< Ezekieli 26 >

1 Hivyo ilikuwa katika mwaka wa kumi na moja, siku ya kwanza ya mwezi, lile neno la Yahwe likanijia, kusema,
And it comes to pass, in the eleventh year, on the first of the month, there has been a word of YHWH to me, saying, “Son of man,
2 “Mwanadamu, kwa sababu Tiro amesema juu ya Yerusalemuu, 'Aha! Malango ya watu waliovunjika! Amenigeukia; Nitajazwa kwa sababu ameharibika.'
Because that Tyre has said of Jerusalem: Aha, she has been broken, The doors of the peoples, She has turned around to me, I am filled—she has been laid waste,
3 Kwa hiyo Bwana Yahwe asema hivi, 'Tazama! Niko juu yako, Tiro, na nitayainua mataifa mengi juu yako kama bahari iiunuavyo mawimbi yake.
Therefore, thus said Lord YHWH: Behold, I [am] against you, O Tyre, And have caused many nations to come up against you, As the sea causes its billows to come up.
4 Wataziharibu kuta za Tiro na kuiangusha chini minara yao. Nitafagia mavumbi yake mbali na kumfanya kama jiwe tupu.
And they have destroyed the walls of Tyre, And they have broken down her towers, And I have scraped her dust from her, And made her for a clear place of a rock.
5 Atakuwa sehemu ya kuwekea nyavu kati ya bahari, kwa kuwa nimesema hilo-hivi ndivyo Bwana Yahwe asemavyo-na atakuwa mateka kwa ajili ya mataifa.
She is a spreading place of nets in the midst of the sea, For I have spoken,” A declaration of Lord YHWH, “And she has been for a spoil to nations.
6 Binti zake walioko mashambani watachinjwa kwa panga, na watajua kwamba mimi ni Yahwe.'
And her daughters who [are] in the field, are slain by sword, And they have known that I [am] YHWH,”
7 Kwa kuwa hivi ndivyo Bwana Yahwe asemavyo: Tazama, kutoka kaskazini namleta Nebukadreza mfalme wa Babeli, mfalme wa wafalme, dhidi ya Tiro, pamoja na farasi na magari ya farasi, na pamoja na waendesha farasi na watu wengi.
For thus said Lord YHWH: “Behold, I am bringing Nebuchadnezzar king of Babylon to Tyre, From the north—a king of kings, With horse, and with chariot, and with horsemen, Even an assembly, and a numerous people.
8 Atawaua binti zako katika shamba. Ataweka kazi ya boma na kujenga ulaghai dhidi ya kuta zako na kuziinua ngao dhidi yao.
He slays your daughters in the field by sword, And he has made a fort against you, And has poured out a mound against you, And has raised a buckler against you.
9 Ataweka vyombo vya kubomolea dhidi ya kuta zako, na vyombo vyake vitaanguka chini ya minara yako.
And he places a battering-ram before him against your walls, And he breaks your towers with his weapons.
10 Farasi zake zitakuwa nyingi kwamba mavumbi yao yatawafunika. Kuta zako zitatikisika kwa mlio wa waendesha farasi, magurudumu, na magari ya farasi. Wakati atakapoingia malango yako, ataingia kama watu waingiavyo kwenye mji ambao kuta zimebomolewa.
From the abundance of his horses their dust cover you, From the noise of horseman, and wheel, and rider, Your walls shake, in his coming into your gates, As the coming into a city that has been broken-up.
11 Kwato za farasi zake zitaikanyaga mitaa yako yote. Atawaua watu wako kwa upanga na nguzo za uweza wako zitaanguka chini.
He treads all your out-places with [the] hooves of his horses, He slays your people by sword, And the pillars of your strength come down to the earth.
12 Watauteka nyara utajiri wako na bidhaa iliyoporwa. Watabomoa kuta zako na kuziharibu nyumba zako za kifahari. Mawe yako, mbao zako, na kokoto watazitupa kwenye maji.
