< Ezekieli 18 >

1 Neno la Yahwe likanijia tena, kusema,
Yahweh gave me another message. [He said, ]
2 “Je mnamaana gani, ninyi mliotumia hii mithali kuhusiana na nchi ya Israeli na kusema, 'Wababa wamekula zabibu mbichi, na meno ya watoto imetiwa ganzi'?
“You people quote [RHQ] this proverb [and say that it is] about Israel: ‘Parents/People eat sour grapes, but it is their children who have a very sour taste in their mouths', [which means that you think that it is not fair for you to be punished for your ancestors’ sins].
3 Kama nishivyo-hivi ndivyo Bwana Yahwe asemavyo-bila shaka hakutakuwa na fursa yoyote tena kwa ajili yenu kuitumia hii mithali katika Israeli.
But [I], Yahweh the Lord, declare that [as surely] as I am alive, you Israeli people will no longer quote that proverb.
4 Tazama! Kila uhai ni mali yangu-uhai wa baba na uhai wa mwana pia, ni mali yangu! roho itendayo dhambi ndiyo itakayokufa!
Everyone [who is alive] belongs to me. That includes children and their parents; they all belong to me. And it is those who sin who will [because of their sins].
5 Itasemwaje kuhusu mtu mwenye haki na achukuaye yaliyo halali na haki-
[So, ] suppose there is a righteous person [always] does what is fair and right [DOU].
6 kama asipokula juu ya milima au kuinua macho yake kwa sananmu za nyumba ya Israeli, na hakumnajisi mke wa jirani yake, wala kumsemesha mwanamke katika kipindi chake cha mwezi, je! Yu mwenye haki?
He does not [meat sacrificed to idols] on the hilltops, he does not request help from idols. He does not have sex with someone else’s wife or have sex with a woman during her monthly menstrual period.
7 Je! Itasemwaje kuhusu mtu ambaye hakumkandamiza yeyote, na kumrudisha mdeni wake kwa kile kilichokuwa kimewekwa kwa ajili ya rehani, na hakuiba lakini kuwapatia chakula wenye njaa na kuwafunika uchi kwa nguo, je yu mwenye haki?
He does not mistreat/oppress people; if [borrows money from him and gives him his cloak to guarantee that he will pay the money back], he always gives the cloak back to that [before the sun goes down]. He does not rob people. He gives food to hungry people. He gives clothing to people who need clothes.
8 Je! Itasemwaje kuhusu mtu ambaye hakuchukua faida kubwa kwa ile pesa aliyokopa, na hakuchukua faida kubwa kwa kile alichokiuza?
When he lends money to people, he does not [do it just to] charge big interest. He does not do [SYN] things that are evil. He [always] decides things fairly.
9 Amesemwa kwamba amechukua yaliyo halali na kuimarisha uaminifu kati ya watu. Kama huyo mtu akitembea katika sheria zangu na kuzishika hukumu zangu kufanya kwa uaminifu, kisha ahadi kwa ajili ya mtu mwenye haki ni hii: Ataishi hakika! -hivi ndivyo Bwana Yahwe asemavyo.
He faithfully obeys all [DOU] my laws. That man is truly righteous; he will remain alive. [That is what I, ] Yahweh the Lord, promise.
10 Lakini akizaa mwana mnyang'anyi mmwaga damu na kufanya mengi katika haya mambo kama yalivyotajwa hapa,
But suppose that man has a son who acts violently, who murders people and does any of these other things, even though his father has not done any of them:
11 hata kama baba yake hakufanya mojawapo katika haya mambo, lakini akala juu ya milima na akamnajisi mke wa jirani yake, Je! itasemwaje juu yake?
He [meat sacrificed to idols] on the hilltops. He has sex with other people’s wives.
12 Huyu mtu huwakandamiza maskini na wahitaji, na huwakamata na kuwanyang'anya, na hawarudishii dhamana, na huyanua macho yake kwa sanamu na kufanya matendo maovu,
He mistreats/oppresses poor and needy people. He robs people. If someone gives him his cloak to [that he will pay the money back], he never gives the cloak back to [before the sun goes down]. He seeks help from idols. He does [other] detestable things.
