< Ezekieli 11 >

1 Kisha Roho akaniacha juu na kunileta kwenye lango la mashariki la nyumba ya Yahwe, kuelekea mashariki, na tazama, kwenye njia ya mlango wa lango kulikuwa na watu ishirini na tano. Nikamwona Yaazania mwana wa Azuri na Pelatia mwana wa Benaya, viongozi wa watu, miongoni mwao.
Then the Spirit lifted me up and brought me to the eastern gate of Yahweh's house, facing east, and behold, in the doorway of the gate there were twenty-five men. I saw Jaazaniah son of Azzur and Pelatiah son of Benaiah, leaders of the people, among them.
2 Mungu akanambia, “Mwana wa adamu, hawa ndio wale watu walioshauri udhalimu, na kuamua mipango miovu kwenye huu mji.
God said to me, “Son of man, these are the men who devise iniquity, and who decide wicked plans in this city.
3 Wakisema, 'Mda wa kujenga nyumba sio sasa; huu mji ni sufuria, na sisi ni nyama.'
They are saying, 'The time to build houses is not now; this city is the pot, and we are the meat.'
4 Kwa hiyo tabiri juu yao. Tabiri, mwana wa adamu.”'
Therefore prophesy against them. Prophesy, son of man.”
5 Kisha Roho wa Yahwe akanijaza na akaniambia, “akisema: Hivi ndivyo Yahwe asemavyo: kama usemavyo, nyumba ya Israeli; kwa kuwa najua kinachoendelea kwenye fikra zenu.
Then the Spirit of Yahweh fell on me and he said for me to say: This is what Yahweh says, “That is what you are saying, house of Israel; for I know what goes through your mind.
6 Mmewazidisha watu mliowaua kwenye huu mji na kuijaza mitaa kwa hao.
You have multiplied the people you have killed in this city and filled its streets with them.
7 Kwa hiyo, Bwana Yahwe asema hivi: Wale watu milowaua, ambao mmeilaza miili yao kati ya Yerusalemu, ni nyama, na huu mji ni sufuria. Lakini mnaenda kutolewa nje kutoka kati ya huu mji.
Therefore, the Lord Yahweh says this: The people you have killed, whose bodies you have laid in the midst of Jerusalem, are the meat, and this city is the pot. But you are going to be brought out from the midst of this city.
8 Mmeuogopa upanga, kwa hiyo nauleta huo upanga juu yenu-huu ndio usemi wa Bwana Yahwe.
You have feared the sword, so I am bringing the sword upon you—this is the declaration of the Lord Yahweh.
9 Nitawatoa nje kutoka kati ya mji, na kuwaweka kwenye mikono ya wageni, kwa kuwa nitaleta hukumu dhidi yenu.
I will bring you out of the midst of the city, and put you into the hands of foreigners, for I will bring judgment against you.
10 Mtaanguka kwa upanga. Nitawahukumu kati ya mipaka ya Israeli hivyo mtajua yakwamba mimi ni Yahwe.
You will fall by the sword. I will judge you within the borders of Israel so you will know that I am Yahweh.
11 Huu mji hautakua sufuria yenu ya kupikia, wala hamtakuwa nyama ndani yake. Nitawahukumu kati ya mipaka ya Israeli.
This city will not be your cooking pot, nor will you be the meat within her midst. I will judge you within the borders of Israel.
12 Kisha mtajua yakwamba mimi ni Yahwe, yule ambaye hamuishe kwenye amri zake na ambaye hamkuzishika sheria zake. Badala yake, mmebeba hukumu za mataifa wanayowazunguka.”
Then you will know that I am Yahweh, the one whose statutes you have not walked in and whose decrees you have not carried out. Instead, you have carried out the decrees of the nations that surround you.”
13 Ikawa kwamba nilipokuwa natabiri, Pelatia mwana wa Benaya, akafa. Hivyo nikaanguka kwenye uso wangu na kulia kwa sauti na kusema, “Ee, Bwana Yahwe, Je utayaharibu kabisa mabaki ya Israeli?”
