< Ezekieli 14 >
1 Baadhi ya viongozi wa Israeli wakaja kwangu na kuketi mbele yangu.
Et quelques-uns des anciens du peuple d'Israël vinrent me trouver, et ils s'assirent devant moi.
2 Ndipo neno la Yahwe likanijia, likisema,
Et la parole du Seigneur me vint, disant:
3 “Mwanadamu, hawa watu wamchukua sanamu zao kwenye mioyo yao na kuweka pingamizi la uovu wao mbele ya nyuso zao wenyewe. Je naweza kuulizwa yote na wao?
Fils de l'homme, ces hommes ont conçu leurs pensées en leurs cœurs, et ils ont mis devant leur visage la punition de leurs iniquités: que dois-je leur répondre?
4 Kwa hiyo watangazie hivi na waambie, 'Bwana Yahwe asema hivi: Kila mtu wa nyumba ya Israeli achukuaye sanamu moyoni mwake, au awekeye pingamizi la uovu mbele ya uso wake, na kisha yule ajaye kwa nabii-Mimi, Yahwe, nitamjibu kulingana na sanamu zake.
Parle et dis-leur: Voici ce que dit le Seigneur: Tout homme, un homme d'Israël, qui aura conçu des pensées en son cœur et qui aura mis devant son visage la punition de son iniquité, et qui viendra devant le prophète, moi le Seigneur je lui répondrai selon les engagements de sa pensée.
5 Nitafanya hivi ili kwamba niweze kuirudisha nyumba ya Israeli katika mioyo yao ambayo ilikuwa mbali nami kwa ajili ya sanamu zao.'
Car il désire tromper la maison d'Israël, pour qu'elle se laisse entraîner par ses convoitises et qu'elle éloigne son cœur de moi.
6 Kwa hiyo sema kwa nyumba ya Israeli, 'Bwana Yahwe asema hivi: Tubuni na rudini kutoka kwenye sanamu zenu! Rudisheni nyuma nyuso zenu kutoka kwenye kachukizo yenu yote.
À cause de cela, dis à la maison d'Israël: Ainsi parle le Seigneur: Convertissez-vous et détournez-vous de vos mauvaises œuvres et de toutes vos iniquités, et détournez-en vos visages.
7 Kwa kuwa kila mmoja kutoka kwenye nyumba ya Israeli na kila mmoja wa wageni wanaoishi katika Israeli ajitengaye nami, achukuaye sanamu zake kwenye moyo wake na kuweka kwazo la uovu wake mbele ya uso wake mwenyewe, na kisha yule ajaye kwa nabii kunitafuta-mimi, Yahwe, nitamjibu mimi mwenyewe.
Car tout homme, un homme de la maison d'Israël, et tout étranger prosélyte en Israël, qui se sera éloigné de moi et aura conçu des pensées en son cœur et aura mis devant son visage la punition de son iniquité, et qui viendra ensuite au prophète pour le questionner sur moi, moi le Seigneur, je lui répondrai selon les engagements où il est lui-même.
8 Hivyo nitauweka uso wangu juu ya huyo mtu na kumfanya ishara na mithali, kwa kuwa nitamkata kutoka kati ya watu wangu, na mtajua kuwa mimi ni Yahwe.
Et je tournerai mon visage contre cet homme, et je le livrerai à la solitude et à l'extermination, et je l'effacerai du milieu de mon peuple, et vous saurez que je suis le Seigneur.
9 Kama nabii atadanganywa na kuongea ujumbe, kisha Mimi Yahwe, nitamdanganya huyo nabii; Nitanyoosha mkono wangu na kumwangamizaku toka kati watu wangu Israeli.
Et si un prophète s'est égaré, et s'il a parlé, c'est moi le Seigneur qui ai égaré ce prophète; et j'étendrai la main sur lui, et je l'exterminerai du milieu de mon peuple d'Israël.
10 Watabeba uovu wao wenyewe; uwovu wa nabii utakua uleule kama uovu wa yule aulizaye kutoka kwake.
Et ils porteront la peine de leur iniquité, selon l'iniquité de celui qui aura interrogé, laquelle sera punie de la même manière que l'iniquité du prophète;
11 Kwa sababu hiyo basi, nyumba ya Israeli haitaenda mbali kutoka kunifuata mimi wala kujinajisi wenyewe kupitia dhambi zao zote. Watakuwa watu wangu, nami nitakuwa Mungu wao-hivi ndivyo Yahwe asemavyo.”'
Afin que la maison d'Israël ne s'égare plus en s'éloignant de moi, qu'elle ne se souille plus par ses péchés; de sorte qu'elle soit mon peuple, et que je sois son Dieu, dit le Seigneur.
