< Ezekieli 16 >

1 Kisha neno la Yahwe likanijia, kusema,
And there is a word of YHWH to me, saying,
2 “Mwanadamu, mwambie Yerusalemu kuhusu machukizo yake,
“Son of man, cause Jerusalem to know her abominations, and you have said,
3 na useme, 'Bwana Yahwe asema hivi kwa Yerusalemu: Mwanzo wako na kuzaliwa kwako kulichukua nafasi katika nchi ya Kanaani; baba yako alikuwa Mwamori, na mama yako alikuwa Mhiti.
Thus said Lord YHWH to Jerusalem: Your birth and your nativity [Are] of the land of the Canaanite, Your father the Amorite, and your mother a Hittite.
4 Katika siku ya kuzaliwa kwako, mama yako hakukata kitovu chako, wala hakukuosha kwenye maji usafishwe au kukuchua kwa chumvi, wala kukusitiri nguo.
As for your nativity, in the day you were born, Your navel has not been cut, And you were not washed in water for ease, And you have not been salted at all, And you have not been swaddled at all.
5 Hakuna jicho lililokuhurumia kufanya haya mambo kwa ajili yako, kukuhurumia wewe. Katika siku uliyozaliwa, kwa kuchukiwa uhai wako, ulitupwa nje uwandani.
No eye has had pity on you, to do any of these to you, To have compassion on you, And you are cast on the face of the field, With loathing of your soul In the day you were born!
6 Lakini nilipita karibu nawe, nalikuona ukijinyonga kwa damu yako mwenyewe, “kubaki hai!”
And I pass over by you, And I see you trodden down in your blood, And I say to you in your blood, Live! Indeed, I say to you in your blood, Live!
7 Nimekufanya ukue kama mmea katika shamba. Umeongezeka na kuwa mkubwa, na umekuwa mzuri wa wazuri. Maziwa yako yakawa thabiti, na nywele zako zikawa nyingi, ingawa ulikuwa uchi huna nguo.
I have made you a myriad as the shoot of the field, And you are multiplied, and are great, And come in with an excellent adornment, Breasts have been formed, and your hair has grown—And you, naked and bare!
8 Nilipita karibu nawe tena, na nalikuona. Tazama! wakati wa upendo umefika kwako, hivyo nikatandika joho langu juu yako na kufunika uchi wako. Kisha nikaapa kwako na kukuleta kwenye agano-hivi ndivyo Bwana Yahwe asemavyo-na ukawa wangu.
And I pass over by you, and I see you, And behold, your time [is] a time of loves, And I spread My skirt over you, And I cover your nakedness, And I swear to you, and come into a covenant with you, A declaration of Lord YHWH, And you become Mine.
9 Basi nilikuosha kwa maji na kukufuta damu yako, na kukupaka mafuta.
And I wash you with water, And I wash away your blood from off you, And I anoint you with oil.
10 Nilikuvalisha nguo ya taraza na kukuwekea makuzi ya ngozi kwenye miguu yako. Nilikufungia kwa kitani kizuri na kukufunika kwa hariri.
And I clothe you with embroidery, And I shoe you with tachash [skin], And I gird you with fine linen, And I cover you with figured silk.
11 Kisha nalikupamba kwa vito, na kukuvalisha vikuku kwenye mikono yako, na mkufu kwenye shingo yako.
And I adorn you with adornments, And I give bracelets for your hands, And a chain for your neck.
12 Nalitia hazama katika pua yako na hereni katika masikio yako, na taji nzuri juu ya kichwa chako.
And I give a ring for your nose, And rings for your ears, And a crown of beauty on your head.
13 Hivyo ulipambwa kwa dhahabu na fedha, na ulivaa kitani safi, hariri, na ngu za taraza; ulikula unga mzuri, asali, na mafuta, na ulikuwa mzuri sana, na ukawa malkia.
And you put on gold and silver, And your clothing [is] fine linen, And figured silk and embroidery, You have eaten fine flour, and honey, and oil, And you are very, very beautiful, And go prosperously to the kingdom.
