< Ezekieli 2 >

1 Akanambia, “Mwana wa adamu, simama kwa miguu yako; kisha nitaongea na wewe.”
“Stand up, son of man, because I want to talk to you,” he said to me.
2 Kisha, alipokuwa akiongea na mimi, Roho akaingia ndani yangu na ikaniweka kwenye miguu yangu, na nikamsikia akiongea na mimi.
As he spoke to me, the Spirit entered me and had me stand up. I listened to him speaking to me.
3 Akanambia, “Mwana wa adamu, nakutuma kwa watu wa Israeli, kwa mataifa yanayoasi ambayo yameasi dhidi yangu-wote wao na babu zao wameasi juu yangu hata hivi leo!
“Son of man,” he told me, “I'm sending you to the people of Israel, a disobedient nation that has rebelled against me. They and their forefathers have continued to rebel against me, even up to today.
4 Vizazi vyao vina sura za kikaidi na mioyo migumu. Nakutuma wewe kwenda kwao, na utawaambia, 'Hivi ndivyo Bwana Yahwe asemavyo.'
They are pig-headed; they are hard-hearted children. I am sending you to tell them that this is what the Lord God says.
5 Labda watasikia au hawatasikia. Ni nyumba za uasi, lakini angalau watajua kwamba nabii alikuwa miongoni mwao.
Whether they listen or not—for they are a rebellious people—they will realize that a prophet has come to them.
6 Wewe, mwanadamu, usiwaogope au maneno yao. Usiogope, ingawa utakuwa pamoja na mitemba na miiba na ijapokuwa unaishi na nge. Usiogope maneno yao au kuvunjika moyo kwa nyuso zao, kwa kuwa ni nyumba zenye kuasi.
Son of man, don't be afraid of them or what they say. You don't need to be afraid even though you're surrounded by brambles and thorns, even though you live among scorpions. Don't be afraid of what they say or be discouraged by the way they look at you, even though they are a rebellious family.
7 Lakini utawaambia maneno yangu, labda watasikia au hapana, kwa sababu ni waasi mno.
Just tell them what I say, whether they listen or not, because they're rebels.
8 Lakini wewe, mwanadamu, silikiliza kile nisemacho kwako. Usiwe muasi kama nyumba za uasi. Fungua mdomo wako na ule kile ninachotaka kukupa!”
As for you, son of man, pay attention to what I tell you. Don't be rebellious like those rebellious people. Open your mouth and eat what I'm about to give you.”
9 Kisha nikaona, na mkono ulikuwa umenyooshwa kwangu; ndani yake kulikuwa na hati ya kukunja.
I looked up and saw a hand stretched out to me holding a scroll.
10 Akaikinjua mbele yangu; ilikuwa imeandikwa pande zote mbele na nyuma, na yalikuwa yameandikwa maombolezo kwenye hiyo hati ya kukunja, na huzuni, na ole.
He spread it out in front of me, and there written on both the front and back were words of grief, mourning, and tragedy.

< Ezekieli 2 >