< Ezekieli 21 >

1 Kisha neno la Yahwe likanijia, kusema,
The word of ye Lord came to me againe, saying,
2 “Mwanadamu, weka uso wako kuelekea Yerusalemu, na neno juu ya patakatifu; tabiri juu ya nchi ya Israeli.
Sonne of man, set thy face toward Ierusalem, and drop thy word toward the holy places, and prophecie against the land of Israel.
3 Sema juu ya nchi ya Israeli, 'Yahwe asema hivi: Tazama! Ni juu yako! Nitautoa upanga wangu kutoka kwenye ala yake na kuwakatilia mbali wote yaani mtu mwenye haki na mtu mwovu kutoka kwako!
And say to the land of Israel, Thus saith the Lord, Beholde, I come against thee, and will drawe my sword out of his sheath, and cut off from thee both the righteous and the wicked.
4 Ili niwakatilie mbali wote, mwenye haki na mwovu kutoka kwako, upanga wangu utatoka kwenye ala yake juu ya wote wenye mwili kutoka kusini hata kaskazini.
Seeing then that I will cut off from thee both the righteous and wicked, therefore shall my sworde goe out of his sheath against all flesh from the South to the North,
5 Kisha wote wenye mwili watajua yakwamba mimi, Yahwe, nimeutoa upanga wangu kutoka kwenye ala yake. Hautarudi tena!'
That all flesh may knowe that I the Lord haue drawen my sworde out of his sheath, and it shall not returne any more.
6 Kwa hiyo, mwanadamu, gumia kama kuvunjika kwa viuno vyako! Katika uchungu gumia mbele ya macho yao!
Mourne therefore, thou sonne of man, as in the paine of thy reines, and mourne bitterly before them.
7 Kisha itatokea kwamba watakuuliza, 'Kwa sababu gani unalia?' Kisha utasema, 'Kwa sababu ya habari inayokuja, kwa kuwa kila moyo utakuwa dhaifu, na kila mkono utasita! Kila roho itazimia, na kila goti litatiririrka kama maji. Tazama! Inakuja na itakuwa kama hivi! -hivi ndivyo Bwana Yahwe asemavyo.”'
And if they say vnto thee, Wherefore mournest thou? then answere, Because of the bruite: for it commeth, and euery heart shall melt, and all handes shall be weake, and all mindes shall faint, and all knees shall fall away as water: beholde, it commeth, and shall be done, saith the Lord God.
8 Kisha neno la Yahwe likanijia, kusema,
Againe, the word of the Lord came vnto me, saying,
9 “Mwanadamu, tabiri na sema, 'Bwana asema hivi: sema: Upanga! Upanga! Utachongwa na kusuguliwa!
Sonne of man, prophecie, and say, Thus saith the Lord God, say, A sworde, a sworde both sharpe, and fourbished.
10 Utanolewa ili kushiriki katika machinjio makubwa! Utasuguliwa ili uwe kama mng'ao wa radi! Je! Tufanye furaha katika fimbo ya mwana wa mfalme? Upanga ujao huchukia kila hiyo fimbo!
It is sharpened to make a sore slaughter, and it is fourbished that it may glitter: how shall we reioyce? for it contemneth the rod of my sonne, as all other trees.
11 Hivyo upanga utatolewa kwa ajili ya kusuguliwa, na kisha kushikika kwa mkono! Upanga umechongwa na umesuguliwa na utatolewa kwenye mkono wa yule auaye!'
And he hath giuen it to be fourbished, that he may handle it: this sword is sharpe, and is fourbished, that he may giue it into ye hand of the slayer.
12 Ita msaada na omboleza, mwanadamu! Kwa kuwa upanga umekuja juu ya watu wangu! Uko juu ya wakuu wote wa Israeli. Wametolewa dhidi ya upanga pamoja na watu wangu. Kwa hiyo, piga paja lako!