And they have spoiled your wealth, And they have plundered your merchandise, And they have thrown down your walls, And they break down your desirable houses, And your stones, and your wood, and your dust, They place in the midst of the waters.
13 Nitaikomesha sauti ya nyimbo zako. Sauti ya vinubi haitasikika tena.
And I have caused the noise of your songs to cease, And the voice of your harps is heard no more.
14 Nitakufanya jiwe tupu, utakuwa mahali ambapo nyavu zitasambazwa kuzikausha. Hutajengwa tena, kwa kuwa mimi, Bwana Yahwe nimesema-hivi ndivyo Bwana Yahwe asemavyo.
And I have given you up for a clear place of a rock, You are a spreading-place of nets, You are not built up anymore, For I, YHWH, have spoken,” A declaration of Lord YHWH.
15 Bwana Yahwe amwambia hivi Tiro, 'Je visiwa havitatetemeka kwa mlio wa kuanguka kwako, na pamoja na watakaogumia kwa jeraha wakati machinjio mabaya yatakapokuwa kati yako?
Thus said Lord YHWH to Tyre: “Do not—from the noise of your fall, In the groaning of the wounded, In the slaying of the slaughter in your midst—The islands shake?
16 Kisha wakuu wote wa bahari watakaposhuka kutoka kwenye viti vyao vya enzi na kuvua mavazi yao rasmi na kutupa mavazi yaliyonakshiwa. Watavaa wenyewe kwa kutetemeka, wataketi chini na kutetemeka kila wakati, na wataogopa kwa sababu yako.
And all princes of the sea have come down from off their thrones, And they have turned their robes aside, And strip off their embroidered garments, They put on trembling, They sit on the earth, And they have trembled every moment, And they have been astonished at you,
17 Watainua maombolezo juu yako na kukwambia, umekuwaje, uliyekuwa umekaliwa na manahodha wa meli, umeharibika. Mji mashuhuri ulikuwa imara sana-sasa umetoka kwenye bahari. Wale wanaoishi ndani yake wanaotia hofu kuhusu wenyewe juu ya kila mmoja aliyeishi karibu nao.
And have lifted up a lamentation for you, And said to you: How you have perished, That are inhabited from the seas, The praised city, that was strong in the sea, She and her inhabitants, Who put their terror on all her inhabitants!
18 Sasa fukwe zitatetemeka katika siku ya kuanguka kwako. Visiwa katika bahari vimeogofya, kwa sababu umekufa.'
Now the islands tremble [on the] day of your fall; The islands that [are] in the sea have been troubled at your outgoing.”
19 Kwa kuwa Bwana Yahwe asema hivi: wakati nitakapokufanya wewe mji kuwa ukiwa, kama miji mingine ambayo haikaliwi, wakati nitakapoviinua vilindi dhidi yako, na wakati maji makuu yatakapokufunika,
For thus said Lord YHWH: “In My making you a city dried up, Like cities that have not been inhabited, In bringing up the deep against you, Then the great waters have covered you.
20 kisha nitakushusha chini kwenda kwa watu wa nyakati za zamani, kama wengingine walioenda chini kwenye shimo; kwa kuwa nitakufanya uishi katika falme za chini za dunia kama uharibifu wa nyakati za zamani. Kwa sababu hii hutarudi na kusimama katika nchi ya walio hai.
And I have caused you to go down, With those going down to the pit, To the people of old, And I have caused you to dwell In the lower parts of the earth—in ancient ruins, With those going down to the pit, So that you are not inhabited, And I have given beauty in the land of the living.
21 Nitaweka janga juu yako, na hutakuwepo tena milele. Kisha utatafutwa, lakini hutapatikana milele tena-hivi ndivyo Bwana Yahwe asemavyo.”
I make you a terror, and you are not, And you are sought, and are not found anymore—for all time,” A declaration of Lord YHWH!

< Ezekieli 26 >