< Ezekieli 26 >

1 Hivyo ilikuwa katika mwaka wa kumi na moja, siku ya kwanza ya mwezi, lile neno la Yahwe likanijia, kusema,
It happened in the eleventh year, in the first day of the month, that the word of the LORD came to me, saying,
2 “Mwanadamu, kwa sababu Tiro amesema juu ya Yerusalemuu, 'Aha! Malango ya watu waliovunjika! Amenigeukia; Nitajazwa kwa sababu ameharibika.'
"Son of man, because Tyre has said against Jerusalem, 'Aha, she is broken: the gate of the peoples; she is turned to me; I shall be replenished, now that she is laid waste':
3 Kwa hiyo Bwana Yahwe asema hivi, 'Tazama! Niko juu yako, Tiro, na nitayainua mataifa mengi juu yako kama bahari iiunuavyo mawimbi yake.
therefore thus says the LORD, 'Look, I am against you, Tyre, and will cause many nations to come up against you, as the sea causes its waves to come up.'
4 Wataziharibu kuta za Tiro na kuiangusha chini minara yao. Nitafagia mavumbi yake mbali na kumfanya kama jiwe tupu.
They shall destroy the walls of Tyre, and break down her towers: I will also scrape her dust from her, and make her a bare rock.
5 Atakuwa sehemu ya kuwekea nyavu kati ya bahari, kwa kuwa nimesema hilo-hivi ndivyo Bwana Yahwe asemavyo-na atakuwa mateka kwa ajili ya mataifa.
She shall be a place for the spreading of nets in the midst of the sea; for I have spoken it," says the LORD; "and she shall become a spoil to the nations.
6 Binti zake walioko mashambani watachinjwa kwa panga, na watajua kwamba mimi ni Yahwe.'
Her daughters who are in the field shall be slain with the sword: and they shall know that I am the LORD.
7 Kwa kuwa hivi ndivyo Bwana Yahwe asemavyo: Tazama, kutoka kaskazini namleta Nebukadreza mfalme wa Babeli, mfalme wa wafalme, dhidi ya Tiro, pamoja na farasi na magari ya farasi, na pamoja na waendesha farasi na watu wengi.
"For thus says the LORD: 'Look, I will bring on Tyre Nebuchadnezzar king of Babylon, king of kings, from the north, with horses, and with chariots, and with horsemen, and a company, and many people.
8 Atawaua binti zako katika shamba. Ataweka kazi ya boma na kujenga ulaghai dhidi ya kuta zako na kuziinua ngao dhidi yao.
He shall kill your daughters in the field with the sword; and he shall make forts against you, and cast up a mound against you, and raise up the buckler against you.
9 Ataweka vyombo vya kubomolea dhidi ya kuta zako, na vyombo vyake vitaanguka chini ya minara yako.
He shall set his battering engines against your walls, and with his axes he shall break down your towers.
10 Farasi zake zitakuwa nyingi kwamba mavumbi yao yatawafunika. Kuta zako zitatikisika kwa mlio wa waendesha farasi, magurudumu, na magari ya farasi. Wakati atakapoingia malango yako, ataingia kama watu waingiavyo kwenye mji ambao kuta zimebomolewa.
By reason of the abundance of his horses their dust shall cover you: your walls shall shake at the noise of the horsemen, and of the wagons, and of the chariots, when he shall enter into your gates, as men enter into a city in which is made a breach.
11 Kwato za farasi zake zitaikanyaga mitaa yako yote. Atawaua watu wako kwa upanga na nguzo za uweza wako zitaanguka chini.
With the hoofs of his horses shall he tread down all your streets; he shall kill your people with the sword; and the pillars of your strength shall go down to the ground.
12 Watauteka nyara utajiri wako na bidhaa iliyoporwa. Watabomoa kuta zako na kuziharibu nyumba zako za kifahari. Mawe yako, mbao zako, na kokoto watazitupa kwenye maji.