12 Kisha neno la Yahwe likanijia, likisema,
Et la parole du Seigneur me vint, disant:
13 “Mwanadamu, wakati nchi itakapo asi dhidi yangu kwa kufanya dhambi ili kwamba ninyooshe mkono wangu dhidi yake na kuvunja tegemea la mkate wake, na kuleta njaa juu yake na kukata mnyama kutoka kwenye nchi;
Fils de l'homme, la terre qui aura péché contre moi en ses transgressions, j'étendrai la main sur elle; je briserai la force du pain, je lui enverrai la famine, et je détruirai les hommes et son bétail.
14 kisha hata kama hawa watu watatu-Nuhu, Danieli, na Ayubu-walikuwa katikati ya nchi, wangeweza kuokoa maisha yao wenyewe kwa haki-hivi ndivyo Bwana Yahwe asemavyo.
Et si, au milieu d'elle, se trouvent trois hommes comme Noé, Daniel et Job, ils seront sauvés à cause de leur justice, dit le Seigneur.
15 Kama nikileta wanyama waovu kwenye nchi na kuwafanya wasizae hivyo basi itakuwa hakuna mtu asiweze kupita kwa sababu ya hao wanyama,
Et si j'amène les bêtes farouches sur cette terre, et si je la punis, et si elle est désolée, et que nul ne la traverse en face des bêtes farouches;
16 kisha hata kama watu hawa hawa watatu ndani yake-kama niishivyo, asema Bwana Yahwe-wasingeweza kuwaokoa hata watoto wao wala binti; isipokuwa maisha yao yataokoka, lakini nchi itakuwa ukiwa.
Si ces trois hommes s'y trouvent, par ma vie, dit le Seigneur, ni leurs fils ni leurs filles ne seront sauvés; eux seuls seront sauvés, mais la terre sera détruite.
17 Au nikileta upanga juu ya hiyo nchi na kusema, 'Upanga, nenda kwenye nchi na wakate wote mtu na mnyama kutoka huo',
Ou bien encore, si je promène le glaive sur cette terre, et si je dis: Que le glaive sillonne toute cette terre, et j'en ôterai les hommes et le bétail;
18 kisha hata kama hawa watu watatu watakuwa katikatai ya nchi-kama niishivyo, asema Bwana Yahwe-wasingeweza kuwaokoa japo watoto wao wala binti; ila tu maisha yao wenyewe yangeokolewa.
Et si ces trois hommes s'y trouvent, par ma vie, dit le Seigneur, ils ne sauveront ni leurs fils ni leurs filles; eux seuls seront sauvés.
19 Au kama nikipeleka tauni juu ya nchi na kumwaga dhahabu yangu juu yake kwa damu, ili kuwakata mtu na mnyama,
Ou bien encore, si j'envoie la peste en cette terre, et si je verse sur elle ma colère, avec le sang, pour détruire ses hommes et son bétail,
20 kisha hata kama Nuhu, Danieli, na Ayubu wangekuwa kwenye hiyo nchi-kama niishivyo, asema Bwana Yahwe-wasingeweza kuokoa hata watoto wao au binti; maisha yao pekee yangeokoka kwa haki.
Et si Noé, Daniel et Jacob s'y trouvent, par ma vie, dit le Seigneur, ni leurs fils ni leurs filles n'échapperont; eux seuls, à cause de leur justice, auront sauvé leurs âmes.
21 Kwa kuwa Bwana Yahwe asema hivi: hakika nitafanya mambo makali sana kwa kuleta adhabu zangu nne-njaa, upanga, wanyama wa porini, na tauni-juu ya Yerusalemu kuwakata wote mtu na mnyama kutoka kwake.
Voici ce que dit le Seigneur: Si j'envoie contre Jérusalem les quatre fléaux: le glaive, la famine, les bêtes farouches et la peste, pour y détruire les hommes et le bétail;
22 Kisha, tazama! mabaki yatasalia kwake, watakaokoka wataenda pamoja na wana na binti. Tazama! Watawatokea, na mtaona njia zao na matendo yao yakiwafariji kuhusu adhabu niliyoipeleka Yerusalemu, na kuhusu kila kitu kingine ambacho nilichopeleka juu ya nchi.
Voilà qu'il restera quelques hommes; et ceux-là seront sauvés; et ils emmèneront de la ville leurs fils et leurs filles; puis voilà qu'ils viendront à vous, et vous verrez leurs voies et leurs pensées; et le repentir vous pénètrera, à cause des maux que j'aurai fait tomber sur Jérusalem, à cause de toutes les afflictions que je lui aurai envoyées.
23 Waliokoka watawafariji ninyi mtakapoona njia zao na matendo yao, hivyo mtayajua haya mambo niliyoyafanya juu yake, kwamba sijayafanya bure! -hivi ndivyo Bwana Yahwe asemavyo.”
Et ils vous consoleront, parce que vous verrez leurs voies et leurs pensées; et vous reconnaîtrez que ce n'est point à tort que j'ai fait tout ce que j'ai fait contre elle, dit le Seigneur.