< Ezekieli 16 >

1 Kisha neno la Yahwe likanijia, kusema,
And the word of Yahweh came unto me, saying:
2 “Mwanadamu, mwambie Yerusalemu kuhusu machukizo yake,
Son of man Let Jerusalem know her abominations,
3 na useme, 'Bwana Yahwe asema hivi kwa Yerusalemu: Mwanzo wako na kuzaliwa kwako kulichukua nafasi katika nchi ya Kanaani; baba yako alikuwa Mwamori, na mama yako alikuwa Mhiti.
Therefore shalt thou say— Thus saith My Lord. Yahweh To Jerusalem, Thine origin and thy birth, were of the land of the Canaanite, — Thy father was the Amorite And thy mother a Hittite
4 Katika siku ya kuzaliwa kwako, mama yako hakukata kitovu chako, wala hakukuosha kwenye maji usafishwe au kukuchua kwa chumvi, wala kukusitiri nguo.
And, as for thy birth, in the day thou wast born, Thy navel-cord was not cut, And, in water, wast thou not bathed to cleanse thee, — And, as for being salted, thou was not salted, And, as for being bandaged, thou wast not bandaged.
5 Hakuna jicho lililokuhurumia kufanya haya mambo kwa ajili yako, kukuhurumia wewe. Katika siku uliyozaliwa, kwa kuchukiwa uhai wako, ulitupwa nje uwandani.
No eye, threw a shield over thee, by doing for thee one of these things taking pity on thee, - But thou wast cast out on the face of the field Because thy person, was abhorred, in the day thou wast born.
6 Lakini nilipita karibu nawe, nalikuona ukijinyonga kwa damu yako mwenyewe, “kubaki hai!”
And I passed by thee, and looked upon thee, thrusting about thee in thy blood, And said to thee— Despite thy blood, live! Yea I said to thee— Despite thy blood, live!
7 Nimekufanya ukue kama mmea katika shamba. Umeongezeka na kuwa mkubwa, na umekuwa mzuri wa wazuri. Maziwa yako yakawa thabiti, na nywele zako zikawa nyingi, ingawa ulikuwa uchi huna nguo.
Into myriads—like the bud of the field, made I thee, And thou didst increase and become well grown, and didst attain to most excellent adornments, — Thy breasts were well-formed And thy hair was grown, But thou thyself wast utterly naked.
8 Nilipita karibu nawe tena, na nalikuona. Tazama! wakati wa upendo umefika kwako, hivyo nikatandika joho langu juu yako na kufunika uchi wako. Kisha nikaapa kwako na kukuleta kwenye agano-hivi ndivyo Bwana Yahwe asemavyo-na ukawa wangu.
And I passed by thee and looked upon thee and lo! thy time was the time for endearments, So I spread my skirt over thee, and covered thy shame, And took an oath to thee And entered into covenant with thee. Declareth My Lord. Yahweh. And thou didst become mine.
9 Basi nilikuosha kwa maji na kukufuta damu yako, na kukupaka mafuta.
And I bathed thee in water, and rinsed thy blood from off thee, And anointed thee with oil;
10 Nilikuvalisha nguo ya taraza na kukuwekea makuzi ya ngozi kwenye miguu yako. Nilikufungia kwa kitani kizuri na kukufunika kwa hariri.
And clothed thee with an embroidered dress, And sandalled thee in red leather, And wrapped thee about with fine linen, And put over thee a mantle of silk.
11 Kisha nalikupamba kwa vito, na kukuvalisha vikuku kwenye mikono yako, na mkufu kwenye shingo yako.
Then decked I thee with ornaments, And put bracelets upon thy hands, And a neckchain upon thy throat;
12 Nalitia hazama katika pua yako na hereni katika masikio yako, na taji nzuri juu ya kichwa chako.
And put a nose-jewel upon thy nose, And earrings in thine ears, And a crown of adorning, upon thy head.
13 Hivyo ulipambwa kwa dhahabu na fedha, na ulivaa kitani safi, hariri, na ngu za taraza; ulikula unga mzuri, asali, na mafuta, na ulikuwa mzuri sana, na ukawa malkia.
Thus wast thou adorned with gold and silver, And thy raiment was of fine linen and silk and embroidered work, Fine flour and honey and oil, didst thou eat, — And so thou becamest exceedingly beautiful, And didst attain unto royalty.
