< Ezekieli 2 >

1 Akanambia, “Mwana wa adamu, simama kwa miguu yako; kisha nitaongea na wewe.”
And he said unto me, —Son of man, Stand upon thy feet, that I may, speak with thee.
2 Kisha, alipokuwa akiongea na mimi, Roho akaingia ndani yangu na ikaniweka kwenye miguu yangu, na nikamsikia akiongea na mimi.
Then the Spirit entered into me as soon as he spake unto me, and it caused me to stand upon my feet, —and I heard one speaking unto me.
3 Akanambia, “Mwana wa adamu, nakutuma kwa watu wa Israeli, kwa mataifa yanayoasi ambayo yameasi dhidi yangu-wote wao na babu zao wameasi juu yangu hata hivi leo!
And he said unto me- Son of man I am sending thee unto the sons of Israel, unto rebellious nations, which have rebelled against me, —they, and their fathers have transgressed against me, until this very day;
4 Vizazi vyao vina sura za kikaidi na mioyo migumu. Nakutuma wewe kwenda kwao, na utawaambia, 'Hivi ndivyo Bwana Yahwe asemavyo.'
and it is unto such sons—of shameless face, and emboldened heart, that I am sending thee, —therefore shalt thou say unto them, Thus saith My Lord, Yahweh.
5 Labda watasikia au hawatasikia. Ni nyumba za uasi, lakini angalau watajua kwamba nabii alikuwa miongoni mwao.
And they! whether they will hear or whether they will forbear, for a perverse house, they are, shall then know that, a prophet, hath been in their midst.
6 Wewe, mwanadamu, usiwaogope au maneno yao. Usiogope, ingawa utakuwa pamoja na mitemba na miiba na ijapokuwa unaishi na nge. Usiogope maneno yao au kuvunjika moyo kwa nyuso zao, kwa kuwa ni nyumba zenye kuasi.
But thou son of man Be not afraid of them Nor of their words, be afraid Though thorns and thistles are about thee, And amongst prickly plants, thou dost dwell, Of their words, be not afraid nor At their faces, be thou dismayed, For a perverse house, they are!
7 Lakini utawaambia maneno yangu, labda watasikia au hapana, kwa sababu ni waasi mno.
Thou shalt therefore speak my words unto them, whether they will hear, or whether they will forbear For perverse, they are!
8 Lakini wewe, mwanadamu, silikiliza kile nisemacho kwako. Usiwe muasi kama nyumba za uasi. Fungua mdomo wako na ule kile ninachotaka kukupa!”
Thou, therefore son of man, hear what I am speaking unto thee., become not perverse like the perverse house, —open thy mouth, and eat that which I am giving unto thee.
9 Kisha nikaona, na mkono ulikuwa umenyooshwa kwangu; ndani yake kulikuwa na hati ya kukunja.
So I looked, and lo! a hand put forth unto me, —and lo! therein a scroll;
10 Akaikinjua mbele yangu; ilikuwa imeandikwa pande zote mbele na nyuma, na yalikuwa yameandikwa maombolezo kwenye hiyo hati ya kukunja, na huzuni, na ole.
and he spread it out before me, and, it was written on the front and the back, —and there were written thereon, lamentation and sighing, and wailing.

< Ezekieli 2 >