< Ezekieli 24 >

1 Neno la Yahwe likanijia katika mwaka wa nane mwezi wa kumi na siku ya kumi ya mwezi, kusema,
The word of Yahweh came to me in the ninth year, in the tenth month, and on the tenth day of the month, saying,
2 “Mwanadamu, andika kwa ajili yako jina la hii siku, siku hii sahihi mfalme wa Babeli ameizingira Yerusalimu.
“Son of man, write for yourself the name of this day, this exact day, for this exact day the king of Babylon has besieged Jerusalem.
3 Basi nena mithali juu ya hii nyumba ya kuasi, fumbo moja. Waambie, 'Bwana Yahwe asema hivi: weka sufuria ya kupikia. Iweke na weka maji kwenye hiyo.
So speak a proverb against this rebellious house, a parable. Say to them, 'The Lord Yahweh says this: Place the cooking pot. Place it and pour water into it.
4 Vikusanye vipande vya chakula ndani yake, kila kipande kizuri-paja na bega-na ijaze kwa mifupa bora.
Gather pieces of food within it, every good piece—the thigh and shoulder— and fill it with the best bones.
5 Chukua kundi bora na jaza mifupa chini yake. Ilete kuchemsha na ipike mifupa ndani yake.
Take the best of the flock and pile up the bones under it. Bring it to a boil and cook the bones in it.
6 Kwa hiyo, Bwana Yahwe asema hivi: Ole kwa mji wa damu. Nitakiongeza chungu cha mbao. Weka kuni nyingi na washa moto. Pika nyama vizuri na changanya katika viungo na iacha mifupa iteketee.
Therefore the Lord Yahweh says this: Woe to the city of blood, a cooking pot that has rust in it and that rust will not come out of it. Take piece after piece from it, but do not cast lots for it.
7 Kwa kuwa damu iko kati yake. Ameiweka juu ya jiwe laini; hakuimwaga juu ya nchi kuifunika kwa mavumbi,
For her blood is in the midst of her. She has set it on the smooth rock; she has not poured it out on the ground to cover it with dust,
8 hivyo inaleta hasira ya kulipa kisasi. Nimeweka damu yake juu ya jiwe laini ili isifunikwe.
so it brings fury up to exact vengeance. I placed her blood on the smooth rock so it could not be covered.
9 Kwa hiyo, Bwana Yahwe asema hivi: Ole kwa mji wa damu. Nitakiongeza chungu cha mbao.
Therefore, the Lord Yahweh says this: Woe to the city of blood. I will also enlarge the pile of wood.
10 Weka kuni nyingi na washa moto. Pika nyama vizuri na changanya katika viungo na acha mifupa iteketee.
Stack up the wood and kindle the fire. Cook the meat well and mix in the spices and let the bones be charred.
11 Kisha weka chungu kitupu juu ya mkaa, ili kuchemsha na kuchoma shaba yake, hivyo uchafu wake ndani yake itayeyushwa, kutu yake imekula.'
Then set the pot on its coals empty, in order to heat and scorch its bronze, so its uncleanness within it will be melted, its corrosion consumed.'
12 Amechoka kwa sababu ya kazi ya taabu, lakini kutu yake haitoki kweke kwa moto.
She has become weary because of toil, but her corrosion has not gone out of her by the fire.
13 Tabia yako ya aibu iko ndani ya uchafu wako, kwa sababu nimekusafisha, lakini bado hutaweza kuwa msafi. Bado hutakuwa huru kutoka uchafu wako hadi hasira yako itakapotulia kutoka kwako.
Your shameful behavior is in your uncleanness. Because I tried to cleanse you but still you would not be cleansed from your uncleanness, you will not be cleansed anymore until I have satisfied my fury upon you.
14 Mimi, Yahwe, nimesema hili, na nitalifanya. Sintotulia wala kupumzika kwa ajili ya hili. Kama njia zako zilivyokuwa, na kama matendo yako, yatakuhukumu! -hivi ndivyo Bwana Yahwe asemavyo.”
I, Yahweh, have declared it, and I will do it. I will not relent nor will I rest from it. As your ways were, and as your activities, they will judge you!—this is the Lord Yahweh's declaration.”