14 Umaarufu wako ukaenda miongoni mwa mataifa kwa sababu ya uzuri wako, kwa kuwa ulikuwa mkamili katika ukuu niliokuwa nimekupa-hivi ndivyo Bwana Yahwe asemavyo.
Then went forth thy fame among the nations. for thy beauty, - For perfect, it was—in my splendour which I had put upon thee, Declareth My Lord, Yahweh.
15 Lakini ulitumaini uzuri wako, na ukafanya kama kahaba kwa sababu ya umaarufu wako; umeyamwaga matendo yako ya kikahaba kwa kila aliyepita karibu, ili kwamba uzuri wako uwe wake.
Then didst thou trust in thy beauty, And become unchaste, because of thy fame, - And didst pour out thine unchastity upon every passer-by, his it was!
16 Kisha ulichukua nguo zako na pamoja nao umepatengeneza mahali pa juu kwa ajili yako palipambwa kwa rangi tofauti tofauti, na hapo ulifanya kama kahaba. Hii haitatokea. Wala haitatokea.
Yea thou didst take of thy raiment and madest thee high places of hangings, And didst commit unchastity thereon, - Which ought not to have befallen And not to have come to pass.
17 Umevichukua vito vizuri vya dhahabu na fedha nilizowapatia, na umejitengenezea sanamu za wanaume, na umefanya pamoja nao ukahaba afanyao.
But thou didst take thine adorning jewels Of my gold and of my silver which I had given thee, And didst make thee images of the male, — And didst act unchastely with them;
18 Ulichukua nguo zako za tarizi na kuwafunika, na kuwawekea mafuta yangu na manukato mbele yao.
And thou didst take thine embroidered raiment, and cover them, - And mine oil and mine incense, didst thou set before them;
19 Mkate wangu niliokupatia-ulitengenezwa kwa unga mzuri, mafuta, na asali-umeviweka mbele yao kwa ajili ya kunukia harufu nzuri, kwa kuwa hivi ndivyo ilivyotokea-hivi ndivyo Bwana Yahwe asemavyo.
And my food which I had given thee, Fine flour and oil and honey wherewith I fed thee, And didst set it before them for a satisfying odour Yea so it was, — Saith My Lord Yahweh.
20 Kisha uliwachukua watoto wako ulionizalia, na kuwatoa sadaka kwa picha ili waliwe kama chakula. Je! matendo yako ya kikahaba ni kitu kidogo?
And thou didst take thy sons and thy daughters, Whom thou hadst borne unto me, And didst sacrifice them unto them to be devoured, - Is this of thine unchastity. a light thing?
21 Umewachinja watoto wangu na kuwatupia kwenye moto.
Yea thou didst slay my children, — And didst deliver them up. that they should be caused to pass through the fire unto them.
22 Katika machukizo yako yote na matendo yako ya kikahaba hukutafakari kuhusu siku za ujana wako, wakati ulipokuwa uchi na bila nguo kama kama umepigwa katika damu.
And in all thine abominations, and thine unchaste ways, thou rememberedst not the days of thy youth, When thou wast utterly naked. When thou wast thrusting about thee in thy blood!
23 Ole! Ole wako! -hivi ndivyo Bwana Yahwe asemavyo-kwahiyo, zaidi ya hapo kwa haya maovu yote,
And it came to pass after all thy wickedness, Woe! Woe! to thee, Exclaimeth My Lord Yahweh;
24 umejijengea chumba cha chini kwa chini katika kila sehemu ya watu wengi.
That thou didst build thee a brothel, — and didst make thee a height in every broadway:
25 Umepajenga mahali pako palipoinuka kwenye kichwa cha kila njia na kuunajisi uzuri wako, kwa kuwa umeutoa mwili wako kwa kila mtu apitaye karibu na umefanya matendo mengi zaidi ya ukahaba.
At the head of every road, didst thou build thy height, And bring thy beauty into disgust, And open thy feet to every passer-by, So didst thou make thine unchaste ways to abound.
26 Umetenda kama kahaba pamoja na Wamisri, tamaa ya jirani zako, na umetenda matendo mengi zaidi ya kikahaba, ili kuchochea hasira yangu.
Then didst thou extend thine unchaste acts unto the sons of Egypt—thy neighbour great of flesh, - And caused thine unchaste ways to abound provoking me to anger.
27 Tazama! Nitakunyooshea mkono wangu na kupunguza chakula chako. Nitauchukua uhai wako juu ya adui zako, binti za Wafilisti, ambao walikuwa na haya ya tabia yako ya uchafu.