14 Umaarufu wako ukaenda miongoni mwa mataifa kwa sababu ya uzuri wako, kwa kuwa ulikuwa mkamili katika ukuu niliokuwa nimekupa-hivi ndivyo Bwana Yahwe asemavyo.
And your name goes forth among nations, Because of your beauty—for it [is] complete, In My honor that I have set on you, A declaration of Lord YHWH.
15 Lakini ulitumaini uzuri wako, na ukafanya kama kahaba kwa sababu ya umaarufu wako; umeyamwaga matendo yako ya kikahaba kwa kila aliyepita karibu, ili kwamba uzuri wako uwe wake.
And you trust in your beauty, And go whoring because of your renown, And pour out your whoredoms on everyone passing by—to him [that would have] it.
16 Kisha ulichukua nguo zako na pamoja nao umepatengeneza mahali pa juu kwa ajili yako palipambwa kwa rangi tofauti tofauti, na hapo ulifanya kama kahaba. Hii haitatokea. Wala haitatokea.
And you take from your garments, And make spotted high-places for yourself, And go whoring on them, They are not coming in—nor will it be!
17 Umevichukua vito vizuri vya dhahabu na fedha nilizowapatia, na umejitengenezea sanamu za wanaume, na umefanya pamoja nao ukahaba afanyao.
And you take your beautiful vessels Of My gold and My silver that I gave to you, And make images of a male for yourself, And go whoring with them,
18 Ulichukua nguo zako za tarizi na kuwafunika, na kuwawekea mafuta yangu na manukato mbele yao.
And you take the garments of your embroidery, And cover them, And you have set My oil and My incense before them.
19 Mkate wangu niliokupatia-ulitengenezwa kwa unga mzuri, mafuta, na asali-umeviweka mbele yao kwa ajili ya kunukia harufu nzuri, kwa kuwa hivi ndivyo ilivyotokea-hivi ndivyo Bwana Yahwe asemavyo.
And My bread, that I gave to you, Fine flour, and oil, and honey, that I caused you to eat. You have even set it before them, For a refreshing fragrance—thus it is, A declaration of Lord YHWH.
20 Kisha uliwachukua watoto wako ulionizalia, na kuwatoa sadaka kwa picha ili waliwe kama chakula. Je! matendo yako ya kikahaba ni kitu kidogo?
And you take your sons and your daughters whom you have born to Me, And sacrifice them to them for food. Is it a little thing because of your whoredoms,
21 Umewachinja watoto wangu na kuwatupia kwenye moto.
that you slaughter My sons, And give them up in causing them to pass over to them?
22 Katika machukizo yako yote na matendo yako ya kikahaba hukutafakari kuhusu siku za ujana wako, wakati ulipokuwa uchi na bila nguo kama kama umepigwa katika damu.
And with all your abominations and your whoredoms, You have not remembered the days of your youth, When you were naked and bare, You were trodden down in your blood!
23 Ole! Ole wako! -hivi ndivyo Bwana Yahwe asemavyo-kwahiyo, zaidi ya hapo kwa haya maovu yote,
And it comes to pass, after all your wickedness (Woe, woe, to you—a declaration of Lord YHWH),
24 umejijengea chumba cha chini kwa chini katika kila sehemu ya watu wengi.
That you build an arch for yourself, And make a high place for yourself in every broad place.
25 Umepajenga mahali pako palipoinuka kwenye kichwa cha kila njia na kuunajisi uzuri wako, kwa kuwa umeutoa mwili wako kwa kila mtu apitaye karibu na umefanya matendo mengi zaidi ya ukahaba.
At every head of the way you have built your high place, And you make your beauty abominable, And open wide your feet to everyone passing by, And multiply your whoredoms,
26 Umetenda kama kahaba pamoja na Wamisri, tamaa ya jirani zako, na umetenda matendo mengi zaidi ya kikahaba, ili kuchochea hasira yangu.
And go whoring to sons of Egypt, Your neighbors—great of appetite! And you multiply your whoredoms, To provoke Me to anger.
27 Tazama! Nitakunyooshea mkono wangu na kupunguza chakula chako. Nitauchukua uhai wako juu ya adui zako, binti za Wafilisti, ambao walikuwa na haya ya tabia yako ya uchafu.