15 Kisha neno la Yahwe likanijia, kusema,
Then the word of Yahweh came to me, saying,
16 “mwanadamu! Tazama, ninachukua tamaa ya macho yako kutoka kwako pamoja na tauni, lakini hutaomboleza wala kulia, na machozi yako hayatatoka.
“Son of man! Behold, I am taking the desire of your eyes from you with a plague, but you must not mourn nor weep, and your tears must not flow.
17 Utagugumia bila kusikika. Usiendeshe mazishi kwa ajili ya aliyekufa. Funga kilemba chako juu yako na vaa makubazi miguuni pako, lakini usivalishe shela nywele zako au kula mkate wa watu waombolezao kwa ajili ya kuwapoteza wake zao.”
You must groan silently. Do not conduct a funeral for the dead. Tie your turban on you and place your sandals on your feet, but do not veil your facial hair or eat the bread of men who mourn for having lost their wives.”
18 Hivyo nimeongea na watu asubuhi, na mke wangu amekufa asubuhi. Asubuhi nimefanya kile nilichokuwa nimeambiwa kukifanya.
So I spoke to the people in the morning, and my wife died in the evening. In the morning I did what I had been commanded to do.
19 Watu wameniuliza, “Ji! hautatuambia haya mambo yanamaana gani, mambo ambayo unayoyafanya?”
The people asked me, “Will you not tell us what these things mean, the things that you are doing?”
20 Hivyo nimewaambia, “Neno la Yahwe likanijia, kusema,
So I said to them, “The word of Yahweh came to me, saying,
21 'Waambie nyumba ya Israeli, Bwana Yahwe asema hivi: Tazama! Nitapanajisi patakatifu pangu-fahari ya nguvu yenu, mahali panapopendeza macho yenu, na panapotamaniwa na roho zenu, na wana wenu na binti zenu ambao mliowaacha nyuma wataanguka kwa upanga.
'Say to the house of Israel, the Lord Yahweh says this: Behold! I will desecrate my sanctuary—the pride of your power, the delight of your eyes, and the yearning of your soul, and your sons and your daughters whom you left behind will fall by the sword.
22 Kisha mtafanya hasa kama nilivyofanya: hutafunika nywele za sehemu ya chini za uso, wala kula mkate wa watu wanaoomboleza!
Then you will do exactly as I have done: you will not veil your facial hair, nor eat the bread of mourning men!
23 Badala yake, vilemba vyenu vitakuwa juu ya vichwa, na makubadhi yenu miguuni mwenu; hutaomboleza wala kulia, kwa kuwa mtayeyuka katika maovu yenu, na kila mtu atagugumia kwa ya ajili ya ndugu yake.
Instead, your turbans will be on your heads, and your sandals on your feet; you will not mourn nor weep, for you will melt away in your iniquities, and each man will groan for his brother.
24 Hivyo Ezekieli atakuwa ishara kwenu, kama kila kitu ambacho alichokifanya mtafanya wakati hili litakapokuja. Kisha mtajua yakwamba mimi ni Bwana Yahwe!”'
So Ezekiel will be a sign for you, as everything that he has done you will do when this comes. Then you will know that I am the Lord Yahweh!'”
25 “Lakini wewe, mwanadamu, siku ambayo nitachukua hekalu lao, ambalo ni furaha yao, kiburi chao, na kile waonacho na kutamani-na wakati nikiwachukua wana wao na binti-
“But you, son of man, on the day that I capture their temple, which is their joy, their pride, and what they see and desire—and when I take away their sons and daughters—
26 siku hiyo, mgeni atakuja kwako kukupatia habari!
on that day, a refugee will come to you to give you the news!
27 Siku hiyo kinywa chako kitafunguliwa kwa huyo mgeni na utaongea-hutakuwa bubu tena. Utakuwa ishara kwao hivyo basi watajua kwamba mimi ni Yahwe.
On that day your mouth will be opened up to that refugee and you will speak—you will no longer be silent. You will be a sign for them so that they will know that I am Yahweh.”

< Ezekieli 24 >