13 na hukopesha pesa kwa faida ya juu sana na kufanya faida kubwa juu ya anachokiuza, Je! huyo mtu ataishi? Hakika hataishi! Atakufa hakika na damu yake itakuwa juu yake kwa sababu amefanya haya mambo ya chuki.
When he lends money, he [very big] interest. If you think that such a person [be allowed to] remain alive [RHQ], you are certainly wrong. Because he has done those detestable things, he will surely be executed, and it will be his own fault [IDM].
14 Lakini Tazama! tuseme kuna mtu aliyezaa mwana, na mwana wake huona dhambi zote za baba yake alizozifanya, na kupitia kuziona, hakuyafanya hayo mambo.
But suppose that man has a son who sees all the sins that his father commits, but he does not do those things:
15 Huyo mwana hakula juu ya milima, na hakuinua macho yake kwa sanamu za nyumba ya Israeli, na hakumtia unajisi mke wa jirani yake, Je! itasemwaje juu yake?
He does not [meat sacrificed to idols] on the hilltops. He does not request help from idols. He does not have sex with other people’s wives.
16 Yule mwana hakumkandamiza yeyote, au kutwaa dhamana, au kupoteza vitu, lakini badala yake kutoa chakula chake kwa wenye njaa na kuwafunika wenye uchi kwa nguo.
He does not mistreat/oppress people. If he lends money to someone, he does not require that person to give him his cloak to guarantee that he will pay the money back. He does not rob anyone. He gives food to those who need it. He gives clothes to those who need clothes.
17 Huyo mwana hakumkandamiza yeyote au au kuchukua faida ambayo ni ya juu sana au kufanya manufaa kwa ajili ya mkopo, lakini ameyashika maagizo yangu na kuenenda sawa sawa na sheria zangu; huyo mwana hatakufa kwa ajili ya dhambi za baba yake: Ataishi hakika!
He does not commit sins, [like his father did], and does not charge big interest [DOU] when he lends money. He faithfully obeys [all] [DOU] my laws. That person will not be executed for his father’s sins; he will surely remain alive.
18 Baba yake, kwa kuwa aliwakandamiza wengine kwa nguvu nyingi na kumnyang'anya ndugu yake, na kufanya yasiyo mema miongoni mwa watu wake-tazama, atakufa katika uovu wake.
But his father will be executed for the sins that he committed, because he cheated people and robbed people and did [other] things that are evil.
19 Lakini ninyi husema, 'Kwa nini mwana asibebe uovu wa baba yake?' Kwa sababu mwana hubeba yaliyo halali na haki na kuzitunza amri zangu; huzifanya. Ataishi hakika!
[If] you ask, ‘Why should the [man’s] son not (suffer/be punished) for the evil things that his father did?’, [I will answer that] the son has done what is fair and right [DOU] and has obeyed all my laws, so he will surely remain alive.
20 Yule atendaye dhambi, ndiye ambaye atakufa. Mwana hatabeba uovu wa baba yake, na baba hatabeba uovu wa mwana wake. Haki ya yule atendaye haki itakuwa juu yakwe mwenyewe, na uovu wa mwenye uovu utakuwa juu yake mwenyewe.
It is those who sin who will [because of their sins]. People will not be punished for the sins of their parents, or for the sins of their children. Good/Righteous people will be rewarded for their being good/righteous, and evil people will be punished for [doing] evil.
21 Lakini kama mwovu ageukapo kutoka dhambi zake zote alizofanya, na kuzitunza sheria zangu zote na kufanya yaliyo halali na haki, kisha hakika ataishi na hatakufa.
But if a wicked person (turns away from/quits) doing all the evil things that he did previously, and if he starts to obey faithfully all my laws, and does what is fair and right [DOU], he will surely remain alive; he will not be executed.