And behold, I have stretched out My hand against you, And I diminish your portion, And give you to the desire of those hating you, The daughters of the Philistines, Who are ashamed of your wicked way.
28 Umetenda kama kahaba pamoja na Waashuru kwa sababu hukuweza kuridhika. Umetenda kama kahaba na bado hukuridhika.
And you go whoring to sons of Asshur, Without your being satisfied, And you go whoring with them, And also—you have not been satisfied.
29 Umefanya matendo mengi zaidi ya kikahaba katika nchi ya jamii ya wana maji wa Ukaldayo, na wala hukuridhika kwa hayo.
And you multiply your whoredoms On the land of Canaan—toward Chaldea, And even with this you have not been satisfied.
30 Jinsi moyo wako ulivyo dhaifu-hivi ndivyo Bwana Yahwe asemavyo-kwamba utaweza kuyafanya haya mambo yote, matendo ya aibu ya kikahaba?
How weak [is] your heart, A declaration of Lord YHWH, In your doing all these, The work of a domineering, whorish woman.
31 Mmepajenga mahali penu pa juu kwenye kichwa cha kila mtaa na kufanya chumba cha chini kwa chini katika kila sehemu ya watu wengi. Bado hukuwa kama kahaba kwa sababu ulikataa kulipwa ujira.
In your building your arch at the head of every way, You have made your high place in every broad place, And have not been as a whore deriding a wage.
32 Wewe mwanamke mzinifu, wewe upokeaye wageni badala ya mume wako.
The wife who commits adultery—Under her husband—receives strangers.
33 Watu hulipa kwa kila kahaba, lakini wewe huwapa mshara wako wapenzi wako wote na kuwapa rushwa ili waje kwako pande zote kwa matendo yako ya kikahaba.
They give a gift to all whores, And you have given your gifts to all your lovers, And bribe them to come in to you, From all around—in your whoredoms.
34 Hivyo kuna tofauti kati yako na hao wanawake wengine, kwa kuwa hakuna hata mmoja ajaye kwako kukuuliza kulala pamoja nao. Badala yake, unawalipa. Hakuna akulipaye.
And you are opposite from [other] women in your whoredoms, That none go whoring after you; And in your giving a wage, And a wage has not been given to you; Therefore you are the opposite.
35 Kwa hiyo, wewe kahaba, lisikilize neno la Yahwe.
Therefore, O whore, hear a word of YHWH!
36 Bwana Yahwe asema hivi: Kwa sababu umemwaga tamaa yako na kuonyesha sehemu zako za siri kupitia matendo yako ya ukahaba pamoja na wapenzi wako wote pamoja na sanamu zako za chukizo, na kwa sababu ya damu ya watoto wako uliyowapatia sanamu zako,
Thus said Lord YHWH: Because of your bronze being poured forth, And your nakedness is revealed in your whoredoms near your lovers, And near all the idols of your abominations, And according to the blood of your sons, Whom you have given to them;
37 kwa hiyo, tazama! Nitawakusanya wapenzi wako wote uliokutana nao, wote ambao uliowapenda na wote uliowachukia, na nitawakusanya juu yako kila upande. Nitawaonyesha wazi sehemu zako za siri hivyo wanaweza kuona uchi wako wote.
Therefore, behold, I am assembling all your lovers, To whom you have been sweet, And all whom you have loved, Besides all whom you have hated; And I have assembled them by you all around, And have revealed your nakedness to them, And they have seen all your nakedness.
38 Kwa kuwa nitakuadhibu kwa uasherati na kumwaga damu, na nitaleta juu yako damu ya hasira yangu na hasira kali.
And I have judged you—judgments of adultresses, And of women shedding blood, And have given you blood, fury, and jealousy.
39 Nitakutia kwenye mikono yao hivyo watakutupa chini kwenye chumba cha chini kwa chini na kupavunja mahali pako pa juu na watakuvua nguo zako na kuchukua vito vyako vyote. watakuacha uchi bila nguo.
And I have given you into their hand, And they have thrown down your arch, And they have broken down your high places, And they have stripped you of your garments, And they have taken your beautiful vessels, And they have left you naked and bare.
