< Ezekieli 20 >
1 Ikawa ikaja katika mwaka wa saba, siku ya kumi ya mwezi wa tano, wazee wa Israeli wakaja kumuuliza Yahwe na kuketi mbele yangu.
И бысть в лето седмое, в пятый месяц, в десятый день месяца, приидоша мужие от старейшин дому Израилева вопросити Господа и седоша пред лицем моим.
2 Kisha neno la Yahwe likanijia, kusema,
И бысть слово Господне ко мне глаголя:
3 “mwanadamu, tangaza kwa wazee wa Israeli na uwaambie, 'Bwana Yahwe asema hivi: Je! Mmekuja kuniuliza swali? Kama niishivyo, sitaulizwa swali na ninyi! -hivi ndivyo Bwana Yahwe asemavyo.'
сыне человечь, глаголи ко старейшинам дому Израилева и речеши к ним: тако глаголет Адонаи Господь: еда вопросити Мене вы приходите? Живу Аз, аще отвещаю вам, глаголет Адонаи Господь.
4 Je! Utawahukumu? Utamuhukumu, mwanadamu? Wajulishe kuhusu machukizo ya baba zao.
Аще отмщением отмщу им: сыне человечь, беззакония отец их засвидетелствуй им,
5 Waambie, 'Bwana Yahwe asema hivi: Katika siku niliyoichagua Israeli na kuinua mkono wangu kuapa kiapo kwa uzao wa nyumba ya Yakobo, na kufanya kujulikana mimi mwenyewe kwao katika nchi ya Misri, wakati nilipoinua mkono wangu kuapa kiapo kwao. Nalisema, “Mimi ni Yahwe Mungu wenu”-
и речеши к ним: сия глаголет Адонаи Господь: от негоже дне избрах дом Израилев, и уведен бых племени дому Иаковля и познан бых им во земли Египетстей, и приях я рукою Моею глаголя: Аз Господь Бог ваш:
6 siku hiyo niliinua mkono wangu kuapa kiapo kwa ajili yao kwamba nitawatoa kutoka nchi ya Misri kwenye nchi ambayo niliyokuwa nimeichagua kwa umakini kwa ajili yao. Ilikuwa ikitiririka maziwa na asali; ilikuwa nzuri sana utukufu miongoni mwa nchi mbali mbali.
в той день подях я рукою Моею, еже извести я из земли Египетския в землю, юже уготовах им, землю кипящую млеком и медом, сот есть паче всех земель,
7 Nikawaambia, “Kila mtu atupilie mabli mambo ya machukizo kutoka mbele ya macho yake na sanamu za Misri. Msijitie unajisi; mimi ni Yahwe Mungu wenu.”
и рекох к ним: кийждо мерзости от очес своих отвержите и во творениих Египетских не оскверняйтеся, Аз Господь Бог ваш.
8 Lakini wameasi juu yangu hawakuwa tayari kunisikiliza. Kila mtu hakutupilia mbali mambo ya machukizo kutoka mbele ya macho yake wala kwa ajili ya sanamu za Misri, hivyo nikaona nimwage ghadhabu yangu juu yao kukamilisha hasira yangu miongoni mwao katikati ya nchi ya Misri.
И отвергошася Мене и не хотеша послушати Мя: кийждо мерзостей от очес своих не отвергоша и творений Египетских не оставиша. И рекох, еже излияти ярость Мою на ня и скончати гнев Мой на них среде земли Египетския.
9 Nilifanya kwa ajili ya jina langu ili lisinajisiwe katika macho ya mataifa ambao walikaa pamoja nao. Nilijifanya mwenyewe kujulikana kwao, katika macho yao, kwa kuwatoa katika nchi ya Misri.
И сотворих, яко да имя Мое весьма не осквернится пред языки, в нихже суть тии среде их, в нихже познан бых им пред лицем их, еже извести я из земли Египетския.
10 Basi nikawatoa katika nchi ya Misri na kuwaleta kwenye jangwa.
И изведох я из земли Египетския и введох я в пустыню,
11 Kisha nikawapa amri zangu na kufanya maagizo yangu kujulikana kwao, kwa kila mwanadamu atakayezishika ataishi.
и дах им заповеди Моя, и оправдания Моя явих им, яже аще сотворит человек, жив будет в них:
12 Pia nikawapatia Sabato zangu kama ishara kati yangu na wao, ili wajue kwamba mimi ni Yahwe niwafanyao wawe watakatifu.
и субботы Моя дах им, еже быти в знамение между Мною и между ими, еже разумети им, яко Аз Господь освящаяй их.
13 Lakini nyumba ya Israeli imeasi dhidi yangu jangwani. Hawakuenenda katika amri zangu; badala yake, wameyakataa maagizo yangu, ambayo mwanadamu ataishi kama akiyatii. Wamezinajisi Sabato zangu sana, basi nikasema nitamwaga hasira yangu juu yao jangwani ili kuwamalliza.
