< Ezekieli 12 >
1 Neno la Yahwe likanijia, kusema,
A message from the Lord came to me, saying,
2 “Mwana wa adamu, unaishi kwenye nyumba ya uasi, wana macho ya kuona lakini hawaoni; na wana masikio ya kusikia lakini hawasikii, kwa sababu wao ni nyumba iliyoasi.
“Son of man, you are living among rebellious people. They have eyes to see but they don't see, and ears to hear but they don't hear, because they are rebellious people.
3 Kwa hiyo wewe mwanadamu, andaa mambo yako kwa ajili ya uhamisho, na anza kuondoka mchana usoni kwao, kwa kuwa nitakuhamisha kwenye uso wao kutoka sehemu yao kwenda sehemu nyingine. Labda wataanza kuona, kuwa wao ni nyumba ya uasi.
So, son of man, go and pack your bags as if you're going into exile. As people watch, get everything ready during the day so you can leave where you are and go somewhere else. Maybe they will realize what this means, even though they are rebellious people.
4 Utatoa vitu vyako kwa ajili ya kuhamisha mchana katika macho yao; toka jioni kwenye macho yao kama ambavyo uendavyo kwenye uhamisho.
Take your bags out for traveling into exile during the day while they watch. But you yourself are to leave in the evening as they watch, just like someone going into exile.
5 Chimba shimo ukutani kwenye uso wa macho yao, na ingia ndani yake.
While they go on watching, knock down part of the wall of your house and take your belongings out through the hole.
6 Kwenye macho yao, chukua vitu vyako kwenye mabega yako, na uwalete kwenye giza. Funika uso wako kama ishara kwenye nyumba ya Israeli.”
When it gets dark, as they continue to watch, put your bags on your shoulder and carry them as you leave. Cover your face so that you can't see the country you're leaving behind, because I'm providing you as a sign to warn the people of Israel.”
7 Hivyo nikafanya hivyo, kama nilivyokuwa nimeamriwa. Nikatoa vitu vya uhamisho wakati wa mchana, na katika jioni nikachimba shimo hata kwenye ukuta kwa mkono. Nikachukua vitu vyangu kwenye giza, na kuviweka juu kwenye bega langu katika macho yao.
So I did as I was told. I took my bags out to go into exile during the day, and in the evening I knocked down part of the wall of my house with my bare hands. I took my belongings out when it got dark, carrying them on my shoulder while they watched.
8 Kisha neno la Yahwe likanijia asubuhi, likisema,
In the morning a message from the Lord came to me, saying,
9 Mwanadamu, je nyumba ya Israeli, ile ni nyumba ya uasi, hawakukwambia, 'Unafanya nini?'
“Son of man, haven't those rebellious Israelites asked you, ‘What are you doing?’
10 Waambie, 'Bwana Yahwe asema hivi: hili tendo la kinabii linamhuusu mwana wa mfalme wa Yerusalemu, na nyumba yote ya Israeli walio kati yao.'
Tell them that this is what the Lord God says: ‘This prophetic sign concerns the prince who is ruling in Jerusalem and all the people of Israel who are living there.’
11 Sema, 'Mimi ni ishara kwenu. Kama nilivyofanya, itafanyika kwao; watakwenda uhamishoni na kuwa wafungwa.
You are to say to them, ‘I'm a sign to you.’ Just as it was demonstrated here, so it will happen to them—they will go into exile as prisoners.
12 Yule mwana wa mfalme aliye miongoni mwao atavibeba vitu vyake kwenye bega lake katika giza, na ataenda zake kupitia kwenye ukuta. Watachimba kwenye ukuta na kutoa vitu vyao nje. Atafunika uso wake, hivyo hataona nchi kwa macho yake.
When it gets dark, their prince will also put his bags on his shoulder and leave. They will knock down the wall to take him away. He will cover his face so he can't see the country he's leaving behind.
13 Nitausambaza wavu wangu juu yake naye atanaswa kwenye mtego wangu; kisha nitamleta Babeli, ncha ya Wakaldayo, lakini hataiona. Atafia huko.
But I will catch him in my net; I will trap him in my snare. I will take him to Babylon in the country of Babylonia. However, won't see it, and he'll die there.
14 Pia nitatawatawanya katika kila mwelekeo wale wote waliomzunguka wanaomsaidia na jeshi lake lote, na nitaufuata upanga nyuma yao.
