< Ezekieli 12 >

1 Neno la Yahwe likanijia, kusema,
The word of Yahweh came to me, saying,
2 “Mwana wa adamu, unaishi kwenye nyumba ya uasi, wana macho ya kuona lakini hawaoni; na wana masikio ya kusikia lakini hawasikii, kwa sababu wao ni nyumba iliyoasi.
“Son of man, you live in the midst of a rebellious house, where they have eyes to see but they do not see; and where they have ears to hear but do not listen, because they are a rebellious house.
3 Kwa hiyo wewe mwanadamu, andaa mambo yako kwa ajili ya uhamisho, na anza kuondoka mchana usoni kwao, kwa kuwa nitakuhamisha kwenye uso wao kutoka sehemu yao kwenda sehemu nyingine. Labda wataanza kuona, kuwa wao ni nyumba ya uasi.
Therefore as for you, son of man, prepare your things for exile, and begin going out by day in their sight, for I will exile you in their sight from your place to another place. Perhaps they will begin to see, though they are a rebellious house.
4 Utatoa vitu vyako kwa ajili ya kuhamisha mchana katika macho yao; toka jioni kwenye macho yao kama ambavyo uendavyo kwenye uhamisho.
You will bring out your things for an exile in the day in their sight; go out in the evening in their sight in the way that anyone goes into exile.
5 Chimba shimo ukutani kwenye uso wa macho yao, na ingia ndani yake.
Dig a hole through the wall in their sight, and go out through it.
6 Kwenye macho yao, chukua vitu vyako kwenye mabega yako, na uwalete kwenye giza. Funika uso wako kama ishara kwenye nyumba ya Israeli.”
In their sight, lift up your things onto your shoulder, and bring them out in the darkness. Cover your face, for you must not see the land, since I have set you as a sign to the house of Israel.”
7 Hivyo nikafanya hivyo, kama nilivyokuwa nimeamriwa. Nikatoa vitu vya uhamisho wakati wa mchana, na katika jioni nikachimba shimo hata kwenye ukuta kwa mkono. Nikachukua vitu vyangu kwenye giza, na kuviweka juu kwenye bega langu katika macho yao.
So I did this, just as I was commanded. I brought out my things of exile in the daytime, and in the evening I dug a hole through the wall by hand. I brought my things out in the dark, and lifted them up on my shoulder in their sight.
8 Kisha neno la Yahwe likanijia asubuhi, likisema,
Then the word of Yahweh came to me in the morning, saying,
9 Mwanadamu, je nyumba ya Israeli, ile ni nyumba ya uasi, hawakukwambia, 'Unafanya nini?'
“Son of man, is the house of Israel, that rebellious house, not asking, 'What are you doing?'
10 Waambie, 'Bwana Yahwe asema hivi: hili tendo la kinabii linamhuusu mwana wa mfalme wa Yerusalemu, na nyumba yote ya Israeli walio kati yao.'
Say to them, 'The Lord Yahweh says this: this prophetic action concerns the prince in Jerusalem, and all the house of Israel in whose midst they are.'
11 Sema, 'Mimi ni ishara kwenu. Kama nilivyofanya, itafanyika kwao; watakwenda uhamishoni na kuwa wafungwa.
Say, 'I am a sign to you.' As I have done, so it will be done to them; they will go into exile and into captivity.
12 Yule mwana wa mfalme aliye miongoni mwao atavibeba vitu vyake kwenye bega lake katika giza, na ataenda zake kupitia kwenye ukuta. Watachimba kwenye ukuta na kutoa vitu vyao nje. Atafunika uso wake, hivyo hataona nchi kwa macho yake.
The prince who is among them will lift up his things upon his shoulder in the dark, and will go out through the wall. They will dig through the wall and bring out their things. He will cover his face, so he will not see the land with his eyes.
13 Nitausambaza wavu wangu juu yake naye atanaswa kwenye mtego wangu; kisha nitamleta Babeli, ncha ya Wakaldayo, lakini hataiona. Atafia huko.
I will spread out my net over him and he will be caught in my snare; then I will bring him to Babylon, the land of the Chaldeans, but he will not see it. He will die there.
14 Pia nitatawatawanya katika kila mwelekeo wale wote waliomzunguka wanaomsaidia na jeshi lake lote, na nitaufuata upanga nyuma yao.
I will also scatter in every direction all of those around him who were to assist him and his entire army, and I will send out a sword after them.