И глаголах ко дому Израилеву в пустыни: в заповедех Моих ходите и оправдания Моя сохраните, еже творити я, яже сотворит человек и жив будет в них. И разгнева Мя дом Израилев в пустыни: в заповедех бо Моих не ходиша и оправдания Моя отвергоша, яже сотворит человек и жив будет в них: и субботы Моя оскверниша зело. И рекох, еже излияти ярость Мою на ня в пустыни, еже потребити их.
14 Lakini nilifanya kwa ajili ya jina langu hivyo lisinajisiwe katika macho ya mataifa, ambao niliwatoa mbele ya macho yao kutoka Misri.
И сотворих, яко да весьма имя Мое не осквернится пред языки, из нихже изведох я пред очима их.
15 Basi mimi mwenyewe pia nimeinua mkono wangu kuapa kiapo kwao jangwani sitawarudisha kwenye nchi ile niliyokuwa naenda kuwapatia, nchi inayotiririkayo maziwa na asali, ambayo ilikuwa nzuri sana ambayo ni nzuri kati ya nchi zote.
И Аз воздвигох руку Мою на ня в пустыни весьма, еже не ввести их в землю, юже дах им, в землю текущую млеком и медом, сот есть паче всея земли:
16 Nimeapa hivi kwa sababu walikataa maagizo yangu na kutotembea katika amri zangu, na wazikufuru Sabato zangu.
понеже судбы Моя отвергоша и в заповедех Моих не ходиша, и субботы Моя оскверниша и вслед помышлений сердца своего хождаху.
17 Lakini jicho langu likawahurumia kutokana na uharibifu na sikuwaangamiza jangwani.
И пощаде я око Мое, еже потребити их, и не сотворих им скончания в пустыни.
18 Nikawaambia watoto wao jangwani, “Msitembee kutokana na amri za wazazi wenu; msiweke maagizo yao au kujinajisi wenyewe kwa sanamu.
И рекох ко чадом их в пустыни: в законех отец ваших не ходите и оправданий их не храните, и ко творением Египетским не примешайтеся и не оскверняйтеся:
19 Mimi ni Yahwe Mungu wenu, tembeeni katika amri zangu; tunzeni maagizo yangu na kuyatii.
Аз Господь Бог ваш: в заповедех Моих ходите, и оправдания Моя снабдите и творите я,
20 Zitunzeni Sabato zangu takatifu ili kwamba zitakuwa ishara kati yangu na ninyi, hivyo basi mtajua yakwamba mimi ni Yahwe Mungu wenu.”
и субботы Моя освящайте и будет в знамение между Мною и между вами, еже ведети вам, яко Аз Господь Бог ваш.
21 Lakini watoto wao waliniasi. Hawakutembea kwenye sheria zangu au kushika maagizo yangu, ambazo mwanadamu ataishi kama akizitii. Wamezinajisi Sabato zangu, hivyo nimeamua kumwaga ghadhabu yangu juu yao kutimiza ghadhabu yangu dhidi yao katika jangwa.
И разгневаша Мя, и чада их в заповедех Моих не ходиша и оправданий Моих не снабдеша, еже творити я: сия бо сотворив человек жив будет в них: и субботы Моя оскверниша зело. И рекох: излию ярость Мою на ня, еже скончати гнев Мой на них в пустыни.
22 Lakini niliurudisha mkono wangu na kutenda kwa ajili ya jina langu, hivyo lisitiwe unajisi katika macho ya mataifa ambao mbele ya macho yao niliwatoa Waisraeli.
И сотворих, яко да имя Мое весьма не осквернавится пред языки, от нихже изведох я пред очима их.
23 Mimi mwenyewe pia nimeuinua mkono wangu kuapa juu yao jangwani, kwamba nitawatawanya kati ya maifa na kuwatawanya miongoni mwa nchi mabali mbali.
И Аз воздвигох руку Мою на ня в пустыни, еже расточити я во языцех и разсеяти я во странах,
24 Nimeamua kufanya hivi kwa kuwa hawakuzitii amri zangu, na tangu walipo zikataa sheria zangu na kuzinajisi Sabato zangu. Macho yao yalizitamani sanamu za baba zao.
понеже оправданий Моих не сотвориша и заповеди Моя отринуша и субботы Моя оскверниша, и вслед кумиров отец их быша очеса их.
25 Kisha niliwapa amri ambazo hazikuwa nzuri, na maagizo ambayo hawakuweza kuishi kwayo.
И дах им заповеди не добры и оправдания, в нихже не будут живи:
26 Nikawafanya unajisi kwa zawadi zao wakati walipofanya dhabihu za kila limbuko la tumbo la uzazi na kutupa kwenye moto. Nalifanya hivi ili kuwaogofya hivyo wangeweza kujua kwamba mimi ni Yahwe!'
