< Ezekieli 2 >
1 Akanambia, “Mwana wa adamu, simama kwa miguu yako; kisha nitaongea na wewe.”
And he seide to me, Thou, sone of man, stonde on thi feet, and Y schal speke with thee.
2 Kisha, alipokuwa akiongea na mimi, Roho akaingia ndani yangu na ikaniweka kwenye miguu yangu, na nikamsikia akiongea na mimi.
And the spirit entride in to me, after that he spak to me, and settide me on my feet. And Y herde oon spekynge to me,
3 Akanambia, “Mwana wa adamu, nakutuma kwa watu wa Israeli, kwa mataifa yanayoasi ambayo yameasi dhidi yangu-wote wao na babu zao wameasi juu yangu hata hivi leo!
and seiynge, Sone of man, Y sende thee to the sones of Israel, to folkis apostatas, `ether goynge a bak fro feith, that yeden awei fro me; the fadris of hem braken my couenaunt til to this dai.
4 Vizazi vyao vina sura za kikaidi na mioyo migumu. Nakutuma wewe kwenda kwao, na utawaambia, 'Hivi ndivyo Bwana Yahwe asemavyo.'
And the sones ben of hard face, and of vnchastisable herte, to whiche Y sende thee. And thou schalt seie to hem, The Lord God seith these thingis;
5 Labda watasikia au hawatasikia. Ni nyumba za uasi, lakini angalau watajua kwamba nabii alikuwa miongoni mwao.
if perauenture nameli thei heren, and if perauenture thei resten, for it is an hous terrynge to wraththe. And thei schulen wite, that a profete is in the myddis of hem.
6 Wewe, mwanadamu, usiwaogope au maneno yao. Usiogope, ingawa utakuwa pamoja na mitemba na miiba na ijapokuwa unaishi na nge. Usiogope maneno yao au kuvunjika moyo kwa nyuso zao, kwa kuwa ni nyumba zenye kuasi.
Therfore thou, sone of man, drede not hem, nether drede thou the wordis of hem; for vnbileueful men and distrieris ben with thee, and thou dwellist with scorpiouns. Drede thou not the wordis of hem, and drede thou not the faces of hem, for it is an hous terrynge to wraththe.
7 Lakini utawaambia maneno yangu, labda watasikia au hapana, kwa sababu ni waasi mno.
Therfor thou schalt speke my wordis to hem, if perauenture thei heren, and resten, for thei ben terreris to wraththe.
8 Lakini wewe, mwanadamu, silikiliza kile nisemacho kwako. Usiwe muasi kama nyumba za uasi. Fungua mdomo wako na ule kile ninachotaka kukupa!”
But thou, sone of man, here what euer thingis Y schal speke to thee; and nyle thou be a terrere to wraththe, as the hows of Israel is a terrere to wraththe. Opene thi mouth, and ete what euer thingis Y yyue to thee.
9 Kisha nikaona, na mkono ulikuwa umenyooshwa kwangu; ndani yake kulikuwa na hati ya kukunja.
And Y siy, and lo! an hond was sent to me, in which a book was foldid togidere.
10 Akaikinjua mbele yangu; ilikuwa imeandikwa pande zote mbele na nyuma, na yalikuwa yameandikwa maombolezo kwenye hiyo hati ya kukunja, na huzuni, na ole.
And he spredde abrood it bifor me, that was writun with ynne and with outforth. And lamentaciouns, and song, and wo, weren writun ther ynne.