Lo! therefore, I have stretched out my hand against thee, And diminished thine allotted portion, — And have delivered thee up unto the desire of them who hate thee The daughters of the Philistines, who are ashamed of thy lewd way.
28 Umetenda kama kahaba pamoja na Waashuru kwa sababu hukuweza kuridhika. Umetenda kama kahaba na bado hukuridhika.
Thou didst also extend thine unchastity unto the sons of Assyria, because thou wast insatiable. Yet though thou didst behave unchastely with them, yet even so couldst thou not be satisfied,
29 Umefanya matendo mengi zaidi ya kikahaba katika nchi ya jamii ya wana maji wa Ukaldayo, na wala hukuridhika kwa hayo.
Thou didst therefore cause thine unchaste ways to abound unto the land of Canaan as towards Chaldea. Yet even herewith, wast thou not satisfied.
30 Jinsi moyo wako ulivyo dhaifu-hivi ndivyo Bwana Yahwe asemavyo-kwamba utaweza kuyafanya haya mambo yote, matendo ya aibu ya kikahaba?
How weak was thy heart! Exclaimeth My Lord Yahweh, — That thou couldst have done all these things, The doing of a lewd woman without shame:
31 Mmepajenga mahali penu pa juu kwenye kichwa cha kila mtaa na kufanya chumba cha chini kwa chini katika kila sehemu ya watu wengi. Bado hukuwa kama kahaba kwa sababu ulikataa kulipwa ujira.
That thou couldst have built thy brothel at the head of every road, And thy height, couldst have made in every broadway, - Yet becamest not as a harlot to lay claim to a harlot’s hire.
32 Wewe mwanamke mzinifu, wewe upokeaye wageni badala ya mume wako.
A wife who committeth adultery, instead of her husband accepteth strangers.
33 Watu hulipa kwa kila kahaba, lakini wewe huwapa mshara wako wapenzi wako wote na kuwapa rushwa ili waje kwako pande zote kwa matendo yako ya kikahaba.
To all harlots, they give a present, — But, thou, didst give thy presents to all thy lovers, And didst bribe them to come in unto thee from every side, in thine unchastity!
34 Hivyo kuna tofauti kati yako na hao wanawake wengine, kwa kuwa hakuna hata mmoja ajaye kwako kukuuliza kulala pamoja nao. Badala yake, unawalipa. Hakuna akulipaye.
And so there came about in thee, the reverse of women, in thine unchastity, In that they did not follow thee for purposes of lewdness, — And in that thou gavest a present while, no present, was given to thee So didst thou become, the reverse.
35 Kwa hiyo, wewe kahaba, lisikilize neno la Yahwe.
Therefore O harlot, hear thou the word of Yahweh;
36 Bwana Yahwe asema hivi: Kwa sababu umemwaga tamaa yako na kuonyesha sehemu zako za siri kupitia matendo yako ya ukahaba pamoja na wapenzi wako wote pamoja na sanamu zako za chukizo, na kwa sababu ya damu ya watoto wako uliyowapatia sanamu zako,
Thus saith My Lord Yahweh, — Because thy money, was poured out, and thy shame, was uncovered, in thine unchastity, unto thy lovers, —and unto all thine abominable manufactured gods, even as the blood of thy children, whom thou didst deliver up unto them,
37 kwa hiyo, tazama! Nitawakusanya wapenzi wako wote uliokutana nao, wote ambao uliowapenda na wote uliowachukia, na nitawakusanya juu yako kila upande. Nitawaonyesha wazi sehemu zako za siri hivyo wanaweza kuona uchi wako wote.
Therefore behold me! gathering together all thy lovers unto whom thou didst make thyself pleasant, Even all whom thou lovedst, With all whom thou hatedst, — Yea I will gather them together unto thee from every side And will uncover thy shame unto them, And they shall see all thy shame.
38 Kwa kuwa nitakuadhibu kwa uasherati na kumwaga damu, na nitaleta juu yako damu ya hasira yangu na hasira kali.
So will I judge thee. with the judgments meted out to adulteresses and shedders of blood, - And will repay thee with the blood of indignation and jealousy;
39 Nitakutia kwenye mikono yao hivyo watakutupa chini kwenye chumba cha chini kwa chini na kupavunja mahali pako pa juu na watakuvua nguo zako na kuchukua vito vyako vyote. watakuacha uchi bila nguo.
And will deliver thee into their hand. And they shall pull down thy brothel And break in pieces thy heights, And strip thee of thy raiment, And take away thine adorning jewels, - And leave thee utterly naked.
