< Ezekieli 11 >

1 Kisha Roho akaniacha juu na kunileta kwenye lango la mashariki la nyumba ya Yahwe, kuelekea mashariki, na tazama, kwenye njia ya mlango wa lango kulikuwa na watu ishirini na tano. Nikamwona Yaazania mwana wa Azuri na Pelatia mwana wa Benaya, viongozi wa watu, miongoni mwao.
[Then God’s] Spirit lifted me up and took me to the gate on the east side of the temple area. There at the gate were 25 men. Among them I saw Jaazaniah the son of Azzur, and Pelatiah the son of Benaiah, who were leaders of the people.
2 Mungu akanambia, “Mwana wa adamu, hawa ndio wale watu walioshauri udhalimu, na kuamua mipango miovu kwenye huu mji.
Yahweh said to me, “You human, these are the [new leaders in Jerusalem] who are planning to do evil things and who are giving wicked advice [to people] in this city.
3 Wakisema, 'Mda wa kujenga nyumba sio sasa; huu mji ni sufuria, na sisi ni nyama.'
They say, ‘[Everything will go well for us, so] it will surely soon be [RHQ] time to build houses. [We are like] [MET] fine/choice pieces of meat that are carefully stored in covered pots, and we are protected [from the bad things that will happen to others].’
4 Kwa hiyo tabiri juu yao. Tabiri, mwana wa adamu.”'
So, you human, prophesy [the terrible things that will happen to] them.”
5 Kisha Roho wa Yahwe akanijaza na akaniambia, “akisema: Hivi ndivyo Yahwe asemavyo: kama usemavyo, nyumba ya Israeli; kwa kuwa najua kinachoendelea kwenye fikra zenu.
Then the Spirit of Yahweh came upon me and told me to [to the people], “This is what Yahweh says: You Israeli people [MTY] are saying those things, but I know what you are thinking.
6 Mmewazidisha watu mliowaua kwenye huu mji na kuijaza mitaa kwa hao.
You have killed many people in this city and filled the streets with their corpses.
7 Kwa hiyo, Bwana Yahwe asema hivi: Wale watu milowaua, ambao mmeilaza miili yao kati ya Yerusalemu, ni nyama, na huu mji ni sufuria. Lakini mnaenda kutolewa nje kutoka kati ya huu mji.
Therefore this is what Yahweh the Lord says: The corpses of the people whom you have killed here are [like] the meat [MET], and this city is [like] the pot [MET], but I will expel you from this city.
8 Mmeuogopa upanga, kwa hiyo nauleta huo upanga juu yenu-huu ndio usemi wa Bwana Yahwe.
You are afraid [being killed by enemies’] swords, and that is what I will cause to happen to you.
9 Nitawatoa nje kutoka kati ya mji, na kuwaweka kwenye mikono ya wageni, kwa kuwa nitaleta hukumu dhidi yenu.
I will expel you from this city and enable foreigners to capture you and punish you.
10 Mtaanguka kwa upanga. Nitawahukumu kati ya mipaka ya Israeli hivyo mtajua yakwamba mimi ni Yahwe.
They will kill [EUP] you with their swords; you will be punished [right here] in Israel. Then people will realize that I, Yahweh, [have the power to do what I say that I will do].
11 Huu mji hautakua sufuria yenu ya kupikia, wala hamtakuwa nyama ndani yake. Nitawahukumu kati ya mipaka ya Israeli.
This city will not be [a place were you will be protected like] [MET] meat in a covered pot. I will punish you wherever you are in Israel.
12 Kisha mtajua yakwamba mimi ni Yahwe, yule ambaye hamuishe kwenye amri zake na ambaye hamkuzishika sheria zake. Badala yake, mmebeba hukumu za mataifa wanayowazunguka.”
And you will know that I, Yahweh, [have predicted that would happen], because you have not obeyed my commands and decrees; instead, you have imitated [wicked] behavior [of the people] of the nearby nations.”
13 Ikawa kwamba nilipokuwa natabiri, Pelatia mwana wa Benaya, akafa. Hivyo nikaanguka kwenye uso wangu na kulia kwa sauti na kusema, “Ee, Bwana Yahwe, Je utayaharibu kabisa mabaki ya Israeli?”
