< Ezekieli 16 >

1 Kisha neno la Yahwe likanijia, kusema,
Again the word of the LORD came unto me, saying:
2 “Mwanadamu, mwambie Yerusalemu kuhusu machukizo yake,
'Son of man, cause Jerusalem to know her abominations,
3 na useme, 'Bwana Yahwe asema hivi kwa Yerusalemu: Mwanzo wako na kuzaliwa kwako kulichukua nafasi katika nchi ya Kanaani; baba yako alikuwa Mwamori, na mama yako alikuwa Mhiti.
and say: Thus saith the Lord GOD unto Jerusalem: Thine origin and thy nativity is of the land of the Canaanite; the Amorite was thy father, and thy mother was a Hittite.
4 Katika siku ya kuzaliwa kwako, mama yako hakukata kitovu chako, wala hakukuosha kwenye maji usafishwe au kukuchua kwa chumvi, wala kukusitiri nguo.
And as for thy nativity, in the day thou wast born thy navel was not cut, neither wast thou washed in water for cleansing; thou was not salted at all, nor swaddled at all.
5 Hakuna jicho lililokuhurumia kufanya haya mambo kwa ajili yako, kukuhurumia wewe. Katika siku uliyozaliwa, kwa kuchukiwa uhai wako, ulitupwa nje uwandani.
No eye pitied thee, to do any of these unto thee, to have compassion upon thee; but thou wast cast out in the open field in the loathsomeness of thy person, in the day that thou wast born.
6 Lakini nilipita karibu nawe, nalikuona ukijinyonga kwa damu yako mwenyewe, “kubaki hai!”
And when I passed by thee, and saw thee wallowing in thy blood, I said unto thee: In thy blood, live; yea, I said unto thee: In thy blood, live;
7 Nimekufanya ukue kama mmea katika shamba. Umeongezeka na kuwa mkubwa, na umekuwa mzuri wa wazuri. Maziwa yako yakawa thabiti, na nywele zako zikawa nyingi, ingawa ulikuwa uchi huna nguo.
I cause thee to increase, even as the growth of the field. And thou didst increase and grow up, and thou camest to excellent beauty: thy breasts were fashioned, and thy hair was grown; yet thou wast naked and bare.
8 Nilipita karibu nawe tena, na nalikuona. Tazama! wakati wa upendo umefika kwako, hivyo nikatandika joho langu juu yako na kufunika uchi wako. Kisha nikaapa kwako na kukuleta kwenye agano-hivi ndivyo Bwana Yahwe asemavyo-na ukawa wangu.
Now when I passed by thee, and looked upon thee, and, behold, thy time was the time of love, I spread my skirt over thee, and covered thy nakedness; yea, I swore unto thee, and entered into a covenant with thee, saith the Lord GOD, and thou becamest Mine.
9 Basi nilikuosha kwa maji na kukufuta damu yako, na kukupaka mafuta.
Then washed I thee with water; yea, I cleansed away thy blood from thee, and I anointed thee with oil.
10 Nilikuvalisha nguo ya taraza na kukuwekea makuzi ya ngozi kwenye miguu yako. Nilikufungia kwa kitani kizuri na kukufunika kwa hariri.
I clothed thee also with richly woven work, and shod thee with sealskin, and I wound fine linen about thy head, and covered thee with silk.
11 Kisha nalikupamba kwa vito, na kukuvalisha vikuku kwenye mikono yako, na mkufu kwenye shingo yako.
I decked thee also with ornaments, and I put bracelets upon thy hands, and a chain on thy neck.
12 Nalitia hazama katika pua yako na hereni katika masikio yako, na taji nzuri juu ya kichwa chako.
And I put a ring upon thy nose, and earrings in thine ears, and a beautiful crown upon thy head.
13 Hivyo ulipambwa kwa dhahabu na fedha, na ulivaa kitani safi, hariri, na ngu za taraza; ulikula unga mzuri, asali, na mafuta, na ulikuwa mzuri sana, na ukawa malkia.
Thus wast thou decked with gold and silver; and thy raiment was of fine linen, and silk, and richly woven work; thou didst eat fine flour, and honey, and oil; and thou didst wax exceeding beautiful, and thou wast meet for royal estate.
