< Ezekieli 2 >
1 Akanambia, “Mwana wa adamu, simama kwa miguu yako; kisha nitaongea na wewe.”
And he said vnto me, Sonne of man, stand vp vpon thy feete, and I wil speake vnto thee.
2 Kisha, alipokuwa akiongea na mimi, Roho akaingia ndani yangu na ikaniweka kwenye miguu yangu, na nikamsikia akiongea na mimi.
And the Spirite entred into me, when he had spoken vnto me, and set me vpon my feete, so that I heard him that spake vnto me.
3 Akanambia, “Mwana wa adamu, nakutuma kwa watu wa Israeli, kwa mataifa yanayoasi ambayo yameasi dhidi yangu-wote wao na babu zao wameasi juu yangu hata hivi leo!
And he said vnto me, Sonne of man, I send thee to the children of Israel, to a rebellious nation that hath rebelled against me: for they and their fathers haue rebelled against me, euen vnto this very day.
4 Vizazi vyao vina sura za kikaidi na mioyo migumu. Nakutuma wewe kwenda kwao, na utawaambia, 'Hivi ndivyo Bwana Yahwe asemavyo.'
For they are impudent children, and stiffe hearted: I do send thee vnto them, and thou shalt say vnto them, Thus saith the Lord God.
5 Labda watasikia au hawatasikia. Ni nyumba za uasi, lakini angalau watajua kwamba nabii alikuwa miongoni mwao.
But surely they will not heare, neither in deede will they cease: for they are a rebellious house: yet shall they knowe that there hath bene a Prophet among them.
6 Wewe, mwanadamu, usiwaogope au maneno yao. Usiogope, ingawa utakuwa pamoja na mitemba na miiba na ijapokuwa unaishi na nge. Usiogope maneno yao au kuvunjika moyo kwa nyuso zao, kwa kuwa ni nyumba zenye kuasi.
And thou sonne of man, feare them not, neither be afraide of their wordes, although rebels, and thornes be with thee, and thou remainest with scorpions: feare not their wordes, nor be afrayde at their lookes, for they are a rebellious house.
7 Lakini utawaambia maneno yangu, labda watasikia au hapana, kwa sababu ni waasi mno.
Therefore thou shalt speake my words vnto them: but surely they will not heare, neither will they in deede cease: for they are rebellious.
8 Lakini wewe, mwanadamu, silikiliza kile nisemacho kwako. Usiwe muasi kama nyumba za uasi. Fungua mdomo wako na ule kile ninachotaka kukupa!”
But thou sonne of man, heare what I say vnto thee: be not thou rebellious, like this rebellious house: open thy mouth, and eate that I giue thee.
9 Kisha nikaona, na mkono ulikuwa umenyooshwa kwangu; ndani yake kulikuwa na hati ya kukunja.
And when I looked vp, beholde, an hande was sent vnto me, and loe, a roule of a booke was therein.
10 Akaikinjua mbele yangu; ilikuwa imeandikwa pande zote mbele na nyuma, na yalikuwa yameandikwa maombolezo kwenye hiyo hati ya kukunja, na huzuni, na ole.
And he spred it before me, and it was written within and without, and there was written therein, Lamentations, and mourning, and woe.