и оскверню я в даяниих их, внегда проводити (им) всякое разверзающее ложесна, да погублю их, да уразумеют, яко Аз Господь.
27 Kwa hiyo, mwanadamu, waambie nyumba ya Israeli na waambie, 'Bwana Yahwe asema hivi: Katika hili pia baba zenu walinikufuru wakati walipokuwa sio waaminifu kwangu.
Сего ради глаголи к дому Израилеву, сыне человечь, и речеши к ним: сия глаголет Адонаи Господь: даже до сего разгневаша Мя отцы ваши во гресех своих, имиже согрешиша ко Мне:
28 Wakati nilipowaleta kwenye nchi ambayo niliyokuwa nimewaapia kuwapatia, na kisha popote walipoona jiwe lolote refu na mti wenye majani, walitoa sadaka zao, walinikasirisha kwa sadaka zao, na huko pia walichoma ubani wao wa kunukia na kumwaga sadaka zao za kinywaji.
и введох я в землю, в нюже воздвигох руку Мою, еже дати ю им: и видеша всяк холм высок и всяко древо присенное, и пожроша тамо богом своим и учиниша тамо ярость даров своих, и положиша тамо воню благовония своего и возлияша тамо возлияния своя.
29 Kisha nikawaambia, “Nini maana ya mahali palipoinuka ambapo mmeleta sadaka huko?” Hivyo jina lake linaitwa Bana hata leo.'
И рекох к ним: что суть Аввама, яко вы входите тамо? И прозваша имя ему Аввама даже до днешняго дне.
30 Kwa hiyo waambie nyumba ya Israeli, 'Bwana Yahwe asema hivi: Je! Kwa nini unajinajisi mwenyewe kwa njia za baba zako? Kwahiyo kwa nini unatenda kama makahaba, kutafuta kwa ajili ya mambo ya machukizo?
Сего ради рцы к дому Израилеву: сия глаголет Адонаи Господь: аще во беззакониих отец ваших вы оскверняетеся и вслед мерзостей их вы соблуждаете,
31 Kwa kuwa wakati mtoapo zawadi zenu na kuwaweka watoto wenu kwenye moto, siku hii mnajitia unajisi pamoja na sanamu zenu zote. Kwa hiyo kwa nini niwaache mniulize mimi, nyumba ya Israeli? Kama niishivyo-Hivi ndivyo Bwana Yahwe asemavyo-Sitawaacha mniulize swali.
и в приношении даров ваших и в нароцех ваших, егда проходят чада ваша сквозе огнь: вы оскверняетеся во всех кумирех ваших даже до днешняго дне, и Аз отвещаю ли вам, доме Израилев? Живу Аз, глаголет Адонаи Господь, аще отвещаю вам и аще взыдет на дух ваш сие.
32 Mawazo yanayoumbika kwenye moyo wako hayatatokea kamwe. Mmesema, “Ngoja tuwe kama mataifa mengine, kama koo za nchi nyingine waabuduo mti na jiwe.”
И не будет, якоже вы глаголете: будем, якоже языцы и якоже племена земная, служити древу и камению.
33 Kama niishivyo-hivi ndivyo Bwana Yahwe asemavyo-Nitatawala hakika juu yenu kwa mkono wenye nguvu, mkono ulionyooshwa, na ghadhabu itakayomwagwa juu yenu.
Сего ради живу Аз, глаголет Адонаи Господь, аще не рукою крепкою и мышцею высокою и в ярости излиянней царствовати буду над вами:
34 Nitawatoa kutoka kwa watu wengine na kuwakusanya kutoka kwenye nchi mlizotawanyika ndani mwao. Nitafanya hivi kwa mkono hodari na kwa ghadhabu iliyomwagika.
и изведу вы от людий и прииму вы от стран, в нихже бесте разсеяни, рукою крепкою и мышцею высокою и яростию излиянною,
35 Kisha nitawaleta kwenye jangwa la watu, na huko nitawahukumu uso kwa uso.
и приведу вас в пустыню людскую и разсуждуся с вами тамо лицем к лицу:
36 Kama nilivyo wahukumu baba zenu katika jangwa la nchi ya Misri, hivyo pia nitawahukumu-hivi ndivyo Bwana Yahwe asemavyo.
якоже судихся со отцы вашими в пустыни земли Египетския, тако сужду и вам, глаголет Адонаи Господь:
37 Nitawafanya mpite chini ya fimbo yangu, na nitawafanya kutii maagizo yangu ya agano.
и проведу вы под жезлом моим и введу вы в числе завета,
38 Nitawasafisha kutoka miongoni mwenu maasi na wale ambao walionichukiza. Nitawatoa kutoka nchi ambayo wanayoishi kama wageni, lakini hawataingia kwenye nchi ya Israeli. Kisha mtajua yakwamba mimi ni Yahwe.
