< Ezekieli 25 >
1 Kisha neno la Yahwe likanijia, kusema,
And the word of the Lord came to me, saying:
2 “Mwanadamu, weka uso wako juu ya watu wa Amoni na tabiri juu yao.
Son of man, set thy face against the children of Ammon, and thou shalt prophesy of them.
3 Waambie watu wa Amoni, 'Sikiliza neno la Bwana Yahwe. Hivi ndivyo Bwana Yahwe asemavyo: Kwa sababu umesema, “Aha!” juu ya patakatifu pangu wakati palipotiwa unajisi, na juu ya nchi ya Israeli wakati ilipokuwa ukiwa, na juu ya nyumba ya Yuda wakati walipoenda utumwani,
And thou shalt say to the children of Ammon: Hear ye the word of the Lord God: Thus saith the Lord God: Because thou hast said: Ha, ha, upon my sanctuary, because it was profaned: and upon the land of Israel, because it was laid waste: and upon the house of Juda, because they are led into captivity:
4 kwa hiyo, tazama, nitakupatia kwa watu katika mashariki kama milki yao. Watafanya kambi juu yako na kuweka mahema miongoni mwako. Watakula matunda yako na watakunywa maziwa yako.
Therefore will I deliver thee to the men of the east for an inheritance, and they shall place their sheepcotes in thee, and shall set up their tents in thee: they shall eat thy fruits: and they shall drink thy milk.
5 Nitamfanya Raba malisho ya ngamia na watu wa Amoni shamba la mifugo. Kisha utajua yakwamba mimi ni Yahwe.
And I will make Rabbath a stable for camels, and the children of Ammon a couching place for flocks: and you shall know that I am the Lord.
6 Kwa kuwa Bwana Yahwe asema hivi: Umepigia makofi mikono yako na kupiga chapa miguu yako, na kufurahi pamoja na dharau ndani yako dhidi ya nchi ya Israeli.
For thus saith the Lord God: Because thou hast clapped thy hands and stamped with thy foot, and hast rejoiced with all thy heart against the land of Israel:
7 Kwa hiyo, tazama! Nitanyoosha mkono wangu na kukupatia kama mateka kwa mataifa. Nitakukatilia mbali kutoka watu na kukuangamiza kutoka miongoni mwa nchi! Nitakuharibu, na utajua yakwamba mimi ni Yahwe.'
Therefore behold I: will stretch forth my hand upon thee, and will deliver thee to be the spoil of nations, and will cut thee off from among the people, and destroy thee out of the lands, and break thee in pieces: and thou shalt know that I am the Lord.
8 Bwana Yahwe asema hivi, 'Kwa sababu Moabu na Seiri husema “Tazama! Nyumba ya Yuda ni kama kila taifa jingine.”
Thus saith the Lord God: Because Moab and Seir have said: Behold the house of Juda is like all other nations:
9 Kwa hiyo, tazama! ntafungua miteremko ya Moabu, kuanzia kwenye miji yake juu ya mpaka-uzuri wa Beth Yeshimothi, Baal Meoni, na Kiriathaimu-
Therefore behold I will open the shoulder of Moab from the cities, from his cities, I say, and his borders, the noble cities of the land of Bethiesimoth, and Beelmeon, and Cariathaim,
10 kwa watu wa mashariki waliokuwa juu ya watu wa Amoni. Nitawapatia kama milki ili kwamba watu wa Amoni hawatakumbukwa miongoni mwa mataifa.
To the people of the east with the children of Ammon, and I will give it them for an inheritance: that there may be no more any remembrance of the children of Ammon among the nations.
11 Hivyo nitafanya hukumu juu ya Moabu, na watajua yakwamba mimi ni Yahwe.'
And I will execute judgments in Moab: and they shall know that I am the Lord.
12 Bwana Yahwe asema hivi, Edomu amelipiza kisasi juu ya nyumba ya Yuda na amefanya makosa katika kufanya hivyo.
Thus saith the Lord God: Because Edom hath taken vengeance to revenge herself of the children of Juda, and hath greatly offended, and hath sought revenge of them:
13 Kwa hiyo, Bwana Yahwe asema hivi: Nitaunyoosha mkono wangu juu ya Edomu na kumharibu kila mtu na wanyama huko. Nitawaharibu, sehemu ya ukiwa, kutoka Temani hata Dedani. Wataanguka kwa upanga.
Therefore thus saith the Lord God: I will stretch forth my hand upon Edom, and will take away out of it man and beast, and will make it desolate from the south: and they that are in Dedan shall fall by the sword.
14 Nitaweka kisasi changu juu ya Edomu kwa mkono wa watu wangu Israeli, na watafanya kwa Edomu kulingana na hasira yangu na ghadhabu yangu, na wakitajua kisasi changu-hivi ndivyo Bwana Yahwe asemavyo.'
And I will lay my vengeance upon Edom by the hand of my people Israel: and they shall do in Edom according to my wrath, and my fury: and they shall know my vengeance, saith the Lord God.
15 Bwana Yahwe asema hivi, 'Wafilisti wamelipiza kisasi pamoja na uovu na kutoka ndani yao wamejaribu kuiharibu Yuda tena na tena.
Thus saith the Lord God: Because the Philistines have taken vengeance, and have revenged themselves with all their mind, destroying and satisfying old enmities:
16 Basi hivi ndivyo Bwana Yahwe asemavyo: Tazam! Nitanyoosha mkono wangu dhidi ya Wafilisti, na nitakalia mbali Wakerethi na kuwaharibu mabaki yaliyobaki karibu na pwani.
Therefore thus saith the Lord God: Behold I will stretch forth my hand upon the Philistines, and will kill the killers, and will destroy the remnant of the sea coast.
17 Kwa kuwa nitalipiza kisasi kikubwa dhidi yao pamoja na matendo ya ghadhabu kubwa ya adhabu, hivyo watajua yakwamba mimi ni Yahwe, nitakapolipiza kisasi juu yao.”'
And I will execute great vengeance upon them, rebuking them in fury: and they shall know that I am the Lord, when I shall lay my vengeance upon them.