Cry, and houle, sonne of man: for this shall come to my people, and it shall come vnto all the princes of Israel: the terrours of the sword shall be vpon my people: smite therefore vpon thy thigh.
13 Kwa kuwa kuna kujaribiwa, lakini itakuwaje kama fimbo ya kifalme haitakuwepo tena? -hivi ndivyo Bwana Yahwe asemavyo.
For it is a triall, and what shall this be, if the sworde contemne euen the rodde? It shall be no more, saith the Lord God.
14 Basi wewe, mwanadamu, tabiri, na piga makofi, kwa kuwa upanga utakushambulia hata mara tatu! Upanga kwa wale watakaochinjwa! Utakuwa upanga kwa ajili ya kuchinjia, ukiwatoboa pande zote!
Thou therefore, sonne of man, prophecie, and smite hand to hand, and let the sworde be doubled: let the sworde that hath killed, returne the third time: it is the sword of the great slaughter entring into their priuie chambers.
15 Ili kuyeyusha mioyo yao na kuongeza kuanguka kwao, nimeweka machinjio ya upanga juu ya malango! Ole! Umeundwa kama mng'ao wa radi, umetengwa kwa ajili ya kuua!
I haue brought the feare of the sword into all their gates to make their heart to faint, and to multiplie their ruines. Ah it is made bright, and it is dressed for the slaughter.
16 Wewe, upanga! Nyooka upande wa kuume! Nyooka upande wa kushoto! Nenda popote ulipoelekeza uso wako.
Get thee alone: goe to the right hande, or get thy selfe to the left hande, whithersoeuer thy face turneth.
17 Kwa kuwa pia nitapiga mikono yangu miwili kwa pamoja (makofi), na kisha nitaleta ghadhabu yangu kwa waliobakia! Mimi, Yahwe, nimesema hivi!”
I wil also smite mine hands together, and wil cause my wrath to cease. I the Lord haue said it.
18 Neno la Yahwe likanijia tena, kusema,
The worde of the Lord came vnto mee againe, saying,
19 “Sasa wewe, mwanadamu, teua njia mbili kwa ajili ya upanga wa mfalme wa Babeli upate kuja. Njia hizo mbili zitaanza katika nchi moja, na kibao cha barabarani kitamwonyesha mmoja wao kama kuuelekea mji.
Also thou sonne of man, appoint thee two wayes, that the sworde of the King of Babel may come: both twaine shall come out of one lande, and chuse a place, and chuse it in the corner of the way of the citie.
20 Onyesha njia moja kwa ajili ya jeshi la Wababeli kuja Raba, mji wa Waamoni. Onyesha nyingine kuelekea jeshi la Yuda na mji wa Yerusalemu, ambayo imeimarishwa.
Appoint a way, that the sworde may come to Rabbath of the Ammonites, and to Iudah in Ierusalem the strong citie.
21 Kwa kuwa mfalme wa Babeli atasimama kwenye makutano ya barabara, kwenye njia panda, ili kufanya uganga. Alitingisha mishale na kuuliza mwelekeo kutoka kwa sanamu na atalichunguza ini.
And the King of Babel stoode at the parting of the way, at the head of the two wayes, consulting by diuination, and made his arrowes bright: hee consulted with idoles, and looked in the liuer.
22 Katika mkono wake wa kuume kutakuwa na dalili kuhusu Yerusalemu, kuweka mitambo ya kubomolea juu ya hiyo, kufungua kinywa chake kupanga kuchinja, kutoa sauti ya vita, kuweka mitambo ya kubomolea juu ya malango, kujenga ngazi, na kusimamisha wima minara ya boma.
At his right hand was the diuination for Ierusalem to appoint captaines, to open their mouth in the slaughter, and to lift vp their voyce with shouting, to laye engines of warre against the gates, to cast a mount, and to builde a fortresse.
