< Kutoka 6 >
1 Kisha Yahweh akasema na Musa, “Sasa utaona nitakacho fanya kwa Farao. Utaona hili, kwa kuwa ata waacha waenda kwa mkono wangu hodari. Kwasababu ya mkono wangu hodari, ata waondoa nje ya nchi.”
Then Yahweh said to Moses, “Now you will see what I will do to Pharaoh. You will see this, for he will let them go because of my strong hand. Because of my strong hand, he will drive them out of his land.”
2 Mungu akasema na Musa na kumwambia, “Mimi ni Yahweh.
God spoke to Moses and said to him, “I am Yahweh.
3 Nilimtokea Ibrahimu, Isaka, na Yakobo kama Mungu mwenye nguvu; lakini kwa jina langu, Yahweh, sikujuliikana kwao.
I appeared to Abraham, to Isaac, and to Jacob as God Almighty; but by my name, Yahweh, I was not known to them.
4 Pia niliimarisha agano langu na wao, ilikuwapatia nchi ya Kanani, nchi walioishi kama sio raia, nchi walio tanga tanga.
I also established my covenant with them, in order to give them the land of Canaan, the land where they lived as non-citizens, the land in which they wandered about.
5 Zaidi ya yote, nimesikia kilio cha Waisraeli ambao wa Misri wame wa chukua watumwa, na nimekumbuka agano langu.
Moreover, I have heard the groaning of the Israelites whom the Egyptians have enslaved, and I have called to mind my covenant.
6 Kisha basi, sema kwa Waisraeli, 'Mimi ni Yahweh. Nitawatoa kwenye utumwa chini ya wa Misri, na kuwaweka huru na nguvu zao. Nitawaokoa kwa kudhihirisha nguvu zangu, na kwa matendo ya ajabu ya hukumu.
Therefore, say to the Israelites, 'I am Yahweh. I will bring you out from slavery under the Egyptians, and I will free you from their power. I will rescue you with a display of my power, and with mighty acts of judgment.
7 Nitawaleta kwangu kama watu wangu, na nitakuwa Mungu wenu. Mtajua kuwa mimi ndiye Yahweh Mungu wenu, aliye watoa kwenye utumwa chini ya wa Misri.
I will take you to myself as my people, and I will be your God. You will know that I am Yahweh your God, who brought you out from slavery under the Egyptians.
8 Nitawaleta kwenye nchi niliyo muahidi kumpa Ibrahimu, Isaka, na Yakobo. Nitawapa kama mali yenu. Mimi ni Yahweh.”'
I will bring you into the land that I swore to give to Abraham, to Isaac, and to Jacob. I will give it to you as a possession. I am Yahweh.'”
9 Musa alipo waambia haya Waisraeli, hawakumsiliza kwasababu ya mateso magumu ya utumwa wao.
When Moses told this to the Israelites, they would not listen to him because of their discouragement about their harsh slavery.
10 Hivyo Yahweh akazungumza na Musa na kumwambia,
Then Yahweh spoke to Moses, saying,
11 “Nenda umwambie Farao, mfalme wa Misri, awaache watu wa Israeli waondoke kwenye nchi yake.”
“Go tell Pharaoh, king of Egypt, to let the people of Israel go from his land.”
12 Musa akamwambia Yahweh, “Kama Waisraeli hawajanisikiliza mimi, kwa nini Farao anisikillize mimi, tangu mimi sio mzuri wakuzungumza?”
Moses said to Yahweh, “If the Israelites have not listened to me, why will Pharaoh listen to me, since I am not good at speaking?”
13 Yahweh akasema na Musa na Aruni. Akawapa amri ya Waisraeli na Farao, mfalme wa Misri, awatoe Waisraeli kutoka nchi ya Misri.
Yahweh spoke to Moses and to Aaron. He gave them a command for the Israelites and for Pharaoh, king of Egypt, to bring the Israelites out of the land of Egypt.
14 Hawa walikuwa vichwa wa nyumba za baba yao: wana wa Rubeni, mzaliwa wa kwanza wa Israeli, walikuwa Hanoki, Palu, Hezroni, na Karmi. Hawa walikuwa mababu wa ukoo wa Rubeni.
These were the heads of their fathers' houses: The sons of Reuben, the firstborn of Israel, were Hanok, Pallu, Hezron, and Karmi. These were the clan ancestors of Reuben.