40 Kisha wataleta kundi la watu juu yako na kukupiga kwa mawe, na kukukata kwa panga zao.
And have caused an assembly to come up against you, And stoned you with stones, And thrust you through with their swords,
41 Watachoma nyumba zako na kufanya matendo mengi ya adhabu juu yako kwenye uso wa wanawake wengi, kwa kuwa nitakusimamisha ukahaba wako, na hutawalipa tena wapenzi wako.
And burned your houses with fire, And done judgments in you before the eyes of many women, And I have caused you to cease from going whoring, And also, you no longer give a wage.
42 Kisha nitatuliza ghadhabu yangu juu yako; hasira yangu itakuacha, kwa kuwa nitaridhika, na sitakuwa na hasira tena.
And I have caused My fury against you to rest, And My jealousy has turned aside from you, And I have been quiet, and I am not angry anymore.
43 Kwa sababu hukuzikumbuka siku za ujana wako na kunifanya nitetemeke kwa hasira kwa sababu ya haya mambo yote, kwa hiyo, tazama! Mimi mwenyewe nitashusha kwa kichwa chako mwenyewe adhabu kwa kile ulichokifanya-hivi ndivyo Bwana Yahwe asemavyo. Hutaongeza ukahaba kwa matendo yako yote ya machukizo?
Because you have not remembered the days of your youth, And give trouble to Me in all these, Therefore I also—behold—I put your way on [your own] head, A declaration of Lord YHWH, And you will not have done—have done this wickedness above all your abominations.
44 Tazama! Kila mtu azungumzaye Mithali kuhusu wewe atasema, “Kama alivyo, hivyo pia ni binti yake.”
Behold, everyone using the allegory against you, Uses [this] allegory concerning [you], saying, As the mother—her daughter!
45 Wewe ni binti wa mama yako, amchukiaye mume wake na mtoto wake, na wewe ni dada wa dada zako aliyewachukia waume zao na watoto wao. Mama yako alikuwa Mhiti, na baba yako alikuwa Mwamori.
You [are] your mother’s daughter, Loathing her husband and her sons, And you [are] your sisters’ sister, Who loathed their husbands and their sons, Your mother [is] a Hittite, and your father an Amorite.
46 Dada yako mkubwa alikuwa Samaria na binti zake walikuwa wale waliokuwa wakiishi kaskazini, wakati dada yako mdogo alikuwa ni yule aliyekuwa akiishi kusini mwako, ambaye ni, Sodoma na binti zake.
And your older sister [is] Samaria, she and her daughters, Who is dwelling at your left hand, And your younger sister, who is dwelling on your right hand, [is] Sodom and her daughters.
47 Hukuenenda katika njia zao na kuchukua tabia zao na matendo yao, lakini katika njia zako zote ulikuwa mbaya zaidi kuliko walivyokuwa wao.
And you have not walked in their ways, And done according to their abominations, It has been loathed as a little thing, Indeed, you do more corruptly than they in all your ways.
48 Kama niishivyo- hivi ndivyo Bwana Yahwe asemavyo-dada yako Sodoma na binti zake, hawajafanya uovu mwingi kama wewe ulivyofanya na binti zako walivyofanya.
[As] I live—a declaration of Lord YHWH, Your sister Sodom has not done—she and her daughters—As you have done—you and your daughters.
49 Tazama! Hii ilikuwa dhambi ya dada yako Sodoma: Alikuwa na kiburi katika mafanikio yake, uzembe na kutojali kuhusu chochote. Hakuitia nguvu mikono ya maskini na watu wahitaji.
Behold, this has been the iniquity of your sister Sodom, Arrogancy, fullness of bread, and quiet ease, Have been to her and to her daughters, And the hand of the afflicted and needy She has not strengthened.
50 Alikuwa na kiburi na kufanya machukizo mbele yangu, hivyo niliwatoa kama nilivyoona.
And they are haughty and do abomination before Me, And I turn them aside when I have seen.
51 Samaria hakufanya hata nusu ya dhambi zako; badala yake, umefanya machukizo mengi kuliko walivyofanya, na umewonyesha hayo dada zako walikuwa bora kuliko wewe kwa sababu ya machukizo yako uyafanyayo!