23 Itaonekana kuwa ishara isiyofaa katika macho ya wale walio katika Yerusalemu, wale walioapa kiapo kwa Wababeli! Lakini mfalme atawashtaki kwa kuvunja sheria ya mkataba ili kuwabariki!
And it shalbe vnto them as a false diuination in their sight for the othes made vnto them: but hee will call to remembrance their iniquitie, to the intent they should be taken.
24 Kwa hiyo Bwana Yahwe asema hivi: Kwa sababu umeuleta uovu wako kwenye kumbukumbu zangu, makosa yenu yatafunuliwa! Dhambi zenu zitaonekana katika matendo yenu yote! Kwa sababu hii utamkumbusha kila mtu mtakamatwa kwa mkono wa adui yenu!
Therefore thus sayeth the Lord God, Because ye haue made your iniquitie to bee remembred, in discouering your rebellion, that in al your workes your sinnes might appeare: because, I say, that ye are come to remembrance, ye shall be taken with the hand.
25 Kama wewe, mchafu na mtawala mwovu wa Israeli, ambaye siku ya hukumu imekuja, na ambaye mda wa kufanya uovu umekoma,
And thou prince of Israel polluted, and wicked, whose day is come, when iniquitie shall haue an ende,
26 Bwana Yahwe asema hivi kwako: Toa kilemba na vua taji! Mambo hayatakuwa tena kama yalivyokuwa! Kiinue kilicho chini na kiinue kilichoinuka!
Thus saith the Lord God, I will take away the diademe, and take off the crowne: this shalbe no more the same: I wil exalt the humble, and will abase him that is hie.
27 Uharibifu! Uharibifu! Nitaiharibu! Haitakuwa tena hadi atakapokuja yeye ambaye ameteuliwa kutekeleza hukumu.
I wil ouerturne, ouerturne, ouerturne it, and it shall be no more vntill he come, whose right it is, and I will giue it him.
28 Basi wewe, mwanadamu, tabiri na sema, 'Bwana Yahwe asema hivi hawa ni watu wa Amoni kuhusiana na ujio wa aibu yao: Upanga, upanga umechirwa! Umenolewa kwa ajili ya kuchinja, hivyo utakuwa kama kimuli muli cha radi!
And thou, sonne of man, prophecie, and say, Thus saith the Lord God to the children of Ammon, and to their blasphemie: say thou, I say, The sword, the sword is drawen foorth, and fourbished to the slaughter, to consume, because of the glittering:
29 Wakati manabii wameona maono ya uongo juu yako, wakati watakapofanya matambiko kuuijia kwa uongo juu yako, huu upanga utaanguka chini juu ya shingo za mwovu ambao wako karibu kuuawa, ambao siku ya ghadhabu imekuja na ambao mda wa uovu unakaribia kuisha.
Whiles they see vanitie vnto thee, and prophecied a lie vnto thee to bring thee vpon the neckes of the wicked that are slaine, whose day is come when their iniquitie shall haue an ende.
30 Rudisha upanga kwenye gala yake. Katika mahali ulipoumbwa, katika nchi ya chimbuko lako, nitakuhukumu!
Shall I cause it to returne into his sheath? I will iudge thee in the place where thou wast created, euen in the land of thine habitation.
31 Nitamwaga hasira yangu juu yako! Nitapuliza upepo wa moto wa ghadhabu juu yako na kukuweka kwenye mkono wa watu wakatili, watu wajuao kuangamiza!
And I wil powre out mine indignation vpon thee, and will blowe against thee in the fire of my wrath, and deliuer thee into the hand of beastly men, and skilfull to destroy.
32 Utakuwa kuni kwa ajili ya moto! Damu yako itakuwa kati ya nchi. Hutakumbukwa tena, kwa kuwa mimi, Yahwe nimesema hivi!”'
Thou shalt bee in the fire to be deuoured: thy blood shall be in the middes of the lande, and thou shalt be no more remembred: for I the Lord haue spoken it.

< Ezekieli 21 >