< Kutoka 1 >
1 Haya ndiyo majina ya wana wa Israeli waliokuja Misri pamoja na Yakobo kila moja na familia yake:
以色列的兒子們,各帶了家眷,同雅各伯來到埃及;他們的名字記載如下:
2 Rubeni, Simioni, Lawi, na Yuda,
勒烏本、西默盎、勒末和猶大,
3 Isakari, Zebuluni, na Benjamini,
依撒加爾,則步隆和本雅明丹,
4 Dani, Naftali, Gadi, na Asheri.
和納裴塔里,加得和阿協爾。
5 Jumla ya watu wa ukoo wa Yakobo walikuwa sabini. Yusufu alikuwa Misri tayari.
他們全是雅各伯所生的,一共七十人;若瑟那時已經在埃及。
6 Ndipo Yusufu, pamoja na kaka zake wote, na kizazi chote wakafa.
若瑟和他的眾兄弟,以及這一代的人死了以後,
7 Waisraeli walifanikiwa sana, wakaongezeka sana idadi yao, na wakawa na nguvu maana nchi ilijazwa na wao.
以色列的子孫生育繁殖,數目增多,極其強盛,佈滿了那地。受壓迫
8 Wakati huu sasa mfalme mpya asiyemjua Yusufu aliinuka katika Misri.
有位不認識若瑟的新王興起,統治了埃及。
9 Akawaambia watu wake, “Tazama, hawa Waisraeli ni wengi na wenye nguvu kuliko sisi.
他對自己的人民說:「看以色列子民,比我們又多又強。
10 Njooni na tukae nao kwa akili, ama sivyo wataendelea kuongezeka na kama vita ikiibuka, wataungana na adui zetu, watapigana nasi, na kisha wataondoka.”
來,我們要用智謀對付他們,免得他們繁盛起來,一遇戰爭,就去與我們的敵人聯合,攻擊我們,然後離開此地。」
11 Hivyo wakawekea walinzi ambao waliwatesa kwa kuwatumikisha kazi ngumu. Waisraeli walijenga maghala ya miji kwa ajili ya Farao: Pishoni na Ramsei.
於是派定督工管制他們,以苦役壓迫他們,叫他們給法朗建築丕通和辣默色斯兩做貯貨城。
12 Lakini kadiri Wamisri walivyowatesa, ndivyo Waisraeli waliendelea kuongezeka na kusambaa. Hivyo Wamisri wakaanza kuwaogopa Waisraeli.
但是越壓迫他們,他們越增多,也越繁殖,以至埃及人都怕以色列子民。
13 Wamisri waliwafanya Waisraeli wafanye kazi kwa nguvu nyingi.
於是埃及人更嚴厲地強迫以色列子民做苦工,
14 Waliyafanya maisha yao kuwa machungu kwa kuwafanyisha kazi ngumu kwa vinu na matofali na kwa kila aina ya kazi za shambani. Kazi zao zote zilikuwa ngumu.
強迫他們作和泥做磚的苦工,田間的一切勞工,以及種種苦工,使他們的生活十分痛苦。殘害男嬰
15 Kisha mfalme wa Misri akawaambia wakunga wa Kiebrania; mmoja wao aliitwa jina lake Shifra, na mwingine aliitwa Puha.
埃及王又吩咐為希伯來女人接生的收生婆,一個名叫史斐辣,一個名叫普亞的說
16 Akasema, “Wakati mnapowasaidia wanawake wa Kiebrania wanapojifungua, chunguzeni wanapozaa. Ikiwa ni mtoto wa kiume, basi muueni; bali ikiwa ni mtoto wa kike, basi mwacheni aishi.”
「你們為希伯來女人接生時,要看著她們臨盆! 若是男孩,就殺死;若是女孩,就讓她活著。」
17 Lakini wale Wakunga walimwogopa Mungu na hawakufanya kama mfalme wa Misri alivyowaagiza; badala yake waliwaacha watoto wa kiume waishi.
但是收生婆敬畏天主,沒有照埃及王的吩咐去作,保留了男孩的性命。
18 Mfalme wa Misri akawaita Wakunga na kuwaambia, “Kwanini mmefanya haya, na kuwaacha watoto wa kiume wakaishi?”
埃及王將收生婆召來,問她們說:「你們為什麼這樣做,竟叫男孩活著呢﹖」
19 Wale Wakunga wakamjibu Farao, “Hawa wanawake wa Kiebrania siyo kama wanawake wa Kimisri. Hawa wana nguvu na jasiri sana maana wao humaliza kuzaa kabla hata mkunga hajafika.”
‧收收婆回答法朗說:「希伯來女人和埃及女人不同,她們富有生機,收生婆還沒有來,她們已生產了。」
20 Mungu aliwalinda hawa Wakunga. Watu waliongezeka kwa idadi na kuwa na nguvu sana.
天主遂恩待了收生婆。以色列的子民更加增多起來,更加強盛。
21 Kwa sababu wale Wakunga walimwogopa Mungu, aliwapa familia.
因為收生婆敬畏天主,天主就使她們家門興旺。
22 Farao akawaagiza watu wote, “Lazima mmutupe kila mtoto wa kiume anayezaliwa katika mto, lakini kila mtoto wa kike wamwache aishi.”
法朗於是訓令他的全體人民說:「凡希伯來人所生的男孩,你們應把他丟在尼羅河裏;凡是女孩,留她活著! 」