< Ezekieli 17 >

1 Neno la Yahwe likanijia, kusema,
And the word of Jehovah came to me, saying:
2 “Mwanadamu, tega kitendawili na sema fumbo kwa nyumba ya Israeli.
Son of man, put forth a riddle, and speak a parable to the house of Israel;
3 Sema, 'Bwana Yahwe asema hivi: Tai mkubwa pamoja na mabawa makubwa na vipapatio virefu, mwenye kujaa manyoya, na aliyekuwa na rangi nyingi alienda Lebanoni na kuchukua kilele cha mti wa mkangazi.
and say, Thus saith the Lord Jehovah: A great eagle, with great wings, with long feathers, full of plumage, which had divers colors, came to Lebanon, and took the highest branch of a cedar.
4 Akakata ncha za matawi na kuzichukua hata nchi ya Kanaani; akaipanda katika mji wa manahodha.
He cropped off the top of its young twigs, and carried it into a land of traffic; he set it in a city of merchants.
5 Pia akachukua mbegu ya nchi na kuipanda katika udongo wenye rutuba. Akaiweka kando ya maji mengi kama mti umeao karibu na maji.
He took also one of the shoots of the land, and put it in a fruitful field; he placed it by great waters, and set it as a willow-tree.
6 Kisha ukachipusha na mzabibu wenye kusambaa chini kwenye aridhi. Matawi yake yakamwelekea yeye, na mizizi yake ikakua chini yake. Hivyo ukawa mzabibu na kuzaa matawi na kutoa matawi.
And it grew and became a spreading vine of low stature, whose branches turned towards him, and whose roots were under him. It became a vine, that brought forth branches, and shot forth boughs.
7 Lakini kulikuwa na tai mwingine mkubwa wenye mabawa makubwa na manyoya mengi. Tazama! Huu mzabibu ukabadilisha mizizi yake kumwelekea tai, na ukasamabaza matawi yake kumwelekea tai kutoka mahali ulipokuwa umepandwa basi upate kumwagiliwa.
There was also another great eagle, with great wings and many feathers; and, behold, this vine bent its roots toward him, and shot forth its branches toward him, that he might water it from the beds where it was planted.
8 Ulikuwa umepandwa kwenye udongo mzuri kando ya maji mengi hivyo ungezaa matawi na kuanza kutoa matunda, ili kuwa mzabibu mzuri kabisa.'
And yet it was planted in a good soil, by great waters, that it might bring forth branches, and that it might bear fruit, and be a goodly vine.
9 Waambie watu, 'Bwana Yahwe asema hivi: Je! huo utafanikiwa? Je! Haitaing'oa mizizi yake na kuyakata matunda yake ili kwamba unyauke, na majani yake yote mabichi yanyauke? Hakuna jeshi imara au watu wengi watahitajika kuivuta kwa mizizi yake.
Say thou, Thus saith the Lord Jehovah: Shall it prosper? Shall not he pull up its roots, and cut off its fruit, that it wither? In all the leaves of its branching shall it wither; even without a mighty arm, or many people, shall he pluck it up by the roots.
10 Basi tazama! Baada ya kuwa umepandwa, je utakuwa? Je hautanyauka wakati upepo wa mashariki utakapoupiga? Utanyauka kabisa katika kiwanja chake.”'
Yea, behold, it is planted; but shall it prosper? Shall it not utterly wither, when the east wind toucheth it? It shall wither in the beds where it grew.
11 Kisha neno la Yahwe likanijia, kusema,
Moreover, the word of Jehovah came to me, saying:
12 “Waambie nyumba ya uasi, 'Je! hamjui haya mambo yana gana gani? Tazama! Mfalme wa Babeli amekuja Yerusalemu na kumchukua mfalme wake na wakuu wake na kuwaleta kwake mpaka Babebli.
Say now to the rebellious house, Know ye not what these things mean? Say, behold, the king of Babylon came to Jerusalem, and took her king and her princes, and led them with him to Babylon,
13 Kisha akauchukua ukoo wa kifalme, akafanya agano pamoja naye, na kumleta chini ya kiapo. Akawachukua watu wa nchi wenye nguvu,
and took one of the king's offspring, and made a covenant with him, and took an oath of him, and the mighty of the land he took away,
14 basi ufalme uwe duni na usijiinue wenyewe. Kwa kulitunza agano lake nchi itaokoka.
that the kingdom might be brought low, so as not to lift itself up; that the covenant might be kept, and stand.