14 Umaarufu wako ukaenda miongoni mwa mataifa kwa sababu ya uzuri wako, kwa kuwa ulikuwa mkamili katika ukuu niliokuwa nimekupa-hivi ndivyo Bwana Yahwe asemavyo.
And thy renown went forth among the nations for thy beauty; for it was perfect, through My splendour which I had put upon thee, saith the Lord GOD.
15 Lakini ulitumaini uzuri wako, na ukafanya kama kahaba kwa sababu ya umaarufu wako; umeyamwaga matendo yako ya kikahaba kwa kila aliyepita karibu, ili kwamba uzuri wako uwe wake.
But thou didst trust in thy beauty and play the harlot because of thy renown, and didst pour out thy harlotries on every one that passed by; his it was.
16 Kisha ulichukua nguo zako na pamoja nao umepatengeneza mahali pa juu kwa ajili yako palipambwa kwa rangi tofauti tofauti, na hapo ulifanya kama kahaba. Hii haitatokea. Wala haitatokea.
And thou didst take of thy garments, and didst make for thee high places decked with divers colours, and didst play the harlot upon them; the like things shall not come, neither shall it be so.
17 Umevichukua vito vizuri vya dhahabu na fedha nilizowapatia, na umejitengenezea sanamu za wanaume, na umefanya pamoja nao ukahaba afanyao.
Thou didst also take thy fair jewels of My gold and of My silver, which I had given thee, and madest for thee images of men, and didst play the harlot with them;
18 Ulichukua nguo zako za tarizi na kuwafunika, na kuwawekea mafuta yangu na manukato mbele yao.
and thou didst take thy richly woven garments and cover them, and didst set Mine oil and Mine incense before them.
19 Mkate wangu niliokupatia-ulitengenezwa kwa unga mzuri, mafuta, na asali-umeviweka mbele yao kwa ajili ya kunukia harufu nzuri, kwa kuwa hivi ndivyo ilivyotokea-hivi ndivyo Bwana Yahwe asemavyo.
My bread also which I gave thee, fine flour, and oil, and honey, wherewith I fed thee, thou didst even set it before them for a sweet savour, and thus it was; saith the Lord GOD.
20 Kisha uliwachukua watoto wako ulionizalia, na kuwatoa sadaka kwa picha ili waliwe kama chakula. Je! matendo yako ya kikahaba ni kitu kidogo?
Moreover thou hast taken thy sons and thy daughters, whom thou hast borne unto Me, and these hast thou sacrificed unto them to be devoured. Were thy harlotries a small matter,
21 Umewachinja watoto wangu na kuwatupia kwenye moto.
that thou hast slain My children, and delivered them up, in setting them apart unto them?
22 Katika machukizo yako yote na matendo yako ya kikahaba hukutafakari kuhusu siku za ujana wako, wakati ulipokuwa uchi na bila nguo kama kama umepigwa katika damu.
And in all thine abominations and thy harlotries thou hast not remembered the days of thy youth, when thou wast naked and bare, and wast wallowing in thy blood.
23 Ole! Ole wako! -hivi ndivyo Bwana Yahwe asemavyo-kwahiyo, zaidi ya hapo kwa haya maovu yote,
And it came to pass after all thy wickedness — woe, woe unto thee! saith the Lord GOD —
24 umejijengea chumba cha chini kwa chini katika kila sehemu ya watu wengi.
that thou hast built unto thee an eminent place, and hast made thee a lofty place in every street.
25 Umepajenga mahali pako palipoinuka kwenye kichwa cha kila njia na kuunajisi uzuri wako, kwa kuwa umeutoa mwili wako kwa kila mtu apitaye karibu na umefanya matendo mengi zaidi ya ukahaba.
Thou hast built thy lofty place at every head of the way, and hast made thy beauty an abomination, and hast opened thy feet to every one that passed by, and multiplied thy harlotries.
26 Umetenda kama kahaba pamoja na Wamisri, tamaa ya jirani zako, na umetenda matendo mengi zaidi ya kikahaba, ili kuchochea hasira yangu.
Thou hast also played the harlot with the Egyptians, thy neighbours, great of flesh; and hast multiplied thy harlotry, to provoke Me.
27 Tazama! Nitakunyooshea mkono wangu na kupunguza chakula chako. Nitauchukua uhai wako juu ya adui zako, binti za Wafilisti, ambao walikuwa na haya ya tabia yako ya uchafu.