It came about that as I was prophesying, Pelatiah son of Benaiah, died. So I fell on my face and cried out with a loud voice and said, “Alas, Lord Yahweh, will you completely destroy the remnant of Israel?”
14 Neno la Yahwe likanijia, likisema,
The word of Yahweh came to me, saying,
15 “Mwana wa adamu, ndugu zako! Ndugu zako! Watu wa ukoo wako na nyumba yote ya Israeli! Wote hao ndio hao ambao inasemekana wale wanaoishi Yerusalemu, 'Wako mbali sana kutoka kwa Yahwe! Hii nchi tulipewa sisi kama milki yetu.'
“Son of man, your brothers! Your brothers! The men of your clan and all the house of Israel! All of them are those of whom it is said by those living in Jerusalem, 'They are far away from Yahweh! This land was given to us as our possession.'
16 Kwa hiyo sema, 'Bwana Yahwe asema hivi: kote nimewapitisha mbali kati ya mataifa, na kote nimewasambaza kati ya nchi, bado nimekuwa patakatifu kwa ajili yao kwa mda kidogo kwenye nchi ambazo walizoenda.'
Therefore say, 'The Lord Yahweh says this: Though I have removed them far off among the nations, and though I have scattered them among the lands, yet I have been a sanctuary for them for a little while in the lands where they have gone.'
17 Kwa hiyo sema, 'Bwana Yahwe asema hivi: Nitawakusanya kutoka kwa watu, na kuwakutanisha kutoka kwenye nchi mlizokuwa mmetawanyika, na nitawapatia nchi ya Israeli.'
Therefore say, 'The Lord Yahweh says this: I will gather you from the peoples, and assemble you from the lands where you were scattered, and I will give you the land of Israel.'
18 Kisha wataenda huko na kuondoa kila kitu chenye karaha na kila chukizo kutoka hiyo sehemu.
Then they will go there and remove every detestable thing and every abomination from that place.
19 Nitawapatia moyo mmoja, na nitaweka roho mpya kati yao. Nitaondoa moyo wa jiwe kutoka kwenye miili wao na kuwapatia moyo wa nyama,
I will give them one heart, and I will put a new spirit within them. I will take out the heart of stone from their flesh and give them a heart of flesh,
20 ili kwamba waweze kutembea kwenye amri zangu, watayachukua maagizo yangu na kuyatenda. Kisha watakuwa watu wangu, na nitakuwa Mungu wao.
so that they will walk in my statutes, they will carry out my decrees and do them. Then they will be my people, and I will be their God.
21 Lakini kwa wale watembeao kwa kujifanya kuendeleza mambo yao ya karaha na machukizo yao, nitaleta tabia yao kwenye vichwa vyao-hivi ndivyo Bwana Yahwe asemavyo.”
But to those who walk with affection toward their detestable things and their abominations, I will bring their conduct on their own heads—this is the Lord Yahweh's declaration.”
22 Makerubi wakainua mabawa yao na magurudumu yaliyokuwa karibu nao, na utukufu wa Mungu wa Israeli ulikuwa juu yao.
The cherubim lifted up their wings and the wheels that were beside them, and the glory of the God of Israel was high up over them.
23 Kisha utukufu wa Yahwe ukaenda juu kutoka katikati ya mji na kusimama kwenye mlima hata mashariki mwa mji.
Then the glory of Yahweh went up from within the midst of the city and stood on the mountain to the east of the city.
24 Roho akanichukua juu na kunileta hata Ukaldayo, hata uhamishoni, katika maono kutoka kwa Roho wa Mungu, na maono niliyokuwa nimeyaona yakaenda juu yakaniacha.
The Spirit lifted me up and brought me into Chaldea, to the exiles, in the vision from the Spirit of God, and the vision that I had seen went up from upon me.
25 Kisha nikawaambia wale watumwa mambo yote ya Yahwe niliyokuwa nimeyaona.
Then I declared to the exiles all the things of Yahweh that I had seen.

< Ezekieli 11 >