15 Kisha watajua kwamba mimi ni Yahwe, wakati nitakapo watawanya kwenye nchi zote.
Then they will know that I am Yahweh, when I scatter them among the nations and disperse them throughout the lands.
16 Lakini nitaacha kuwaangamiza watu wachache kutoka miongoni mwao kutoka kwenye upanga, njaa, na tauni, hivyo wanaweza kukumbuka maovu yao yote katika nchi zao nilipowachukulia, hivyo watajua kwamba mimi ni Yahwe.”'
But I will spare a few men from among them from the sword, famine, and plague, so they may record all of their abominations in the lands where I take them, so they will know that I am Yahweh.”
17 Neno la Yahwe likanijia, likisema,
The word of Yahweh came to me, saying,
18 “Mwanadamu, kula mkate wako kwa kutetemeka, na kunywa maji yako kwa mtetemo na hofu.
“Son of man, eat your bread with trembling, and drink your water with shaking and worry.
19 Kisha waambie watu wa nchi, 'Bwana Yahwe asema hivi kuhusiana na wale wakaao Yerusalemu, na nchi ya Israeli: Watakula mikate yao kwa kutetemeka na kunywa maji yao wakiwa wanatetemeka, kwa kuwa nchi itaporwa vitu vyote viijazavyo kwa sababu ya kuwa kinyume na waishio huko.
Then say to the people of the land, 'The Lord Yahweh says this concerning the inhabitants of Jerusalem, and the land of Israel, “They will eat their bread with trembling and drink their water while shaking, since the land will be despoiled of its fullness because of the violence of all those who live there.
20 Hivyo ile miji iliyokuwa wenyeji itachukuliwa, na nchi itakuwa ukiwa; hivyo mtajua kwamba mimi ni Yahwe.”'
So the cities that were inhabited will be desolate, and the land will become a wasteland; so you will know that I am Yahweh.”'”
21 Tena neno la Yahwe likanijia, likisema,
Again the word of Yahweh came to me, saying,
22 “Mwanadamu, je ni mithali gani hii mlio nayo katika nchi ya Israeli mliyoisema, 'Siku zimerefushwa, na kila ono linaanguka'?
“Son of man, what is this proverb that you have in the land of Israel that says, 'The days are prolonged, and every vision fails'?
23 Kwa hiyo, waambie, 'Bwana Yahwe asema hivi: Nitaweka mwisho wa hii mithali, na watu wa Israeli hawataitumia tena.' Waambie, 'Siku zi karibu wakati kila ono litatimizwa.
Therefore, say to them, 'The Lord Yahweh says this: I will put an end to this proverb, and the people of Israel will no longer use it.' Say to them, 'The days have drawn near when every vision will be fulfilled.
24 Kwa kuwa hakutakuwa na maono ya uongo yoyote wala upendeleo wa mgawanyiko kati ya nyumba ya Israeli.
For there will no longer be any false visions or favorable divinations within the house of Israel.
25 Kwa kuwa mimi Yahwe! Nimesema, na nitayatiza yale maneno nilyoyasema. Hakuna kitu kitakacho chelewesha. Kwa kuwa nitaongea hili neno katika siku zenu, nyumba ya uasi, na nitalitimiza! -hivi ndivyo Bwana Yahwe asemavyo.””
For I am Yahweh! I speak, and I carry out the words that I speak. The matter will no longer be delayed. For I will speak this word in your days, rebellious house, and I will carry it out!—this is the Lord Yahweh's declaration.'”
26 Tena neno la Yahwe likanijia, likisema,
Again the word of Yahweh came to me, saying,
27 “Mwanadamu! Tazama, nyumba ya Israeli imesema, 'Lile ono alionalo ni kwa siku nyingi kutoka sasa, na ametabiri kipindi kilicho mbali sana.'
“Son of man! Behold, the house of Israel has said, 'The vision that he sees is for many days from now, and he prophesies of far off times.'
28 Kwa hiyo waambie, 'Bwana Yahwe asema hivi: Neno langu halitacheleweshwa sana, lakini lile neno nililoliongea litatimizwa-hivi ndivyo Yahwe asemavyo.'”
Therefore say to them, 'The Lord Yahweh says this: My words will not be delayed any longer, but the word that I have spoken will be done—this is the Lord Yahweh's declaration.'”

< Ezekieli 12 >