< Kutoka 5 >

1 Baada ya mambo haya kutokea, Musa na Aruni walienda kwa Farao na kumwambia, ““Hivi ndivyo Yahwe, Mungu wa Israeli anasema: 'Waache watu wangu waende, ili wapate kunifanyia karamu jangwani.'”
And after that, Moses and Aaron came to Pharaoh, and said, The Lord, the God of Israel, says, Let my people go so that they may keep a feast to me in the waste land.
2 Farao akasema, “Yahwe ni nani? Kwa nini mimi nisikiliz sauti yake na kuwaacha Israeli waende? Mimi simjui Yahwe; na la zaidi, sitawaacha Israeli waende.”
And Pharaoh said, Who is the Lord, to whose voice I am to give ear and let Israel go? I have no knowledge of the Lord and I will not let Israel go.
3 Wakasema, “Mungu wa Waebrania amekutana nasi. Tuache twende safari jangwani kwa siku tatu ili tutoe sadaka kwa Yahwe Mungu wetu ili asituadhibu kwa mapigo au kwa upanga.”
And they said, The God of the Hebrews has come to us: let us then go three days' journey into the waste land to make an offering to the Lord our God, so that he may not send death on us by disease or the sword.
4 Lakini mfalme wa Misri aliwaambia, “Musa na Aruni, kwa nini mnawatoa watu kazini mwao? Nendeni kazini kwenu.”
And the king of Egypt said to them, Why do you, Moses and Aaron, take the people away from their work? get back to your work.
5 Pia alisema, “Sasa kuna Waebrania wengi nchini mwetu, na ninyi mnawafanya waache kazi zao.”
And Pharaoh said, Truly, the people of the land are increasing in number, and you are keeping them back from their work.
6 Siku ile ile, Farao alitoa amri kwa wasimamizi na wanyapara wa wale watu. Akasema,
The same day Pharaoh gave orders to the overseers and those who were responsible for the work, saying,
7 “Tofauti na ilivyokuwa mwanzo, “Tofauti ni ilivyokuwa awali, msiwapatie tena watu majani ya kutengenezea tofali. Waacheni wao waende kujitafutia majani wenyewe.
Give these men no more dry stems for their brick-making as you have been doing; let them go and get the material for themselves.
8 Ingawa wanapaswa kuleta hesabu sawa ya matofali watakayotengeneza kama ilivyokuwa awali. Msipokee pungufu, kwasababu wao ni wavivu. Ndiyo maana wanapiga kelele na kusema, 'turuhusu tuende tukamtolee sadaka Mungu wetu.'
But see that they make the same number of bricks as before, and no less: for they have no love for work; and so they are crying out and saying, Let us go and make an offering to our God.
9 Waongezeeni kazi wanaume ili wasipate tena muda wa kusikiliza maneno ya upotoshaji.”
Give the men harder work, and see that they do it; let them not give attention to false words.
10 Kwa hiyo viongozi wa watu na waangalizi wao waliwajulisha watu. Walisema, “Hivi ndivyo farao amesema: 'Sitawapeni tena malighafi.
And the overseers of the people and their responsible men went out and said to the people, Pharaoh says, I will give you no more dry stems.
11 Nyinyi wenyewe mtaenda kutafuta majani popote mtakapopata, lakini kazi zenu hazitapunguzwa.
Go yourselves and get dry stems wherever you are able; for your work is not to be any less.
12 Basi watu hao wakatawanyika katika nchi yote ya Misri ili wapate kukusanya matakataka badala ya majani.
So the people were sent in all directions through the land of Egypt to get dry grass for stems.
13 Wasimamizi wao wakawahimiza na kusema, “Malizeni kazi zenu, sawa na wakati ule majani yalipokuwapo.”
And the overseers went on driving them and saying, Do your full day's work as before when there were dry stems for you.
14 Wanyapara wa Farao wakawapiga wasimamizi wa Waisraeli, watu walewale ambao waliwaweka kuwa wasimamizi wa watumishi. Wale Wanyapara wakakazana kuwauliza, “Kwanini hamjatimiza idadi ya matofali inayotakiwa kwenu, siku ya jana na hata leo kama ambavyo mlifanya siku za nyuma?”
And the responsible men of the children of Israel, whom Pharaoh's overseers had put over them, were given blows, and they said to them, Why have you not done your regular work, in making bricks as before?
15 Basi Wanyapara wa wana wa Israeli wakamwendea Farao na kumlilia. Walisema, “Kwanini unawatendea watumishi wako hivi?
Then the responsible men of the children of Israel came to Pharaoh, protesting and saying, Why are you acting in this way to your servants?
16 Sisi watumishi wako hatupewi majani tena, lakini bado wanatuambia sisi, “Tengenezeni tofali!' Sisi watumwa wako tunapigwa sasa, lakini kosa hilo ni la watu wako.”
They give us no dry stems and they say to us, Make bricks: and they give your servants blows; but it is your people who are in the wrong.
17 Lakini Farao akasema, “Ninyi ni wavivu! Wavivu ninyi! Ninyi mwasema, 'Turuhusu twende kumtolea Yahwe sadaka.'
But he said, You have no love for work: that is why you say, Let us go and make an offering to the Lord.
18 Sasa rudini kazini. Hamtapewa majani tena, lakini mnapaswa kutengeneza idadi ile ile ya matofali.”
Go now, get back to your work; no dry stems will be given to you, but you are to make the full number of bricks.
19 Wanyapara wa wana wa Israeli wakagundua ya kuwa walikuwa kwenye shida kubwa mara walipoambiwa, “Hamtapunguza kamwe idadi ya matofali mnayotengeneza kila siku.”
Then the responsible men of the children of Israel saw that they were purposing evil when they said, The number of bricks which you have to make every day will be no less than before.
20 Wakakutana na Musa na Haruni, waliokuwa wamesimama nje ya Ikulu wakati wanatoka kwa Farao.
And they came face to face with Moses and Aaron, who were in their way when they came out from Pharaoh:
21 Wakawaambia Musa na Haruni, “Yahwe awatazame ninyi na kuwaadhibu, kwa sababu mmetufanya sisi kuonekana wabaya mbele ya Farao na watumishi wake. Mmetia upanga mikononi mwao ili watuue.”
And they said to them, May the Lord take note of you and be your judge; for you have given Pharaoh and his servants a bad opinion of us, putting a sword in their hands for our destruction.
22 Musa akarudi kwa BWANA na kumwambia, “Bwana, kwanini umewatenda mabaya watu hawa? Kwanini kunituma mimi kwanza?
And Moses went back to the Lord and said, Lord, why have you done evil to this people? why have you sent me?
23 Tangu nilipokuja kwa Farao kusema naye kwa jina lako, amewatenda mabaya watu hawa, wala hujawaokoa watu wako hata kidogo.”
For from the time when I came to Pharaoh to put your words before him, he has done evil to this people, and you have given them no help.

< Kutoka 5 >