< Ezekieli 11 >

1 Kisha Roho akaniacha juu na kunileta kwenye lango la mashariki la nyumba ya Yahwe, kuelekea mashariki, na tazama, kwenye njia ya mlango wa lango kulikuwa na watu ishirini na tano. Nikamwona Yaazania mwana wa Azuri na Pelatia mwana wa Benaya, viongozi wa watu, miongoni mwao.
Then the spirit lifted me up, and brought me to the east gate of the house of Jehovah, that looketh toward the east; and behold, at the entrance of the gate were five and twenty men; among whom I saw Jaazaniah, the son of Azur, and Pelatiah, the son of Benaiah, princes of the people.
2 Mungu akanambia, “Mwana wa adamu, hawa ndio wale watu walioshauri udhalimu, na kuamua mipango miovu kwenye huu mji.
Then said He to me: These are the men that devise mischief, and form evil designs in this city;
3 Wakisema, 'Mda wa kujenga nyumba sio sasa; huu mji ni sufuria, na sisi ni nyama.'
who say, “The time is not near that we should build houses. This city is the caldron, and we are the flesh.”
4 Kwa hiyo tabiri juu yao. Tabiri, mwana wa adamu.”'
Therefore, prophesy against them, prophesy, O son of man!
5 Kisha Roho wa Yahwe akanijaza na akaniambia, “akisema: Hivi ndivyo Yahwe asemavyo: kama usemavyo, nyumba ya Israeli; kwa kuwa najua kinachoendelea kwenye fikra zenu.
And the spirit of Jehovah fell upon me, and he said to me, Speak: Thus saith Jehovah: Thus have ye said, O house of Israel! For I know the things that come into your mind, every one of them.
6 Mmewazidisha watu mliowaua kwenye huu mji na kuijaza mitaa kwa hao.
Ye have multiplied your slain in this city, and ye have filled the streets thereof with the slain.
7 Kwa hiyo, Bwana Yahwe asema hivi: Wale watu milowaua, ambao mmeilaza miili yao kati ya Yerusalemu, ni nyama, na huu mji ni sufuria. Lakini mnaenda kutolewa nje kutoka kati ya huu mji.
Therefore thus saith the Lord Jehovah: Your slain, whom ye have laid in the midst of it, they are the flesh, and this city is the caldron; but you will I bring forth out of the midst of it.
8 Mmeuogopa upanga, kwa hiyo nauleta huo upanga juu yenu-huu ndio usemi wa Bwana Yahwe.
Ye have feared the sword, and the sword will I bring upon you, saith the Lord Jehovah.
9 Nitawatoa nje kutoka kati ya mji, na kuwaweka kwenye mikono ya wageni, kwa kuwa nitaleta hukumu dhidi yenu.
And I will bring you out of the midst thereof, and deliver you into the hands of strangers, and execute judgments upon you.
10 Mtaanguka kwa upanga. Nitawahukumu kati ya mipaka ya Israeli hivyo mtajua yakwamba mimi ni Yahwe.
Ye shall fall by the sword; on the borders of Israel will I judge you, that ye may know that I am Jehovah.
11 Huu mji hautakua sufuria yenu ya kupikia, wala hamtakuwa nyama ndani yake. Nitawahukumu kati ya mipaka ya Israeli.
This city shall not be your caldron, neither shall ye be the flesh in the midst thereof. On the borders of Israel will I judge you,
12 Kisha mtajua yakwamba mimi ni Yahwe, yule ambaye hamuishe kwenye amri zake na ambaye hamkuzishika sheria zake. Badala yake, mmebeba hukumu za mataifa wanayowazunguka.”
that ye may know that I am Jehovah, in whose statutes ye have not walked, and whose ordinances ye have not observed, but have done according to the manners of the nations, that are round about you.
13 Ikawa kwamba nilipokuwa natabiri, Pelatia mwana wa Benaya, akafa. Hivyo nikaanguka kwenye uso wangu na kulia kwa sauti na kusema, “Ee, Bwana Yahwe, Je utayaharibu kabisa mabaki ya Israeli?”