15 Wana wa Simeoni walikuwa Yemueli, Yamini, Ohadi, Yakini, Zohari, na Shauli - mwana wa mwanamke wa Kanani. Hawa walikuwa mababu wa ukoo wa Simeoni.
The sons of Simeon were Jemuel, Jamin, Ohad, Jakin, Zohar, and Shaul—the son of a Canaanite woman. These were the clan ancestors of Simeon.
16 Hapa yameorodheshwa majina ya wana wa Lawi, pamoja na uzo wao. Walikuwa ni Gerishoni, Kohathi, na Merari. Lawi aliishi mpaka alipo kuwa na miaka 137.
Here are listed the names of the sons of Levi, together with their descendants. They were Gershon, Kohath, and Merari. Levi lived until he was 137 years old.
17 Wana wa Gerishoni walikuwa Libni na Shimei.
The sons of Gershon were Libni and Shimei.
18 Wana wa Kohathi walikuwa Amramu, Izhari, Hebroni, na uzieli. Kohathi aliishi hadi miaka 133.
The sons of Kohath were Amram, Izhar, Hebron, and Uzziel. Kohath lived until he was 133 years old.
19 Wana wa Merari walikuwa Mahli na Mushi. Hawa walikuja kuwa mababu wa ukoo wa Walawi, pamoja na uzao wao.
The sons of Merari were Mahli and Mushi. These became the clan ancestors of the Levites, together with their descendants.
20 Amramu alimuoa Yokebedi, dada yake baba yake. Alimzalia Aruni na Musa. Amramu aliishi miaka 137 na akafa.
Amram married Jochebed, his father's sister. She bore him Aaron and Moses. Amram lived 137 years and then died.
21 Wana wa Izhari walikuwa Kora, Nefegi, na Zikri.
The sons of Izhar were Korah, Nepheg, and Zichri.
22 Wana wa Uzieli walikuwa Mishaeli, Elizafani na Sithri.
The sons of Uzziel were Mishael, Elzaphan, and Sithri.
23 Aruni alimuoa Elisheba, binti wa Aminadabu, dada wa Nashoni. Alimzaa Nadabu na Abihu, Eleazari na Ithamari.
Aaron married Elisheba, daughter of Amminadab, sister of Nahshon. She bore him Nadab and Abihu, Eleazar and Ithamar.
24 Wana wa Kora walikuwa Asiri, Elikana na Abiasa. Hawa walikuwa mababu wa ukoo wa Wakora.
The sons of Korah were Assir, Elkanah, and Abiasaph. These were the clan ancestors of the Korahites.
25 Eleazari, mwana wa Aruni, alimuoa mmoja wa mabinti Wa Putieli. Alimzalia Fineazi. Hawa walikuwa vichwa wa nyumba za baba yao miongoni mwa Walawi, pamoja na uzao wao.
Eleazar, Aaron's son, married one of the daughters of Putiel. She bore him Phinehas. These were the heads of the fathers' houses among the Levites, together with their descendants.
26 Hawa wanaume wawili walikuwa Musa na Aruni ambao Yahweh alisema, “Waleteni Waisraeli kutoka nchi ya Misri, kwa makundi ya wanaume wapiganaji.”
These two men were the Aaron and Moses to whom Yahweh said, “Bring out the Israelites from the land of Egypt, by their groups of fighting men.”
27 Aruni na Musa wakazungumza na Farao, mfalme wa Misri, awaruhusu Waisraeli watoke Misri. Hawa walikuwa Musa na Aruni wale wale.
Aaron and Moses spoke to Pharaoh, king of Egypt, to allow them bring out the Israelites from Egypt. These were the same Moses and Aaron.
28 Pale Yahweh alipo zungumza na Musa katika nchi ya Misri,
When Yahweh spoke to Moses in the land of Egypt,
29 alimwambia, “Mimi ni Yahweh. Sema kwa Farao, mfalme wa MIsri, kila kitu nitacho kwambia.”
he said to him, “I am Yahweh. Say to Pharaoh, king of Egypt, everything that I will tell you.”
30 Lakini Musa alimwambia Yahweh, “Mimi sio mzuri wa kuongea, hivyo kwanini Farao anisikilize mimi?”
But Moses said to Yahweh, “I am not good at speaking, so why will Pharaoh listen to me?”