< Ezekieli 2 >

1 Akanambia, “Mwana wa adamu, simama kwa miguu yako; kisha nitaongea na wewe.”
He said to me, “You human, stand up while I speak to you.”
2 Kisha, alipokuwa akiongea na mimi, Roho akaingia ndani yangu na ikaniweka kwenye miguu yangu, na nikamsikia akiongea na mimi.
While he spoke to me, [God’s] Spirit entered me and enabled me to stand up. Then I heard him speak to me.
3 Akanambia, “Mwana wa adamu, nakutuma kwa watu wa Israeli, kwa mataifa yanayoasi ambayo yameasi dhidi yangu-wote wao na babu zao wameasi juu yangu hata hivi leo!
He said, “You human, I will send you to the Israeli people. They are people who have turned away from me and rebelled against me. Their ancestors rebelled against me, and they themselves are still rebelling against me.
4 Vizazi vyao vina sura za kikaidi na mioyo migumu. Nakutuma wewe kwenda kwao, na utawaambia, 'Hivi ndivyo Bwana Yahwe asemavyo.'
The people to whom I will send you are very stubborn [DOU]. But say to them, ‘This is what Yahweh the Lord says to you.’
5 Labda watasikia au hawatasikia. Ni nyumba za uasi, lakini angalau watajua kwamba nabii alikuwa miongoni mwao.
[when you tell them my messages], perhaps those rebellious people will heed those messages and perhaps they will not heed them, but they will know [you are] a prophet who has been among them.
6 Wewe, mwanadamu, usiwaogope au maneno yao. Usiogope, ingawa utakuwa pamoja na mitemba na miiba na ijapokuwa unaishi na nge. Usiogope maneno yao au kuvunjika moyo kwa nyuso zao, kwa kuwa ni nyumba zenye kuasi.
And you human, you must not be afraid of them or afraid of what they say. [Living among them will be like] living in the midst of briers or scorpions, but do not be afraid of them. They are rebellious people [MTY], but do not allow them to cause you to become afraid.
7 Lakini utawaambia maneno yangu, labda watasikia au hapana, kwa sababu ni waasi mno.
Tell them my message, but do not expect them to pay attention to it, because they [very] rebellious.
8 Lakini wewe, mwanadamu, silikiliza kile nisemacho kwako. Usiwe muasi kama nyumba za uasi. Fungua mdomo wako na ule kile ninachotaka kukupa!”
But human, you must pay attention to what I say. Do not be rebellious like they are. [Now] open your mouth and eat what I give to you.”
9 Kisha nikaona, na mkono ulikuwa umenyooshwa kwangu; ndani yake kulikuwa na hati ya kukunja.
Then, as I watched, I saw his hand that was stretched toward me. In his hand was a scroll.
10 Akaikinjua mbele yangu; ilikuwa imeandikwa pande zote mbele na nyuma, na yalikuwa yameandikwa maombolezo kwenye hiyo hati ya kukunja, na huzuni, na ole.
He unrolled the scroll. On both sides of it were written words that expressed sorrow and mourning and words about trouble/disaster.

< Ezekieli 2 >