And it came to pass, when I prophesied, that Pelatiah, the son of Benaiah, died. Then I fell down on my face, and cried with a loud voice, and said, Ah, Lord Jehovah, wilt thou make a full end of the remnant of Israel?
14 Neno la Yahwe likanijia, likisema,
And the word of Jehovah came to me, saying:
15 “Mwana wa adamu, ndugu zako! Ndugu zako! Watu wa ukoo wako na nyumba yote ya Israeli! Wote hao ndio hao ambao inasemekana wale wanaoishi Yerusalemu, 'Wako mbali sana kutoka kwa Yahwe! Hii nchi tulipewa sisi kama milki yetu.'
Son of man, thy brethren, even thy brethren, the men of thy near kindred, and the whole house of Israel, are they to whom the inhabitants of Jerusalem say, “Remove ye far from Jehovah; to us is the land given in possession!”
16 Kwa hiyo sema, 'Bwana Yahwe asema hivi: kote nimewapitisha mbali kati ya mataifa, na kote nimewasambaza kati ya nchi, bado nimekuwa patakatifu kwa ajili yao kwa mda kidogo kwenye nchi ambazo walizoenda.'
Therefore say, Thus saith the Lord Jehovah: Though I have cast them far off among the nations, and scattered them among the countries, yet I will be to them as a sanctuary for a short time in the countries whither they are come.
17 Kwa hiyo sema, 'Bwana Yahwe asema hivi: Nitawakusanya kutoka kwa watu, na kuwakutanisha kutoka kwenye nchi mlizokuwa mmetawanyika, na nitawapatia nchi ya Israeli.'
Therefore say, Thus saith the Lord Jehovah: I will gather you from the nations, and assemble you from the countries where ye have been scattered, and I will give you the land of Israel.
18 Kisha wataenda huko na kuondoa kila kitu chenye karaha na kila chukizo kutoka hiyo sehemu.
And they shall come thither, and they shall take away from thence all the detestable things thereof, and all the abominations thereof.
19 Nitawapatia moyo mmoja, na nitaweka roho mpya kati yao. Nitaondoa moyo wa jiwe kutoka kwenye miili wao na kuwapatia moyo wa nyama,
And I will give them one heart, and I will put a new spirit within them; and I will take out of them the heart of stone, and will give them a heart of flesh,
20 ili kwamba waweze kutembea kwenye amri zangu, watayachukua maagizo yangu na kuyatenda. Kisha watakuwa watu wangu, na nitakuwa Mungu wao.
that they may walk in my statutes, and observe my ordinances, and keep them; and they shall be my people, and I will be their God.
21 Lakini kwa wale watembeao kwa kujifanya kuendeleza mambo yao ya karaha na machukizo yao, nitaleta tabia yao kwenye vichwa vyao-hivi ndivyo Bwana Yahwe asemavyo.”
But as for them whose heart walketh according to the pleasure of their detestable things and their abominations, I will recompense their way upon their heads, saith the Lord Jehovah.
22 Makerubi wakainua mabawa yao na magurudumu yaliyokuwa karibu nao, na utukufu wa Mungu wa Israeli ulikuwa juu yao.
Then did the cherubs lift up their wings, and the wheels were beside them; and the glory of the God of Israel was over them above.
23 Kisha utukufu wa Yahwe ukaenda juu kutoka katikati ya mji na kusimama kwenye mlima hata mashariki mwa mji.
And the glory of Jehovah went up from the midst of the city, and stood upon the mountain which is on the east side of the city.
24 Roho akanichukua juu na kunileta hata Ukaldayo, hata uhamishoni, katika maono kutoka kwa Roho wa Mungu, na maono niliyokuwa nimeyaona yakaenda juu yakaniacha.
Then the spirit took me up, and brought me to Chaldaea, to them of the captivity, in vision, by the spirit of God. And the vision which I had seen went up from me.
25 Kisha nikawaambia wale watumwa mambo yote ya Yahwe niliyokuwa nimeyaona.
Then I spake to them of the captivity all the words of Jehovah which he had showed me.

< Ezekieli 11 >