15 Lakini mfalme wa Yerusalemu ameasi juu yake kwa kupeleka mabalozi kwenda Misri ili kujipatia farasi na jeshi. Je! Atafanikiwa? Je! yeye anayeyafanya haya mambo ataokoka?
But he rebelled against him, in sending his ambassadors into Egypt, that they might give him horses and much people. Shall he prosper? Shall he escape that doeth such things? Shall he break the covenant and be delivered?
16 Kama niishivyo! -hivi ndivyo Bwana Yahwe asemavyo-atakufa hakika katika nchi ya mfalme aliyemfanya mfalme, yule mfalme ambaye aliyekidharau kiapo chake, na ambaye aliyevunja agano lake. atakufa kati ya Babeli.
As I live saith the Lord Jehovah, surely in the place where the king dwelleth that made him king, whose oath he despised, and whose covenant he broke, even with him in the midst of Babylon shall he die.
17 Farao na jeshi lake lenye nguvu na kusanyiko la watu wengi kwa ajili ya vita hawatamlinda katika vita, wakati jeshi la Wababeli watakapojenga tuta la ngome na kuta za ngome ili kuyaharibu maisha ya wengi.
Neither shall Pharaoh with his mighty army and great multitude accomplish anything for him in war, when they shall cast up mounds, and build forts to cut off many persons,
18 Kwa kuwa mfalme amedharau kiapo chake kwa kulivunja agano. Tazama, ameunyoosha kwa mkono wake ili kufanya ahadi na bado ameyafanya haya mambo yote. Hataokoka.
he hath despised the oath, and broken the covenant; behold, he hath given the hand, and yet done all these things; he shall not escape!
19 Kwa hiyo Bwana Yahwe asema hivi: Kama niishivyo, Je! hiki hakikuwa kiapo changu kwamba alidharau agano langu alilo livunja? Basi nitaleta nitamwadhibu juu ya kichwa chake!
Therefore thus saith the Lord Jehovah: As I live, surely mine oath, which he hath despised, and my covenant, which he hath broken, will I recompense upon his own head.
20 Nitausambaza wavu wangu juu yake, na atanaswa katika wavu wangu wa kutegea. Kisha nitamleta hata Babeli na kuzitekeleza hukumu juu yake huko kwa ajili ya uhaini wake alioufanya amenisaliti!
And I will spread my net upon him, and he shall be taken in my snare, and I will bring him to Babylon, and will contend with him there for his trespass which he hath committed against me.
21 Wakimbizi wake wote katika majeshi yake yataanguka kwa upanga, na wale watakaobakia watatawanyika kila mahali. Kisha utajua yakwamba mimi ni Yahwe; nimesema hili litatokea.”
And all his fugitives with all his hosts shall fall by the sword, and they that remain shall be scattered to all the winds; and ye shall know that I, Jehovah, have spoken it.
22 Bwana Yahwe asema hivi, 'Basi mimi mwenyewe nitaichukua sehemu ya juu ya mti wa mkangazi, na nitaupanda mbali na matawi yake laini. Nitaukata, na mimi mwenyewe nitaupanda juu ya mlima mrefu.
Thus saith the Lord Jehovah: I also will take from the top of the high cedar, and will get it; and from the highest of its twigs will I crop a tender one, and plant it upon a high and lofty mountain.
23 Nitaupanda juu ya milima ya Israeli hivyo utazaa matawi na kuzaa matunda, na utakuwa mkangazi wa fahari ili kwamba kila ndege arukaye ataishi chini ya huo. Watajenga viota chini ya kivuli cha matawi yake.
Upon a high mountain of Israel will I plant it, and it shall bring forth boughs, and bear fruit, and be a goodly cedar; and under it shall dwell birds of every wing; in the shadow of its branches shall they dwell.
24 Kisha miti yote ya shambani itajua kwamba mimi ni Yahwe. Nimeishusha miti mirefu na nimeiinua juu miti mifupi. Naunyausha mti mbichi na kuufanya mti mkavu kuchanua. Mimi Yahwe, nimesema hivyo hii itatokea; nami nimelifanya hili.'”
And all the trees of the field shall know that I, Jehovah, have brought down the high tree, and exalted the low tree; that I have dried up the green tree, and made the dry tree green. I, Jehovah, have spoken, and will do it.

< Ezekieli 17 >