< Ezekieli 22 >
1 Kisha neno la Yahwe likanijia, kusema,
Moreover the word of the LORD came to me, saying,
2 “Sasa wewe, mwanadamu, Je! Utanihukumu? Utauhukumu mji kwa damu? Mfanye ajue machukizo yake yote.
Now, you son of man, will you judge, will you judge the bloody city? yes, you shall show her all her abominations.
3 Utasema, 'Bwana Yahwe asema hivi: Huu ndiyo mji umbao umwagao damu kati yake ili kwamba mda wake ufike; mji ufanyao sanamu ili ujitie unajisi.
Then say you, Thus says the Lord GOD, The city sheds blood in the middle of it, that her time may come, and makes idols against herself to defile herself.
4 Umekuwa na hatia kwa damu uliyoimwaga, na kufanya unajisi kwa sanamu ulizozitengeneza. Kwa kuwa umezileta karibu siku zako na kuzikaribia siku zako za mwisho. Kwa hiyo nitakufanya lawama kwa mataifa na kejeli katika uso wa kila nchi.
You are become guilty in your blood that you have shed; and have defiled yourself in your idols which you have made; and you have caused your days to draw near, and are come even to your years: therefore have I made you a reproach to the heathen, and a mocking to all countries.
5 Wote walio karibu na wale walio mbali nawe watakudhihaki, wewe mji mchafu, ujulikanao kila mahali kwa sifa mbaya kama kujaa machafuko.
Those that be near, and those that be far from you, shall mock you, which are infamous and much vexed.
6 Tazama! Wakuu wa Israeli, kila mmoja kwa nguvu yake, wamekuja kwako kumwaga damu.
Behold, the princes of Israel, every one were in you to their power to shed blood.
7 Wamefanya udanganyifu kwa baba na mama ndani yako, na wametenda yaliyo kinyume juu ya wageni kati yako. Wamewatenda vibaya yatima na wajane ndani mwako.
In you have they set light by father and mother: in the middle of you have they dealt by oppression with the stranger: in you have they vexed the fatherless and the widow.
8 Umevidharau vitu vyangu vitakatifu na kuinajisi Sabato yangu.
You have despised my holy things, and have profaned my sabbaths.
9 Watu wasingiziaji wamekuja kati yako ili kumwaga damu, na hula juu ya milima. Hufanya uovu kati yako.
In you are men that carry tales to shed blood: and in you they eat on the mountains: in the middle of you they commit lewdness.
10 Uchi wa baba umefunuliwa ndani yako. Wamemtukana mwanamke mchafu ndani yako wakati wa uchafu wake.
In you have they discovered their fathers’ nakedness: in you have they humbled her that was set apart for pollution.
11 Watu waliofanya machukizo pamoja na wake za majirani zao, na watu wafanyao uchafu wa aibu kwa mke wa mwanao mwenyewe; watu wawatukanao dada zao wenyewe-binti za baba zao wenyewe-haya yote yapo miongoni mwanu.
And one has committed abomination with his neighbor’s wife; and another has lewdly defiled his daughter in law; and another in you has humbled his sister, his father’s daughter.
12 Hawa watu huchukua rushwa kati yenu ili kumwaga damu. Umechukua faida na kuongeza riba nyingi sana, na umenisahau-hivi ndivyo Bwana Yahwe asemavyo.
In you have they taken gifts to shed blood; you have taken usury and increase, and you have greedily gained of your neighbors by extortion, and have forgotten me, says the Lord GOD.
13 Tazama! Kwa mkono wangu nimeipiga faida ambayo uliyoitengeneza kwa njia isiyo halali, na damu iliyo kati yako.
Behold, therefore I have smitten my hand at your dishonest gain which you have made, and at your blood which has been in the middle of you.
14 Je! Moyo wako utasimama, mikono yako itakuwa hodari katika siku wakati mimi mwenyewe nitakapo kushughulikia? Mimi, Yahwe, nasema hivi, na nitalifanya.
Can your heart endure, or can your hands be strong, in the days that I shall deal with you? I the LORD have spoken it, and will do it.
15 Hivyo nitakutawanya kati ya mataifa na kukutawanya kati ya nchi mbali mbali. Katika njia hii, nitausafisha uchafu kutoka kwako.
And I will scatter you among the heathen, and disperse you in the countries, and will consume your filthiness out of you.
16 Hivyo utakuwa mchafu machoni mwa mataifa. Kisha utajua kwamba mimi ni Yahwe.”'
And you shall take your inheritance in yourself in the sight of the heathen, and you shall know that I am the LORD.
17 Kisha neno la Yahwe likanijia, kusema,
And the word of the LORD came to me, saying,
18 “Mwanadamu, nyumba ya Israeli imekuwa takataka kwangu. Wote wamekuwa masazo ya shaba na bati, na chuma na risasi kati yenu. Watakuwa kama takataka ya fedha katika tanuu.
