< Ezekieli 17 >
1 Neno la Yahwe likanijia, kusema,
La parole de Yahvé me fut adressée, en ces mots:
2 “Mwanadamu, tega kitendawili na sema fumbo kwa nyumba ya Israeli.
Fils d'homme, raconte une énigme, et dis une parabole à la maison d'Israël.
3 Sema, 'Bwana Yahwe asema hivi: Tai mkubwa pamoja na mabawa makubwa na vipapatio virefu, mwenye kujaa manyoya, na aliyekuwa na rangi nyingi alienda Lebanoni na kuchukua kilele cha mti wa mkangazi.
Tu diras: « Le Seigneur Yahvé dit: Un grand aigle aux grandes ailes et aux longues plumes, plein de plumes de diverses couleurs, vint au Liban et prit la cime du cèdre.
4 Akakata ncha za matawi na kuzichukua hata nchi ya Kanaani; akaipanda katika mji wa manahodha.
Il coupa le plus haut de ses jeunes rameaux, et le transporta dans un pays de trafic. Il le planta dans une ville de marchands.
5 Pia akachukua mbegu ya nchi na kuipanda katika udongo wenye rutuba. Akaiweka kando ya maji mengi kama mti umeao karibu na maji.
"''Il prit aussi une partie de la semence du pays et la planta dans une terre fertile. Il la plaça près de nombreuses eaux. Il la plaça comme un saule.
6 Kisha ukachipusha na mzabibu wenye kusambaa chini kwenye aridhi. Matawi yake yakamwelekea yeye, na mizizi yake ikakua chini yake. Hivyo ukawa mzabibu na kuzaa matawi na kutoa matawi.
Il grandit et devint une vigne étalée, de petite taille, dont les branches étaient tournées vers lui, et dont les racines étaient sous lui. Elle devint donc une vigne, produisit des branches et poussa des rameaux.
7 Lakini kulikuwa na tai mwingine mkubwa wenye mabawa makubwa na manyoya mengi. Tazama! Huu mzabibu ukabadilisha mizizi yake kumwelekea tai, na ukasamabaza matawi yake kumwelekea tai kutoka mahali ulipokuwa umepandwa basi upate kumwagiliwa.
"''Il y avait aussi un autre grand aigle, avec de grandes ailes et beaucoup de plumes. Voici, cette vigne a plié ses racines vers lui, et elle a poussé ses rameaux vers lui, depuis le sol où elle était plantée, afin qu'il l'arrose.
8 Ulikuwa umepandwa kwenye udongo mzuri kando ya maji mengi hivyo ungezaa matawi na kuanza kutoa matunda, ili kuwa mzabibu mzuri kabisa.'
Elle était plantée dans un bon sol, près de beaucoup d'eaux, afin qu'elle produise des branches et qu'elle porte du fruit, pour être une bonne vigne. »''
9 Waambie watu, 'Bwana Yahwe asema hivi: Je! huo utafanikiwa? Je! Haitaing'oa mizizi yake na kuyakata matunda yake ili kwamba unyauke, na majani yake yote mabichi yanyauke? Hakuna jeshi imara au watu wengi watahitajika kuivuta kwa mizizi yake.
Dis: « Le Seigneur Yahvé dit: « Prospère-t-il? N'arrachera-t-il pas ses racines et ne coupera-t-il pas ses fruits, pour qu'il se dessèche, pour que toutes ses feuilles fraîches et printanières se flétrissent? Ce n'est pas par un bras fort ou par un grand nombre de personnes qu'elle pourra être relevée de ses racines.
10 Basi tazama! Baada ya kuwa umepandwa, je utakuwa? Je hautanyauka wakati upepo wa mashariki utakapoupiga? Utanyauka kabisa katika kiwanja chake.”'
Oui, voici, étant plantée, prospérera-t-elle? Ne se desséchera-t-elle pas quand le vent d'orient la touchera? Elle se flétrira dans le sol où elle a poussé. »'"
11 Kisha neno la Yahwe likanijia, kusema,
La parole de Yahvé me fut adressée en ces termes:
12 “Waambie nyumba ya uasi, 'Je! hamjui haya mambo yana gana gani? Tazama! Mfalme wa Babeli amekuja Yerusalemu na kumchukua mfalme wake na wakuu wake na kuwaleta kwake mpaka Babebli.
« Dis maintenant à la maison rebelle: « Ne savez-vous pas ce que signifient ces choses? ». Dis-leur: Voici, le roi de Babylone est venu à Jérusalem, il a pris son roi et ses chefs, et les a emmenés avec lui à Babylone.
13 Kisha akauchukua ukoo wa kifalme, akafanya agano pamoja naye, na kumleta chini ya kiapo. Akawachukua watu wa nchi wenye nguvu,
Il prit l'un des descendants royaux, et fit alliance avec lui. Il le fit aussi jurer, et il enleva les puissants du pays,
14 basi ufalme uwe duni na usijiinue wenyewe. Kwa kulitunza agano lake nchi itaokoka.
afin d'abaisser le royaume, de l'empêcher de se relever, et de le faire subsister en respectant son alliance.