40 Kisha wataleta kundi la watu juu yako na kukupiga kwa mawe, na kukukata kwa panga zao.
Then will they bring up against thee a gathered host, And they will stone thee with stones, - And cut thee to pieces with their swords;
41 Watachoma nyumba zako na kufanya matendo mengi ya adhabu juu yako kwenye uso wa wanawake wengi, kwa kuwa nitakusimamisha ukahaba wako, na hutawalipa tena wapenzi wako.
And burn up thy houses with fire, And execute upon thee judgments before the eyes of many women, —So will I cause thee to cease from acting unchastely, Moreover also a present, shalt thou not give any more.
42 Kisha nitatuliza ghadhabu yangu juu yako; hasira yangu itakuacha, kwa kuwa nitaridhika, na sitakuwa na hasira tena.
So will I let mine indignation find rest in thee, And my jealousy shall depart from thee, —And I will be quiet, and not be provoked any more.
43 Kwa sababu hukuzikumbuka siku za ujana wako na kunifanya nitetemeke kwa hasira kwa sababu ya haya mambo yote, kwa hiyo, tazama! Mimi mwenyewe nitashusha kwa kichwa chako mwenyewe adhabu kwa kile ulichokifanya-hivi ndivyo Bwana Yahwe asemavyo. Hutaongeza ukahaba kwa matendo yako yote ya machukizo?
Because thou hast not remembered the days of thy youth, But hast enraged me with all these things Therefore also behold! I thy way, upon thine own head, will place Declareth My Lord Yahweh, And thou shalt not commit a crime above all thine abominations
44 Tazama! Kila mtu azungumzaye Mithali kuhusu wewe atasema, “Kama alivyo, hivyo pia ni binti yake.”
Lo! every one who useth proverbs, against thee, shall use a proverb saying, — Like the mother, so her daughter!
45 Wewe ni binti wa mama yako, amchukiaye mume wake na mtoto wake, na wewe ni dada wa dada zako aliyewachukia waume zao na watoto wao. Mama yako alikuwa Mhiti, na baba yako alikuwa Mwamori.
The daughter of thy mother, thou art! One abhorring her own husband and her own children, — Yea the sister of thy sisters, thou art Who abhorred their own husbands and their own children, Your mother was a Hittite, And your father an Amorite.
46 Dada yako mkubwa alikuwa Samaria na binti zake walikuwa wale waliokuwa wakiishi kaskazini, wakati dada yako mdogo alikuwa ni yule aliyekuwa akiishi kusini mwako, ambaye ni, Sodoma na binti zake.
And thine elder sister, was Samaria, she and her daughters, dwelling on thy left hand, — And thy sister younger than thou dwelling on thy right hand was Sodom and her daughters.
47 Hukuenenda katika njia zao na kuchukua tabia zao na matendo yao, lakini katika njia zako zote ulikuwa mbaya zaidi kuliko walivyokuwa wao.
Yet not in their ways, didst thou walk, nor according to their abominations, didst thou do, — As though that were quite too little, thou didst corrupt thyself beyond them in all thy ways.
48 Kama niishivyo- hivi ndivyo Bwana Yahwe asemavyo-dada yako Sodoma na binti zake, hawajafanya uovu mwingi kama wewe ulivyofanya na binti zako walivyofanya.
As I live, Declareth My Lord Yahweh, Very! Sodom thy sister had not done, neither she nor her daughters, —as thou and thy daughters have done.
49 Tazama! Hii ilikuwa dhambi ya dada yako Sodoma: Alikuwa na kiburi katika mafanikio yake, uzembe na kutojali kuhusu chochote. Hakuitia nguvu mikono ya maskini na watu wahitaji.
Lo! this became the iniquity of Sodom thy sister, — Pride, fulness of bread, and careless security came to her and to her daughters, And the hand of the oppressed and the needy, she strengthened not.
50 Alikuwa na kiburi na kufanya machukizo mbele yangu, hivyo niliwatoa kama nilivyoona.
So then they became haughty, and committed abomination before me, - And I took them away. when I saw [it],
51 Samaria hakufanya hata nusu ya dhambi zako; badala yake, umefanya machukizo mengi kuliko walivyofanya, na umewonyesha hayo dada zako walikuwa bora kuliko wewe kwa sababu ya machukizo yako uyafanyayo!