Behold, therefore I have stretched out My hand over thee, and have diminished thine allowance, and delivered thee unto the will of them that hate thee, the daughters of the Philistines, that are ashamed of thy lewd way.
28 Umetenda kama kahaba pamoja na Waashuru kwa sababu hukuweza kuridhika. Umetenda kama kahaba na bado hukuridhika.
Thou hast played the harlot also with the Assyrians, without having enough; yea, thou hast played the harlot with them, and yet thou wast not satisfied.
29 Umefanya matendo mengi zaidi ya kikahaba katika nchi ya jamii ya wana maji wa Ukaldayo, na wala hukuridhika kwa hayo.
Thou hast moreover multiplied thy harlotry with the land of traffic, even with Chaldea; and yet thou didst not have enough herewith.
30 Jinsi moyo wako ulivyo dhaifu-hivi ndivyo Bwana Yahwe asemavyo-kwamba utaweza kuyafanya haya mambo yote, matendo ya aibu ya kikahaba?
How weak is thy heart, saith the Lord GOD, seeing thou doest all these things, the work of a wanton harlot;
31 Mmepajenga mahali penu pa juu kwenye kichwa cha kila mtaa na kufanya chumba cha chini kwa chini katika kila sehemu ya watu wengi. Bado hukuwa kama kahaba kwa sababu ulikataa kulipwa ujira.
in that thou buildest thine eminent place in the head of every way, and makest thy lofty place in every street; and hast not been as a harlot that enhanceth her hire.
32 Wewe mwanamke mzinifu, wewe upokeaye wageni badala ya mume wako.
Thou wife that committest adultery, that takest strangers instead of thy husband —
33 Watu hulipa kwa kila kahaba, lakini wewe huwapa mshara wako wapenzi wako wote na kuwapa rushwa ili waje kwako pande zote kwa matendo yako ya kikahaba.
to all harlots gifts are given; but thou hast given thy gifts to all thy lovers, and hast bribed them to come unto thee from every side in thy harlotries.
34 Hivyo kuna tofauti kati yako na hao wanawake wengine, kwa kuwa hakuna hata mmoja ajaye kwako kukuuliza kulala pamoja nao. Badala yake, unawalipa. Hakuna akulipaye.
And the contrary is in thee from other women, in that thou didst solicit to harlotry, and wast not solicited; and in that thou givest hire, and no hire is given unto thee, thus thou art contrary.
35 Kwa hiyo, wewe kahaba, lisikilize neno la Yahwe.
Wherefore, O harlot, hear the word of the LORD!
36 Bwana Yahwe asema hivi: Kwa sababu umemwaga tamaa yako na kuonyesha sehemu zako za siri kupitia matendo yako ya ukahaba pamoja na wapenzi wako wote pamoja na sanamu zako za chukizo, na kwa sababu ya damu ya watoto wako uliyowapatia sanamu zako,
Thus saith the Lord GOD: Because thy filthiness was poured out, and thy nakedness uncovered through thy harlotries with thy lovers; and because of all the idols of thy abominations, and for the blood of thy children, that thou didst give unto them;
37 kwa hiyo, tazama! Nitawakusanya wapenzi wako wote uliokutana nao, wote ambao uliowapenda na wote uliowachukia, na nitawakusanya juu yako kila upande. Nitawaonyesha wazi sehemu zako za siri hivyo wanaweza kuona uchi wako wote.
therefore behold, I will gather all thy lovers, unto whom thou hast been pleasant, and all them that thou hast loved, with all them that thou hast hated; I will even gather them against thee from every side, and will uncover thy nakedness unto them, that they may see all thy nakedness.
38 Kwa kuwa nitakuadhibu kwa uasherati na kumwaga damu, na nitaleta juu yako damu ya hasira yangu na hasira kali.
And I will judge thee, as women that break wedlock and shed blood are judged; and I will bring upon thee the blood of fury and jealousy.
39 Nitakutia kwenye mikono yao hivyo watakutupa chini kwenye chumba cha chini kwa chini na kupavunja mahali pako pa juu na watakuvua nguo zako na kuchukua vito vyako vyote. watakuacha uchi bila nguo.
I will also give thee into their hand, and they shall throw down thine eminent place, and break down thy lofty places; and they shall strip thee of thy clothes, and take thy fair jewels; and they shall leave thee naked and bare.
