< Kutoka 1 >

1 Haya ndiyo majina ya wana wa Israeli waliokuja Misri pamoja na Yakobo kila moja na familia yake:
以色列的眾子,各帶家眷,和雅各一同來到埃及。他們的名字記在下面。
2 Rubeni, Simioni, Lawi, na Yuda,
有呂便、西緬、利未、猶大、
3 Isakari, Zebuluni, na Benjamini,
以薩迦、西布倫、便雅憫、
4 Dani, Naftali, Gadi, na Asheri.
但、拿弗他利、迦得、亞設。
5 Jumla ya watu wa ukoo wa Yakobo walikuwa sabini. Yusufu alikuwa Misri tayari.
凡從雅各而生的,共有七十人。約瑟已經在埃及。
6 Ndipo Yusufu, pamoja na kaka zake wote, na kizazi chote wakafa.
約瑟和他的弟兄,並那一代的人,都死了。
7 Waisraeli walifanikiwa sana, wakaongezeka sana idadi yao, na wakawa na nguvu maana nchi ilijazwa na wao.
以色列人生養眾多,並且繁茂,極其強盛,滿了那地。
8 Wakati huu sasa mfalme mpya asiyemjua Yusufu aliinuka katika Misri.
有不認識約瑟的新王起來,治理埃及,
9 Akawaambia watu wake, “Tazama, hawa Waisraeli ni wengi na wenye nguvu kuliko sisi.
對他的百姓說:「看哪,這以色列民比我們還多,又比我們強盛。
10 Njooni na tukae nao kwa akili, ama sivyo wataendelea kuongezeka na kama vita ikiibuka, wataungana na adui zetu, watapigana nasi, na kisha wataondoka.”
來吧,我們不如用巧計待他們,恐怕他們多起來,日後若遇甚麼爭戰的事,就連合我們的仇敵攻擊我們,離開這地去了。」
11 Hivyo wakawekea walinzi ambao waliwatesa kwa kuwatumikisha kazi ngumu. Waisraeli walijenga maghala ya miji kwa ajili ya Farao: Pishoni na Ramsei.
於是埃及人派督工的轄制他們,加重擔苦害他們。他們為法老建造兩座積貨城,就是比東和蘭塞。
12 Lakini kadiri Wamisri walivyowatesa, ndivyo Waisraeli waliendelea kuongezeka na kusambaa. Hivyo Wamisri wakaanza kuwaogopa Waisraeli.
只是越發苦害他們,他們越發多起來,越發蔓延;埃及人就因以色列人愁煩。
13 Wamisri waliwafanya Waisraeli wafanye kazi kwa nguvu nyingi.
埃及人嚴嚴地使以色列人做工,
14 Waliyafanya maisha yao kuwa machungu kwa kuwafanyisha kazi ngumu kwa vinu na matofali na kwa kila aina ya kazi za shambani. Kazi zao zote zilikuwa ngumu.
使他們因做苦工覺得命苦;無論是和泥,是做磚,是做田間各樣的工,在一切的工上都嚴嚴地待他們。
15 Kisha mfalme wa Misri akawaambia wakunga wa Kiebrania; mmoja wao aliitwa jina lake Shifra, na mwingine aliitwa Puha.
有希伯來的兩個收生婆,一名施弗拉,一名普阿;埃及王對她們說:
16 Akasema, “Wakati mnapowasaidia wanawake wa Kiebrania wanapojifungua, chunguzeni wanapozaa. Ikiwa ni mtoto wa kiume, basi muueni; bali ikiwa ni mtoto wa kike, basi mwacheni aishi.”
「你們為希伯來婦人收生,看她們臨盆的時候,若是男孩,就把他殺了;若是女孩,就留她存活。」
17 Lakini wale Wakunga walimwogopa Mungu na hawakufanya kama mfalme wa Misri alivyowaagiza; badala yake waliwaacha watoto wa kiume waishi.
但是收生婆敬畏上帝,不照埃及王的吩咐行,竟存留男孩的性命。
18 Mfalme wa Misri akawaita Wakunga na kuwaambia, “Kwanini mmefanya haya, na kuwaacha watoto wa kiume wakaishi?”
埃及王召了收生婆來,說:「你們為甚麼做這事,存留男孩的性命呢?」
19 Wale Wakunga wakamjibu Farao, “Hawa wanawake wa Kiebrania siyo kama wanawake wa Kimisri. Hawa wana nguvu na jasiri sana maana wao humaliza kuzaa kabla hata mkunga hajafika.”
收生婆對法老說:「因為希伯來婦人與埃及婦人不同;希伯來婦人本是健壯的,收生婆還沒有到,她們已經生產了。」
20 Mungu aliwalinda hawa Wakunga. Watu waliongezeka kwa idadi na kuwa na nguvu sana.
上帝厚待收生婆。以色列人多起來,極其強盛。
21 Kwa sababu wale Wakunga walimwogopa Mungu, aliwapa familia.
收生婆因為敬畏上帝,上帝便叫她們成立家室。
22 Farao akawaagiza watu wote, “Lazima mmutupe kila mtoto wa kiume anayezaliwa katika mto, lakini kila mtoto wa kike wamwache aishi.”
法老吩咐他的眾民說:「以色列人所生的男孩,你們都要丟在河裏;一切的女孩,你們要存留她的性命。」

< Kutoka 1 >