22 Makosa yote aliyoyafanya hayatakumbukwa juu yake. Ataishi kwa hiyo haki aliyoitenda.
He will not be punished for the sins he committed [previously]. Because of the good/righteous things that he has done [since that time], he [be allowed to] remain alive.
23 Je! Nitafurahia juu ya kifo cha mwovu-hivi ndivyo Bwana Yahwe asemavyo-na sio katika kugeuka kwake kutoka njia yake ili kwamba aweze kuishi?
[I], Yahweh the Lord, declare that I certainly am not [RHQ] happy about wicked people dying. Instead, I am happy when they turn away from their wicked behavior, [because of that, they] remain alive.
24 Lakini kama mtu mwenye haki ageukapo kutoka kwenye haki yake na kufanya maovu na kutenda machukizo kama machukizo yote ambayo mtu mwovu afanyayo, basi ataishi? Haki yake yote aliyoifanya haitakumbukwa wakati atakaponisaliti katika uhaini wake. Hivyo atakufa katika dhambi alizofanya.
But if a righteous person stops doing righteous things and [starts to] commit sins and does the same detestable things that wicked people do, he will certainly not [RHQ] [be allowed to] remain alive. I will not think about the righteous things that he did previously. Because he did not [do what pleases me], and because of [all] the sins that he has committed, he will be executed.
25 Lakini ninyi husema, 'Njia ya Bwana si sawa!' sikilizeni, nyumba ya Israeli! Je njia zangu haziko sawa? Je si njia ambazo haziko sawa?
But you say, ‘Yahweh does not act fairly!’ You Israeli people, listen to what I say: It is certainly not [RHQ] what I do that is unfair, it is what you continually do that is not fair/right!
26 Wakati mtu mwenye haki ageukapo kutoka kwenye makosa yake, na kufanya maovu na kufa kwa sababu ya hayo, kisha atakufa katika uovu ambao alioufanya.
If a righteous person (turns away from/quits) doing what is righteous and commits sins, he will [for committing those sins].
27 Lakini wakati mtu mwovu ageukapo kutoka uovu wake alioufanya na kufanya yaliyo halali na haki, kisha ataulinda uhai wake.
But if a wicked person turns away from doing wicked things and does what is just and right [DOU], he will save [from being executed/punished].
28 Kwa kuwa ameona na kugeuka kutokana na makosa yake yote ambayo aliyoyafanya. Hakika ataishi, na hatakufa.
Because he has thought about all the evil things that he did and has turned away from doing them, he will [be allowed to] live. He will not be executed [for having done evil things].
29 Lakini nyumba ya Israeli husema, 'Njia ya Bwana haiko sawa!' Ni namna gani njia zangu si sawa, nyumba ya Israeli? Ni njia zenu ndizo si sawa.
But [you] Israeli people [MTY] say, ‘Yahweh does not act fairly.’ You people of Israel, my behavior is certainly not [RHQ] unfair! It is your behavior that is not right.
30 Kwa hiyo nitamuhukumu kila mtu miongoni mwenu kulingana na njia zake, nyumba ya Israeli! -hivi ndivyo Bwana Yahwe asemavyo. Tubuni na rudini kutoka kwenye makosa yenu yote ili kwamba wasiwe kikwazo cha uovu dhidi yenu.
Therefore, you Israeli people [MTY], I, Yahweh the Lord, will judge each of you according to what you have done. Repent! Turn [away] from all your wicked behavior! Then you will not be destroyed [PRS] because of your sins.
31 Tupilia mbali makosa yenu yote mliyoyafanya; jifanyieni moyo mpya na roho mpya. Kwa nini mfe, nyumba ya Israeli?
Get rid of all your wicked behavior, and get a new way of thinking [IDM, DOU]. You Israeli people [MTY], (do you really want to be executed for your sins?/you act as though you want to be executed [for your sins]) [RHQ].
32 Kwa kuwa sifurahii kifo cha yule afaye-hivi ndivyo Bwana Yahwe asemavyo-hivyo tubuni na muishi!”
[I], Yahweh the Lord, declare that I am not pleased about your dying. So repent, and remain alive!”

< Ezekieli 18 >