< Ezekieli 25 >

1 Kisha neno la Yahwe likanijia, kusema,
A message from the Lord came to me, saying,
2 “Mwanadamu, weka uso wako juu ya watu wa Amoni na tabiri juu yao.
“Son of man, face towards the Ammonites and prophesy against them.
3 Waambie watu wa Amoni, 'Sikiliza neno la Bwana Yahwe. Hivi ndivyo Bwana Yahwe asemavyo: Kwa sababu umesema, “Aha!” juu ya patakatifu pangu wakati palipotiwa unajisi, na juu ya nchi ya Israeli wakati ilipokuwa ukiwa, na juu ya nyumba ya Yuda wakati walipoenda utumwani,
Tell the Ammonites to listen to the message from the Lord God, for this is what the Lord God says: Because you said, ‘Oh good!’ when my sanctuary was made unclean, when the country of Israel was turned into a wasteland, and when the people of Judah were taken into exile,
4 kwa hiyo, tazama, nitakupatia kwa watu katika mashariki kama milki yao. Watafanya kambi juu yako na kuweka mahema miongoni mwako. Watakula matunda yako na watakunywa maziwa yako.
this is why I will make you subject to the people of the East. They will make camp and set up their tents right where you live. They will eat your fruit and drink your milk.
5 Nitamfanya Raba malisho ya ngamia na watu wa Amoni shamba la mifugo. Kisha utajua yakwamba mimi ni Yahwe.
I will make Rabbah a camel pasture, and Ammon a sheep-pen. Then you will know that I am the Lord.
6 Kwa kuwa Bwana Yahwe asema hivi: Umepigia makofi mikono yako na kupiga chapa miguu yako, na kufurahi pamoja na dharau ndani yako dhidi ya nchi ya Israeli.
For this is what the Lord God says: Because you clapped your hands and stamped your feet in a celebration of hate over what happened to Israel,
7 Kwa hiyo, tazama! Nitanyoosha mkono wangu na kukupatia kama mateka kwa mataifa. Nitakukatilia mbali kutoka watu na kukuangamiza kutoka miongoni mwa nchi! Nitakuharibu, na utajua yakwamba mimi ni Yahwe.'
this is why I will reach out and attack you, and hand you over to be looted by other nations. I will wipe you out so completely that you will no longer exist as a nation. I will destroy you, and then you will know that I am the Lord.
8 Bwana Yahwe asema hivi, 'Kwa sababu Moabu na Seiri husema “Tazama! Nyumba ya Yuda ni kama kila taifa jingine.”
This is what the Lord God says: Because the people of Moab and Seir said, ‘Look, the people of Judah are just like everybody else,’
9 Kwa hiyo, tazama! ntafungua miteremko ya Moabu, kuanzia kwenye miji yake juu ya mpaka-uzuri wa Beth Yeshimothi, Baal Meoni, na Kiriathaimu-
that's why I will open Moab's border to attack, including Beth-jeshimoth, Baal-meon, and Kiriathaim, the country's famous cities.
10 kwa watu wa mashariki waliokuwa juu ya watu wa Amoni. Nitawapatia kama milki ili kwamba watu wa Amoni hawatakumbukwa miongoni mwa mataifa.
I will hand Moab over to the people of the East for them to rule so that will no longer exist as a nation just like the Ammonites.
11 Hivyo nitafanya hukumu juu ya Moabu, na watajua yakwamba mimi ni Yahwe.'
This is how I'm going to punish the Moabites, and they will know that I am the Lord.
12 Bwana Yahwe asema hivi, Edomu amelipiza kisasi juu ya nyumba ya Yuda na amefanya makosa katika kufanya hivyo.
This is what the Lord God says: Because Edom committed serious sins by taking vicious revenge on the people of Judah,
13 Kwa hiyo, Bwana Yahwe asema hivi: Nitaunyoosha mkono wangu juu ya Edomu na kumharibu kila mtu na wanyama huko. Nitawaharibu, sehemu ya ukiwa, kutoka Temani hata Dedani. Wataanguka kwa upanga.
this is why the Lord God says: I will reach out to attack Edom and destroy all its people and animals. I will turn it into a wasteland. All the way from Teman in the north to Dedan in the south they will die by the sword.
14 Nitaweka kisasi changu juu ya Edomu kwa mkono wa watu wangu Israeli, na watafanya kwa Edomu kulingana na hasira yangu na ghadhabu yangu, na wakitajua kisasi changu-hivi ndivyo Bwana Yahwe asemavyo.'
I will take revenge on the Edomites through my people Israel. They will deal with the Edomites so that they experience my anger. Then they will know what my vengeance is like, declares the Lord God.
15 Bwana Yahwe asema hivi, 'Wafilisti wamelipiza kisasi pamoja na uovu na kutoka ndani yao wamejaribu kuiharibu Yuda tena na tena.
This is what the Lord God says: Because the Philistines in their hatred repeatedly took revenge on Judah, trying to destroy the people,
16 Basi hivi ndivyo Bwana Yahwe asemavyo: Tazam! Nitanyoosha mkono wangu dhidi ya Wafilisti, na nitakalia mbali Wakerethi na kuwaharibu mabaki yaliyobaki karibu na pwani.
this is why the Lord God says: Watch out! I'm going to reach out to attack the Philistines, and I will wipe out the Kerethites and destroy those who are left along the coast.
17 Kwa kuwa nitalipiza kisasi kikubwa dhidi yao pamoja na matendo ya ghadhabu kubwa ya adhabu, hivyo watajua yakwamba mimi ni Yahwe, nitakapolipiza kisasi juu yao.”'
My revenge against them will be severe as I punish them in my anger. Then they will know that I am the Lord, when they experience my anger.”

< Ezekieli 25 >