и изберу от вас нечестивыя и отвергшыяся: из земли бо обитания их изведу я, и в землю Израилеву не внидут, и познаете, яко Аз Господь Бог.
39 Basi kwenu, nyumba ya Israeli, Bwana Yahwe asema hivi: Kila mmoja wenu ataenda kwa sanamu zake mwenyewe. Muwaabudu kama mtakataa kunisikiliza, lakini hamtalikufuru tena jina langu takatifu kwa zawadi zenu na sanamu zenu.
Вы же, доме Израилев, сице глаголет Адонаи Господь: кийждо кумиры своя отимите, и потом аще послушаете Мене, и имене Моего святаго не осквернавите ксему в дарех ваших и рукотворениих ваших:
40 Kwa kuwa juu ya mlima wangu mtakatifu, juu ya kilele cha mlima wa Israeli-hivi ndivyo Bwana Yahwe asemavyo-wote wa nyumba ya Israeli mtaniabudu huko katika nchi. Nitabarikiwa kwa kutaka sadaka zenu huko, na pia malimbuko yenu ya shukrani pamoja na vitu vyenu vyote vitakatifu.
понеже на горе Моей святей, на горе высоце Израилеве, глаголет Адонаи Господь, тамо послужат Ми весь дом Израилев до конца на земли, и тамо прииму я и тамо присещу на приношения ваша и начатки обетов ваших во всех освященных ваших.
41 Nitawapokea kama harufu nzuri ya ubani wakati nitakapowatoa kutoka wale watu na kuwakusanya toka nchi ambazo mlizotawanyika. Nitajifunua mimi mwenyewe kama mtakatifu ndani yenu kwa ajili ya mataifa waone.
В воню благовония прииму вы, егда изведу вы из людий и прииму вы от стран, в няже расточени бысте, и освящуся в вас пред очима людскима:
42 Kisha, wakati nitakapowaleta katika nchi ya Israeli, kwenye nchi ambayo niliuinulia mkono wangu kuapa kuwapatia baba zenu, mtajua yakwamba mimi ni Yahwe.
и увесте, яко Аз Господь, егда введу вы в землю Израилеву, в землю, на нюже воздвигох руку Мою дати ю отцем вашым:
43 Kisha mtazikumbuka njia zenu mbaya huko, na matendo yenu yote machafu mliyoyafanya wenyewe, na mtajichukia wenyewe katika macho yenu kwa matendo yenu yote maovu mliyoyafanya.
и помянете тамо пути вашя и вся мерзкия грехи вашя, в нихже осквернистеся, и посрамите лица ваша во всех злобах ваших, яже сотвористе:
44 Hivyo mtajua kwamba mimi ni Yahwe nifanyapo haya kwenu kwa ajili ya jina langu, sio kwa njia zenu mbaya au matendo yenu mabovu, nyumba ya Israeli-hivi ndivyo Bwana Yahwe asemavyo.”'
и познаете, яко Аз Господь, егда сотворю вам тако, яко да имя Мое не осквернится по путем вашым злым и по рукотворением вашым растленным, доме Израилев, глаголет Адонаи Господь.
45 Kisha neno la Yahwe likanijia, kusema,
И бысть слово Господне ко мне глаголя:
46 “Mwanadamu, weka uso wako kuelekea nchi za kusini, na kuongea juu ya kusini; tabiri juu ya msitu wa Negebu.
сыне человечь, утверди лице твое на юг и воззри на дарома, и прорцы на дубраву старейшину нагева
47 Uuambie msitu wa Negebu, 'Hivi ndivyo Yahwe asemavyo-Bwana Yahwe asema hivi: Tazama, nitaweka moto ndani yako. Utakula kila mti mbichi na kila mti mkavu ndani yako. Miali ya moto haitazimika; na kila uso utokao kusini hata kaskazini utateketezwa kwa moto.
и речеши дубраве нагевове: слыши слово Господне, сия глаголет Адонаи Господь: се, Аз возгнещу в тебе огнь, и пожжет в тебе всяко древо зеленое и всяко древо сухое, не угаснет пламень разжженый, и изгорит в нем всяко лице от полудне до севера,
48 Kisha watu wote wenye mwili watajua yakwamba mimi ni Yahwe nimeuwasha moto, na hautazimika.”'
и увесть всяка плоть, яко Аз Господь разжегох его, и не угаснет.
49 Kisha nimesema, Ee! Bwana Yahwe, Wananisema mimi, 'Je! yeye sio mwenye kusema mafumbo?”'
И рекох: никакоже, Господи, Господи! Сии глаголют ко мне: не притча ли есть сия глаголема?