Son of man, the house of Israel is to me become dross: all they are brass, and tin, and iron, and lead, in the middle of the furnace; they are even the dross of silver.
19 Kwa hiyo Bwana Yahwe asema hivi, 'Kwa sababu mmekuwa kama takataka, kwa hiyo, tazama! Nataka kuwakusanya katikakati ya mji wa Yerusalemu.
Therefore thus says the Lord GOD; Because you are all become dross, behold, therefore I will gather you into the middle of Jerusalem.
20 Kama kukusanya fedha na shaba, chuma, risasi na chuma kati ya tanuu ili kuvifukutia moto na kuviyeyusha juu yake, nitawayeyusha. Hivyo nitawakusanya katika hasira yangu na ghadhabu. Nitawaweka hapo na kufukutisha moto juu yake ili kuiyeyusha; hivyo nitawakusanya katika hasira yangu na ghadhabu yangu, na nitawaweka hapo na kuwayeyusha.
As they gather silver, and brass, and iron, and lead, and tin, into the middle of the furnace, to blow the fire on it, to melt it; so will I gather you in my anger and in my fury, and I will leave you there, and melt you.
21 Basi nitawakusanya na kuwafukutia kwa moto wa hasira yangu juu yenu hivyo basi mtamwagwa kati yake.
Yes, I will gather you, and blow on you in the fire of my wrath, and you shall be melted in the middle therof.
22 Kama kuyeyusha fedha kati ya tanuu, mtayeyushwa chini kati yake, na mtajua yakwamba mimi, Yahwe, nimemwaga ghdhabu yangu juu yenu!”'
As silver is melted in the middle of the furnace, so shall you be melted in the middle thereof; and you shall know that I the LORD have poured out my fury on you.
23 Neno la Yahwe likanijia, kusema,
And the word of the LORD came to me, saying,
24 “Mwanadamu, mwambie, 'Wewe ni nchi ambayo haijasafishwa. Hakuna mvua siku ya hasira!
Son of man, say to her, You are the land that is not cleansed, nor rained on in the day of indignation.
25 Kuna njama ya manabii wake kati yake, kama simba angurumaye akirarua mawindo. Wamekula uhai na kuchukua utajiri wa thamani; wamewafanya wajane wengi ndani yake!
There is a conspiracy of her prophets in the middle thereof, like a roaring lion ravening the prey; they have devoured souls; they have taken the treasure and precious things; they have made her many widows in the middle thereof.
26 Makuhani wake hufanya kinyume na sheria yangu, na wamevinajisi vitu vyangu vitakatifu. Hawawezi kutofautisha kati ya vitu vitakatifu na vitu vya najisi. Wanaficha macho yao kutoka Sabato zangu hivyo basi nimetiwa unajisi kati yao.
Her priests have violated my law, and have profaned my holy things: they have put no difference between the holy and profane, neither have they showed difference between the unclean and the clean, and have hid their eyes from my sabbaths, and I am profaned among them.
27 Wakuu wake ndani mwake wamekuwa kama mbwa mwitu wakirarua mawindo yao. Wamemwaga damu na kuharibu maisha, ili kupata faida kwa njia ya udanganyifu.
Her princes in the middle thereof are like wolves ravening the prey, to shed blood, and to destroy souls, to get dishonest gain.
28 Manabii wake wamepakwa chokaa; wanaona maono ya uongo na kutabiri uongo kwao. Wanasema “Bwana Yahwe asema hivi”' wakati Yahwe hajanena.
And her prophets have daubed them with untempered mortar, seeing vanity, and divining lies to them, saying, Thus says the Lord GOD, when the LORD has not spoken.
29 Watu wa nchi wamewakandamiza kwa kutaka kwa nguvu na kuwanyang'anya kwa nguvu, na wamewatesa maskini na wahitaji, na kuwakandamiza wageni bila haki.
The people of the land have used oppression, and exercised robbery, and have vexed the poor and needy: yes, they have oppressed the stranger wrongfully.
30 Hivyo nimetafuta mtu kutoka kwao ambaye ataweza kujenga ukuta na ambaye atakayeweza kusimama mbele yangu katika uvunjaji wake kwa ajili ya nchi basi sitaweza kuiharibu, lakini sikuona mtu.
And I sought for a man among them, that should make up the hedge, and stand in the gap before me for the land, that I should not destroy it: but I found none.
31 Hivyo nitaimwaga ghadhabu yangu juu yao. Nitawamaliza kwa moto wa ghadhabu yangu na kuweka njia yao juu ya vichwa vyao wenyewe-hivi ndivyo Bwana Yahwe asemavyo.”'
Therefore have I poured out my indignation on them; I have consumed them with the fire of my wrath: their own way have I recompensed on their heads, says the Lord GOD.