I'm going to scatter all his attendants and all his troops in every direction, and I will chase after them with a drawn sword.
15 Kisha watajua kwamba mimi ni Yahwe, wakati nitakapo watawanya kwenye nchi zote.
They will know that I am the Lord when I scatter them among the different nations and countries.
16 Lakini nitaacha kuwaangamiza watu wachache kutoka miongoni mwao kutoka kwenye upanga, njaa, na tauni, hivyo wanaweza kukumbuka maovu yao yote katika nchi zao nilipowachukulia, hivyo watajua kwamba mimi ni Yahwe.”'
But I will let a few of them survive war, famine, and disease so that they can tell the nations where they're exiled about all their disgusting sins. Then they will know that I am the Lord.”
17 Neno la Yahwe likanijia, likisema,
A message from the Lord came to me, saying,
18 “Mwanadamu, kula mkate wako kwa kutetemeka, na kunywa maji yako kwa mtetemo na hofu.
“Son of man, tremble as you eat your bread; shake with worry as you drink your water.
19 Kisha waambie watu wa nchi, 'Bwana Yahwe asema hivi kuhusiana na wale wakaao Yerusalemu, na nchi ya Israeli: Watakula mikate yao kwa kutetemeka na kunywa maji yao wakiwa wanatetemeka, kwa kuwa nchi itaporwa vitu vyote viijazavyo kwa sababu ya kuwa kinyume na waishio huko.
Then explain to the people of this country that this is what the Lord God says to those living in Jerusalem and in the country of Israel: They will be worried as eat their bread and they will be in despair as they drink their water, for their land will be stripped bare because of the violent crimes committed by everyone who lives there.
20 Hivyo ile miji iliyokuwa wenyeji itachukuliwa, na nchi itakuwa ukiwa; hivyo mtajua kwamba mimi ni Yahwe.”'
The towns will be destroyed, and the countryside turned into a wasteland. Then you will know that I am the Lord.”
21 Tena neno la Yahwe likanijia, likisema,
Another message from the Lord came to me, saying,
22 “Mwanadamu, je ni mithali gani hii mlio nayo katika nchi ya Israeli mliyoisema, 'Siku zimerefushwa, na kila ono linaanguka'?
“Son of man, what's this proverb you people have in the land of Israel: ‘Time goes by, and no vision comes true’?
23 Kwa hiyo, waambie, 'Bwana Yahwe asema hivi: Nitaweka mwisho wa hii mithali, na watu wa Israeli hawataitumia tena.' Waambie, 'Siku zi karibu wakati kila ono litatimizwa.
So tell them that this is what the Lord God says: ‘I will put a stop to this proverb. No one in Israel will quote it anymore.’ Instead tell them: The time is soon coming when every vision will come true.
24 Kwa kuwa hakutakuwa na maono ya uongo yoyote wala upendeleo wa mgawanyiko kati ya nyumba ya Israeli.
There won't be any more false visions or fake prophecies among the Israelites,
25 Kwa kuwa mimi Yahwe! Nimesema, na nitayatiza yale maneno nilyoyasema. Hakuna kitu kitakacho chelewesha. Kwa kuwa nitaongea hili neno katika siku zenu, nyumba ya uasi, na nitalitimiza! -hivi ndivyo Bwana Yahwe asemavyo.””
because I, the Lord, will say whatever I choose to say, and it will happen immediately. Right now, you rebellious people, I will say something and make sure it happens, declares the Lord God.”
26 Tena neno la Yahwe likanijia, likisema,
An additional message from the Lord came to me, saying,
27 “Mwanadamu! Tazama, nyumba ya Israeli imesema, 'Lile ono alionalo ni kwa siku nyingi kutoka sasa, na ametabiri kipindi kilicho mbali sana.'
“Son of man, notice what the people of Israel are saying, ‘The vision that he's describing won't happen for a long time. He's prophesying about a time in the distant future.’
28 Kwa hiyo waambie, 'Bwana Yahwe asema hivi: Neno langu halitacheleweshwa sana, lakini lile neno nililoliongea litatimizwa-hivi ndivyo Yahwe asemavyo.'”
So tell them that this is what the Lord God says: Everything I've said is about to happen. There won't be any more delay, declares the Lord God.”