Nor did, Samaria, commit, one-half thy sins, — But thou didst multiply thine abominations more than they, And didst cause thy sisters to appear righteous, by all the abominations which thou didst commit.
52 Hasa wewe, umeonyesha aibu yako mwenyewe; kwa njia hii umewaonyesha dada zako walikuwa bora kuliko wewe, kwa sababu ya dhambi ulizozifanya katika hayo machukizo yako yote. Dada zako sasa wanaonekana bora kuliko wewe. Hasa wewe, umeonyesha aibu yako mwenyewe, kwa njia hii umewaonyesha kwamba dada zako walikuwa bora kuliko wewe.
Thou also bear thine own reproach, which thou didst adjudge to thy sisters, by thy sins in which thou wast more abominable than they, thou didst make them appear more righteous than thou, — Thou also, therefore turn thou pale and bear thine own reproach, for making thy sisters appear righteous!
53 Kwa kuwa nitarudisha masalia wao-masalia ya Sodoma na binti zake, na masalia ya Samaria na binti zake; lakini masalia yako yatakuwa miongoni mwao.
When therefore I bring back their captivity, The captivity of Sodom and her daughters, And the captivity of Samaria and her daughters Then will I bring back thy captivities in their midst:
54 Kwa kufikiria haya mambo utaonyesha aibu yako; utakuwa mnyenyekevu kwa sababu ya kila kitu ulichokifanya, na kwa njia hii utakuwa faraja kwao.
That thou mayest bear thine own reproach, And take to thyself reproach because of all that thou didst in comforting them.
55 Hivyo dada yako Sodoma na binti zake watarudishwa kwenye hali yao ya zamani, na Samaria na binti zake watarudishwa kwenye mashamba yao ya zamani. Kisha wewe na binti zako watarudishwa kwenye hali yako ya kawaida.
When thy sisters Sodom and her daughters shall return to their former estate, And Samaria and her daughters shall return to their former estate Then thou and thy daughters, shall return to your former estate.
56 Sodoma dada yako hakutajwa hata kwa kinywa chako katika siku ulipojiinua,
And Sodom thy sister was never heard in thy mouth, —In the day of thy pride:
57 kabla uovu wako haujafunuliwa. Lakini sasa wewe ni kitu cha dharau kwa binti za Edomu na binti wote wa Wafilisti waliomzunguka. Watu wote wanakudharau wewe.
Before thy wickedness was discovered, As now, [thou art] the reproach of the daughters of Syria and all round about her the daughters of the Philistines, —who are despising thee on every side.
58 Utaonyesha aibu yako na matendo yako ya machukizo! -hivi ndivyo Yahwe asemavyo!
As for thy crime and thine abominations, thou thyself, dost bear them, — Declareth Yahweh.
59 Bwana Yahwe asema hivi: Nitashughulika na wewe kama unavyostahili, wewe uliyedharau kiapo chako kwa kulivunja agano.
For Thus, saith My Lord, Yahweh, Therefore will I deal with thee just as thou hast dealt, - In that thou didst despise an oath by breaking a covenant.
60 Lakini mimi mwenyewe nitalikumbuka agano langu nililolifanya pamoja nawe katika siku za ujana wako, nitaliimarisha agano la milele pamoja na wewe.
Therefore will I remember my covenant with thee in the days of thy youth, — And will establish for thee a covenant age-abiding.
61 Kisha utazikumbuka njia zako na kuona aibu utakapo wapokea dada zako wakubwa na dada zako wadogo. Nitakupatia wao kama binti zako, lakini kwa sababu ya agano lako.
Thou shalt therefore remember thy ways and take to thyself reproach, by receiving thy sisters. The older than thou, And the younger than thou, - And I will give them unto thee for daughters Though not by thine own covenant.
62 Mimi nitaweka imara agano lango pamoja nawe, nawe utajua yakwamba mimi ni Yahwe.
But I myself, will establish my covenant with thee— And thou shalt know that I, am Yahweh:
63 Kwa sababu ya haya mambo, utakumbuka kila kitu na kuona aibu, hutafungua mdomo wako tena kuongea kwa sababu ya aibu yako, wakati nitakapokusamehe kwa yale yote uliyoyafanya-hivi ndivyo Bwana Yahwe asemavyo.”'
To the end thou mayest remember and turn pale, and there be to thee no more, an opening of mouth, because of thy reproach, - In that I have accepted a propitiatory covering for thee as to all that thou hast done, Declareth My Lord. Yahweh.

< Ezekieli 16 >