And Samaria has not sinned even half of your sins, But you multiply your abominations more than they, And justify your sisters by all your abominations that you have done.
52 Hasa wewe, umeonyesha aibu yako mwenyewe; kwa njia hii umewaonyesha dada zako walikuwa bora kuliko wewe, kwa sababu ya dhambi ulizozifanya katika hayo machukizo yako yote. Dada zako sasa wanaonekana bora kuliko wewe. Hasa wewe, umeonyesha aibu yako mwenyewe, kwa njia hii umewaonyesha kwamba dada zako walikuwa bora kuliko wewe.
You also—bear your shame, That you have adjudged for your sisters, Because of your sins that you have done more abominably than they, They are more righteous than you, And you, also, be ashamed and bear your shame, In your justifying your sisters.
53 Kwa kuwa nitarudisha masalia wao-masalia ya Sodoma na binti zake, na masalia ya Samaria na binti zake; lakini masalia yako yatakuwa miongoni mwao.
And I have turned back [to] their captivity, The captivity of Sodom and her daughters, And the captivity of Samaria and her daughters, And the captivity of your captives in their midst,
54 Kwa kufikiria haya mambo utaonyesha aibu yako; utakuwa mnyenyekevu kwa sababu ya kila kitu ulichokifanya, na kwa njia hii utakuwa faraja kwao.
So that you bear your shame, And have been ashamed of all that you have done, In your comforting them.
55 Hivyo dada yako Sodoma na binti zake watarudishwa kwenye hali yao ya zamani, na Samaria na binti zake watarudishwa kwenye mashamba yao ya zamani. Kisha wewe na binti zako watarudishwa kwenye hali yako ya kawaida.
And your sisters, Sodom and her daughters, Return to their former state, And Samaria and her daughters return to their former state, And you and your daughters return to your former state.
56 Sodoma dada yako hakutajwa hata kwa kinywa chako katika siku ulipojiinua,
And your sister Sodom has not been for a report in your mouth, In the day of your arrogancy,
57 kabla uovu wako haujafunuliwa. Lakini sasa wewe ni kitu cha dharau kwa binti za Edomu na binti wote wa Wafilisti waliomzunguka. Watu wote wanakudharau wewe.
Before your wickedness is revealed, As [at] the time of the reproach of the daughters of Aram, And of all her neighbors, the daughters of the Philistines, Who are despising you all around.
58 Utaonyesha aibu yako na matendo yako ya machukizo! -hivi ndivyo Yahwe asemavyo!
Your wicked plans and your abominations, You have borne them, a declaration of YHWH.
59 Bwana Yahwe asema hivi: Nitashughulika na wewe kama unavyostahili, wewe uliyedharau kiapo chako kwa kulivunja agano.
For thus said Lord YHWH: I have dealt with you as you have done, In that you have despised an oath—to break covenant.
60 Lakini mimi mwenyewe nitalikumbuka agano langu nililolifanya pamoja nawe katika siku za ujana wako, nitaliimarisha agano la milele pamoja na wewe.
And I have remembered My covenant with you, In the days of your youth, And I have established a perpetual covenant for you.
61 Kisha utazikumbuka njia zako na kuona aibu utakapo wapokea dada zako wakubwa na dada zako wadogo. Nitakupatia wao kama binti zako, lakini kwa sababu ya agano lako.
And you have remembered your ways, And you have been ashamed, In your receiving your sisters—Your older with your younger, And I have given them to you for daughters, And not by your covenant.
62 Mimi nitaweka imara agano lango pamoja nawe, nawe utajua yakwamba mimi ni Yahwe.
And I have established My covenant with you, And you have known that I [am] YHWH.
63 Kwa sababu ya haya mambo, utakumbuka kila kitu na kuona aibu, hutafungua mdomo wako tena kuongea kwa sababu ya aibu yako, wakati nitakapokusamehe kwa yale yote uliyoyafanya-hivi ndivyo Bwana Yahwe asemavyo.”'
So that you remember, And you have been ashamed, And there is not an opening of the mouth to you anymore because of your shame, In My receiving atonement for you, For all that you have done, A declaration of Lord YHWH!”

< Ezekieli 16 >