While I was prophesying that, Pelatiah the son of Benaiah [suddenly] died. Then I prostrated myself on the ground and cried out loudly, “Yahweh my Lord, are you going [similarly] get rid of all the Israeli people who are still alive?”
14 Neno la Yahwe likanijia, likisema,
Then Yahweh gave me this message:
15 “Mwana wa adamu, ndugu zako! Ndugu zako! Watu wa ukoo wako na nyumba yote ya Israeli! Wote hao ndio hao ambao inasemekana wale wanaoishi Yerusalemu, 'Wako mbali sana kutoka kwa Yahwe! Hii nchi tulipewa sisi kama milki yetu.'
“You human, the people who are still in Jerusalem are talking about you and your own relatives and about all the other people who were (exiled/forced to go to other countries), saying, ‘They [in Babylonia], far from Yahweh. They have left their [here in Israel, so] their property now belongs to us!’”
16 Kwa hiyo sema, 'Bwana Yahwe asema hivi: kote nimewapitisha mbali kati ya mataifa, na kote nimewasambaza kati ya nchi, bado nimekuwa patakatifu kwa ajili yao kwa mda kidogo kwenye nchi ambazo walizoenda.'
So tell [them], “This is what Yahweh the Lord says: Although I caused them to be taken far [from Israel] and scattered them among other nations, for a short time I will (be like a refuge for/protect) them in the countries to which they have been taken.”
17 Kwa hiyo sema, 'Bwana Yahwe asema hivi: Nitawakusanya kutoka kwa watu, na kuwakutanisha kutoka kwenye nchi mlizokuwa mmetawanyika, na nitawapatia nchi ya Israeli.'
So also tell them, “This is what Yahweh the Lord says: [Some day] I will gather you from the [to which you have been taken] and bring you back to Israel, and you will live in your country/land [again].
18 Kisha wataenda huko na kuondoa kila kitu chenye karaha na kila chukizo kutoka hiyo sehemu.
When you return to your country, you will get rid of all the vile statues of gods and detestable idols.
19 Nitawapatia moyo mmoja, na nitaweka roho mpya kati yao. Nitaondoa moyo wa jiwe kutoka kwenye miili wao na kuwapatia moyo wa nyama,
I will put a new way of thinking [IDM] within you. I will cause you to no longer be stubborn [IDM], and I will enable you to obey me completely [IDM].
20 ili kwamba waweze kutembea kwenye amri zangu, watayachukua maagizo yangu na kuyatenda. Kisha watakuwa watu wangu, na nitakuwa Mungu wao.
When I do that, you will carefully obey all my laws [DOU]. You will be my people, and I will be your God.
21 Lakini kwa wale watembeao kwa kujifanya kuendeleza mambo yao ya karaha na machukizo yao, nitaleta tabia yao kwenye vichwa vyao-hivi ndivyo Bwana Yahwe asemavyo.”
But as for those who are devoted [worshiping] their vile statues and detestable idols, I will punish them as they deserve for the evil things that they have done.’”
22 Makerubi wakainua mabawa yao na magurudumu yaliyokuwa karibu nao, na utukufu wa Mungu wa Israeli ulikuwa juu yao.
Then the winged creatures, with their wheels beside them, spread their [and flew up into the air], and the dazzling brightness of Yahweh was above them.
23 Kisha utukufu wa Yahwe ukaenda juu kutoka katikati ya mji na kusimama kwenye mlima hata mashariki mwa mji.
That light went up away from the city and stopped above the mountain to the east of the city.
24 Roho akanichukua juu na kunileta hata Ukaldayo, hata uhamishoni, katika maono kutoka kwa Roho wa Mungu, na maono niliyokuwa nimeyaona yakaenda juu yakaniacha.
In the vision [that I had been seeing, God’s] Spirit lifted me up and brought me [back] to the (exiles in/people who had been forced to go to) Babylonia. Then the vision ended,
25 Kisha nikawaambia wale watumwa mambo yote ya Yahwe niliyokuwa nimeyaona.
and I told the exiles everything that Yahweh had shown [in the vision].

< Ezekieli 11 >