< Ezekieli 25 >

1 Kisha neno la Yahwe likanijia, kusema,
Et la parole du Seigneur me vint, disant:
2 “Mwanadamu, weka uso wako juu ya watu wa Amoni na tabiri juu yao.
Fils de l'homme, tourne ta face contre les fils d'Ammon, et prophétise contre eux.
3 Waambie watu wa Amoni, 'Sikiliza neno la Bwana Yahwe. Hivi ndivyo Bwana Yahwe asemavyo: Kwa sababu umesema, “Aha!” juu ya patakatifu pangu wakati palipotiwa unajisi, na juu ya nchi ya Israeli wakati ilipokuwa ukiwa, na juu ya nyumba ya Yuda wakati walipoenda utumwani,
Et dis aux fils d'Ammon: Écoutez la parole du Seigneur; ainsi parle le Seigneur: En punition de ce que vous vous êtes réjouis contre mes choses saintes, parce qu'elles ont été profanées, et contre Israël, parce qu'il a été détruit, et contre la maison de Juda, parce qu'elle a été emmenée en captivité;
4 kwa hiyo, tazama, nitakupatia kwa watu katika mashariki kama milki yao. Watafanya kambi juu yako na kuweka mahema miongoni mwako. Watakula matunda yako na watakunywa maziwa yako.
En punition de cela, je vous livre en héritage aux fils de Cédem, et ils séjourneront chez toi, avec leurs bagages, et ils y dresseront leurs tentes; ils mangeront tes fruits et ils boiront ton lait.
5 Nitamfanya Raba malisho ya ngamia na watu wa Amoni shamba la mifugo. Kisha utajua yakwamba mimi ni Yahwe.
Et je ferai de la ville d'Ammon un pâturage pour leurs chameaux, et des fils d'Ammon un pâturage pour leurs brebis, et vous saurez que je suis le Seigneur.
6 Kwa kuwa Bwana Yahwe asema hivi: Umepigia makofi mikono yako na kupiga chapa miguu yako, na kufurahi pamoja na dharau ndani yako dhidi ya nchi ya Israeli.
Car voici ce que dit le Seigneur: En punition de ce que tu as battu des mains et frappé du pied, et de ce que tu t'es réjoui en ton âme contre la terre d'Israël,
7 Kwa hiyo, tazama! Nitanyoosha mkono wangu na kukupatia kama mateka kwa mataifa. Nitakukatilia mbali kutoka watu na kukuangamiza kutoka miongoni mwa nchi! Nitakuharibu, na utajua yakwamba mimi ni Yahwe.'
En punition de cela, j'étendrai sur toi ma main, et je te livrerai en proie aux nations, et je te détruirai parmi les peuples, et je t'anéantirai, et tu sauras que je suis le Seigneur.
8 Bwana Yahwe asema hivi, 'Kwa sababu Moabu na Seiri husema “Tazama! Nyumba ya Yuda ni kama kila taifa jingine.”
Voici ce que dit le Seigneur: En punition de ce que Moab a dit: La maison d'Israël n'est-elle point maintenant comme toutes les nations?
9 Kwa hiyo, tazama! ntafungua miteremko ya Moabu, kuanzia kwenye miji yake juu ya mpaka-uzuri wa Beth Yeshimothi, Baal Meoni, na Kiriathaimu-
En punition de cela, voilà que je vais briser l'épaule de Moab, loin de ses villes frontières, sa terre choisie, la maison de Béthasimuth, située sur la fontaine de la ville maritime.
10 kwa watu wa mashariki waliokuwa juu ya watu wa Amoni. Nitawapatia kama milki ili kwamba watu wa Amoni hawatakumbukwa miongoni mwa mataifa.
J'ai envoyé les fils de Cédem contre les fils d'Ammon, pour qu'ils en fassent leur héritage, et qu'il ne reste plus de souvenir des fils d'Ammon:
11 Hivyo nitafanya hukumu juu ya Moabu, na watajua yakwamba mimi ni Yahwe.'
Et je tirerai aussi vengeance de Moab, et ils sauront que je suis le Seigneur.
12 Bwana Yahwe asema hivi, Edomu amelipiza kisasi juu ya nyumba ya Yuda na amefanya makosa katika kufanya hivyo.
Voici ce que dit le Seigneur: En punition de ce qu'a fait l'Idumée, qui, en châtiant la maison de Juda, s'est souvenue de sa propre haine, et s'est elle-même vengée;
13 Kwa hiyo, Bwana Yahwe asema hivi: Nitaunyoosha mkono wangu juu ya Edomu na kumharibu kila mtu na wanyama huko. Nitawaharibu, sehemu ya ukiwa, kutoka Temani hata Dedani. Wataanguka kwa upanga.
À cause de cela, voici ce que dit le Seigneur: J'étendrai aussi la main sur l'Idumée, et j'y exterminerai les hommes et le bétail, et j'en ferai un désert; et ceux de Théman que l'on poursuivra tomberont sous le glaive.
14 Nitaweka kisasi changu juu ya Edomu kwa mkono wa watu wangu Israeli, na watafanya kwa Edomu kulingana na hasira yangu na ghadhabu yangu, na wakitajua kisasi changu-hivi ndivyo Bwana Yahwe asemavyo.'
Et je punirai l'Idumée par les mains de mon peuple d'Israël, et ils traiteront l'Idumée selon ma colère et ma fureur, et ils connaîtront ma vengeance, dit le Seigneur.
15 Bwana Yahwe asema hivi, 'Wafilisti wamelipiza kisasi pamoja na uovu na kutoka ndani yao wamejaribu kuiharibu Yuda tena na tena.
À cause de cela, voici ce que dit le Seigneur: En punition de ce que les Philistins, en châtiant mon peuple, ont fait revivre leur propre vengeance, et se sont enorgueillis en leur âme de les faire périr jusqu'au dernier;
16 Basi hivi ndivyo Bwana Yahwe asemavyo: Tazam! Nitanyoosha mkono wangu dhidi ya Wafilisti, na nitakalia mbali Wakerethi na kuwaharibu mabaki yaliyobaki karibu na pwani.
À cause de cela, ainsi dit le Seigneur: Voilà que j'étendrai ma main sur les étrangers, et j'exterminerai les Crétois, et je détruirai le reste des habitants de la côte.
17 Kwa kuwa nitalipiza kisasi kikubwa dhidi yao pamoja na matendo ya ghadhabu kubwa ya adhabu, hivyo watajua yakwamba mimi ni Yahwe, nitakapolipiza kisasi juu yao.”'
Et je les frapperai de mes grandes vengeances, et ils sauront que je suis le Seigneur, quand ma vengeance tombera sur eux.

< Ezekieli 25 >