40 Kisha wataleta kundi la watu juu yako na kukupiga kwa mawe, na kukukata kwa panga zao.
They shall also bring up an assembly against thee, and they shall stone thee with stones, and thrust thee through with their swords.
41 Watachoma nyumba zako na kufanya matendo mengi ya adhabu juu yako kwenye uso wa wanawake wengi, kwa kuwa nitakusimamisha ukahaba wako, na hutawalipa tena wapenzi wako.
And they shall burn thy houses with fire, and execute judgments upon thee in the sight of many women; and I will cause thee to cease from playing the harlot, and thou shalt also give no hire any more.
42 Kisha nitatuliza ghadhabu yangu juu yako; hasira yangu itakuacha, kwa kuwa nitaridhika, na sitakuwa na hasira tena.
So will I satisfy My fury upon thee, and My jealousy shall depart from thee, and I will be quiet, and will be no more angry.
43 Kwa sababu hukuzikumbuka siku za ujana wako na kunifanya nitetemeke kwa hasira kwa sababu ya haya mambo yote, kwa hiyo, tazama! Mimi mwenyewe nitashusha kwa kichwa chako mwenyewe adhabu kwa kile ulichokifanya-hivi ndivyo Bwana Yahwe asemavyo. Hutaongeza ukahaba kwa matendo yako yote ya machukizo?
Because thou hast not remembered the days of thy youth, but hast fretted Me in all these things; lo, therefore I also will bring thy way upon thy head, saith the Lord GOD; or hast thou not committed this lewdness above all thine abominations?
44 Tazama! Kila mtu azungumzaye Mithali kuhusu wewe atasema, “Kama alivyo, hivyo pia ni binti yake.”
Behold, every one that useth proverbs shall use this proverb against thee, saying: As the mother, so her daughter.
45 Wewe ni binti wa mama yako, amchukiaye mume wake na mtoto wake, na wewe ni dada wa dada zako aliyewachukia waume zao na watoto wao. Mama yako alikuwa Mhiti, na baba yako alikuwa Mwamori.
Thou art thy mother's daughter, that loatheth her husband and her children; and thou art the sister of thy sisters, who loathed their husbands and their children; your mother was a Hittite, and your father an Amorite.
46 Dada yako mkubwa alikuwa Samaria na binti zake walikuwa wale waliokuwa wakiishi kaskazini, wakati dada yako mdogo alikuwa ni yule aliyekuwa akiishi kusini mwako, ambaye ni, Sodoma na binti zake.
And thine elder sister is Samaria, that dwelleth at thy left hand, she and her daughters; and thy younger sister, that dwelleth at thy right hand, is Sodom and her daughters.
47 Hukuenenda katika njia zao na kuchukua tabia zao na matendo yao, lakini katika njia zako zote ulikuwa mbaya zaidi kuliko walivyokuwa wao.
Yet hast thou not walked in their ways, nor done after their abominations; but in a very little while thou didst deal more corruptly than they in all thy ways.
48 Kama niishivyo- hivi ndivyo Bwana Yahwe asemavyo-dada yako Sodoma na binti zake, hawajafanya uovu mwingi kama wewe ulivyofanya na binti zako walivyofanya.
As I live, saith the Lord GOD, Sodom thy sister hath not done, she nor her daughters, as thou hast done, thou and thy daughters.
49 Tazama! Hii ilikuwa dhambi ya dada yako Sodoma: Alikuwa na kiburi katika mafanikio yake, uzembe na kutojali kuhusu chochote. Hakuitia nguvu mikono ya maskini na watu wahitaji.
Behold, this was the iniquity of thy sister Sodom: pride, fulness of bread, and careless ease was in her and in her daughters; neither did she strengthen the hand of the poor and needy.
50 Alikuwa na kiburi na kufanya machukizo mbele yangu, hivyo niliwatoa kama nilivyoona.
And they were haughty, and committed abomination before Me; therefore I removed them when I saw it.
51 Samaria hakufanya hata nusu ya dhambi zako; badala yake, umefanya machukizo mengi kuliko walivyofanya, na umewonyesha hayo dada zako walikuwa bora kuliko wewe kwa sababu ya machukizo yako uyafanyayo!