15 Lakini mfalme wa Yerusalemu ameasi juu yake kwa kupeleka mabalozi kwenda Misri ili kujipatia farasi na jeshi. Je! Atafanikiwa? Je! yeye anayeyafanya haya mambo ataokoka?
Mais il s'est rebellé contre lui en envoyant ses ambassadeurs en Égypte, pour qu'ils lui donnent des chevaux et un peuple nombreux. Prospérera-t-il? Celui qui fait de telles choses échappera-t-il? Viendra-t-il à bout de l'alliance, et échappera-t-il quand même?
16 Kama niishivyo! -hivi ndivyo Bwana Yahwe asemavyo-atakufa hakika katika nchi ya mfalme aliyemfanya mfalme, yule mfalme ambaye aliyekidharau kiapo chake, na ambaye aliyevunja agano lake. atakufa kati ya Babeli.
« Je suis vivant, dit le Seigneur Yahvé, dans le lieu où habite le roi qui l'a fait roi, dont il a méprisé le serment et rompu l'alliance, il mourra avec lui au milieu de Babylone.
17 Farao na jeshi lake lenye nguvu na kusanyiko la watu wengi kwa ajili ya vita hawatamlinda katika vita, wakati jeshi la Wababeli watakapojenga tuta la ngome na kuta za ngome ili kuyaharibu maisha ya wengi.
Pharaon, avec sa puissante armée et sa grande troupe, ne l'aidera pas dans la guerre, quand on élèvera des monticules et qu'on construira des forts pour exterminer de nombreuses personnes.
18 Kwa kuwa mfalme amedharau kiapo chake kwa kulivunja agano. Tazama, ameunyoosha kwa mkono wake ili kufanya ahadi na bado ameyafanya haya mambo yote. Hataokoka.
Car il a méprisé le serment en rompant l'alliance; et voici, il avait donné sa main, et pourtant il a fait toutes ces choses. Il ne s'échappera pas.
19 Kwa hiyo Bwana Yahwe asema hivi: Kama niishivyo, Je! hiki hakikuwa kiapo changu kwamba alidharau agano langu alilo livunja? Basi nitaleta nitamwadhibu juu ya kichwa chake!
C'est pourquoi le Seigneur Yahvé dit: 'Je suis vivant! Je ferai retomber sur sa tête mon serment qu'il a méprisé et mon alliance qu'il a rompue.
20 Nitausambaza wavu wangu juu yake, na atanaswa katika wavu wangu wa kutegea. Kisha nitamleta hata Babeli na kuzitekeleza hukumu juu yake huko kwa ajili ya uhaini wake alioufanya amenisaliti!
J'étendrai mon filet sur lui, et il sera pris dans mon piège. Je l'emmènerai à Babylone, et là j'entrerai en jugement avec lui pour la faute qu'il a commise envers moi.
21 Wakimbizi wake wote katika majeshi yake yataanguka kwa upanga, na wale watakaobakia watatawanyika kila mahali. Kisha utajua yakwamba mimi ni Yahwe; nimesema hili litatokea.”
Tous ses fugitifs, dans toutes ses bandes, tomberont par l'épée, et ceux qui resteront seront dispersés à tout vent. Alors vous saurez que c'est moi, Yahvé, qui l'ai dit ».
22 Bwana Yahwe asema hivi, 'Basi mimi mwenyewe nitaichukua sehemu ya juu ya mti wa mkangazi, na nitaupanda mbali na matawi yake laini. Nitaukata, na mimi mwenyewe nitaupanda juu ya mlima mrefu.
« Le Seigneur Yahvé dit: 'Je prendrai aussi une partie de la cime du cèdre et je la planterai. J'arracherai de la cime de ses jeunes rameaux un rameau tendre, et je le planterai sur une montagne élevée et haute.
23 Nitaupanda juu ya milima ya Israeli hivyo utazaa matawi na kuzaa matunda, na utakuwa mkangazi wa fahari ili kwamba kila ndege arukaye ataishi chini ya huo. Watajenga viota chini ya kivuli cha matawi yake.
Je le planterai sur la montagne élevée d'Israël; il produira des rameaux, il portera du fruit, et il sera un bon cèdre. Des oiseaux de toute espèce habiteront à l'ombre de ses branches.
24 Kisha miti yote ya shambani itajua kwamba mimi ni Yahwe. Nimeishusha miti mirefu na nimeiinua juu miti mifupi. Naunyausha mti mbichi na kuufanya mti mkavu kuchanua. Mimi Yahwe, nimesema hivyo hii itatokea; nami nimelifanya hili.'”
Tous les arbres des champs sauront que moi, Yahvé, j'ai fait tomber le grand arbre, j'ai élevé le petit arbre, j'ai desséché l'arbre vert, et j'ai fait prospérer l'arbre sec. "'Moi, Yahvé, j'ai parlé et je l'ai fait.'"