema-hivi ndivyo Bwana Yahwe asemavyo.
Je ferai de toi un rocher nu. Tu seras un lieu où l'on étendra les filets. On ne te bâtira plus, car c'est moi, Yahvé, qui ai parlé, dit le Seigneur Yahvé.
15 Bwana Yahwe amwambia hivi Tiro, 'Je visiwa havitatetemeka kwa mlio wa kuanguka kwako, na pamoja na watakaogumia kwa jeraha wakati machinjio mabaya yatakapokuwa kati yako?
Le Seigneur Yahvé dit à Tyr: « Les îles ne trembleront-elles pas au bruit de ta chute, quand les blessés gémiront, quand le carnage sera fait en toi?
16 Kisha wakuu wote wa bahari watakaposhuka kutoka kwenye viti vyao vya enzi na kuvua mavazi yao rasmi na kutupa mavazi yaliyonakshiwa. Watavaa wenyewe kwa kutetemeka, wataketi chini na kutetemeka kila wakati, na wataogopa kwa sababu yako.
Alors tous les princes de la mer descendront de leurs trônes, ils déposeront leurs robes, ils se dépouilleront de leurs vêtements brodés. Ils se revêtiront de tremblements. Ils s'assiéront à terre, ils trembleront à chaque instant, et ils seront stupéfaits de toi.
17 Watainua maombolezo juu yako na kukwambia, umekuwaje, uliyekuwa umekaliwa na manahodha wa meli, umeharibika. Mji mashuhuri ulikuwa imara sana-sasa umetoka kwenye bahari. Wale wanaoishi ndani yake wanaotia hofu kuhusu wenyewe juu ya kila mmoja aliyeishi karibu nao.
Ils se lamenteront sur toi, et te diront, « Comment vous êtes détruits, qui étaient habités par des hommes de la mer, la ville renommée, qui était fort dans la mer, elle et ses habitants, qui a fait régner la terreur sur tous ceux qui vivaient là! »
18 Sasa fukwe zitatetemeka katika siku ya kuanguka kwako. Visiwa katika bahari vimeogofya, kwa sababu umekufa.'
Maintenant, les îles trembleront au jour de ta chute. Oui, les îles qui sont dans la mer seront consternées par votre départ.
19 Kwa kuwa Bwana Yahwe asema hivi: wakati nitakapokufanya wewe mji kuwa ukiwa, kama miji mingine ambayo haikaliwi, wakati nitakapoviinua vilindi dhidi yako, na wakati maji makuu yatakapokufunika,
Car le Seigneur Yahvé dit: « Quand je ferai de toi une ville déserte, comme les villes qui ne sont pas habitées, quand je ferai monter sur toi l'abîme et que les grandes eaux te couvriront,
20 kisha nitakushusha chini kwenda kwa watu wa nyakati za zamani, kama wengingine walioenda chini kwenye shimo; kwa kuwa nitakufanya uishi katika falme za chini za dunia kama uharibifu wa nyakati za zamani. Kwa sababu hii hutarudi na kusimama katika nchi ya walio hai.
je te ferai descendre avec ceux qui descendent dans la fosse, vers les peuples d'autrefois, et je te ferai habiter dans les bas-fonds de la terre, dans les lieux déserts d'autrefois, avec ceux qui descendent dans la fosse, afin que tu ne sois pas habitée; et je mettrai la gloire dans le pays des vivants.
21 Nitaweka janga juu yako, na hutakuwepo tena milele. Kisha utatafutwa, lakini hutapatikana milele tena-hivi ndivyo Bwana Yahwe asemavyo.”
Je ferai de toi une terreur, et tu n'auras plus d'existence. On te cherchera, mais on ne te retrouvera jamais, dit le Seigneur Yahvé. »

< Ezekieli 26 >