Neither hath Samaria committed even half of thy sins; but thou hast multiplied thine abominations more than they, and hast justified thy sisters by all thine abominations which thou hast done.
52 Hasa wewe, umeonyesha aibu yako mwenyewe; kwa njia hii umewaonyesha dada zako walikuwa bora kuliko wewe, kwa sababu ya dhambi ulizozifanya katika hayo machukizo yako yote. Dada zako sasa wanaonekana bora kuliko wewe. Hasa wewe, umeonyesha aibu yako mwenyewe, kwa njia hii umewaonyesha kwamba dada zako walikuwa bora kuliko wewe.
Thou also, bear thine own shame, in that thou hast given judgment for thy sisters; through thy sins that thou hast committed more abominable than they, they are more righteous than thou; yea, be thou also confounded, and bear thy shame, in that thou hast justified thy sisters.
53 Kwa kuwa nitarudisha masalia wao-masalia ya Sodoma na binti zake, na masalia ya Samaria na binti zake; lakini masalia yako yatakuwa miongoni mwao.
And I will turn their captivity, the captivity of Sodom and her daughters, and the captivity of Samaria and her daughters, and the captivity of thy captives in the midst of them;
54 Kwa kufikiria haya mambo utaonyesha aibu yako; utakuwa mnyenyekevu kwa sababu ya kila kitu ulichokifanya, na kwa njia hii utakuwa faraja kwao.
that thou mayest bear thine own shame, and mayest be ashamed because of all that thou hast done, in that thou art a comfort unto them.
55 Hivyo dada yako Sodoma na binti zake watarudishwa kwenye hali yao ya zamani, na Samaria na binti zake watarudishwa kwenye mashamba yao ya zamani. Kisha wewe na binti zako watarudishwa kwenye hali yako ya kawaida.
And thy sisters, Sodom and her daughters, shall return to their former estate, and Samaria and her daughters shall return to their former estate, and thou and thy daughters shall return to your former estate.
56 Sodoma dada yako hakutajwa hata kwa kinywa chako katika siku ulipojiinua,
For thy sister Sodom was not mentioned by thy mouth in the day of thy pride;
57 kabla uovu wako haujafunuliwa. Lakini sasa wewe ni kitu cha dharau kwa binti za Edomu na binti wote wa Wafilisti waliomzunguka. Watu wote wanakudharau wewe.
before thy wickedness was uncovered, as at the time of the taunt of the daughters of Aram, and of all that are round about her, the daughters of the Philistines, that have thee in disdain round about.
58 Utaonyesha aibu yako na matendo yako ya machukizo! -hivi ndivyo Yahwe asemavyo!
Thou hast borne thy lewdness and thine abominations, saith the LORD.
59 Bwana Yahwe asema hivi: Nitashughulika na wewe kama unavyostahili, wewe uliyedharau kiapo chako kwa kulivunja agano.
For thus saith the Lord GOD: I will even deal with thee as thou hast done, who hast despised the oath in breaking the covenant.
60 Lakini mimi mwenyewe nitalikumbuka agano langu nililolifanya pamoja nawe katika siku za ujana wako, nitaliimarisha agano la milele pamoja na wewe.
Nevertheless I will remember My covenant with thee in the days of thy youth, and I will establish unto thee an everlasting covenant.
61 Kisha utazikumbuka njia zako na kuona aibu utakapo wapokea dada zako wakubwa na dada zako wadogo. Nitakupatia wao kama binti zako, lakini kwa sababu ya agano lako.
Then shalt thou remember thy ways, and be ashamed, when thou shalt receive thy sisters, thine elder sisters and thy younger; and I will give them unto thee for daughters, but not because of thy covenant.
62 Mimi nitaweka imara agano lango pamoja nawe, nawe utajua yakwamba mimi ni Yahwe.
And I will establish My covenant with thee, and thou shalt know that I am the LORD;
63 Kwa sababu ya haya mambo, utakumbuka kila kitu na kuona aibu, hutafungua mdomo wako tena kuongea kwa sababu ya aibu yako, wakati nitakapokusamehe kwa yale yote uliyoyafanya-hivi ndivyo Bwana Yahwe asemavyo.”'
that thou mayest remember, and be confounded, and never open thy mouth any more, because of thy shame; when I have forgiven thee all that thou hast done, saith the Lord GOD.'

< Ezekieli 16 >