< Kutoka 1 >
1 Haya ndiyo majina ya wana wa Israeli waliokuja Misri pamoja na Yakobo kila moja na familia yake:
These are the names of the sons of Israel, who went into Egypt with Jacob. They entered, each one with his house:
2 Rubeni, Simioni, Lawi, na Yuda,
Reuben, Simeon, Levi, Judah,
3 Isakari, Zebuluni, na Benjamini,
Issachar, Zebulun, and Benjamin,
4 Dani, Naftali, Gadi, na Asheri.
Dan and Naphtali, Gad and Asher.
5 Jumla ya watu wa ukoo wa Yakobo walikuwa sabini. Yusufu alikuwa Misri tayari.
Therefore, all the souls of those who went forth from Jacob’s thigh were seventy. Now Joseph was in Egypt.
6 Ndipo Yusufu, pamoja na kaka zake wote, na kizazi chote wakafa.
When he had died, along with all of his brothers and all of that generation,
7 Waisraeli walifanikiwa sana, wakaongezeka sana idadi yao, na wakawa na nguvu maana nchi ilijazwa na wao.
the sons of Israel increased, and they multiplied like seedlings. And having been strengthened exceedingly, they filled the land.
8 Wakati huu sasa mfalme mpya asiyemjua Yusufu aliinuka katika Misri.
Meanwhile, there arose a new king over Egypt, who was ignorant of Joseph.
9 Akawaambia watu wake, “Tazama, hawa Waisraeli ni wengi na wenye nguvu kuliko sisi.
And he said to his people: “Behold, the people of the sons of Israel are many, and they are stronger than we are.
10 Njooni na tukae nao kwa akili, ama sivyo wataendelea kuongezeka na kama vita ikiibuka, wataungana na adui zetu, watapigana nasi, na kisha wataondoka.”
Come, let us wisely oppress them, lest they multiply; and if any war should advance against us, they may be added to our enemies, and having fought against us, they might depart from the land.”
11 Hivyo wakawekea walinzi ambao waliwatesa kwa kuwatumikisha kazi ngumu. Waisraeli walijenga maghala ya miji kwa ajili ya Farao: Pishoni na Ramsei.
And so he set over them masters of the works, in order to afflict them with burdens. And they built for Pharaoh the cities of the tabernacles: Pithom and Raamses.
12 Lakini kadiri Wamisri walivyowatesa, ndivyo Waisraeli waliendelea kuongezeka na kusambaa. Hivyo Wamisri wakaanza kuwaogopa Waisraeli.
And the more they oppressed them, so much more did they multiply and increase.
13 Wamisri waliwafanya Waisraeli wafanye kazi kwa nguvu nyingi.
And the Egyptians hated the sons of Israel, and they afflicted them and mocked them.
14 Waliyafanya maisha yao kuwa machungu kwa kuwafanyisha kazi ngumu kwa vinu na matofali na kwa kila aina ya kazi za shambani. Kazi zao zote zilikuwa ngumu.
And they led their life directly into bitterness, with hard work in clay and brick, and with all kinds of servitude, so that they were being overwhelmed with the works of the land.
15 Kisha mfalme wa Misri akawaambia wakunga wa Kiebrania; mmoja wao aliitwa jina lake Shifra, na mwingine aliitwa Puha.
Then the king of Egypt spoke to the midwives of the Hebrews, (one of whom one was called Shiphrah, another Puah)
16 Akasema, “Wakati mnapowasaidia wanawake wa Kiebrania wanapojifungua, chunguzeni wanapozaa. Ikiwa ni mtoto wa kiume, basi muueni; bali ikiwa ni mtoto wa kike, basi mwacheni aishi.”
instructing them: “When you will act as a midwife to the Hebrew women, and the time of delivery has arrived: if it is male, put it to death; if it is female, retain it.”
17 Lakini wale Wakunga walimwogopa Mungu na hawakufanya kama mfalme wa Misri alivyowaagiza; badala yake waliwaacha watoto wa kiume waishi.
But the midwives feared God, and so they did not act according to the precept of the king of Egypt, but they kept the males safe.
18 Mfalme wa Misri akawaita Wakunga na kuwaambia, “Kwanini mmefanya haya, na kuwaacha watoto wa kiume wakaishi?”
And summoning them, the king said, “What did you intend to do, so that you would save the boys?”
19 Wale Wakunga wakamjibu Farao, “Hawa wanawake wa Kiebrania siyo kama wanawake wa Kimisri. Hawa wana nguvu na jasiri sana maana wao humaliza kuzaa kabla hata mkunga hajafika.”
They responded: “The Hebrew women are not like the Egyptian women. For they themselves have the wisdom of a midwife, and so they give birth before we can come to them.”
20 Mungu aliwalinda hawa Wakunga. Watu waliongezeka kwa idadi na kuwa na nguvu sana.
Therefore, God acted favorably toward the midwives. And the people increased, and they were strengthened exceedingly.
21 Kwa sababu wale Wakunga walimwogopa Mungu, aliwapa familia.
And because the midwives feared God, he built houses for them.
22 Farao akawaagiza watu wote, “Lazima mmutupe kila mtoto wa kiume anayezaliwa katika mto, lakini kila mtoto wa kike wamwache aishi.”
Therefore, Pharaoh instructed all his people, saying: “Whatever will be born of the male sex, cast it into the river; whatever will be born of the female sex, retain it.”