They shall make a spoil of your riches, and make a prey of your merchandise; and they shall break down your walls, and destroy your pleasant houses; and they shall lay your stones and your timber and your dust in the midst of the waters.
13 Nitaikomesha sauti ya nyimbo zako. Sauti ya vinubi haitasikika tena.
I will cause the noise of your songs to cease; and the sound of your harps shall be no more heard.
14 Nitakufanya jiwe tupu, utakuwa mahali ambapo nyavu zitasambazwa kuzikausha. Hutajengwa tena, kwa kuwa mimi, Bwana Yahwe nimesema-hivi ndivyo Bwana Yahwe asemavyo.
I will make you a bare rock; you shall be a place for the spreading of nets; you shall be built no more: for I the LORD have spoken it,' says the LORD.
15 Bwana Yahwe amwambia hivi Tiro, 'Je visiwa havitatetemeka kwa mlio wa kuanguka kwako, na pamoja na watakaogumia kwa jeraha wakati machinjio mabaya yatakapokuwa kati yako?
"Thus says the LORD to Tyre: 'Shall not the islands shake at the sound of your fall, when the wounded groan, when the slaughter is made in the midst of you?
16 Kisha wakuu wote wa bahari watakaposhuka kutoka kwenye viti vyao vya enzi na kuvua mavazi yao rasmi na kutupa mavazi yaliyonakshiwa. Watavaa wenyewe kwa kutetemeka, wataketi chini na kutetemeka kila wakati, na wataogopa kwa sababu yako.
Then all the princes of the sea shall come down from their thrones, and lay aside their robes, and strip off their embroidered garments: they shall clothe themselves with trembling; they shall sit on the ground, and shall tremble every moment, and be astonished at you.
17 Watainua maombolezo juu yako na kukwambia, umekuwaje, uliyekuwa umekaliwa na manahodha wa meli, umeharibika. Mji mashuhuri ulikuwa imara sana-sasa umetoka kwenye bahari. Wale wanaoishi ndani yake wanaotia hofu kuhusu wenyewe juu ya kila mmoja aliyeishi karibu nao.
They shall take up a lamentation over you, and tell you, "How you are destroyed, you have vanished from the seas, the renowned city, who was strong in the sea, she and her inhabitants, who caused their terror to be on all who lived there.
18 Sasa fukwe zitatetemeka katika siku ya kuanguka kwako. Visiwa katika bahari vimeogofya, kwa sababu umekufa.'
Now shall the islands tremble in the day of your fall; yes, the islands that are in the sea shall be dismayed at your departure."'
19 Kwa kuwa Bwana Yahwe asema hivi: wakati nitakapokufanya wewe mji kuwa ukiwa, kama miji mingine ambayo haikaliwi, wakati nitakapoviinua vilindi dhidi yako, na wakati maji makuu yatakapokufunika,
"For thus says the LORD: 'When I shall make you a desolate city, like the cities that are not inhabited; when I shall bring up the deep on you, and the great waters shall cover you;
20 kisha nitakushusha chini kwenda kwa watu wa nyakati za zamani, kama wengingine walioenda chini kwenye shimo; kwa kuwa nitakufanya uishi katika falme za chini za dunia kama uharibifu wa nyakati za zamani. Kwa sababu hii hutarudi na kusimama katika nchi ya walio hai.
then will I bring you down with those who descend into the pit, to the people of old time, and will make you to dwell in the lower parts of the earth, in the places that are desolate of old, with those who go down to the pit, that you be not inhabited; and I will set glory in the land of the living:
21 Nitaweka janga juu yako, na hutakuwepo tena milele. Kisha utatafutwa, lakini hutapatikana milele tena-hivi ndivyo Bwana Yahwe asemavyo.”
I will make you a terror, and you shall no more have any being; though you are sought for, yet you will never be found again,' says the LORD."

< Ezekieli 26 >