< Ezekieli 2 >

1 Akanambia, “Mwana wa adamu, simama kwa miguu yako; kisha nitaongea na wewe.”
His appearance [was] of the likeness of the glory of YHWH, and I see, and fall on my face, and I hear a voice speaking, and He says to me, “Son of man, stand on your feet, and I speak with you.”
2 Kisha, alipokuwa akiongea na mimi, Roho akaingia ndani yangu na ikaniweka kwenye miguu yangu, na nikamsikia akiongea na mimi.
And [the] Spirit comes into me when He has spoken to me, and causes me to stand on my feet, and I hear Him who is speaking to me.
3 Akanambia, “Mwana wa adamu, nakutuma kwa watu wa Israeli, kwa mataifa yanayoasi ambayo yameasi dhidi yangu-wote wao na babu zao wameasi juu yangu hata hivi leo!
And He says to me, “Son of man, I am sending you to the sons of Israel, to rebelling nations who have rebelled against Me; they and their fathers have transgressed against Me, to this very day.
4 Vizazi vyao vina sura za kikaidi na mioyo migumu. Nakutuma wewe kwenda kwao, na utawaambia, 'Hivi ndivyo Bwana Yahwe asemavyo.'
And the sons [are] brazen-faced and hard-hearted to whom I am sending you, and you have said to them: Thus said Lord YHWH.
5 Labda watasikia au hawatasikia. Ni nyumba za uasi, lakini angalau watajua kwamba nabii alikuwa miongoni mwao.
And they—whether they hear, or whether they refrain, for they [are] a house of rebellion—have known that a prophet has been in their midst.
6 Wewe, mwanadamu, usiwaogope au maneno yao. Usiogope, ingawa utakuwa pamoja na mitemba na miiba na ijapokuwa unaishi na nge. Usiogope maneno yao au kuvunjika moyo kwa nyuso zao, kwa kuwa ni nyumba zenye kuasi.
And you, son of man, you are not afraid of them, indeed, you are not afraid of their words, for briers and thorns are with you, and you are dwelling near scorpions, you are not afraid of their words, and you are not frightened of their faces, for they [are] a house of rebellion,
7 Lakini utawaambia maneno yangu, labda watasikia au hapana, kwa sababu ni waasi mno.
and you have spoken My words to them, whether they hear or whether they refrain, for they [are] a rebellion.
8 Lakini wewe, mwanadamu, silikiliza kile nisemacho kwako. Usiwe muasi kama nyumba za uasi. Fungua mdomo wako na ule kile ninachotaka kukupa!”
And you, son of man, hear that which I am speaking to you; do not be of rebellion like the house of rebellion, open your mouth and eat that which I am giving to you.”
9 Kisha nikaona, na mkono ulikuwa umenyooshwa kwangu; ndani yake kulikuwa na hati ya kukunja.
And I look, and behold, a hand [is] sent forth to me, and behold, a roll of a scroll [is] in it,
10 Akaikinjua mbele yangu; ilikuwa imeandikwa pande zote mbele na nyuma, na yalikuwa yameandikwa maombolezo kwenye hiyo hati ya kukunja, na huzuni, na ole.
and He spreads it before me, and it is written in front and behind, and written on it [are] lamentations, and mourning, and woe!

< Ezekieli 2 >